Magufuli siyo shujaa wa Afrika, Kikwete ni shujaa wa Afrika

Labda kisukuma yule mutu hakujua kiswahili kwa kwel
Kwa hiyo hujaona MAGUFULI alipowasuruhisha Odinga na Uhuru?

Hujaona Magufuli alipopeleka majeshi Sudani na Kongo?


ANYAWAYS.

1. MAGUFULI aliwafundisha mataifa ya Africa kujitegemea. Kufanya kazi bila kulamba miguu ya wazungu. Hapa JK hawezi.

2. Mafuguli kasambaza Kiswahili. Sasa kinafundishwa mataifa mengi ikiwemo. Ghana, SA, Botswana, Ethiopia n.k.

3. Kkaifanya Afreica ijifunze kutoka kwake katika kuwekeza kwenye miundo mbinu mikubwa na ya kimkakati.


Bado una swali?
 
Ndo ushangae kwa namna gani alifanya Kiswahili kianze kufundishwa na kutumika kwenye mikutano ya AU.
kweli kabisa yaani wasukusu kiswahili chao utacheka mpaka ukae chini halafu yale majamaa hayonagi aibu!! Ni full confidence!!!

Likikosea linaendelea tu.km jiwe alivokuwa vilevile!!

Mtu hujui unachotaka watu wajue sasa huyo si mjinga???
Mtu anae kubali ujinga anaitwaje??.....
 
kweli kabisa yaani wasukusu kiswahili chao utacheka mpaka ukae chini halafu yale majamaa hayonagi aibu!! Ni full confidence!!!

Likikosea linaendelea tu.km jiwe alivokuwa vilevile!!

Mtu hujui unachotaka watu wajue sasa huyo si mjinga???
Mtu anae kubali ujinga anaitwaje??.....
Hapa sio kundi sogozi. Chukua maarifa sepa.
 
Nikichogundua kwenye msiba wa Magufuli ni kwamba maadui wa JPM hadi leo hawaamini mtu waliemchukia anaweza kuombolezwa na kuliliwa na watu wengi kiasi kile ndani na nje ya nchi hususa ni Afrika.

Waafrika wengi walipenda staili yake ya uongozi ya kukemea mambo ya ovyo hadharani bila kumuonea mtu aibu. Alikuwa ni mtu mwenye maamuzi na alichukia watu wazembe, Wala rushwa, mafisadi na wahujumu uchumi. Ilifikia hatua hadi Wakenya wanaomba wamuazime Magufuli kwa mwezi mmoja tu ili apambane na ufisadi.

Jina la Magufuli haliwezi kuisha midomoni mwa watu ukizingatia alama alizoacha kwa mengi aliyofanya kwa miaka mitano pekee achilia kazi ya ujenzi wa miundo mbinu aliyofanya kwa miaka 20 akiwa waziri wa ujenzi.
1. Kwa upande wa Africa, Magufuli hakufanya chochote! Kikwete kafanya madogo, hayawezi kutosha kuitwa shujaa.

2. Kwa Tanzania, Magufuli ni Maarufu sana kwa mema na mabaya.

2.1 Ukweli ni kwamba Magufuli alifanya mengi mazuri makubwa kwa Tanzania (ni mengi yanajulikana sina haja kuyataja).

2.2 Lakini, kiutu, Magu alifanya mambo mengi ya laana na kuumiza watu. Mambo hayo yanafuta mema mengi aliyofanya (sala nyingi za majonzi huenda ndo sababu ya kifo cha Magu). Watanzania wengi (a.k.a wanyonge) wanamshabikia sana Magu lakini hawachambui kwa undani:-

a) Tumbua tumbua ya Magu ukichunguza kwa undani utakuta imejaa double standards na uonevu mkubwa. Kuna watu walitumbuliwa kwa makosa madogo ya kuonywa, wengine kwa makosa ya kudhaniwa, wengine kwa kudhaniwa ni network ya fulani, etc, lakini wako wengi waliteuliwa na kulindwa kwenye nafasi zao hata kama mienendo yao ilikuwa wazi kuwa ni ya kifisadi na dhuluma na uenevu kwa watu. Kubomoa makazi ya watu bila fidia, kufukuza watu wenye vyeti vyenye kasoro, akimwacha Bashite, n.k.

b) Kuna kundi dogo lilipiga sana ufisadi kipindi cha Magu. Magufuli alikuwa muongo sana, aliaminisha watu kuwa anapambana na ufisadi (huku akikumbatia genge la mafisadi wachache aliokuwa anakula nao).

c) Magufuli alikuwa muongo sana, alijua kucheza na akili za wanyonye (wasiojua kuchambua akawaaminisha kila kitu). Unakuta kuna watu wanajua kabisa ukweli wa jambo, lakini utashangaa Magufuli anasimama hadharani au wakati mwingine dhabahuni Kanisani kabisa anasema uwongo, kuna wakati alikuwa anamkufuru sana Mungu. Mfano, Magu anajua kabisa Serikali inafanya direct borrowing kutoka kwenye mabenki ya kibiashara ya kutoka nje kugharamia miradi mikubwa ambayo, mwisho wa siku tutalipa tu kwa kodi zetu kwa vizazi vijavyo, lakini anadanganya eti ni makusanyo ya ndani ya TRA. TRA kwa mwezi inakusanya fedha zinazoweza kulipia public wage bill, public debt service na OC- tena OC ya kiwango cha mil. 2 kwa ofisi ya DC kwa mfano.

d) Magu alianzisha miradi na mikataba mikubwa bila kuwepo kwenye bajeti, na bila idhini ya Bunge, na hakukuwa na uwazi wowote katika mikataba. Alijua atakufa na kutuachia mzigo wa madeni. Mfano, aliaminisha Taifa mradi wa Bagamoyo ni wa kifisadi wakati issue ni masharti ya financing ambayo ukiona hayafai unaacha, unatafuta financing nyingine, lakini yeye aliaminisha Taifa mradi haufai. Masharti aliyozungumzia yalibaki tu kwenye speech yake, hayakuwekwa wazi mfano Bungeni, kwa hiyo hatuwezi kujua ukweli, kisa kujustify miradi ya Chato ambayo siyo strategic.

e) Magu alifunga midomo watu wote, aliua utafiti, vyuo vikuu vilizibwa midomo hakuna ushauri wa kitaalamu, na alitoa wataalamu wazuri wa kufundisha vyuo vikuu akawapeleka Serikali na kuanza kuwatukana!

f) Magu alifanya siasa za chuki na uonevu wa wazi na kuligawa Taifa kwa misingi ya vyama, dini na ukanda (badala ya mbinu zingine nzuri za kupambana na upinzani- zipo mbinu nyingi za kistaarabu), halafu anasimama kanisani eti tusibaguane kwa vyama wala dini, dahhh- alijitoa ufahamu sana.
g) Magu aliondoa uwazi (transparency) katika utawala wake, alichukua mrengo wa udikteta (RCs, DCs na Watendaji wengine walijiewekea walinzi na ulinzi bila kustahili), kuzuia bunge live, vyombo vya habari vilipiga tu pambio za kuisifu Serikali, magazeti yalibakia na habari za michezo ndo angalau ununue usome. Kwa ujumla, mrengo wa udikteta, kutokuwepo kwa uwazi na uanzishwaji wa miradi mikubwa bila mpango mara nyingi ni dalili kubwa za Serikali inayokula rushwa na kuitafuna nchi na kundi dogo.

Mpaka leo, kuna watu hawajajua kuwa Magu alikuwa na magumashi mengi! R.I.P, wenye akili hasa viongozi wajifunze kuishi vizuri na watu, watende haki, utawala wako hautadumu milele, Tanzania itadumu. Ukiamua kunyoosha nchi, nyoosha kwa uwazi na bila double standards, hata ukifa uheshimiwe na wote, siyo usifiwe na baadhi na ulaaniwe na baadhi.
 
Kikwete pia si shujaa wa Africa kwa lipi hasa? Shujaa wa Africa ni Baba wa Taifa pekee yake.

Kama alivyoainisha BAK, shujaa wa Afrika ni Baba wa Taifa peke yake kwani alikuwa na vision ya wapi bara letu linatakiwa liende! Kikwete alikuwa na vision gani? Kikwete alikuwa anaongozwa na ideology ipi? Huyu ni mtawala aliyependa starehe na ndio maana alikuwa anaabudu fedha zaidi kuliko utu!!! Enzi ya utawala wake nchi iliibiwa sana maliasili zake kwa yeye kushirikiana na mafisadi wa nje na ndani ya Nchi. Tanzania Ndio Ikawa kinara wa biashara ya madara ya kulevya na marafiki zake ndio wakisimamia biashsra hiyo. Kiongozi kama huyo hawezi kuwa shujaa wa Africa.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Watu mtaumia sana kumaliza Mambo ya Magufuli ila amini nawaambia ameacha legacy pia hajafa yupo mioyoni mwa watu muda utaongea katika hili
Ni kweli yule Pimbi ameacha Legacy ya Akina Sabaya na Makonda na ndio maana tunawashughulikia na Mungu akaona yeye apelekwe moja kwa moja kuzimu kwa kuwa uovu wake hauvumiliki machoni kwa Mungu
 
Mbona marehemu anawahangaisha sana? Mbona mnahangaika kuua legacy ya magufuli? , mtu ameshafariki bado roho zinawauma au mlitakaje sasa? Si alikua dictator? C ameshakufa? Ni nini kinawawasha kila siku kumtaja?
 
Mbona marehemu anawahangaisha sana? Mbona mnahangaika kuua legacy ya magufuli? , mtu ameshafariki bado roho zinawauma au mlitakaje sasa? Si alikua dictator? C ameshakufa? Ni nini kinawawasha kila siku kumtaja?
Tena huwa wanasema sasa hivi analiwa na funza!

Mara sijui ‘dead and buried’.

Lakini bado tu wanamuwaza. Amewakaa akilini na hawawezi kujizuia kumuwaza na kumtaja taja!

SMH
 
Nilipokuwa nafuatilia msiba wa Magufuli, kwenye Television ya Taifa TBC, walikuwa wameweka maneno kumhusu Magufuli kuwa ni Shujaa wa Afrika lakini nikawa navuta fikra. Je, ushujaa wa Magufuli kwa Afrika ni upi?, Nikasema pengine ni kwa "Rhetoric" zake za kutukana Wazungu na kuwaita Mabeberu, lakini Mabeberu hao walipokuwa wakikohoa tu, mzee mzima anagwaya na anatii.

Kiufupi Magufuli alikuwa akiogopa sana Kibinyo cha Wazungu kuliko kelele za raia wake wenyewe. Tuliona kwa mfano “Mabeberu" wakimwambia abadilishe sheria za takwimu na akatii, Walimwambia aruhusu watoto wajawazito waendelee na masomo akabadili mwelekeo. "Mabeberu" ndiyo walioingilia kati Lissu apewe safe passage kurudi Ulaya na serikali ya Magufuli ikampa na passport kabisa, la sivyo habari leo hii ingeukwa nyingine!.

Mfano mwingine ni kwenye Makubaliano na Barick kuhusu mustakbali wa kampuni hiyo juu ya uchimbaji madini nchini, Kabla ya makubaliano hayo Serikali ya Magufuli ilipeleka muswada chapuchapu bungeni juu ya rasilamli zetu, na mle ndani sheria iliyotengenezwa ikasema Makinikia yatakuwa yanachenjuliwa hapahapa Tanzania, Lakini cha ajabu kwenye makubaliano na Barick mwaka mmoja au miwili baadae akavunja sheria yake mwenyewe, kwa kuruhusu makinikia yawe yanasafirishwa nje!. Sasa hiyo hype ya kuwa alipambana na Mabeberu inatoka wapi?

Najiuliza ushujaa wa Magufuli kwa Afrika ni upi wakati dalili zote za aina ya uongozi wake ilikuwa ni kutaka kuturudisha kwenye Afrika ya kale ambapo mtawala akiongea hakuna wa kuquestion la sivyo utakiona cha mtema kuni. Kiufupi Magufuli aliparalyse mifumo ambayo ingeijenga nchi kusimama kitaasisi na badala yake akaanza kutunga sheria na kufanya matendo ambayo yanazidi kumlibikizia yeye madaraka, chukulia mfano sheria ya rasilimali za Taifa, Hiyo sheria ilienda kuweka madini yote chini ya ofisi ya rais

Kwa kweli nikiangalia kitu chochote exclusive ambacho Magufuli amefanya kwa ajili ya Afrika nzima ni kama hakuna!

Lakini hii ni tofauti na Mstaafu Kikwete, Kikwete kuna mambo aliyafanya naweza kusema bila wasiwasi na kwa rekodi kuwa huyu mwana wa Afrika anastahili kupewa heshima yake na Afrika nzima

1. Kikwete alishiriki katika Usuluhishi wa Kenya
Baada ya uchaguzi mkuu wa Kenya mwaka 2007,wakati Wakenya wakichinjana na kuhasimiana kitu kilichohatarisha kuzuka kwa vita ya wenyewe kwa Wenyewe, Rais Kikwete aliingilia kati kusuluhisha kambi hasimu za Raila Odinga na Mwai Kibaki, Pamoja na Juhudi za Kikwete pia walikuwepo marais wastaafu wa Afrika akiwemo hayati Mkapa. Ni kutokana na kazi hii Nchi ya Kenya ilimpa heshima ndugu Kikwete kuhutubia mabunge mawili ya Kenya, heshima ambayo ilikuwa hajawahi kupewa rais yeyote wa Tanzania kabla yake. Pia kwa kutambua kazi ya kikwete kwenye kuleta amani Kenya, barabara moja nchini Kenya , jijini nairobi ilibadilishwa na kupewa jina lake

2. Kikwete ainusuru Comoro dhidi ya kikosi cha Wahuni cha kanali Bacar
Wakati Comoro ikiwa inaelekea katika mtanzuko wa machafuko baada ya kikosi cha Muasi Kanali Bacar kuasi, Ni dhahiri visiwa hivi vya Comoro vingekuwa katika machafuko makubwa ikiwemo umwagaji damu, Ilikuwa ni Intervention ya Rais Kikwete kupeleka jeshi letu la JWTZ kwenda kuweka mambo sawa. JWTZ walipiga kazi nzuri na ndani ya wiki moja nchi ile ikawa imeshakuwa stabilized. Je ni watu wangap wangeuawa kama si kwa intervention ya Tanznaia, Ni wanawake wangapi wangebakwa?.Ikumbukwe siyo JK wa kwanza kuisapoti Comoro kijeshi, Hata mwalimu Nyerere amewahi kuisaidia Comoro ili kupambana na wakoloni wa ufaransa.

3. Kikwete ainusuru Congo dhidi ya Wahuni wa M23
Hawa wanayarwanda walikuwa wakiiba mali, kuua watu congo, Ni mpaka Viongozi wenye maono kama Kikwete waliojitolea kuendesha mission ya UN ya kuwadhibiti hao waasi. JWTZ kwa kushirikiana na majeshi ya Afrika ya kusini na Malawi walifanya kazi nzuri sana ya kuwadhibiti hao akina Jenerali Nkunda. Bila shaka ukiwauliza watu wa mashariki ya Congo kuhusu Intervention hiyo ya Kikwete, watakwambia huyu mtu ni shujaa wao

4. Usuluhishi wa Mgogoro Madagascar
Hali ya Madagascar ilikuwa imeshakuwa tete, magonvi na kupinduana kukiwa kumeiweka ile nchi katika hali ya sintofahamu, hali ya hofu mitaani. Ilikuwa ni kazi nzuri ya Kikwete kutafuta usuluhishi wa kisiasa huko

Maandiko yanasema heri wapatanishi!

Nikimpima Kikwete na Magufuli katika kutafuta ustawi wa bara la afrika, ikiwemo usuluhishi na upatanaishi, kutafuta amani ya watu wake, Kwa kweli Kikwete aliifanyia makubwa Afrika. Huyu anafaa kuitwa shujaa wa Afrika katika viongozi wa rika la hivi karibuni.

Magufuli yeye ni shujaa wa Afrika katika lipi?
Nishauliza hilo swal kwa wazee wa legacy kila mmoja anaingia mitini 🤣🤣🤣🤣
 
Ni kweli yule Pimbi ameacha Legacy ya Akina Sabaya na Makonda na ndio maana tunawashughulikia na Mungu akaona yeye apelekwe moja kwa moja kuzimu kwa kuwa uovu wake hauvumiliki machoni kwa Mungu
Mungu kamwaachia Shetani hadi leo na anamvumilia ndio ashindwe kumvumilia huyo Jiwe?
 
Back
Top Bottom