Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,898
JPM usichanganye majukumu yako ya kisiasa na ya Kiserikali. Pesa za walipa kodi watanzania zinatumika vibaya.
---------------------------------------------------
Inakuwaje JPM anafanya siasa za chama chake katika Mikutano ya Kiserikali? Mikutano ya wananchi? Kwa kawaida ziara za Rais hugharamiwa na fedha za watanzania wote bila kuangalia kama ni mwanaCCM au chama kingine cha siasa.
...
Siasa ya namna hii ya JPM haikubaliki? Unapokeaje wanachama waliohama toka chama kingine katika mkutano wa kiserikali, mkutano wa wananchi?
JPM pia anajikaanga kwa kuwapigia debe madiwani hao waliohama toka CHADEMA kwa kuwaomba viongozi wa CCM wawape nafasi za kugombea kupitia chama cha CCM; Hii maana yake nini?
Hii maana yake ni kwamba tayari JPM anakiuka utaratibu na kanuni za uongozi na uchaguzi ndani ya chama chake kwa kutoa maelekezo yanayoashiria kuwatenga WanaCCM wengine kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi wa ndani wa chama hicho! Mwenyekiti wa Taifa wa chama anayehubiri maadili na CCM mpya leo anafanya haya kwa kutamka!
Yuko wapi HUMPHREY POLEPOLE anayeshadidia kuwa chini ya JPM kuna CCM mpya inatengenezwa ? Chini ya JPM hakuna CCM mpya bali CCM inayorudi kwenye mfumo wa " Zidumu fikra za Mwenyekiti" hii ndiyo CCM inayojengwa chini ya JPM na wanaCCM mnapaswa kulitambua hili.
Nikirejea kwenye matumizi isivyo sahihi za pesa Umma, JPM anapaswa kutenganisha ziara zake za kisiasa na Kiserikali. Anapaswa kuishi kwa kile anachokihubiri na isiwe ni usanii wa kudanganya umma kwamba tunapigania maslahi ya wanyonge ilhali wanyonge hao ni WanaCCM milioni 6 na si Watanzania milioni 54!
Kwenye Mkutano wa kuwa Commission Maafisa wa Jeshi na Mkutano wa wananchi kama ilivyokuwa agenda ya mkutano huo, Rais anafanya siasa, anapokea wanachama wapya ? Hii ndio Tanzania inayorudi miaka 50 nyuma katika demokrasia chini ya JPM!
Tunahitaji matumizi sahihi ya kodi zetu, ni lazima watanzania tupaaze sauti tuseme kwa vinywa vyetu na maneno makali: "Tunahitaji Matumizi sahihi ya fedha zinazotokana na kodi zetu"
Ghafla nimemkumbuka kaka yangu Tundu Lissu, najua angelisemea hili pia. Mungu amponye haraka arudi kuendelea na majukumu ya kutetea na kulinda rasilimali za nchi yetu.
[HASHTAG]#PrayforTunduLissu[/HASHTAG]
2017 Septemba, 23
---------------------------------------------------
Inakuwaje JPM anafanya siasa za chama chake katika Mikutano ya Kiserikali? Mikutano ya wananchi? Kwa kawaida ziara za Rais hugharamiwa na fedha za watanzania wote bila kuangalia kama ni mwanaCCM au chama kingine cha siasa.
...
Siasa ya namna hii ya JPM haikubaliki? Unapokeaje wanachama waliohama toka chama kingine katika mkutano wa kiserikali, mkutano wa wananchi?
JPM pia anajikaanga kwa kuwapigia debe madiwani hao waliohama toka CHADEMA kwa kuwaomba viongozi wa CCM wawape nafasi za kugombea kupitia chama cha CCM; Hii maana yake nini?
Hii maana yake ni kwamba tayari JPM anakiuka utaratibu na kanuni za uongozi na uchaguzi ndani ya chama chake kwa kutoa maelekezo yanayoashiria kuwatenga WanaCCM wengine kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi wa ndani wa chama hicho! Mwenyekiti wa Taifa wa chama anayehubiri maadili na CCM mpya leo anafanya haya kwa kutamka!
Yuko wapi HUMPHREY POLEPOLE anayeshadidia kuwa chini ya JPM kuna CCM mpya inatengenezwa ? Chini ya JPM hakuna CCM mpya bali CCM inayorudi kwenye mfumo wa " Zidumu fikra za Mwenyekiti" hii ndiyo CCM inayojengwa chini ya JPM na wanaCCM mnapaswa kulitambua hili.
Nikirejea kwenye matumizi isivyo sahihi za pesa Umma, JPM anapaswa kutenganisha ziara zake za kisiasa na Kiserikali. Anapaswa kuishi kwa kile anachokihubiri na isiwe ni usanii wa kudanganya umma kwamba tunapigania maslahi ya wanyonge ilhali wanyonge hao ni WanaCCM milioni 6 na si Watanzania milioni 54!
Kwenye Mkutano wa kuwa Commission Maafisa wa Jeshi na Mkutano wa wananchi kama ilivyokuwa agenda ya mkutano huo, Rais anafanya siasa, anapokea wanachama wapya ? Hii ndio Tanzania inayorudi miaka 50 nyuma katika demokrasia chini ya JPM!
Tunahitaji matumizi sahihi ya kodi zetu, ni lazima watanzania tupaaze sauti tuseme kwa vinywa vyetu na maneno makali: "Tunahitaji Matumizi sahihi ya fedha zinazotokana na kodi zetu"
Ghafla nimemkumbuka kaka yangu Tundu Lissu, najua angelisemea hili pia. Mungu amponye haraka arudi kuendelea na majukumu ya kutetea na kulinda rasilimali za nchi yetu.
[HASHTAG]#PrayforTunduLissu[/HASHTAG]
2017 Septemba, 23