Magufuli: The Road To Hell Is Paved With Good Intentions

MwendaOmo

JF-Expert Member
Dec 16, 2013
774
723
Mara kadhaa katika jukwa hili na majukwaa mengine, nilisema kwamba Kenya inahitaji Rais Kama Magufuli. Nakumbuka hata kuna wakati tulipingana sana na MK254 kuhusu systems vs personalities. MK254 alimsifu Magufuli kwa nia yake, lakini alikuwa very cautious kuhusu mtindo wake wa kufanya mambo. Mimi naye, nilikuwa upande ule mwingine wa kutaka ule mtindo wa Magufuli. Siku ya leo, nakubali kuwa nilikuwa nimekosea. Ingawa taifa linahitaji kiongozi mwenye mamlaka kama vile Kagame, kiongozi huyu yafaa awe na nia ya kuweka taasisi zitakazodumu kuliko madaraka yake mwenyewe.

Magufuli ni kiongozi ambaye anatakia taifa lake mema. Tatizo lake ni kukurupuka na kuwafanya wote ambao wako upande wake kuwa adui ikiwa hawatakubaliana naye kwa vitu vyote. Juzi amekurupuka kwa hili la kuibiwa mali ya taifa, na vile ninavyoona, kuna vile kamati imemdanganya hata kwa mambo ya kiupuzi. Kwa mfano; kamati yamuambia kuwa Kampuni ya Acacia, haijasajiliwa Kule Tanzania; itakuwaje basi kampuni hii iwe inalipa Ushuru, PAYE na mengine yote? Huu sio upuuzi tu? Wakati anapokea ripoti hii, Rais alisema kuwa anakubaliana na mapendekezo yote 100%. Hii ni ripoti amabyo hata hajasoma na ndio anapokea tu. Hata hujawauliza civil servants walio ndani for second opinion?

Upuuzi huu huu ndio alioufanya kule kwenye bandari. Sasa hivi, vitu vinavyopita kwa bandari ya Dar vimepunguwa kwa asilimia 13%. Vitu vinavyopitia bandari ya Mombasa na kuingia Tanzania vimeongezeka kutoka 1% hadi 2.7%. Ni kitu gani kinafanyika huku? Kwa kweli uongozi unahitaji busara. Ndiposa wazungu walinena: "The road to hell is paved with good intentions."

Ukitazama video hii ya mbunge wa CCM, utaona kuanzia dakika 7, akiongelea ya bandari

 
Hiyo video ya mbunge unamjua vizuri huyo mbunge? Ni mfuasi wa Edward Lowassa, kwa hakika 2020 abadili chama maana hatapata nafasi tena ndani ya CCM.

Kuhusu bandarini, kilichofanya mizigo ipungue sio Magufuli. Ni sheria ya kuweka VAT kwenye transit goods Julai 1, 2015 chini ya Jakaya Kikwete na wizi uliopitiliza. Sasa hivi mizigo imeongezeka na inazidi kuongezeka.

Kuhusu Acacia kusajiliwa ama kutokusajiliwa, kwa hakika watu waliopewa kazi ya uchunguzi wanajua mambo kuliko wewe. Wewe hujui hata sheria moja ya Tanzania madai yako hayana nguvu hata kidogo.

Madai yako ya kukurupuka hayana msingi maana hujui ngazi za maamuzi Tanzania.
 
Hiyo video ya mbunge unamjua vizuri huyo mbunge? Ni mfuasi wa Edward Lowassa, kwa hakika 2020 abadili chama maana hatapata nafasi tena ndani ya CCM.

Kuhusu bandarini, kilichofanya mizigo ipungue sio Magufuli. Ni sheria ya kuweka VAT kwenye transit goods Julai 1, 2015 chini ya Jakaya Kikwete na wizi uliopitiliza. Sasa hivi mizigo imeongezeka na inazidi kuongezeka.

Kuhusu Acacia kusajiliwa ama kutokusajiliwa, kwa hakika watu waliopewa kazi ya uchunguzi wanajua mambo kuliko wewe. Wewe hujui hata sheria moja ya Tanzania madai yako hayana nguvu hata kidogo.

Madai yako ya kukurupuka hayana msingi maana hujui ngazi za maamuzi Tanzania.

1. Kwa kuwa yeye ni Mfuasi wa Lowassa anachosema ni Uongo? Hukumu mtu kulingana na ukweli wa jambo analosema.

2. 2015 ilikuwa asilimia moja; 2016 ikawa asilimia 2.7 unataka kusema huo ni kuongezeka? Una data yoyote ya kuonyehsa kuwa inaongezeka mwaka wa 2017?

3. Acacia kuna vitu vya common sense. Tatizo lako ni kuamini serika "Inajua" kushinda wewe. Kwani hii miaka iliyopita si watetezi wa serikali na sycophants wa CCM walikuwa wakikariri tu hayohayo? Kuwa serika inajua kuliko wewe?

Nipe tu jibu moja; Hilo serikali lenyu lenye lajua kuliko mwananchi, ilikusanyaje kodi kutoka kwa kampuni ghushi? Wasomi wenyu kweli wako taabani ikiwa wanasheria hawawezi kuelewa kitu kama hicho na kuufanya ukawa mjadala mkumbwa.
 
1. Kwa kuwa yeye ni Mfuasi wa Lowassa anachosema ni Uongo? Hukumu mtu kulingana na ukweli wa jambo analosema.

2. 2015 ilikuwa asilimia moja; 2016 ikawa asilimia 2.7 unataka kusema huo ni kuongezeka? Una data yoyote ya kuonyehsa kuwa inaongezeka mwaka wa 2017?

3. Acacia kuna vitu vya common sense. Tatizo lako ni kuamini serika "Inajua" kushinda wewe. Kwani hii miaka iliyopita si watetezi wa serikali na sycophants wa CCM walikuwa wakikariri tu hayohayo? Kuwa serika inajua kuliko wewe?

Nipe tu jibu moja; Hilo serikali lenyu lenye lajua kuliko mwananchi, ilikusanyaje kodi kutoka kwa kampuni ghushi? Wasomi wenyu kweli wako taabani ikiwa wanasheria hawawezi kuelewa kitu kama hicho na kuufanya ukawa mjadala mkumbwa.

Asemavyo Bashir Yakub kuhusu ACACIA kutosajiliwa Tanzania kisheria
 
1. Kwa kuwa yeye ni Mfuasi wa Lowassa anachosema ni Uongo? Hukumu mtu kulingana na ukweli wa jambo analosema.

2. 2015 ilikuwa asilimia moja; 2016 ikawa asilimia 2.7 unataka kusema huo ni kuongezeka? Una data yoyote ya kuonyehsa kuwa inaongezeka mwaka wa 2017?

3. Acacia kuna vitu vya common sense. Tatizo lako ni kuamini serika "Inajua" kushinda wewe. Kwani hii miaka iliyopita si watetezi wa serikali na sycophants wa CCM walikuwa wakikariri tu hayohayo? Kuwa serika inajua kuliko wewe?

Nipe tu jibu moja; Hilo serikali lenyu lenye lajua kuliko mwananchi, ilikusanyaje kodi kutoka kwa kampuni ghushi? Wasomi wenyu kweli wako taabani ikiwa wanasheria hawawezi kuelewa kitu kama hicho na kuufanya ukawa mjadala mkumbwa.
MwendaOmo hujui unalozungumza, ni vyema ukauliza kuliko kuanza kuropoka.

1) Bandari, Magu amejitahidi kusafisha uozo mwingi uliokuwa bandarini, kabla ya Magu Bandari ilikuwa inatoa mapato kati 250bn hadi 350bn Tsh per month, saivi mapato ya bandari ni 350 hadi 500bn Tsh per month, je kwako wewe hii ni hasara? Ni kweli kuna tatizo la mizigo kupungua bandari ya Dar tatizo kubwa likiwa ni VAT iliyokuwa inatozwa kwa transit goods, hii sheria ilipitishwa July 2015 na uongozi uliopita na katika bajeti hii ya 2017/2018 hii VAT kwa transit goods imeondolewa. Kwa ufupi mapato ya bandari yameongezeka vivyo hivyo kwa ubora na ulinzi wa Bandari ya Dar.

2) Kusajiliwa kwa Acacia, that's a fact, hao watu hawajasajiliwa, wakati Prof Ossoro anasema hilo, Magu ana PM Majaliwa wote walikuwa wanashangaa wakiwa midomo wazi, hakuna aliyetegemea kampuni kubwa kama Acacia inaweza kufanya uzembe kama huo, ilikuwaje wakaruhusiwa kutumia usajili wa Barrick kwa shughuli ni maswali ambayo majibu wanayo wao wenyewe.

Mwisho, usipende kuropoka usivyovijua uliza kistaarabu, utaelekezwa. Magu ana matatizo yake ila kwa haya tupo naye pamoja na atafanikiwa upende husipende.
 
Copy & Paste

]UFAFANUZI MUHIMU KUHUSU USAJILI WA ACCACIA.

Waraka wa BASHIR YAKUB
+255784482959.

Kwa kutumia kigezo cha usajili, Tanzania tunazo aina kuu mbili za kampuni. Kampuni za ndani(Local companies) na kampuni za kigeni ( foreign companies).

Kampuni za ndani ni zile zote zilizoanzishwa hapa nchini na kusajiliwa hapa nchini. Hata kama wanahisa wake wote ni raia wa kigeni kwasababu tu ya kuanzishwa hapa na kusajiliwa hapa zinakuwa ni kampuni za ndani.

Kampuni ya kigeni ni ile iliyoanzishwa na kusajiliwa nje ya Tanzania lakini ikaanzisha ofisi/biashara/tawi hapa Tanzania. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni kifungu cha 433 kinasema hivyo. Kampuni kama imeanzishwa nje hata kama wanahisa wake wote ni Watanzania, hapa kwetu hiyo bado ni kampuni ya kigeni.

Kampuni ya ndani inaposajiliwa hupatiwa cheti cha usajili kiitwacho "Certificate of Incorporation" kwa mujibu wa kifungu cha 15(2) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya ndani inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na inatambulika rasmi kama kampuni ya ndani.

Kampuni ya kigeni inaposajiliwa hapa Tanzania hupatiwa cheti kiitwacho "Certificate of Compliance" kwa mujibu wa kifungu cha 435(1) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya kigeni inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na hutambulika rasmi kama kampuni ya kigeni.

Acacia ni kampuni ya kigeni. Kwa maana kuwa ilianzishwa nje ya Tanzania na kufungua shughuli zake hapa nchini. Kwa hiyo ili ihesabike imesajiliwa Tanzania ilitakiwa kuwa na cheti kiitwacho"Certificate of Compliance". Kutokuwa na cheti hiki maana yake ni kuwa haijasajiliwa Tanzania na haitambuliki.

Nimesikia mjadala BBC SWAHILI leo wanaojadili wakijiuliza inawezekanaje kampuni kubwa kama hii ikafanya biashara bila usajili. Watanzania wengi pia wanajiuliza swali hili.

Jibu lake ni hili. Acacia ni kampuni tanzu(Subsidiary Company) ya Barrick. Kampuni inakuwa tanzu pale ambapo zaidi ya nusu ya hisa zake zinamilikiwa na kampuni nyingine. Ile inayomiliki huitwa "holding company" na inayomilikiwa huitwa "subsidiary company". Kwahiyo Barick ni " holding" wakati Acacia ni "subsidiary".

Barrick inamiliki hisa za Acacia 63.9%. Kwa kusema hivi maana yake Barrick ndiye mwenye Acacia. Hata hivyo kwa mujibu wa sheria hizi zinahesabika kampuni mbili tofauti na kila moja inabeba wajibu na hatia zake yenyewe(its own responsibility& liability).

Basi kumbe kilichotokea ni kuwa Acacia walikuwa wakifanya biashara kwa jina la Acacia lakini wakibebwa na mgongo wa Barrick. Walijificha hapa na wakaweza kuishi bila usajili wa kwao kama wao. Walijibeba kwenye usajili wa Barrick.

Barrick wao wanao usajili na wanayo " Certificate of Compliance" ya kwao ambayo tayari wameitoa hadharani. Kwakuwa haya ni makampuni mawili tofauti kila moja inatakiwa kuwa na cheti chake kwa mujibu wa kifungu cha 487 Sheria ya Makampuni na kutokufanya hivyo ni kosa kabisa. Kwa hiyo hivi ndivyo ilivyowezekana kampuni hii kufanya biashara bila usajili miaka hii yote.

Adhabu ya kosa kama hilo ni kifungo jela. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni iliyofanyiwa Marekebisho mwaka 2002, kifungu cha 472 kinasema hivyo.
 
Copy & Paste

]UFAFANUZI MUHIMU KUHUSU USAJILI WA ACCACIA.

Waraka wa BASHIR YAKUB
+255784482959.

Kwa kutumia kigezo cha usajili, Tanzania tunazo aina kuu mbili za kampuni. Kampuni za ndani(Local companies) na kampuni za kigeni ( foreign companies).

Kampuni za ndani ni zile zote zilizoanzishwa hapa nchini na kusajiliwa hapa nchini. Hata kama wanahisa wake wote ni raia wa kigeni kwasababu tu ya kuanzishwa hapa na kusajiliwa hapa zinakuwa ni kampuni za ndani.

Kampuni ya kigeni ni ile iliyoanzishwa na kusajiliwa nje ya Tanzania lakini ikaanzisha ofisi/biashara/tawi hapa Tanzania. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni kifungu cha 433 kinasema hivyo. Kampuni kama imeanzishwa nje hata kama wanahisa wake wote ni Watanzania, hapa kwetu hiyo bado ni kampuni ya kigeni.

Kampuni ya ndani inaposajiliwa hupatiwa cheti cha usajili kiitwacho "Certificate of Incorporation" kwa mujibu wa kifungu cha 15(2) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya ndani inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na inatambulika rasmi kama kampuni ya ndani.

Kampuni ya kigeni inaposajiliwa hapa Tanzania hupatiwa cheti kiitwacho "Certificate of Compliance" kwa mujibu wa kifungu cha 435(1) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya kigeni inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na hutambulika rasmi kama kampuni ya kigeni.

Acacia ni kampuni ya kigeni. Kwa maana kuwa ilianzishwa nje ya Tanzania na kufungua shughuli zake hapa nchini. Kwa hiyo ili ihesabike imesajiliwa Tanzania ilitakiwa kuwa na cheti kiitwacho"Certificate of Compliance". Kutokuwa na cheti hiki maana yake ni kuwa haijasajiliwa Tanzania na haitambuliki.

Nimesikia mjadala BBC SWAHILI leo wanaojadili wakijiuliza inawezekanaje kampuni kubwa kama hii ikafanya biashara bila usajili. Watanzania wengi pia wanajiuliza swali hili.

Jibu lake ni hili. Acacia ni kampuni tanzu(Subsidiary Company) ya Barrick. Kampuni inakuwa tanzu pale ambapo zaidi ya nusu ya hisa zake zinamilikiwa na kampuni nyingine. Ile inayomiliki huitwa "holding company" na inayomilikiwa huitwa "subsidiary company". Kwahiyo Barick ni " holding" wakati Acacia ni "subsidiary".

Barrick inamiliki hisa za Acacia 63.9%. Kwa kusema hivi maana yake Barrick ndiye mwenye Acacia. Hata hivyo kwa mujibu wa sheria hizi zinahesabika kampuni mbili tofauti na kila moja inabeba wajibu na hatia zake yenyewe(its own responsibility& liability).

Basi kumbe kilichotokea ni kuwa Acacia walikuwa wakifanya biashara kwa jina la Acacia lakini wakibebwa na mgongo wa Barrick. Walijificha hapa na wakaweza kuishi bila usajili wa kwao kama wao. Walijibeba kwenye usajili wa Barrick.

Barrick wao wanao usajili na wanayo " Certificate of Compliance" ya kwao ambayo tayari wameitoa hadharani. Kwakuwa haya ni makampuni mawili tofauti kila moja inatakiwa kuwa na cheti chake kwa mujibu wa kifungu cha 487 Sheria ya Makampuni na kutokufanya hivyo ni kosa kabisa. Kwa hiyo hivi ndivyo ilivyowezekana kampuni hii kufanya biashara bila usajili miaka hii yote.

Adhabu ya kosa kama hilo ni kifungo jela. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni iliyofanyiwa Marekebisho mwaka 2002, kifungu cha 472 kinasema hivyo.

Hehe..Nawaona kweli mkihepa swali very obvious.
 
Hili la madini kwa kweli imebidi nilitazame kwa mbali maana wanazungushana zungushana kwenye mbuyu hadi watu wote wanabaki ovyo. Kwa kweli Watanzania wamekua wakipigwa miaka yote hii, hiyo sio siri, tena kizembe sana. Sote tunajua wana madini mengi, wana raslimali nyingi lakini kwa kuwa wana umaskini mkubwa, hiyo ni ishara tosha wao huibiwa na kwa ushirikiano wa Watanzania wachache.

Nilisoma hiyo ripoti hadi nikabaki kinywa wazi, hayo mabilioni yanasomwa hadi naishia kulewa maana zero zinakua nyingi na inatia hasira hata kwa mimi Mwafrika ambaye sio Mtanzania.

Lakini kama ulivyosema, Magufuli amejitoa ufahamu na kutoa matamko ambayo haonekani kuwa makini. Ni kweli ni rais mzalendo, ni rais mwenye uchungu na nchi yake, hilo halina ubishi, ni rais mwenye kuitakia nchi yake mazuri, lakini aidha hana wanasheria wanaomshauri hatua kwa hatua, au wote wanamwambia vitu anavyovitaka kuviskia ili wamfurahishe, na hili litakua kweli, ukiwaangalia sana sana wafuasi wa CCM hata huku kwenye mitandao hubadilika badilika na kufuata mkumbo, kwamba rais akiibuka na hili leo wote wanalitetea, akiliponda kesho, wote vivyo hivyo wanaliponda hiyo kesho. Sasa kwa kauli hiyo, anakosa washauri wa kweli na wanaompa taarifa kama jinsi zilivyo.

Kwa Tanzania ambapo rais ana nguvu kupitiliza kwamba hawezi kuhojiwa wala kuzuiwa na taasisi yoyote tofauti na ilivyo Kenya, inakua hatari sana. Leo hii Watanzania wanalipia umeme hewa ambapo waliingia kwenye mikataba kiholela hadi ikawatokea puani. Sasa usipokua makini kwenye haya maamuzi, utajikuta unalipia mpaka basi maana humo kuna makubaliano hata ya kimataifa. Yaani nawaza hivi marais waliostaafu wanahisi vipi wakiona hizi show zote maana kama kweli, itakua haya mambo yote yalikua yanatendeka ndani ya uongozi wao.

Hebu itazame hii hotuba ya Tundu Lissu
 
Hiyo video ya mbunge unamjua vizuri huyo mbunge? Ni mfuasi wa Edward Lowassa, kwa hakika 2020 abadili chama maana hatapata nafasi tena ndani ya CCM.

Kuhusu bandarini, kilichofanya mizigo ipungue sio Magufuli. Ni sheria ya kuweka VAT kwenye transit goods Julai 1, 2015 chini ya Jakaya Kikwete na wizi uliopitiliza. Sasa hivi mizigo imeongezeka na inazidi kuongezeka.

Kuhusu Acacia kusajiliwa ama kutokusajiliwa, kwa hakika watu waliopewa kazi ya uchunguzi wanajua mambo kuliko wewe. Wewe hujui hata sheria moja ya Tanzania madai yako hayana nguvu hata kidogo.

Madai yako ya kukurupuka hayana msingi maana hujui ngazi za maamuzi Tanzania.
Majibu yako yanatosha
 
Hili la madini kwa kweli imebidi nilitazame kwa mbali maana wanazungushana zungushana kwenye mbuyu hadi watu wote wanabaki ovyo. Kwa kweli Watanzania wamekua wakipigwa miaka yote hii, hiyo sio siri, tena kizembe sana. Sote tunajua wana madini mengi, wana raslimali nyingi lakini kwa kuwa wana umaskini mkubwa, hiyo ni ishara tosha wao huibiwa na kwa ushirikiano wa Watanzania wachache.

Nilisoma hiyo ripoti hadi nikabaki kinywa wazi, hayo mabilioni yanasomwa hadi naishia kulewa maana zero zinakua nyingi na inatia hasira hata kwa mimi Mwafrika ambaye sio Mtanzania.

Lakini kama ulivyosema, Magufuli amejitoa ufahamu na kutoa matamko ambayo haonekani kuwa makini. Ni kweli ni rais mzalendo, ni rais mwenye uchungu na nchi yake, hilo halina ubishi, ni rais mwenye kuitakia nchi yake mazuri, lakini aidha hana wanasheria wanaomshauri hatua kwa hatua, au wote wanamwambia vitu anavyovitaka kuviskia ili wamfurahishe, na hili litakua kweli, ukiwaangalia sana sana wafuasi wa CCM hata huku kwenye mitandao hubadilika badilika na kufuata mkumbo, kwamba rais akiibuka na hili leo wote wanalitetea, akiliponda kesho, wote vivyo hivyo wanaliponda hiyo kesho. Sasa kwa kauli hiyo, anakosa washauri wa kweli na wanaompa taarifa kama jinsi zilivyo.

Kwa Tanzania ambapo rais ana nguvu kupitiliza kwamba hawezi kuhojiwa wala kuzuiwa na taasisi yoyote tofauti na ilivyo Kenya, inakua hatari sana. Leo hii Watanzania wanalipia umeme hewa ambapo waliingia kwenye mikataba kiholela hadi ikawatokea puani. Sasa usipokua makini kwenye haya maamuzi, utajikuta unalipia mpaka basi maana humo kuna makubaliano hata ya kimataifa. Yaani nawaza hivi marais waliostaafu wanahisi vipi wakiona hizi show zote maana kama kweli, itakua haya mambo yote yalikua yanatendeka ndani ya uongozi wao.

Hebu itazame hii hotuba ya Tundu Lissu

Kuweka Video ya huyo Tundulissu umevuruga kila kitu
Huyo ni Mchumia Tumbo
 
Kuweka Video ya huyo Tundulissu umevuruga kila kitu
Huyo ni Mchumia Tumbo
Hiy0 miaka yote alipukuwa akiiponda CCM kuhusu rasilimali za taifa wakati Sisiemu walikuwa wakila maisha with a big spoon, bado alikua Mchumia Tumbo?
 
Wewe MwendaOmo peleka utaahira wako kabla ya hiyo kampuni kuitwa Acacia ilikuwa Africa Barrick Gold na kabla ya hapo iliitwa Barrick Gold sasa uwezekano upo majina hayo ya kabla kuwa yalijasajiliwa na hilo la Acacia halipo BRELA. Kwa hiyo kodi ilikusanywa kwa majina ya zamani. Kaa mbali na hii issue kama Mkenya huna upeo wa kujua kinachoendelea!
 
Wakenya elite wanaaza kuogopa wakiona jinsi Tanzania tunafanya reform, wanajuwa kuna siku wananchi wa kawaida watakuja kudai mali yao.



Mbona unachukua wazo la mtu mmoja kama la watu wote?? Umeona hapa watu wakisema ama ni mtu anasema?
SMH http://
9e443740-9ffd-0132-44ed-0ebc4eccb42f.gif
?
 
Kuweka Video ya huyo Tundulissu umevuruga kila kitu
Huyo ni Mchumia Tumbo
Mrahaba 4%?

Kama kina magufuli hawakuzitia zingine tumboni ni nini kiliwapumbaza????

Magufuli alichumia tumboni!!!
UNABISHA?
 
Back
Top Bottom