MAGUFULI, Moram juu ya lami Sekenke ni sawa?

KANYAMA

JF-Expert Member
Aug 7, 2011
1,481
2,272
Sijawahi kuona japo mimi sio injinia wa maswala ya barabara, nimepita katika milima ya Sekenke nikaona wakandarasi wakiweka "molamu" au changarawe juu ya lami na kukandamiza...sijui hii ni stone base gani inayowekwa juu ya lami ambayo inaonekana haikukandamizwa vizuri ndio maana ikwa na mashimo.

my take:
Ni kweli inawezekana kuweka stone base juu ya lami iliyobomoka bila kufumua na ku kandamiza upya?kwa wanaofahamu watuambie la sivyo tutakuwa tunaibiwa mchana kweupe.
 
Mkuu umeweka uzi wa maana kweli, nimepita jana nilichokiona sikuamini, wale jamaa wanachofanya ni kuweka moram juu ya rami na kushindilia
 
Wakuu, ni mlima upi wa sekenke? au ni ile njia ya zamani?
 
ni barabara mpya iliyokabidhiwa miaka kama mitatu kama sikosei huwezi amini.."wenzetu" wa kichina ndo wanafanya ukarabati.simu yangu ilikuwa haina chaji ningepiga picha..ila ninauhakika wana JF wengi tunapita barabara hii kwa yeyote atakayepita anaweza kudhihirisha hili.kama wahusika wamelala basi nguvu ya umma ikemee kwa nguvu zote uozo huu kama itabainika wanafanya bila authority kutoka kwa ma consultants wa Tanroads.."nothing about us without us"
 
Duh! awa mawaziri wetu hawaeleweki. Morogoro road imetinduliwa, ilijengwa juzi juzi tu' kwa hela nyingi ya walala hio' kisa mabasi yaendayo kasi, sasa nahiyo mpya ya Sekenke. Jamani kodi zetu zinafisadiwa hivi hivi? Na kama sijakosea ni huyu huyu Magufuli wakati barabara hizi zinajengwa alikuwa waziri! Sipati picha kabisa!
 
only in tanzania
Wakuu kitu kama icho kilifanyika arusha-moshi road ,waliweka kokote juu ya lami,mwanzo nlishangaa kidogo afu ilikua inakera ila baada ya muda flani ile sehemu imekua poa sana yani ata ukipita hapo unaskia tofauti ,me naona si kitu kibaya ila ni ufundi tu,wataalam wa civil mtusaidie zaidi apo
 
Hili ni tatizo ambalo watanzania tumeshafanywa Majuha!! Siku Zote watu wanasema ubora wa nyumba ni Msingi!! Huu msemo Hauna Mhandisi wala Mchumi ila ndio Ukweli wenyewe!! Kama ndugu umeona hayo unayosema ujue Hapo ni changa la Macho!! Kwani wanasema wajinga ndio waliwao!! sasa hapo akili kumkichwa!! Ungetuwekea Picha ingekuwa poa sana!!
 
Check on Google au Wikipedia kuhusu " SURFACE DRESSING" na utaelewa kwa nini wanaweka changarawe juu ya lami.
 
Bandugu mambo mengine huyu Magufuli anachemka na sijui kama ana washauri maana suala la kuondoa foleni katika miji hasa Dar ilikuwa sio upanuzi wa barabara bali ilikuwa ni kuboresha (feeder road) na nina uhakika kama sio foleni kuisha basi ingepungua kwa kiasi kikubwa
 
Check on Google au Wikipedia kuhusu " SURFACE DRESSING" na utaelewa kwa nini wanaweka changarawe juu ya lami.
surface dressing kwa barabara muhimu kama hiyo ni ufisadi. badala yake asphalt reinforced concrete ndiyo ingefaa kwa barabara na sehemu hiyo
 
Nilipita juzi na basi la Mohammed Trans nikitokea DAR, ukweli hata mie hii ilinishangaza mno. Mbaya zaidi walisababisha tukae zaidi ya saa nzima pale MISIGIRI kusubiri mpishano mlimani SEKENKE.

Molamu juu ya lami hili nalo yawezekana ni ajabu lingine la kuingizwa hata kwenye rekodi za dunia!!!
 
Wapi vijana wa civil eng pale mlimani,ST joseph eng university,vijana DIT waje watushushie nondo hapa maana tunadanganjwa sana Watanzania.
 
surface dressing kwa barabara muhimu kama hiyo ni ufisadi. badala yake asphalt reinforced concrete ndiyo ingefaa kwa barabara na sehemu hiyo

Cha msingi ni ubora wa sub-base, base pamoja na sub-grade, na sio wearing course. "REINFORCED CONCRETE" si mchezo na gharama yake iko juu sana, ila kwa materials wanazotumia itakidhi loading since tests have been done before construction ndo maana serikali ikapitisha fungu la barabara ya aina hiyo.
 
Nilipita juzi na basi la Mohammed Trans nikitokea DAR, ukweli hata mie hii ilinishangaza mno. Mbaya zaidi walisababisha tukae zaidi ya saa nzima pale MISIGIRI kusubiri mpishano mlimani SEKENKE.

Molamu juu ya lami hili nalo yawezekana ni ajabu lingine la kuingizwa hata kwenye rekodi za dunia!!!

Pigia kura ukarabati wa Sekenke ili iingie kwenye maajabu ya dunia : Hili tangazo linatakiwa kuanza kuruka kwenye TV na REDIO
 
Mnaelewa kwamba kuna aina tofauti za "wearing course". Maana yake tabaka linaloisha. Kwenye ujenzi wa barabara kuna matabaka makuu matatu na muhimu ni zaidi ni kwamba haya matabaka lazima yawekwe kuanzia kwenye udongo usio na vitilifu, au samadi. Ndio maana utaona kabla ya kujenga barabara ni lazima wachimbe kuondoa tabaka lenye mbolea au linalootesha.

Baada ya hapo inakuja sub-base, ambayo ni mchanganyiko wa mawe na udongo ili kuanza kuimarisha eneo ambalo magari yatapita. Hii huwa ni 30 cm zilizokandamizwa ( compacted) au zaidi kulingana na matumizi ya barabara. Baada ya hapo inafuata Base course ambayo ndiyo barabara yenyewe. Hii huwa ni mchanganyiko wa saizi tofauti za udongo, mchanga na mawe (kokoto) pia tabaka hili huwekwa na kukandamizwa likiwa na kiasi fulani cha unyevu ili kufikia mkandamizo unaotakiwa. Hili tabaka ndio barabara yenyewe, maana yake ni kuwa ndio linaeleza ubora na uhai wa barabara husika. Na mwishoni ndio linakuja tabaka la tatu ambalo ni tabaka uso linalokwisha.

Tabaka uso linalokwisha kazi kubwa ni kupendezesha barabara husika na kuzuia maji kupenya kuingia kwenye matabaka ya awali. Kulingana na ubora wa kokoto na idadi ya magari ndio unaweza kuchagua nia aina gani ya uso itatumika, kama ni surface dressing, asphalt concrete, rigid concrete au reinforced concrete.

Kwa barabara nyingi za trunk za TANROADS zilijengwa kwa surface dressing ili kupata kilomita nyingi kwa gharama nafuu. Ni barabara chache zilizojengwa kwa asphalt concrete kama ile ya makuyuni - ngorongoro, stretch za morogoro road, iringa road kutokea moro n.k ila sehemu za vilima korofi walitumia reinforced concrete kama kilima cha kitonga na maeneo ya kilosa.

Kwa maana hiyo, lile eneo la sekenke yale mashimo yalisababishwa na base na subbase kutokuwa imara na ikizingatiwa kuwa pale walipasua miamba, inawezekana yale maeneo ambayo ndio ilikuwa wametega baruti walishindwa ku-compact vizuri.
 
Photo0316.jpg Photo0317.jpg
dah... na mimi nimepita hapa sekenke... nilikuwa na mohamed trans narudi dar.. lami yenyewe ndo hii wadau,,,yaani foleni hadi huku porini... duh..hapa tulipigwa stop na hao maafande ili tupishane mlimani........
 
Back
Top Bottom