Magufuli kiboko: Meneja wa TANROADS akemewa kama mhudumu!

Huko sasa ni kuzidisha na kupitiliza. Meneja/kiongozi unaweza kabisa ukawa firm bila kufokea watu na kuwaadhirisha hadharani. Kufanya hivyo ni kama kutafuta sifa vile. Unataka watu wakusifie...flani mkali bana..flani hana mchezo.

Sijavutiwa kabisa na management na leadership style ya Magufuli.

Lakini jamani,ikiwa kila mtu anayo mapungufu yake,na sisi wote ni binadamu hakuna aliye Mungu kati yetu,...si vema sana kuwa na kiongozi mropokaji lakini anayehakikisha kunakuwa na utekelezaji thabiti wa mipango ya serikali kuliko mtu kama kikwete ambaye ni very diplomatic in public(in fact the best I ever saw)lakini akanyamazia matatizo yetu yote ikiwamo rushwa iliyokithiri??...

sidhani kama sifa ya kwanza ya kiongozi inatakiwa kuwa upole ama huo ukali.sifa ya kwanza ya kiongozi ni uwezo wa utekelezaji wa maazimio ya maendeleo,na uwezo wa kusimamia maslahi ya wengi bila kutetereka...

nikisema hivi,ningewiwa kumuunga mkono maghufuli kama angegombea kupitia ccm ingawa sina mahaba hata chembe na hiki chama..pengine huyu aweza kuwa mtu pekee mwenye guts za kufanya maamuzi magumu na kushughulika na hawa wanyonyaji wetu wa siku nyingi wanaoendelea kuishi kati yetu kama vile wako juu ya sheria.
 
Hii actually ni weakness na sloppy management style. Anatengeneza tension bure, anawa demoralize wafanyakazi wake, anawaumbua hadharani watu wazima, anatengeneza uadui etc.

Angeweza kufanya yote hayo kwa maandishi, akawa na ushahidi wa kimaandishi kwamba alikwishaonya etc.

Hata mtoto wako akifikisha umri wa miaka 18 si uungwana kumshambulia mbele ya wenzake, unamuita pembeni na kumpa kisago.

Magufuli kwa kuwaka hivi anatuonyesha kwamba hapati taarifa mapema inavyotakiwa au anataka kuuza sura aonekane mnoko/mfuatiliaji.

Siku moja atakutana na mchizi asiyetegemea kazi yake atamkaripia atapewa majibu ya ajabu ya hapo kwa papo kama aliyopewa Lowassa na yule mjeshi mkuu wa wilaya kule Mwanza.

Approach ya magufuli kwa hali tunayokwenda nayo ndiyo inayostahili, na hata huyumtoto wa mkulima anapaswa kuwa hivyo, wote tunajua kazi ya uwaziri ni ukilanja tu, anstahili pongezi sana tena sana tuache kuwa wanafiki kwa kumkatisha tamaa, nchi hii inazama, hawa mameneja ni bure tu.
 
Hela mkuu. Hawa mameneja huwa wanakula posho kwa kugombezwa na Magufuli. Hili liko wazi sana na mara nyingi mameneja wenyewe wamekuwa wakimuandikia Magufuli barua za kuomba kugombezwa mbele ya kamera za TV.

Sina hakika kama huu si utani
 
skatai pale tunaposhindwa kufanya tusemwe ila namna aliyotumia wazir sio.sawa jamaa hakuwa site lakin makufuli hakujua huko aliko anafanya nn pia kumgombeza mtu mwenye akil km zako ama zaid yako ni uzalilishaji mwelekeze kwa upendo atafanya kwa moyo kwan ubabe huzalisha utendaji wa hovyo,kwa vile mtu atafanya kwa hasira ama woga.waziri ajiwekee mipaka ya kisiasa na kiutendaji kuwa jembe sio mpaka ubwate km mbwa kila mahali.
 
Tanzania has a very very very long way to go as a country!!
Inasikitisha kuona watu na akili zao(I suppose kuwa wana akili!!) kushangilia upuuzi wa waziri kukaripia watendaji hadharani - inasikitisha!!
Mimi nilitegemea hii mentality ya mabwana na watwana itakuwa imefifia au kufa lakini naona hata hao ambao wanajiita magreat thinkers wanachekelea. Hii ni tabia waliyokuwa nayo wakoloni dhidi ya watanganyika - na sikumoja Mr. Nyerere(RIP) amewahi kutamka kuwa tuliwakataa wakoloni si kwasababu ya rangi zao bali kwasababu ya tabia zao za ukandamizaji...

Mr/Dr whatever, acha upumbavu wa kukaripia watu wazima hadharani,acha upubavu wa kudharirisha watendaji wa serikali hata kama wana mapungufu - waite ofisi au waonye kwa barua ecc shame on you Magufuri!!

sasa bwana kaka.. Huyo meneja angetimiza wajibu wake angekalipiwa?? Na mabya zaidi kaulizwa uko wapi anamdanganya waziri yuko saiti na hali ya kuwa hayupo? Kwa asijibu logicaly kwamba sipo hapo au sijafanya hiyo kazi kwa sababu hihi na hii.. Huo ni uvivu na uzembe wa kibongo bana.. Tusimtete huyo meneja ila hata magufuri anapenda kuonekana kwenye vyombo vya habari angeweza hata kumkaripia nyuma ya kamera jamaa mbona angemuelewa??
 
Ninayeandika hapa nafanya kazi TANROADS. Ukweli ni kwamba, bila KUGOMBEZWA mambo hayaendi kabisa jamani. Wacheni Magufuli atupelekeshe angalau tutafanya kazi. Watanzania kila siku mnalalamika humu kuwa Mkuu wa Nchi hachukui hatua, sasa anafanya hivyo Magufuli mnaanza kulalama ahhhhhh! wacheni maneno yenu jamani. Magufuli chapa kazi tusonge mbele katika sekta ya Barabara na ndiyo maana JK alikurejesha na Wananchi kushangilia. Wengine walienda mbali zaidi na kusema kuwa JK alikuchelewesha katika sekta hiyo ya Barabara.

Wacheni kulalama. Tunahitaji kusonga mbele. Najua wanaopinga humu hatua ya Magufuli ni watumishi wenzngu wa TANROADS.

Sawa,

Kama kweli unafanya kazi TANROADS siwezi kukubishia, labda unaelewa hali halisi kuliko ninavyoelewa mie.

Tatizo ukifanyakazi viwanjani unakuwa unafikiria standards za kimtoni-mtoni, kazi kwa kuheshimiana, haki za binadamu, mikataba ya ILO, morality boosting communication patterns, with a pinch of political correctnes etc, watu wanaambiwa vitu kiheshima wanafanya etc.

Labda bongo watu wenyewe wanapenda kupelekwa ki-ng'ombeng'ombe, na bila hivyo kazi haiendi.

Hii ni aibu lakini, kwa maana nina hakika hawa watu si unskilled workers, ni watu wakubwa tu na wamesomea kazi zao.
 
Usikurupuke.

Jana kwenye taarifa ya habari nimemsikia magufuli akiwaagiza wakandarasi kuhakikisha barabara zilizobomka kwa mvua zirekebishwe haraka sana na aliwashutumu ma engineer wa Iringa kwa kuwa mpaka sasa hawajachukuwa hatua za kukarabati Kitonga wakati fedha zipo.

Wewe ambae hujui kinachoendelea ndio unaona kakaa kimya. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Mkuu jana si nimesoma kwenye mtandao humu Dr. akilalamika kwamba Mkulo anamhujumu kwa kuwa hawalipi wakandarasi. sasa hizo pesa ambazo zipo ziko wapi?
 
Inasikitisha kuwa Watanzania standards zetu tulizojiwelea zipo chini kiasi cha kuwa tunamshabikia kiongozi anaekwenda na kutoa maagizo yake ya kiofisi mbele ya vyombo vya habari
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Inasikitisha kuwa Watanzania standards zetu tulizojiwelea zipo chini kiasi cha kuwa tunamshabikia kiongozi anaekwenda na kutoa maagizo yake ya kiofisi mbele ya vyombo vya habari

Kazi ipo kwa Rotarians wanaotaka kurudi nyumbani kufanya kazi kwenye mazingira haya sasa.
 
Kuonyesha msisitizo zaidi ameagiza mameneja na waandisi wote wasichukue likizo za krismasi na mwaka mpya hadi madaraja yapitike
 
Kazi ipo kwa Rotarians wanaotaka kurudi nyumbani kufanya kazi kwenye mazingira haya sasa.

Kazi tena si ndogo.

Adabu ya viongozi wa aina hii wapate mtu awaburuze mahakamani kwa kuwavunjia heshima
 
Kuonyesha msisitizo zaidi ameagiza mameneja na waandisi wote wasichukue likizo za krismasi na mwaka mpya hadi madaraja yapitike

Bongo hamna rule of law, anachosema Waziri go, typical Banana Republic. Likizo watu wanapanga mwaka mzima.

Imekuwaje? Huyu Waziri ndio kwanza anayasikia haya? Communication network yake ikoje?

Mbona anakurupusha mambo last minute kama mtoto? Haya mambo ya kufanya on the fly, especially katika ujenzi, yanaweza kutu-cost sana.
 
Waandishi wa habari wasipotokea, anaahirisha ziara ya kikaz!!!!!!!!! Ndo utendaji wake
 
Bongo hamna rule of law, anachosema Waziri go, typical Banana Republic. Likizo watu wanapanga mwaka mzima.

Imekuwaje? Huyu Waziri ndio kwanza anayasikia haya? Communication network yake ikoje?

Mbona anakurupusha mambo last minute kama mtoto? Haya mambo ya kufanya on the fly, especially katika ujenzi, yanaweza kutu-cost sana.
Anachotakiwa ni kuongeza incentives kwa wataofanya kazi wakati huu, ili mtu aamue kubaki mwenyewe kwa khiari yake, sio kulazimisha watu kuvunja mambo yao.

Kwenye ujenzi eneo ambalo limekuwa cut off kabisa, kunafanyika ujenzi wa haraka wa dharura ili kuruhusu accessibility lakini hali ikikaa sawa tu, panafumuliwa na kujengwa upya.

Sasa huyu mkuu hata haeleweki. Kama madaraja tukitaka ya kudumu muda mrefu hiyo design process tu basi ni ndefu.

Haeleweki
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Anachotakiwa ni kuongeza incentives kwa wataofanya kazi wakati huu, ili mtu aamue kubaki mwenyewe kwa khiari yake, sio kulazimisha watu kuvunja mambo yao.

Kwenye ujenzi eneo ambalo limekuwa cut off kabisa, kunafanyika ujenzi wa haraka wa dharura ili kuruhusu accessibility lakini hali ikikaa sawa tu, panafumuliwa na kujengwa upya.

Sasa huyu mkuu hata haeleweki. Kama madaraja tukitaka ya kudumu muda mrefu hiyo design process tu basi ni ndefu.

Haeleweki
....G hii mipango ya kujenga drainage system ya jiji la Dar inahitaji pesa nyingi sana, si chini ya shilingi bilioni 300 (pesa ambazo naamini zipo) ili kuweza kujenga miundo mbinu ambayo itakuwa ya kisasa na yenye uwezo mkubwa wa kuweza kuhimili mvua kubwa sana na hivyo kuweza kuzuia mafuriko mengine au kupunguza athari yake. Na kazi hii ni ya muda mrefu ambayo inahitaji kufanywa na kampuni zenye uwezo mkubwa kama Kajima au kampuni nyingine za kutoka Japan.

Kwa nchi yetu ilivyo inaelekea hawa wanaojiita viongozi watakakurupuka (dalili zimeanza kuonyesha hivyo) bila ya kuwa na mipango ya muda mrefu na hivyo kujenga madaraja ya haraka haraka ambayo hayatakuwa na uwezo wa kuhimili nguvu ya maji pindi ikitokea mvua kubwa nyingine.

Huyu Magufuli pamoja na kuwa wengi wanamsifia kwamba ni mtendaji mzuri na hata kudai anastahili kuwa Rais 2015, kwa maoni yangu ni bomu kabisa ambaye utendaji wake ni wa kukurupuka tu (zima moto)
 
Tanzania has a very very very long way to go as a country!!
Inasikitisha kuona watu na akili zao(I suppose kuwa wana akili!!) kushangilia upuuzi wa waziri kukaripia watendaji hadharani - inasikitisha!!
Mimi nilitegemea hii mentality ya mabwana na watwana itakuwa imefifia au kufa lakini naona hata hao ambao wanajiita magreat thinkers wanachekelea. Hii ni tabia waliyokuwa nayo wakoloni dhidi ya watanganyika - na sikumoja Mr. Nyerere(RIP) amewahi kutamka kuwa tuliwakataa wakoloni si kwasababu ya rangi zao bali kwasababu ya tabia zao za ukandamizaji...

Mr/Dr whatever, acha upumbavu wa kukaripia watu wazima hadharani,acha upubavu wa kudharirisha watendaji wa serikali hata kama wana mapungufu - waite ofisi au waonye kwa barua ecc shame on you Magufuri!!

Hallow Mimi sikuiona hiyo lakini ni jambo zuri kwa uongozi tulionao Tanzania kwa sasa.
Kama inafikia hatua nyingine wananchi wa kawaida hata watoto wanauliza serikali iko wapi that means wameona utendaji na usimamizi mbovu. Sasa kama umepewa majukumu kwa makubaliano ya kipato kizuri na unatimiziwa. If you can't play your part what do you expect uchekewe na uombwe kufanya kazi. Kiongozi mzuri lazima umdefine msimamo wake na reaction zake ktk kusimamia kazi.
MARRY CHRISTMAS
 
Maskini Magufuli, kwenye hiyo PHD yako haikuwa na masomo ya leadership! Si TANROAD inaongozwa na CEO, kwa nini usisukumane na huyo meneja wa mkoa? au wewe sasa ndio CEO.... achana na vyombo vya habari na misifa isiyokuwa na miguu wala kichwa, simply wewe kula sahani moja na CEO the rest mwachie mwenyewe....
 
Back
Top Bottom