Uchaguzi 2020 Magufuli(Mlowa): Ubunge sio 'madigrii' ni kipaji kutoka kwa Mungu; mkichagua Wapinzani nitashindwa kuwatumbua wasipofanya kazi

CCMkuelekeaUchaguzi

Senior Member
Aug 18, 2015
179
77


Katika kipindi cha miaka 5 tumefanya mengi, hata kuhamishia Makao Makuu Dodoma halikuwa jambo dogo. Miaka 47 haijawezekana ila miaka 5 tumeweza. Makao Makuu yanamaanisha ustawi wa eneo hili unakuja kwa nguvu.

Tunajenga Uwanja wa Ndege mkubwa huko Msalato ili ndege za kimataifa zije. Tumeleta stendi ya kisasa, soko la kisasa n.k. Tunatimiza ndoto ya Mwl. Nyerere.

Uongozi sio madegree ni kipaji toka kwa Mungu, Lusinde ni kijana mzuri na anafanya kazi nzuri ndio maana ni mjumbe wa NEC. Nyie wananchi mnajua kuchagua.

Natoa ahadi kwa watani zangu Wagogo, niliahidi km 16 toka Mlowa hadi Mvumi zitengenezwe kwa lami.

Anamuita Mkuu wa Mkoa...

"Nataka umuagize RM wa TANROADS Dodoma ndani ya miezi 2 barbr ya Mlowa kwenda Mvumi itangazwe tenda kwa ajili ya kujengwa kiwango cha lami.

Nataka wagonjwa wanaougua macho hapa wawe wanapelekwa kwa haraka Mvumi. Tunataka jombi lililo karibu na Makao Makuu lifanane na hadhi hiyo. Tunataka tubadilishe Wilaya ya Mvumi. Nina hiostoria nayo, nilikuwa na kaka yangu hapa alishafariki. Nilishawahi kuleta mzee mmoja kutoka Chato ameshatangulia mbele za haki.

Ndugu zangu wa Mvumi, mna mbunge mchapakazi. Narudia ubunge sio Degree ni kuwakilisha mawazo na shida za wananchi anaowaongoza. Lusinde anaweza mumpe kura nyingi. Au kapita bila kupingwa au wapo wanaompinga? Wanaompiga waonesheni tarehe 28 lakini pia mniletee madiwani wa CCM ili kazi ifanyika vizuri

Nitashangaa sana tumeleta Makao Makuu hapa halafu shukrani iwe ni kutunyima kura? Kweli watu wa hapa hamfaidiki na Makao Makuu ya Dodoma?

Kabla ya miaka 2 kupita, vijiji 30 vilivyobaki vitakuwa na umeme. Mimi nakaa hapa, haiwezi kunishinda"

Dkt. Magufuli anasisitiza madiwani wote wawe wa CCM ili Halmashauri ya Wilaya itakayoundwa pesa zitakazoletwa zitumiwe vizuri na wa CCM sababu nina uwezo wa kuwatumbua. Mkileta wengine (vyama vingine) sitoweza kuwatumbua, wakila msinilaumu

Kisha Dkt. Magufuli anatania kuwa anawapenda sana Wagogo, "Inawezekana Lusinde akanitaufutia kasichana kazuri ka kigogo"
 
Akiwa jimboni kwa Lusinde mbali na kutoa amri ya kuwekwa lami barabara ya KM 16 pia amesisitiza kuwa aletewe Wabunge wa CCM maana akiletewa wa upinzani fedha zitaliwa na hana uwezo wa kuwatumbua.

Hili jambo nimekuwa nikiliwaza sana. Mbona Rais Magufuli anatupiga kamba waziwazi kabisa?

Je, kwa kuangalia tu kati ya Wabunge wa upinzani na wale wa CCM ni wepi wameonyesha uwezo hata majimboni mwao? Ni wepi wameonyesha kuwa bega kwa bega na wapiga kura wao? Ni wepi wamesimama kidete kutetea maslahi ya umma?

Na swali la mwisho kabisa, kati ya wapinzani na wale wa CCM kina nani wamekithiri kwa tuhuma za wizi? Je amewahi kuonyesha mfano wa hata mbunge mmoja wa CCM aliyemtumbua kwa tuhuma za wizi bunge lililopita? Walikuwepo watuhumiwa au hawakuwepo?

My take
Nimeona kabisa lengo la Magufuli la kutaka Wabunge wa CCM watupu siyo hili analotuaminisha, lipo lingine amelificha. Halafu naona kama Rais anataka kutuchota watanzania wote atulazimishe tuwe kundi moja!
 
CCM wapo ila wakizipiga tunawatumbua...rejea Chenge, Ngereja, nk walivyonyolewa kwenye mchujo wa kamati kuu! Ukitaka kupata kibano muulize mbowe kuhusu ruzuku, au ahata fedha za maendeleo ya mfuko wa jimbo!
 
Akiwa jimboni kwa Lusinde mbali na kutoa amri ya kuwekwa lami barabara ya KM 16 pia amesisitiza kuwa aletewe wabunge wa CCM maana akiletewa wa upinzani fedha zitaliwa na hana uwezo wa kuwatumbua.

Hili jambo nimekuwa nikiliwaza sana. Mbona Rais Magufuli anatupiga kamba waziwazi kabisa?

Je, kwa kuangalia tu kati ya wabunge wa upinzani na wale wa CCM ni wepi wameonyesha uwezo hata majimboni mwao? Ni wepi wameonyesha kuwa bega kwa bega na wapiga kura wao? Ni wepi wamesimama kidete kutetea maslahi ya umma?

Na swali la mwisho kabisa, kati ya wapinzani na wale wa CCM kina nani wamekithiri kwa tuhuma za wizi? Je amewahi kuonyesha mfano wa hata mbunge mmoja wa CCM aliyemtumbua kwa tuhuma za wizi bunge lililopita? Walikuwepo watuhumiwa au hawakuwepo?

My take
Nimeona kabisa lengo la Magufuli la kutaka wabunge wa CCM watupu siyo hili analotuaminisha, lipo lingine amelificha. Halafu naona kama Rais anataka kutuchota watanzania wote atulazimishe tuwe kundi moja!

HAPA KAZI TUU
 
Jamani mshaurini mgombea wetu wa CCM ajizuie kutoa kauli tata. Ukweli ni kwamba Rais hana uwezo wa kutumbua mbunge, hata wa CCM maana wabunge wako chini ya mhimili mwingine.

Hakuna anayeweza kuwa rais, mbunge au diwani anayeweza bila dhamana ya chama
 
Hapa Mahera kavaa miwani ya mbao, huyu mgombea anaewatisha wapiga kura kwamba atawashughulikia wasipomchagulia awatakao hapa tume mbona Ni kigugumizi
 
Asitudanganye hapa ..... Miaka 5 iliyopita alitumbua Wambunge na Madiwani wangapi zaidi ya kuishia kuiba wa Upinzani .....!!
 
Akiwa jimboni kwa Lusinde mbali na kutoa amri ya kuwekwa lami barabara ya KM 16 pia amesisitiza kuwa aletewe wabunge wa CCM maana akiletewa wa upinzani fedha zitaliwa na hana uwezo wa kuwatumbua.

Hili jambo nimekuwa nikiliwaza sana. Mbona Rais Magufuli anatupiga kamba waziwazi kabisa?

Je, kwa kuangalia tu kati ya wabunge wa upinzani na wale wa CCM ni wepi wameonyesha uwezo hata majimboni mwao? Ni wepi wameonyesha kuwa bega kwa bega na wapiga kura wao? Ni wepi wamesimama kidete kutetea maslahi ya umma?

Na swali la mwisho kabisa, kati ya wapinzani na wale wa CCM kina nani wamekithiri kwa tuhuma za wizi? Je amewahi kuonyesha mfano wa hata mbunge mmoja wa CCM aliyemtumbua kwa tuhuma za wizi bunge lililopita? Walikuwepo watuhumiwa au hawakuwepo?

My take
Nimeona kabisa lengo la Magufuli la kutaka wabunge wa CCM watupu siyo hili analotuaminisha, lipo lingine amelificha. Halafu naona kama Rais anataka kutuchota watanzania wote atulazimishe tuwe kundi moja!
Si bure, huyu mtu kuna kitu sehemu fulani hakipo sawa kabisa. Hana uwezo kabisa wa kuinadi ilani ya chama chake, wala kutangaza sera mpya wala kujenga hoja zenye mashiko. Naam! Amepatwa na "Lissuphobia" kiasi kwamba anaomba siku za kampeni ziishe tu na tume imtangaze mshindi kwa hila.

Ukisikiliza porojo za 'political naïve" hawa, yaani Polepole & Bashiru, ukirudi kwa matendo na kauli za msajili wa vyama mwenye ajenda kuu ya kuvidhibiti CDM na ACT Wazalendo, hasusani Lissu, Maalim Seif na Zitto, ukiongeza na kauli za huyu kada wa CCM anayetambuliwa kwa cheo mkurugenzi wa NEC, basi utatambua mtu kamasi nyembamba zinamtoka kwa kiwewe.
 
Back
Top Bottom