Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,397
- 3,884
Kuna mchezo mmoja wa watoto unaitwa 'Who Will Blink First'. Katika mchezo huo watu wawili wanaangaliana na anayekuwa wa kwanza ku 'blink' au kupepesa macho anakuwa ameshindwa.
Katika sakata linaloendelea huko ndani ya CCM mchezo ambao umekuwa unachezwa ni huu nilioutaja hapo juu.
Toka audio clips zilipoanza kutoka nilisema hizi zimerekodiwa na kuachiwa na wahusika wenyewe kwa lengo maalumu (sikulitaja kwa sababu nilikuwa bado nafanya tathmini).
Team CCM-Asilia kama walivyosikika wanasema ni kwamba wanajaribu kuchochea na kuwapa ujasiri wana CCM-Asilia wengine waanze kutoa hisia zao waziwazi kuhusu mienendo ya chama na nchi.
Nimetoka kusikiliza clip ya Membe na Katibu Kata, hii clip na yenyewe imeachiwa kimkakati kabisa. Ukizungumza ngazi ya Kata unaongelea CCM wa chini huku, hii wamefanya ili isionekane kuwa hili ni suala la wazito walio juu tu.
Kwa kumalizia, kitendo cha The Gang of Five kwa mpigo kujihusisha na waraka na audio clips pia haikuwa kwa bahati mbaya. Wanajua Magufuli pamoja na jeuri yake hawezi kuwavua uanachama wote Membe, Makamba Sr na Jr, Nape, Kinana kwa mpigo. Swali linabaki, je atatoa adhabu gani huku akiwaweka hawa siyo tu 'at arms length' lakini ikiwezekana pia kuwatenganisha na wakati huo huo aweze kuproject mamlaka isiyotikisika? Hilo ndiyo zoezi kubwa linalomkabili.
Je akifukuza baadhi yao na wengine akawapa onyo kali kama alivyofanya wakati ule kwa Sophia Simba na Nchimbi, je haitaonekana amewaogopa? Ukizingatia ukubwa wa 'kosa' wanaloshutumiwa nalo hiyo italeta tafsiri gani kwa wengine wanaosikilizia upepo unaelekea wapi? Je, The Gang of Five hawataonekana mashujaa wanaostahili kuigwa?
Wasiwasi wangu ni kuwa hili jambo linaweza kabisa kwenda out of control na likatuathiri hata watazamaji. Ni dhahiri The Gang of Five hawako peke yao. Ni wazi Magufuli analijua hilo. Na yeye anapalilia vitu ili mambo yakienda ndivyo sivyo aende kama Tony Montana. Huo ndiyo wasiwasi wangu.
Katika sakata linaloendelea huko ndani ya CCM mchezo ambao umekuwa unachezwa ni huu nilioutaja hapo juu.
Toka audio clips zilipoanza kutoka nilisema hizi zimerekodiwa na kuachiwa na wahusika wenyewe kwa lengo maalumu (sikulitaja kwa sababu nilikuwa bado nafanya tathmini).
Team CCM-Asilia kama walivyosikika wanasema ni kwamba wanajaribu kuchochea na kuwapa ujasiri wana CCM-Asilia wengine waanze kutoa hisia zao waziwazi kuhusu mienendo ya chama na nchi.
Nimetoka kusikiliza clip ya Membe na Katibu Kata, hii clip na yenyewe imeachiwa kimkakati kabisa. Ukizungumza ngazi ya Kata unaongelea CCM wa chini huku, hii wamefanya ili isionekane kuwa hili ni suala la wazito walio juu tu.
Kwa kumalizia, kitendo cha The Gang of Five kwa mpigo kujihusisha na waraka na audio clips pia haikuwa kwa bahati mbaya. Wanajua Magufuli pamoja na jeuri yake hawezi kuwavua uanachama wote Membe, Makamba Sr na Jr, Nape, Kinana kwa mpigo. Swali linabaki, je atatoa adhabu gani huku akiwaweka hawa siyo tu 'at arms length' lakini ikiwezekana pia kuwatenganisha na wakati huo huo aweze kuproject mamlaka isiyotikisika? Hilo ndiyo zoezi kubwa linalomkabili.
Je akifukuza baadhi yao na wengine akawapa onyo kali kama alivyofanya wakati ule kwa Sophia Simba na Nchimbi, je haitaonekana amewaogopa? Ukizingatia ukubwa wa 'kosa' wanaloshutumiwa nalo hiyo italeta tafsiri gani kwa wengine wanaosikilizia upepo unaelekea wapi? Je, The Gang of Five hawataonekana mashujaa wanaostahili kuigwa?
Wasiwasi wangu ni kuwa hili jambo linaweza kabisa kwenda out of control na likatuathiri hata watazamaji. Ni dhahiri The Gang of Five hawako peke yao. Ni wazi Magufuli analijua hilo. Na yeye anapalilia vitu ili mambo yakienda ndivyo sivyo aende kama Tony Montana. Huo ndiyo wasiwasi wangu.