Magufuli Na Kambi Mbili: CCM Maslahi na CCM Mabadiliko

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
DSC_0660.jpg
Kwa muda mrefu niliamini kuwa CCM ilivyo sasa siyo tu haiwezi kuongoza mabadiliko lakini pia haipaswi kuongoza mabadiliko hayo. Sababu kubwa ni kuwa CCM ilikuwa ni moja; ilikuwa ni chama chenye mwelekeo mmoja na maslahi ya aina moja. Na ndio maana hata watu walipoimba "CCM ni ile ile" kwa kiasi kikubwa walikuwa wanaakisi ukweli huo.

Niliamini pia kuwa CCM inapaswa kuvunjika ili Taifa lipone. Sikuona ni jinsi gani CCM inaweza kuokoleka; na hili sina shaka nilikuwa sahihi. Kitu ambacho labda sijawahi kukidhania kwa kina ni jinsi gani CCM inapenda kujifunga yenyewe kamba shingoni na kujitundika; wapinzani huwa hawana kazi zaidi ya kushabikia na kuchekelea.

Ujio wa Magufuli na ajenda ya mabadiliko umetufundisha jambo moja kubwa - CCM inaelekea kuvunjika kutokea ndani. Mjadala wa masuala ya posho kwa namna fulani na kauli za baadhi ya wana CCM kuonekana kutokuwa katika mstari wa kutaka mabadiliko unanifanya niamini kabisa kuwa CCM inaenda kuvunjika kutoka ndani kuelekea kambi mbili; kambi hizi mbili si mpya kwa wengi wetu kwani zilishakuwepo. Zilikuwepo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 na inaonekana pamoja na kuwa wote wanaonekana kuvaa kijani na njano, lakini ndani yao wako kama nyeusi na nyeupe!

Kuna kambi ya maslahi - hii ni kambi ya wale ambao uwepo wa CCM madarakani ni mafanikio kwao, watoto wao na jamaa zao. NI kambi ambayo imetusumbua sana kama taifa kwa miaka hii hasa ishirini; ni kambi ambayo haijali sana siasa, haijali sana utawala, haijali sana serikali inafanya nini; kambi hii inajali zaidi inapata nini. NI kambi ya kimahesabu sana; ilipoona kuwa Magufuli na Watanzania wanaelekea kumkubali Magufuli kuliko yule mtu wao; watu hawa hawa ambao waliapa "aliko tuko" wakajikuta wameamua kujibanza humo humo CCM ili wajue watapata nini.

Tatizo ni kuwa hadi hivi sasa hawajui kama wanapata; na dalili zinaoonesha kuwa wasipoangalia wanaenda kukosa zaidi! Na hili la kukosa wakati wao ni watawala linawasumbua na hivyo wanaanza kujikuta wanasumbua. Hawa ni unprincipled.

Kambi hii ya pili ya CCM mabadiliko inawezekana ni kambi inayoundwa na watu ambao walikataa kabisa kupiga magoti mbele ya mafisadi na inawezekana na wao walikuwa wanajua kuwa ile kambi nyingine ingepata basi wao pia wasingepata. Hata hivyo, kambi hii inaamini kuwa Tanzania inahitaji mabadiliko ya kweli na kuwa nafasi ya kuwa kiongozi au mtawala ni nafasi ya kuwaongoza watu kupitia utawala kufikia mafanikio. Kambi hii naweza kusema ni principled.

Hawa wako tayari kusimama na Magufuli hata kama wanajua kuwa na wenyewe wanaisoma namba; lakini wanasema na "tunaisoma namba pamoja na Watanzania wenzetu". Kambi hii sidhani kama ni kubwa sana kulinganisha na ile nyingine; ni kambi ambayo watetezi wake hawajajipambanua sana kama wa ile kambi nyingine.

Kuelekea Uenyekiti wa Magufuli CCM nina uhakika wa asilimia 100 wale wa kambi ile nyingine - wale wanaotaka kupata - sitoshangaa watajikuta wanaanza kurudi na kuanza kuimba sifa za Magufuli na kuanza kujibanza kwenye jukwaa la 'mabadiliko' ili na wao wawemo. Tatizo ni kuwa wanajua kwa uhakika mkubwa kuwa hilo peke yake siyo hakikisho la wao kuja kupata. Wengi wa hawa - nikiruhusiwa kutabiri - wataanguka sana kwenye chaguzi zijazo kwani walikuwa wanasimama miguu yote upande ule kaini vichwa tu viko upande wa CCM.

Uenyekiti wa Magufuli ni tishio; ni tishio kwa sababu nguvu ya Mwenyekiti wa Chama ni kubwa mno na hili linawatatiza watu kwa sababu 'ukichaa' wa Magufuli ambao ameuonesha hadi hivi sasa wa kugusa visivyoguswa, kusema visivyosemwa na kutenda visivyowahi kufikiriwa vinaweza kutendwa vinawasumbua. Itakuwaje akishika chama; hivi Sekretariati yake itakuwa na watu gani? Je, wataweka maslahi ya CCM mbele kama Katiba ya CCM inavyotaka au yale ya Taifa kwanza?

Binafsi nafurahia mgongano huu na mpasuko huu; kwani ni mpasuko wa kifikra kwanza. Ni mpasuko na mgongano kama uliowahi kutokea ndani ya ANC; ni mgongano ambao unaweza kuwa umewahi kutokea kwenye vyama vingine vikongwe. Mpasuko wa CCM ambao wengine tulikuwa tunausubiria kwa muda mrefu na kuuombea inawezekana unaelekea kutokea ndani ya miezi hii michache.

Kumchelewesha Magufuli kuwa Mwenyekiti na kumchelewesha kuongoza Chama ni aina fulani ya hujuma - sijali sababu zinazotolewa. Ni hujuma kwa sababu kwenye nchi kama ya kwetu yenye masalia ya mfumo ule wa kisoshalisti (ni kweli mfumo wetu wa kisiasa una masalia hayo) Chama tawala ndicho kina nguvu sana ya kusimamia nchi; Rais asipokuwa kiongozi wa chama vile vile ni sawasawa na Rais wa China kutokuwa kiongozi mkuu wa chama cha Kikomunisti; au yule wa Korea ya Kaskazini kutokuwa kiongozi mkuu au Cuba, au Viet Nam.

Mpaka pale mfumo wetu utakapoweza kujengwa na kutenganisha uongozi wa kisiasa na uongozi wa kiserikaake ili, Rais wa nchi ili afanikiwe ajenda zake ni lazima awe kiongozi wa chama chake cha siasa vile vile. HIli ni kweli si kwa CCM tu bali hata kwa chama kingine kikija kushika.

NI wito wangu, uamuzi wa kumkabidhi Magufuli Uenyekiti uharakishwe; kwani nje ya hapo ni kutengeneza nguvu mbili zenye kushindana kuongoza taifa. Kuna mmoja tu aliyepigiwa kura na taifa zima kuliongoza kwa miaka mitano (siyo baadhi ya miezi ya miaka hiyo mitano). CCM na uongozi wake waamue hata kuuza majengo yao yote ili wakamilishe makabidhiano hayo na nchi iwe katika utaratibu wake uliozoeleka. Hata kama hawapendi au wanaona labda wacheleweshe kidogo.

Kumkabidhi Rais Magufuli Uenyekiti wa CCM mapema ndio njia pekee ya kutenganisha kambi hizi mbili za CCM Maslahi na CCM Mabadiliko. Hakuna njia nyingine, kwa sasa.

MMM
 
Bei ya sukari ipo juu kila kitu kinaenda mrama tumechoka hizi ngonjera za kumpamba Magufuli tunataka mabadiliko yanayoleta unafuu wa maisha sio ugumu wa maisha
 
Bei ya sukari ipo juu kila kitu kinaenda mrama tumechoka hizi ngonjera za kumpamba Magufuli tunataka mabadiliko yanayoleta unafuu wa maisha sio ugumu wa maisha

Mtu anaenda kulima unataka asitoke jasho; ni kudeka gani huku? Mbona wenzenu hapa (US nazungumzia) bei ya mafuta tu ya gari inaweza kupanda na kupanda na watu wananung'unika lakini ndio maisha yalivyo. Sukari tu watu wameanza kulia; hivi mlikuwa mnataka mabadiliko kweli au kuendelea kudeka? WEngine wanalalamika ati hawawezi kupata nyama choma tena!
 
Ccm mnahangaika nyie wenyewe huwa mnasema sasa hv kufanya vitu kwa mazoea iwe basi-sasa kama rais anakabidhiwa uenyekiti baada ya miez 6 sio lazima iwe hvyo tumuache kikwete mda wake uishe hiyo 2017 ndipo amkabidhi.

Hata hivyo jinsi JPM anavyoonesha akipata full authority na power kwenye chama na serikalini ataleta shida so wanaona ni bora aendelee kuwa chini ya mtu kwanza.
Na ninaamini ndio sababu kubwa ya kusita kufanya hvyo-kikwete endelee
 
Mzee kwa mbali umeanza kulainika...CCM NI ILE ILE MZEE! Mtarudi tu kwenye mstari,mnaye muamini aba dhamira nzuri,lakini tatizo ni namna ya kutekeleza dhamira hiyo! CCM Maslahi watamshinda kirahisi sana, angalia kila akipew a I hutubia anatoa kioja! Hili ni tatizo ,achilia mbali out shaurika ! Tulipoamua kuchagua jiwe ili CCM ife hatukuwa tumelala ,tulijua CCM NI ILEILE,BAHATI NZURI MZEE AMESEMA HATAFUKUA MAKABURI...,ILA KAMA UNAVYOTABIRI ,MAKABURI YATAJIFUKUA TTU,
Wamemtegea mengi,sukari j mfano, anatutesa na sukar kg 5000 bila sababu!
 
"Chama tawala kimekuwa kikijishughulisha sana na kuziba kila mwanya uliojitokeza kuleta mabadiliko ya kweli ya kuisukuma nchi hii mbele, kikiwa zaidi kina shauku ya kulinda maslahi binafsi ya wakuu hao na washirika wao. Hii haina maana kwamba kila mtu ndani ya chama hicho ni muovu, la hasha. Hili ni suala la kimfumo, na mfumo ndio unaotawala na kuwalazimisha hata watu wema kupoteza uwezo na/au utashi wa kukemea uovu, uzembe na ufisadi.

Ndiyo maana suala kuu tunalohitaji kulishughulikia ili tupate maendeleo ya kweli, maendeleo ambayo angalau wajukuu wetu wataweza kunufaika nayo, ni kubadilisha mifumo, miundo na mikondo ya utawala wetu katika mabadiliko yatakayoondosha kabisa uchafu uliojaa katika jinsi tunavyojitawala. Hili haliwezi kufanywa chini ya chama-tawala tulicho nacho hivi sasa kwa sababu CCM imekwisha kudhihirisha kwamba haitaki kuandika Katiba mpya inayotokana na maoni ya wananchi.

Katiba inayotakiwa na CCM ni ile iliyoandikwa na Samuel Sitta na Andrew Chenge na washirika wao, ambao wanajulikana hawawezi kuitaka Katiba itakayowabana katika yale wanayotaka kuyafanya, ambayo ni muendelezo wa ufisadi" - Jenerali Ulimwengu

"Katika kuidurusu historia, sijawahi kuona mtu mmoja, na awe hodari kiasi gani, aliyeweza kubadilisha hali za wananchi wake kwa uwezo wake peke yake. Kila mara maendeleo na mabadiliko ya kweli yameletwa na jamii iliyopevuka, na iliyopiga hatua katika nyanja kuu fulani, na maendeleo na mabadiliko hayo huja hatua baada ya hatua, hatua ya awali ikiwa ni msingi wa kuipokea hatua inayofuata.

Kutaraji kwamba tunaweza kupata mabadiliko ya haraka kutokana na mtu mmoja ni aina fulani ya ushirikina ambayo inanitisha kwa sababu nilikwisha kuibaini ingawa nadhani kwamba watu wetu walio wengi, na jamii yetu kwa ujumla, hatuitambui. Wale tulio na umri fulani tulikwisha kushuhudia wale wanasiasa wa miaka ya 1990, Mrema na Mtikila. Baadhi yetu tuliowashabikia leo tumebaki tukiona haya tukikumbushwa juu ya ushabiki huo.

Hatutaki kukumbushwa kwa sababu leo tunawaona kama walikuwa hawana lolote la maana la kutufanya tuwashabikie kwa kiwango hicho. Lakini tukumbuke vile vile kwamba ushabiki huu hauna tofauti kubwa na ule tulioushuhudia miaka 10 iliyopita wakati mgombea wa CCM ni Jakaya Kikwete, na kaulimbinu ikiwa “Ari Mpya, Nguvu Mpya, Kasi Mpya!”" - Jenerali Ulimwengu
 
Mtu anaenda kulima unataka asitoke jasho; ni kudeka gani huku? Mbona wenzenu hapa (US nazungumzia) bei ya mafuta tu ya gari inaweza kupanda na kupanda na watu wananung'unika lakini ndio maisha yalivyo. Sukari tu watu wameanza kulia; hivi mlikuwa mnataka mabadiliko kweli au kuendelea kudeka? WEngine wanalalamika ati hawawezi kupata nyama choma tena!
Huko Muleba afya za wazee zimeanza kuathirika kwa kukosa kunywa chai kwa miezi miwili sasa. Wanasema hawashibi. Mkuu wa wilaya alipoulizwa kuhusu hali hiyo akasema wazee siyo muhimu sana. Alimkemea mwandishi wa radio Karagwe kwa kumuuliza mswali ya kuudhi. Habari ndo hiyo
 
Mtu anaenda kulima unataka asitoke jasho; ni kudeka gani huku? Mbona wenzenu hapa (US nazungumzia) bei ya mafuta tu ya gari inaweza kupanda na kupanda na watu wananung'unika lakini ndio maisha yalivyo. Sukari tu watu wameanza kulia; hivi mlikuwa mnataka mabadiliko kweli au kuendelea kudeka? WEngine wanalalamika ati hawawezi kupata nyama choma tena!
Kwa taarifa yako mtu wa kwanza kulalamikia bei ya sukari ni Magufuli huyo huyo!
 
yani stori za ccm bila kumtaja Lowasa awaridhiki kabisa.Na ccm ikisambaratika utasikia ilikua ni nguvu za Lowasa.Jaribuni kusimama kivyenu bila ya kutafuta sababu ya kusimamia.
 
Analysis maridhawa ila kwa upande wangu kama tunataka mabadiliko ya kweli Dr Magufuli asiwe Mwenyekiti wa Chama ila katiba iwekewe viraka ili kuondoa kipengele kinachomfanya awajibike zaidi katika chama chake baadala ya kuwajibika kwa wananchi anaowaongoza ambao kwao ni wanachama wenzake na wengine ambao ni vyama vingine au hawana chama. Rejea:::: Njia rahisi ya kuondokana na yanayojiri katika Bunge letu tukufu
 
Mtu anaenda kulima unataka asitoke jasho; ni kudeka gani huku? Mbona wenzenu hapa (US nazungumzia) bei ya mafuta tu ya gari inaweza kupanda na kupanda na watu wananung'unika lakini ndio maisha yalivyo. Sukari tu watu wameanza kulia; hivi mlikuwa mnataka mabadiliko kweli au kuendelea kudeka? WEngine wanalalamika ati hawawezi kupata nyama choma tena!
Je ni halali sukari kupanda bei? Hapa ni Tanzania na huko ni USA.Kwa sababu US vitu vinapanda bei basi na TZ vipande bei? Bei elekezi tumeambiwa mara 1800,2200,2500 then unasema tusilalamike,tunataka wasimamie yale waliyopanga kuyasimamia.Tunataka matokeo yanayoonekana sio maneno mengi
 
Mtu anaenda kulima unataka asitoke jasho; ni kudeka gani huku? Mbona wenzenu hapa (US nazungumzia) bei ya mafuta tu ya gari inaweza kupanda na kupanda na watu wananung'unika lakini ndio maisha yalivyo. Sukari tu watu wameanza kulia; hivi mlikuwa mnataka mabadiliko kweli au kuendelea kudeka? WEngine wanalalamika ati hawawezi kupata nyama choma tena!

Deko lenyewe ni la raia wasiozidi 10%. Huko kwetu Mbunda ni familia ngapi zinauwezo wa kunywa chai?

Garama kubwa ya sukari ni kwa wale wenye kula milo mitatu kwa wachumi wanafahamu kuwa Mh. Rais ameamua kuangalia walio wengi na kwa kawaida katika uchumi lazima kuwe na waathirika. Kwangu mimi sioni ubaya kwa hiyo paercent ndogo kuumia kwa muuda ilinwale wengi waone mwanga wa jua nao wakisha ingia kwenye uzalishaji sote kama taifa tufaidike....

Haya yote yanahitaji muda pamoja na vision ya pamoja na wala siyo kumkomoa Mh. Rais kama elite wengi wanavyo jinasabisha....hawatoi msaada zaidi sana wako ku kosoa zaidi huku nyuma wakiwa na agenda ya hao "maslahi"...wanatumia udhaifu kuhujumu dhamira njema ya Mh. Rais...kwa taarifa tu hata shindwa hata kama wanataka iwe hivyo bali wasipokubali lazima maumivu yawe makubwa hata kwa ambao hawakidhamiriwa kuumia...

Kupanga ni kuchagua...um support ili tu songe mbele au umhujumu tuumie kwa muda mpaka pale atakapofanikiwa kisaidiwa na nature kwakua dhamira njema haishindwi....

Kama siyo chuki ya dhati kwa hilo li chama lao pengine na mimi ningeingia kwenye siasa kupambana at fron lakini hilo lichama hilo....Na bakia na utaifa wangu zaidi na pamoja na hilo bado nipo at front na kwa hakika tutashinda!
 
Magufuli kachuja katika kipindi cha miezi michache sana. Uthibitisho ni kwamba, wapiga zumari (waliomsifu) wake wote wameanza kulia lia kwamba huyo Malaika wao anahujumiwa. Ukweli ni kwamba Magufuli ni kiongozi mwenye hulka ya kukurupuka na SI muumini wa utawala wa sheria. Hakuna atakayemvumilia hata siku moja iwe kwa wanaCCM wanaojitambua ama wapinzani.
 
We jamaa una akili sana aisee nahisi ulipata 1 ya 3 fm6 maana umechambua vizuri sana.
 
DSC_0660.jpg
Kwa muda mrefu niliamini kuwa CCM ilivyo sasa siyo tu haiwezi kuongoza mabadiliko lakini pia haipaswi kuongoza mabadiliko hayo. Sababu kubwa ni kuwa CCM ilikuwa ni moja; ilikuwa ni chama chenye mwelekeo mmoja na maslahi ya aina moja. Na ndio maana hata watu walipoimba "CCM ni ile ile" kwa kiasi kikubwa walikuwa wanaakisi ukweli huo.

Niliamini pia kuwa CCM inapaswa kuvunjika ili Taifa lipone. Sikuona ni jinsi gani CCM inaweza kuokoleka; na hili sina shaka nilikuwa sahihi. Kitu ambacho labda sijawahi kukidhania kwa kina ni jinsi gani CCM inapenda kujifunga yenyewe kamba shingoni na kujitundika; wapinzani huwa hawana kazi zaidi ya kushabikia na kuchekelea.

Ujio wa Magufuli na ajenda ya mabadiliko umetufundisha jambo moja kubwa - CCM inaelekea kuvunjika kutokea ndani. Mjadala wa masuala ya posho kwa namna fulani na kauli za baadhi ya wana CCM kuonekana kutokuwa katika mstari wa kutaka mabadiliko unanifanya niamini kabisa kuwa CCM inaenda kuvunjika kutoka ndani kuelekea kambi mbili; kambi hizi mbili si mpya kwa wengi wetu kwani zilishakuwepo. Zilikuwepo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 na inaonekana pamoja na kuwa wote wanaonekana kuvaa kijani na njano, lakini ndani yao wako kama nyeusi na nyeupe!

Kuna kambi ya maslahi - hii ni kambi ya wale ambao uwepo wa CCM madarakani ni mafanikio kwao, watoto wao na jamaa zao. NI kambi ambayo imetusumbua sana kama taifa kwa miaka hii hasa ishirini; ni kambi ambayo haijali sana siasa, haijali sana utawala, haijali sana serikali inafanya nini; kambi hii inajali zaidi inapata nini. NI kambi ya kimahesabu sana; ilipoona kuwa Magufuli na Watanzania wanaelekea kumkubali Magufuli kuliko yule mtu wao; watu hawa hawa ambao waliapa "aliko tuko" wakajikuta wameamua kujibanza humo humo CCM ili wajue watapata nini.

Tatizo ni kuwa hadi hivi sasa hawajui kama wanapata; na dalili zinaoonesha kuwa wasipoangalia wanaenda kukosa zaidi! Na hili la kukosa wakati wao ni watawala linawasumbua na hivyo wanaanza kujikuta wanasumbua. Hawa ni unprincipled.

Kambi hii ya pili ya CCM mabadiliko inawezekana ni kambi inayoundwa na watu ambao walikataa kabisa kupiga magoti mbele ya mafisadi na inawezekana na wao walikuwa wanajua kuwa ile kambi nyingine ingepata basi wao pia wasingepata. Hata hivyo, kambi hii inaamini kuwa Tanzania inahitaji mabadiliko ya kweli na kuwa nafasi ya kuwa kiongozi au mtawala ni nafasi ya kuwaongoza watu kupitia utawala kufikia mafanikio. Kambi hii naweza kusema ni principled.

Hawa wako tayari kusimama na Magufuli hata kama wanajua kuwa na wenyewe wanaisoma namba; lakini wanasema na "tunaisoma namba pamoja na Watanzania wenzetu". Kambi hii sidhani kama ni kubwa sana kulinganisha na ile nyingine; ni kambi ambayo watetezi wake hawajajipambanua sana kama wa ile kambi nyingine.

Kuelekea Uenyekiti wa Magufuli CCM nina uhakika wa asilimia 100 wale wa kambi ile nyingine - wale wanaotaka kupata - sitoshangaa watajikuta wanaanza kurudi na kuanza kuimba sifa za Magufuli na kuanza kujibanza kwenye jukwaa la 'mabadiliko' ili na wao wawemo. Tatizo ni kuwa wanajua kwa uhakika mkubwa kuwa hilo peke yake siyo hakikisho la wao kuja kupata. Wengi wa hawa - nikiruhusiwa kutabiri - wataanguka sana kwenye chaguzi zijazo kwani walikuwa wanasimama miguu yote upande ule kaini vichwa tu viko upande wa CCM.

Uenyekiti wa Magufuli ni tishio; ni tishio kwa sababu nguvu ya Mwenyekiti wa Chama ni kubwa mno na hili linawatatiza watu kwa sababu 'ukichaa' wa Magufuli ambao ameuonesha hadi hivi sasa wa kugusa visivyoguswa, kusema visivyosemwa na kutenda visivyowahi kufikiriwa vinaweza kutendwa vinawasumbua. Itakuwaje akishika chama; hivi Sekretariati yake itakuwa na watu gani? Je, wataweka maslahi ya CCM mbele kama Katiba ya CCM inavyotaka au yale ya Taifa kwanza?

Binafsi nafurahia mgongano huu na mpasuko huu; kwani ni mpasuko wa kifikra kwanza. Ni mpasuko na mgongano kama uliowahi kutokea ndani ya ANC; ni mgongano ambao unaweza kuwa umewahi kutokea kwenye vyama vingine vikongwe. Mpasuko wa CCM ambao wengine tulikuwa tunausubiria kwa muda mrefu na kuuombea inawezekana unaelekea kutokea ndani ya miezi hii michache.

Kumchelewesha Magufuli kuwa Mwenyekiti na kumchelewesha kuongoza Chama ni aina fulani ya hujuma - sijali sababu zinazotolewa. Ni hujuma kwa sababu kwenye nchi kama ya kwetu yenye masalia ya mfumo ule wa kisoshalisti (ni kweli mfumo wetu wa kisiasa una masalia hayo) Chama tawala ndicho kina nguvu sana ya kusimamia nchi; Rais asipokuwa kiongozi wa chama vile vile ni sawasawa na Rais wa China kutokuwa kiongozi mkuu wa chama cha Kikomunisti; au yule wa Korea ya Kaskazini kutokuwa kiongozi mkuu au Cuba, au Viet Nam.

Mpaka pale mfumo wetu utakapoweza kujengwa na kutenganisha uongozi wa kisiasa na uongozi wa kiserikaake ili, Rais wa nchi ili afanikiwe ajenda zake ni lazima awe kiongozi wa chama chake cha siasa vile vile. HIli ni kweli si kwa CCM tu bali hata kwa chama kingine kikija kushika.

NI wito wangu, uamuzi wa kumkabidhi Magufuli Uenyekiti uharakishwe; kwani nje ya hapo ni kutengeneza nguvu mbili zenye kushindana kuongoza taifa. Kuna mmoja tu aliyepigiwa kura na taifa zima kuliongoza kwa miaka mitano (siyo baadhi ya miezi ya miaka hiyo mitano). CCM na uongozi wake waamue hata kuuza majengo yao yote ili wakamilishe makabidhiano hayo na nchi iwe katika utaratibu wake uliozoeleka. Hata kama hawapendi au wanaona labda wacheleweshe kidogo.

Kumkabidhi Rais Magufuli Uenyekiti wa CCM mapema ndio njia pekee ya kutenganisha kambi hizi mbili za CCM Maslahi na CCM Mabadiliko. Hakuna njia nyingine, kwa sasa.

MMM
Nimependa uchambuzi wako
 
Hussein Bashe yuko upande gani? Maslahi au mabadiliko? Kwa maoni yako tafadhali
 
CCM haiwezi kupasuka wakati Rais anayeongoza serikali anatoka CCM. Hao watanzania mnaosema wamegawanyika ndani ya CCM ni wapi hao.

Mtatamani sana itokee hivyo lakini haitatokea. Wagawanyike wakati wanajua anayewapa mkate ameshika dola. Halafu wagawanyike Kwa lipi.

Yaani we mwanachama uanze tu kwenda upande ambao huwezi kupata chochote kisa siasa, watu wa namna hiyo sidhani kama mpaka leo wako ndani ya chama. Kwa hiyo Magu uwenyekiti atapewa na CCM ataiongoza vzr bila mgawanyiko.

Yale mashindano ya tumweke mtu wetu wakati wa kumpata mgombea ni kipindi hicho tu wala sio Kwa ajili ya mabadiliko au mgawaniko wa kudumu.
 
Back
Top Bottom