Maseto
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 944
- 545
Jana ilikuwa sherehe za kumpongeza Magufuli na kujipongeza kwa washindi wa ubunge na udiwani nyumbani kwa Magufuli Wilayani Chato. Sherehe hizo zilianza na baraka ya mvua.
Wanachama wa CCM walifika kwenye sherehe hizo kwa njia ya miguu na magari. Wale wa mbali kama Buseresere walifika kwa magari. Nilichojifunza ni kwamba bado CCM hawajawa na mshikamano wa kutosha mkoani Geita. Kwa mfano katika sherehe hizo Mwenyekiti wa CCM Mkoa MSUKUMA hakuonekana bila maelezo yoyote ya nini kilichosababisha asiwepo.
Lakini jambo lililo nifanya niandike ni uongo uliotaarifiwa na radio RFA. Kuwa watu walitembea kwa miguu kilometa 72 kwenda kwenye sherehe hizo. Wakati watu wote waliotoka kuanzia kilometa 5 walifika kwa magari. Hakuna mtu aliyetembea kwa miguu kutoka Buseresere.
Hili ni jambo dogo lakini ndiyo utamaduni wa CCM kudanganya hata kwa mambo ambayo hayahitaji uongo.
Magufuli kama kweli anataka aondoe unafiki aanze na kuwathibiti matapeli na wababaishaji kama Viongozi wa CCM Mkoa wa Geita na Wilaya ya Chato.
Pia awathibiti mafisadi kama akina Madabida Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar.
Wanachama wa CCM walifika kwenye sherehe hizo kwa njia ya miguu na magari. Wale wa mbali kama Buseresere walifika kwa magari. Nilichojifunza ni kwamba bado CCM hawajawa na mshikamano wa kutosha mkoani Geita. Kwa mfano katika sherehe hizo Mwenyekiti wa CCM Mkoa MSUKUMA hakuonekana bila maelezo yoyote ya nini kilichosababisha asiwepo.
Lakini jambo lililo nifanya niandike ni uongo uliotaarifiwa na radio RFA. Kuwa watu walitembea kwa miguu kilometa 72 kwenda kwenye sherehe hizo. Wakati watu wote waliotoka kuanzia kilometa 5 walifika kwa magari. Hakuna mtu aliyetembea kwa miguu kutoka Buseresere.
Hili ni jambo dogo lakini ndiyo utamaduni wa CCM kudanganya hata kwa mambo ambayo hayahitaji uongo.
Magufuli kama kweli anataka aondoe unafiki aanze na kuwathibiti matapeli na wababaishaji kama Viongozi wa CCM Mkoa wa Geita na Wilaya ya Chato.
Pia awathibiti mafisadi kama akina Madabida Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar.