Subira the princess
JF-Expert Member
- Mar 3, 2018
- 2,463
- 2,640
Wasalaam.
Nakumbuka july 26 mwaka 2017 aliekuwa spika wa bunge JMT mh ndugai aliwavua ubunge wabunge 8 wa CUF mara baada ya wabunge hao kuvuliwa uanachama na barua ya kuvuliwa uanachama kupokelewa na bunge japo wabunge hao walifungua kesi mahakamani. Spika ndugai alisema nanukuu 'unapovuliwa uanachama moja kwa moja unapoteza sifa ya kuwa mbunge mpaka mahakama itapoamua vinginevyo'
Sasa leo hii inashangaza spika huyu anatafsiri kanuni ile ile kwa namna tofauti na kuwaruhusu COVID 19 kuendelea kuhudhuria vikao vya bunge kwa point dhaifu ya shauri kuwa mahakamani. Tunakumbuka spika Tulia wakati anakula kiapo aliulizwa juu covid 19 akajibu hajapokea barua ya chadema, leo hii anapokea barua anapata kigugumizi cha nini?
Bunge kuendelea kuwakumbatia na kuwalipa mishahara na posho wabunge feki wasiokuwa na chama ni wizi na ufisadi na ni matumizi ya hovyo ya kodi za watanzania. Haishangazi maana wizi na ufisadi ni jambo la kawaida ndani ya serikali ya ccm lakini watanzania tuna macho tunaona na masikio yanasikia na mungu atawahukumu kwa karama zake.
Nakumbuka july 26 mwaka 2017 aliekuwa spika wa bunge JMT mh ndugai aliwavua ubunge wabunge 8 wa CUF mara baada ya wabunge hao kuvuliwa uanachama na barua ya kuvuliwa uanachama kupokelewa na bunge japo wabunge hao walifungua kesi mahakamani. Spika ndugai alisema nanukuu 'unapovuliwa uanachama moja kwa moja unapoteza sifa ya kuwa mbunge mpaka mahakama itapoamua vinginevyo'
Sasa leo hii inashangaza spika huyu anatafsiri kanuni ile ile kwa namna tofauti na kuwaruhusu COVID 19 kuendelea kuhudhuria vikao vya bunge kwa point dhaifu ya shauri kuwa mahakamani. Tunakumbuka spika Tulia wakati anakula kiapo aliulizwa juu covid 19 akajibu hajapokea barua ya chadema, leo hii anapokea barua anapata kigugumizi cha nini?
Bunge kuendelea kuwakumbatia na kuwalipa mishahara na posho wabunge feki wasiokuwa na chama ni wizi na ufisadi na ni matumizi ya hovyo ya kodi za watanzania. Haishangazi maana wizi na ufisadi ni jambo la kawaida ndani ya serikali ya ccm lakini watanzania tuna macho tunaona na masikio yanasikia na mungu atawahukumu kwa karama zake.