CHARLES2016
JF-Expert Member
- Mar 22, 2016
- 376
- 435
Wewe umeandika upupu gani, Kama alichukua hela kwa wafanyabiashara akajenga miundo mbinu itakayotumiwa na watanzania wote huyo ni kiongozi mbaya??!! Angekuwa mbinafsi so angekula yeye na familia yake.Nimesimuliwa jambo fulani na mtu mkubwa tu ikanishangaza sana. Kwamba JIWE alikuwa na watu wake kila kona ya nchi hii ambao walitumia ubabe, ukatili na vitisho hasa kwa wafanyabiashara wakubwa ili wawe wanatoa fedha ambazo alizitumia kujenga miundombinu mbalimbali ya serikali na yake binafsi nje ya bajeti. Lengo lilikuwa ni kujipa uhalali wa kutawala mbele ya watanzania, na pia alipiga marufuku kuwanyanyasa machinga na mama lishe ili aonekane ni mtu wa wanyonge maana ndio wengi Tanzania. Huyo mtu anasema walikuwepo wakuu wa wilaya, mikoa na viongozi wengine ndani ya chama chake waliokuwa "wanakula" pamoja naye hayo mapato haramu. Anasema fedha zingine alikuwa anatembea nazo kwenye gari yake ili azigawe kwa wanaoitwa wahitaji barabarani na kununulia mahindi ya kula. Sasa ili siri zake hizo zisifichuke aliamua na kupanga kutokomeza kabisa upinzani na wasipate ubunge maana wangeweza kubaini na kuhoji anakopata fedha za miradi mbalimbali ikiwemo ya Chato na anazogawa barabarani wakati hakuna bajeti iliyopitishwa na bunge kwa matumizi hayo. Lengo lake lilikuwa ni kutawala zaidi ya vipindi viwili. Huyo ndugu anasema hata huyo DC aliyekamatwa kwa tuhuma za ujambazi na kumiliki genge la Uhalifu ni mwanachama wa kundi hilo la JIWE. Inahisiwa kwamba wengine wapo Dar, Tunduma, Arusha, Mwanza, Mara, Mtwara, Mbeya na Kigoma.
Bahati mbaya hakutambua kuwa anamchukiza Mungu kwa yote aliyoyafanya.
Tujifunze kuwachambua vizuri watu tunaowapa dhamana ya kutuongoza hasa ngazi ya Rais. Tumejifunza, tusirudie makosa.
Kama alitaka wajasiriamali wadogo wadogo Kama wamachinga, mama lishe na boda boda wasisumbuliwe huyo alikuwa kiongozi mbaya??!! Mmesahau kipindi cha awamu ya 4 hawa watu walivyotaabishwa kwa kufukuzwa kila mahali na kuporwa vitu vyao au kumwagiwa vyakula vyao?
Ama kweli nimeamini watanzania hatujui nini tunataka.