TL. Marandu
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 3,625
- 5,805
Mimi siwaelewi na Naaza Kuwadharau sana, Watu ambao Kila akitokea Mkuu wa Wilaya au Mkoa Kufanya Jambo la Kishenzi dhidi ya Wapinzani au Wananchi moja kwa moja, Basi watu hawa Wanasema Kuwa Rais hahusiki, hajawatuma.
Hawa Wakuu wa Wilaya, na Wakuu wa Mikoa wanateuliwa na Rais, Na Rais Mwenye akili Timamu hawezi Kunyamazia Wateule wake wanapofanya Mambo ambayo ni Uvunjifu wa Sheria. Kuna Matukio Mengi ya Kukera, ya Kihuni na Kihalifu yamefanywa na Wakuu wa Wilaya na wa Mikoa! Kama Kupora Rambi Rambi, Kuvuruga Misiba, Kuingilia Kihamba cha asili cha Mtu na Kuharibu Mazao tena bila hata amri ya Mahakama! Unamwingilia Mtu kwenye shamba la Asili! Ni kama Kumwingilia Magufuli Shambani kwake Chato! Kumkamata meya wa Ubungo, Kuvamia Clouds!
Rais Magufuli Kama hawatumi hawa , Yeye au Mtetezi wake yeyote hapa anieleze ni lini alishawahi Kukemea tabia hizi au kumwajibisha angalau mmoja wa Watu wake hawa Washenzi na wahalifu, maana siwezi kuwaita wahuni viongozi!
Nani Kawaloga Watanzania Mpaka wanaheshimu watu Wanaobeba Mbeleko uhuni wa aina hii?
Hawa Wakuu wa Wilaya, na Wakuu wa Mikoa wanateuliwa na Rais, Na Rais Mwenye akili Timamu hawezi Kunyamazia Wateule wake wanapofanya Mambo ambayo ni Uvunjifu wa Sheria. Kuna Matukio Mengi ya Kukera, ya Kihuni na Kihalifu yamefanywa na Wakuu wa Wilaya na wa Mikoa! Kama Kupora Rambi Rambi, Kuvuruga Misiba, Kuingilia Kihamba cha asili cha Mtu na Kuharibu Mazao tena bila hata amri ya Mahakama! Unamwingilia Mtu kwenye shamba la Asili! Ni kama Kumwingilia Magufuli Shambani kwake Chato! Kumkamata meya wa Ubungo, Kuvamia Clouds!
Rais Magufuli Kama hawatumi hawa , Yeye au Mtetezi wake yeyote hapa anieleze ni lini alishawahi Kukemea tabia hizi au kumwajibisha angalau mmoja wa Watu wake hawa Washenzi na wahalifu, maana siwezi kuwaita wahuni viongozi!
Nani Kawaloga Watanzania Mpaka wanaheshimu watu Wanaobeba Mbeleko uhuni wa aina hii?