Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,136
Mahabusu adaiwa kufa baada ya kulawitiwa Segerea
Na James Magai
MAHABUSU katika Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam, wanadaiwa kumlawiti mwenzao hadi kufa.
Habari zilizolifikia gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita zilisema mahabusu huyo Hasara Omar anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 20 alifanyiwa kitendo hicho Jumatano iliyopita.
Alipoulizwa na Mwananchi jana kuhusiana na tukio hilo, Msemaji wa Jeshi la Magereza Kamishna Msaidizi wa Magereza, (ACP) Mtiga Omari, alikiri kupata taarifa za kifo cha mahabusu huyo.
Hata hivyo ACP Omari alisema taarifa anazozifahamu ni kwamba mahabusu huyo anadaiwa kupigwa na mahabusu wenzake na kwamba alifia hospitalini.
Lakini habari zilizopatikana kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu(SMS) kutoka kwa mtu ambaye hata hivyo hakujitambulisha zilisema mahabusu huyo alifikishwa gerezani hapo siku ya Mei 27 na kufanyiwa vitendo hivyo usiku hali iliyosababisha kifo chake.
Katika SMS hiyo ambayo hata hivyo haikuwa na ufafanuzi wa kina kuhusiana na tukio hilo, mtumaji ambaye alionekana kutuma ujumbe huo kwa hofu huku akiliita tukio hilo kifo cha kinyama, aliomba msaada wa vyombo vya habari pamoja na vyombo vya kisheria kuingilia kati katika tukio hilo ili wahusika waweze kuchukukliwa hatua.
ACP Omar alisema mahabusu huyo alifikishwa gerezani hapo Mei 27 na kwamba inadaiwa alipigwa na mahabusu wenzake usiku, na alitolewa gerezani hapo Mei 28 na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
Licha ya kuwa na taarifa hizo za mahabusu huyo kupigwa na mahabusu wenzake, ACP Omar alisema kuhusu chanzo cha kifo cha mahabusu huyo bado wanasubiri taarifa ya uchunguzi wa chanzo hicho (Postmortem Report) kutoka hospitalini hapo.
Ninachofahamu mimi ni kwamba Segerea kuna mahabusu alifariki dunia, na alifariki akiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, taratibu zetu za kisheria ni kwamba cause of death(Sababu ya kifo) ni baada ya kufanyika postmortem(uchunguzi), alisema ACP Omar.
Alipoulizwa sababu ya mahabusu hao kumpiga mahabusu mwenzao, ACP Omar alisema kwa sasa bado wanafanya uchunguzi juu ya sababu ya mahabusu hao kuchukua hatua hiyo.
Aliongeza kuwa watakaogundulika kuhusika na tukio hilo watachukulia hatua za kisheria.
Kama unavyojua kumuua mtu ni kosa la jinai, kwa hiyo bado tunasubiri kujua taarifa ya kifo, waliompiga watafikishwa mahakamani kufunguliwa mashtaka, alisisitiza ACP Omari.
Na James Magai
MAHABUSU katika Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam, wanadaiwa kumlawiti mwenzao hadi kufa.
Habari zilizolifikia gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita zilisema mahabusu huyo Hasara Omar anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 20 alifanyiwa kitendo hicho Jumatano iliyopita.
Alipoulizwa na Mwananchi jana kuhusiana na tukio hilo, Msemaji wa Jeshi la Magereza Kamishna Msaidizi wa Magereza, (ACP) Mtiga Omari, alikiri kupata taarifa za kifo cha mahabusu huyo.
Hata hivyo ACP Omari alisema taarifa anazozifahamu ni kwamba mahabusu huyo anadaiwa kupigwa na mahabusu wenzake na kwamba alifia hospitalini.
Lakini habari zilizopatikana kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu(SMS) kutoka kwa mtu ambaye hata hivyo hakujitambulisha zilisema mahabusu huyo alifikishwa gerezani hapo siku ya Mei 27 na kufanyiwa vitendo hivyo usiku hali iliyosababisha kifo chake.
Katika SMS hiyo ambayo hata hivyo haikuwa na ufafanuzi wa kina kuhusiana na tukio hilo, mtumaji ambaye alionekana kutuma ujumbe huo kwa hofu huku akiliita tukio hilo kifo cha kinyama, aliomba msaada wa vyombo vya habari pamoja na vyombo vya kisheria kuingilia kati katika tukio hilo ili wahusika waweze kuchukukliwa hatua.
ACP Omar alisema mahabusu huyo alifikishwa gerezani hapo Mei 27 na kwamba inadaiwa alipigwa na mahabusu wenzake usiku, na alitolewa gerezani hapo Mei 28 na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
Licha ya kuwa na taarifa hizo za mahabusu huyo kupigwa na mahabusu wenzake, ACP Omar alisema kuhusu chanzo cha kifo cha mahabusu huyo bado wanasubiri taarifa ya uchunguzi wa chanzo hicho (Postmortem Report) kutoka hospitalini hapo.
Ninachofahamu mimi ni kwamba Segerea kuna mahabusu alifariki dunia, na alifariki akiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, taratibu zetu za kisheria ni kwamba cause of death(Sababu ya kifo) ni baada ya kufanyika postmortem(uchunguzi), alisema ACP Omar.
Alipoulizwa sababu ya mahabusu hao kumpiga mahabusu mwenzao, ACP Omar alisema kwa sasa bado wanafanya uchunguzi juu ya sababu ya mahabusu hao kuchukua hatua hiyo.
Aliongeza kuwa watakaogundulika kuhusika na tukio hilo watachukulia hatua za kisheria.
Kama unavyojua kumuua mtu ni kosa la jinai, kwa hiyo bado tunasubiri kujua taarifa ya kifo, waliompiga watafikishwa mahakamani kufunguliwa mashtaka, alisisitiza ACP Omari.