MtuloBM
JF-Expert Member
- Feb 26, 2020
- 542
- 477
Ni heri nionekane nina roho mbaya na kauzu kuliko kufadhili binadamu, binadamu hajawahi kuwa na shukrani hata siku moja ( ni wachache mno). Magufuli alijitoa sana kwa wananchi wa Tanzania alifanya kazi usiku na mchana, aligusa kila nyanja na hakuna kipindi chochote watanzania tulichoshuhudia maendeleo ya haraka kama kipindi cha JPM. Wengi mlioshupaza shingo kutaka kuharibu legacy ya Magu wengi wenu ni wezi, majambazi, wala rushwa, wapinzani msiojielewa au watu msiolitakia mema taifa letu.
NB: mtu kama kikwete anaonekana ndio kipenzi cha wengi kwa sasa ni kwasababu alikua ni kiongozi dhaifu sana, watu walipiga sana hela hali ya kuwa yeye mwenyewe yupo bize akipiga picha na Marais wa dunia. Zaidi na zaidi Magu pia ni binadamu hivyo ana mapungufu ya kiubinadam, ila ukweli ni kwamba ukiachana na nyerere basi rais bora wa muda wote atabaki kuwa ni magufuli, ndiye rais aliyeliliwa na karibu Africa nzima pindi mauti ilipomfika .. RIP MAGUFULI MUNGU AKULAZE MAHALI PEMA PEPONI AMEEN ..
Kujitoa ni kwenda kujificha chato kipindi cha Corona.