Magufuli kupewa wizara ya lawama ni kumkwamisha urais 2015?

mzambia

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
885
60
Great thinkers nimekuwa nikitafakari kuhusu raisajaye kupitia ccm nikaona anayefaa labda kidogo dr. Magufuli, lkn hiyo wizara aliyopewa si anaweza kukwamishwa kwa makusudi kiutendaji ili aonekane hafai kuwa rais maana mafisadi wana mbinu nyingi sana.

Na kuhusu 6 wamempa wizara ambayo wananchi wa kawaida kujua anapafomu vipi ni kazi sana sasa si ndiyo kifo cha kisiasa hicho kwa samuel?

Nawasilisha
 
Wasipompa Magufuli...nchi itaenda kwa CDM.....heri wampe hata kama mafisadi hawatamtaka ila wanyonge tunamtaka....hope katibu hatakuwa huyu kichefuchefu!!!
 
2015 atagombea jk,subiri uone kama hawaja "pitisha" katika katiba kwamba raisi aongoze kwa vipindi vi3
 
Mi simkubali mapadlock japo nampenda kwa kazi kama anazofanya sasa. hana hekima.
 
Tayari wameanza kumwekea zengwe mbona viwanja vya ndege havgusi?
bt hawa wanakuaga wakali hapa 2,mnakua na hope,bt wakiwa maraisi,wanakua kama mabata,na hao usalama wa taifa ndo wamelala kabisa?
 
Hiyo Wizara inaweza kumpandisha chati na akapata umaarufu zaidi kuweza kugombea 2015. Hopefully, Mwakyembe anakuwa Waziri Mkuu. Mafisadi wanakula kona kiaina!
 
when you in deep sh!t, you turn to anyone even those you dont like... That is what KJ did... hiyo wizara iko kwenye deep sh!t kutokana na uzembe wa kawambwa na "ushamba" wa waziri mkuu katika kusimamia wizara zake... SO KJ HAS TO TURN BACK TO THE RIGHT MAN, JPM

This post will make Magufuli even a better candidate
 
Kwani lazima rais atoke ccm? Halafu huyu si ndo yule aliye asisi kugawana nyumba za serikali ili wengine wanaokuja wakapange hoteli kwa gharama za serikali? Kwa kusimamia tu wachache kugawana nyumba za serikali anakosa sifa za kuiongoza nchi kwani hachelewi kuamua kugawana migodi ya umma kama alivyo fanya bosi wake wa kwanza, BM!
 
Magufuli alikwamisha tangu miaka ya 2000 kwa mambo mengi kwanza inaaminika kuwa hana mtandao wa kutosha ndani ya kamati kuu ya ccm na nadhani yeye magufuli si mjumbe wa kamati kuu,kawaida mjumbe wa kamati kuu ana nafasi kubwa,hapa labda tunamuona Benard membe kwa mbali. Dr. Magufuli pia alipewa wizara tata mara zote,pia uhamisha amishwa ili mchango wake upotee bila kibali. Ikumbukwe pia kuna Wanyakyusa wawili tishio waliokwamisha kijanja na mwishowe hatuwafikirii tena. Walipewa wizara mara za watoto,afya pengine kumwagilia mboga mboga,mpaka wakapotea kisiasa. Si wengne kina mwakyusa na mwandosya kwisha kisiasa. Nadhani tufike hatua tukubali ccm wanamweka mtu wamtakae wala si vigezo vya utendaji. Correct me plz!
 
jamani tusikae hata kidogo kufikiria kama ccm itarudi madarakani kwanza ni kwa nn warudi wakati tuna watu wazuri pale chadema amalbao wanauwezo mzuri na ajenda yetu kubwa kwa wale wanao hitaji mabadiliko ni kuwa na mkakati wa kuiweka chadema kushika dola
 
Mie binafsi nina wasiwasi na MZAMBIA jana kamtest Benard Membe, kachemsha sasa leo unamleta Magufuli kama ulitumwa kutest leo umepatia huyo huyo unayemtaja leo ana nafuu mara 200 kuliko mnyenyekevu Membeeee. Tunajua unaweza kuwa na shida na limao, lakini kwenye meza ya Maliomao 100 yakawa yote mabovu. Kwa vile shida yako ni limao itabidi kati ya hayo malimao 100 mabovu uchague lenye unafuu.

Sasa nakueleza hivi katika watu wa CCM wote wanaweza kuwa wabovu na hata CDM pia lakini lazima 2015 apatikane president mwingine na si JK tena. Kwa hiyo wadau eleweni kuwa katika malimao mabovu tunaangalia moja lenye unafuu. Whatever it is pale CCM yeye Magufuli ndiye limao jenye at least unafuu. Utendaji wake wa kazi angalau tunaujua. Tuliona enzi za Ben alivyochakarika ukilinganisha na wengine. Na kila wizara anayowekwa anasikika.

Pia kumbuka aliwahi kupewa ulinzi baada ya kuwashinikisha Vigogo waliojimilikisha magari ya serikali kuyapaki pale kidongo chekundu dar na kuwafedhehesha vya kutosha. Jk kabla ya kuwa rais alikuwa na CHARISMA ya kupendwa lakini si kwamba alishafanya kitu cha kijasiri kama MAGUFULI. Hadi kitengo cha samaki sasa wale wachina na wajapan wanasainiana mkataba ili wavue ki- halali na wengine wezi wa samaki bahali ya Hindi bado wako rumande. Huyu at least hawafumbii macho wezi wa raslimali za nchi.

Kipindi cha nyuma hapa uvuvi haramu mwananchi kupata samaki mzuri wa kula ilikuwa issue. Huku maeneo ya kanda ya Ziwa ilikuwa tabu. kwa sasa samaki wengi kwa Tsh 1000/= unapata mboga ya kutosha ( japo hii ni weak point ya kuwa presidaa kwa great thinkers kama nyinyi) lakini kwa wananchi wa kawaida wapiga kura wanamsifu kwa hilo. Haya hebu wewe MZAMBIA peleka habari kwa mhusika.
 
CCM ina wengi wenye kufaa kuwa wagombea urais wa Jamhuri na wa Zanzibar na kwa vile katiba mpya itafanya kazi na Mgombea wa kiti cha Tanganyika
 
CCM ina wengi wenye kufaa kuwa wagombea urais wa Jamhuri na wa Zanzibar na kwa vile katiba mpya itafanya kazi na Mgombea wa kiti cha Tanganyika
:bump::bump::bump:kweeeli we mtu wa pwani.............hebu kacheze ngoma na mkweere mwenzio na sio kuja kuposts comments za kipuuzi.nakabidhi.
 
akipew wizara ndogo mnalalamika, akipewaw wizara kubwa mnalalamika. You poor thinkers!
Hata akipewa urais bado mtalalamika. Na mtalalamika sana tu. Vichwa vimejaa pombe/bangi.
 
hata mawe yanaweza kuwa marais, usiumize kichwa ndugu, hayo mambo ukifika muda wake yatajipanga yenyewe
 
Back
Top Bottom