Magufuli; Walimu Kupata Maisha Bora kama Mapadre. Ahadi hii Imekaaje?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,753
71,126
Mgombea wa CCM amewaahidi Walimu kuwa akichaguliwa atawapatia maisha bora kama Mapadre. Ahadi hiyo imeleta maswali mengi zaidi kwani ni Watanzania wachache wanaojua maisha hayo bora ya Mapadre kwani wao wanaishi maisha ya kitawa katika maeneo yao wanayoishi ambayo kwa kawaida huwa wanajitenga kulingana na kanuni za kazi yao.
Au huu nao ni mwendelezo wa ahadi za kukurupuka kama zile ambazo tuliziona 2010 na zimebaki kama riwaya kwenye vitabu? Jee kiongozi anaposimama na kujiropokea ahadi anazojua hazipo na haziwezi kuwepo ni dharau kwa wapiga kura au ni maagizo ya chama anachokiwakilisha?
Wapo walimu ambao kutokana na Imani zao za kidini hawawezi kuishi maisha yao kama mapadre hao amewachukuliaje?
 
Hata nikiwa stand nikikutana na Kondakta/ mpiga debe mwenye maneno mengi sana Gari yake sipandi
 
wameshindwa maisha bora kwa kila watanzania kuishi kama mapadre ndo wataweza?
 
Kwa maghufuli utakosoa kila kitu, ila lowasa akijam.a utasema ' lowasa anatoa ushuzi kama rais'. Punguzeni mahaba, alinselema, mtaimba tu. Msipoimba kwa Magufuli, atawaimbisha lowasa akimsindikiza Magufuli magogoni.
 
Ngoja nimpigie rafiki yangu Mwalimu Jumanne Hamisi nimuulize yuko tayari kuishi maisha ya kiseja kama Padre? Pia anakubaliana na lunch box yake kuwekewa soseji za pork? Maana ndio chakula bora cha mapadre.
 
Kwa maghufuli utakosoa kila kitu, ila lowasa akijam.a utasema ' lowasa anatoa ushuzi kama rais'. Punguzeni mahaba, alinselema, mtaimba tu. Msipoimba kwa Magufuli, atawaimbisha lowasa akimsindikiza Magufuli magogoni.

Kweli kukosoa kila kitu sio sawa. Lakini suala la kuwapa maisha bora Waalimu yawe kama mapadre wewe unalionaje?
 
Chakaza haya ndio matusi tuliyosema CCM wanatusi wananchi wake. Ni upumbavu kuropoka bila kufikiria
 
Last edited by a moderator:
Ccm muwe makini na hizi ahadi,mkiendelea mtazomewa sana,naskia mgombea mwenza naye juzi katia ndimu kuhusu madini ya iron,
 
Ccm muwe makini na hizi ahadi,mkiendelea mtazomewa sana,naskia mgombea mwenza naye juzi katia ndimu kuhusu madini ya iron,

Yes, kasema yanaweza kuchimbwa na serikali ya ccm kwa muda wa miaka milioni 200. Nilicheka mpaka nahisi mbavu zangu zinahitaji kufanyiwa check up.
 
Yes, kasema yanaweza kuchimbwa na serikali ya ccm kwa muda wa miaka milioni 200. Nilicheka mpaka nahisi mbavu zangu zinahitaji kufanyiwa check up.


Yeah... mgombea mwenza kaharibu na kaonyesha jinsi alivyo kilaza haswa... it seems akipewa data anazimeza tu..

Samia hata shule zake za kunga unga tu...
😨😨😨😨 imagine eti Tanzania kuna madini ya chuma inaweza kuchimbwa mfululizo kwa miaka milioni 200...😨😨😨😨😨.

Kichwani kwa Samia, hajui anaongea nn, sbb her academic background, ni shida..

Anyway... Magufuli jana HAJAMEZA DAWA ZILE ZA UKICHAA...?

Si nasikia hayuko sawa, labda jana alisahau dose...!!!
 
Huyo jamaa ni hamnazo, kazi pekee anayoweza ni kusimamia maelekezo aliyopewa na ikitokea muelekezaji alikosea jamaa hana ile akili ya kuchanganya na zake. Ndio maana wakti flani alikurupuka kutekeleza sheria na kuanza bomoa nyumba za wanyonge hovyo bila hata kuwapa notice hadi jk alipomstopisha na kumshangaa. Alipoulizwa akasema yeye anafata sheria haijalishi watu wafe.
 
Mtajadili sana na mtamkosoa sana lakn ikulu lazma aende. Ukiwa na ubongo mwepesi huwez kuielewa hyo kauli na utaichukulia kama matusi na ndivyo akili za wanaukawa zilivyo haziwez kufikir upande wa pili wao kila wanalolisikia wanajua ndivyo ilivyo...
 
Duh kwahiyo mapadre wana maisha bora sana kuwashinda walimu? vipi masheikh wetu??

CC: kahtaan Ritz FaizaFoxy

Hapo sasa! Nadhani kifuatacho atasema Madaktari wataishi maisha bora kama Maaskofu, na Mainjinia kwa vile ndio fani yake watapata maisha bora kama Papa Francis
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom