Magufuli hajasema kweli; Anaficha Udhaifu wa Serikali na Wizara yake

Mheshimiwa Mnyika!Kupanda au kushuka kwa bei ya bidhaa yoyote inategemea na "simple theory of demand and supply". Masuala ya kupanga bei yaachiwe soko kwani usafiri uko huria na dynamics hizo zitumike.

Hapo tutahitaji nguvu za ziada. Nauli za vivuko vyote viko juu Kigamboni I am told ndiyo ya chini zaidi! Tuangalie na kushupalia bei ya umeme ambayo inagusa kila mtu nchi nzima aliye hai na hata !

Sasa wewe pia unaleta 'Simple Theory of Kata Schools Standards' kwenye bidhaa muhimu ktk maisha. Mh. Mnyika hakusema kuwa soko litakwama, yeye amechelea kuwa huduma zitakuwa ghali. Tuwe tunazingatia application ya theories tunazofundishwa darasani na impact yake ktk maisha ya watu. Hebu niambie namna ambayo demand inaweza ikashusha price ya bidhaa chini zaidi ya accumulated cost of production kiasi niamini tuache tu gharama za usafiri zipande na bei itashuka yenyewe.

Kama unaona alilolisema Mh.Mnyika halina maana kwa wakazi wa Kigamboni juu ya kupanda bei za bidhaa za vyakula, ilitoka wapi haja ya Mkuu wa Nchi kukemea kupanda kwa bei ya sukari? Kwa nini asingeacha demand iishushe?

Kuwa juu kwa gharama za vivuko mahali pengine hakutoi uhalali wa kupandisha Kigamboni
. Kama lengo ni kuweka sawa viwango kwa nini wasishushe huko gharama zilipo juu? Kumbuka ile ni huduma na sio biashara na ukileta mambo ya kulinganisha nitakuomba utulinganishe na Kenya ambako kivuko cha Mombasa (Likoni) ni bure.

Mwalimu wako alipaswa kukuelewesha kuwa elasticity of demand inakuwa determined na price kama other costs zitabakia kuwa constant. Gharama za usafiri zikipanda mwenye Guta hazimuumizi, anazihamishia kwa mwenye Genge ambaye naye anazipost kwa mlaji. Hakuna namna ya kuwapa nafuu wenzetu wa Kigamboni ktk hili zaidi ya kushusha gharama zisizo za lazima.

Ni kawaida ya CCM kukosa ubunifu na ndio maana bajeti ikicheza kidogo tunapandishiwa kodi kwenye sigara na bia. Na hili ni zao la wachumi wa namna yako ya kufikiri.

Na kwa yeyote mwenye FIKRA KUWA MAGUFULI NA TEMESA ni watu smart asome hapa:
Kati ya mwaka 2008 au 2009(sina hakika na muda) hiki kivuko kipya kikubwa kilivyoletwa nchini, wataalam wa kukiunganisha waliestimate assembly time kuwa miezi 5 lkn badala yake ikawa 8.(hoja yangu haiko hapa)

Kwa muda woooote huo wa miezi hiyo ya kuunga ferry mpya, TEMESA hawakuwahi kufikiri ni wapi kitakuwa kikitia nanga. Ni baada ya kivuko kukamilika ndio zikaanza pilika pilika za kutengeneza GATI ya kupaki kivuko kipya kwani ni kikubwa kuliko vile vilivyokuwa vikitumika. Matokeo yake ikawa usumbufu mkubwa wa kuvuka kwani ferry moja ilitumika kuvusha watu na magari na nyingine ilikuwa bize kubeba mawe kwa ajili ya ujenzi wa gati upande wa magogoni. Ikumbukwe wakati huo huo daraja la Mto Kizinga (karibu na Mtongani kama unaenda Mbagala) nalo lilikuwa under construction (KAJIMA) kwa hiyo barabara ilifungwa. Hii ni kudhihirisha uzembe kwani gati zingeweza kujengwa taratibu kwa ferries kubeba mawe usiku taratibu kwa miezi ile ambayo assembling ilikuwa inafanyika. Hili linajirudia tena kwenye vigezo gani vimezingatiwa ktk kupandisha bei ya GUTA na MKOKOTENI. Mimi siamini kama TEMESA na MAGUFULI ndio watu sahihi wa kulifanyia kazi suala hili. Wachumi na Wataalam wa Sayansi ya Jamii ndio walitakiwa walifanyie kazi hili, tuone tofauti ya ukandarasi wa majengo na usimamizi wa huduma za jamii. Si kila sehemu siasa inafaa kutumika
 
1. Kwani mradi wa Mwenge - tegeta unagharimu kiasi gani?....
Hizo barabara za pembezoni ziependekezwa na wataalamu siku nyingi mno, hata kaba Mnyika hakuw mbuge... baadh ya hizo barabara zilinadiwa na JK kwenye kampeni 2010.
Labda ungeangalia gharama za malipo kwa mabanda yaliyojengwa kinyume cha sheria, over 17bn... hizi zingejenga km ngapi?
2. Linashughulikiwa?... ndiyo nini hiyo sasa, mnaomba hela kwa whisani wakati halmashauri inafanya biashara nyingine?
3 na 4. Sheria eeh?...... huo ndiyo ujanja usio na mpango. Watu huenda shule kufundishwa sheria, ukiipitia juujuu unaweza kuchanganya mambo. Tuliza boli.

Wewe unaleta ubishi wa kiswahili wa nani anastahili sifa ya kufanya jambo fulani. Kwani hawa wakurugenzi wa halmashauri wanaripoti kwa Mbunge au kwa aliyewateua?
 
Yupo kwenye halmashauri ya jiji?.. kama yupo, kwanini sheria zinazoruhusu ujenzi holela jijini hazifutwi? Kwanini wananchi wanaokaa mabondeni hawaondolewi?.... kwanini hajatuambia kikao chao kuhusu mafuriko kilisemaje kuhusu wakazi wa jangwani?...... mifereji au wahame? imechwa juujuu mno.
Kuhusu unconstitutionality of ferries act....... Hatuna hata haja ya kwenda huko, let it go cos it's a dumb explanation.

Uamuzi haukua sahihi kivipi? ..... mambo ya kubemelezana ni siasa za kipuuzi. weka X kwenye nyumba, halafu pitisha greda! .... Nairobi wamefyeka maghorofa sita ya nguvu ili flyovers zipite .... sembuse mabanda. Acheni kupigia debe mambo holela ili mpate umaarufu.

Tukimuona mtu anatupa kokwa la embe dodo barabarani...... tumwambie aokote au akamatwe sio akingiwe kifua.
Mkuu, unachokifanya hapa ni upinzani wa jadi tu, hakuna hoja hapo kabisa.

Yupo kwenye halmashauri ya jiji?.. kama yupo, kwanini sheria zinazoruhusu ujenzi holela jijini hazifutwi? Kwanini wananchi wanaokaa mabondeni hawaondolewi?..
Mkuu, ulikuwa uanataka Mnyika afanye miujiza ndni ya miaka miwili? umeona mambo aliyoyahoji kwa uchache hapo kwenye post yake? Labda tukuulize wewe, wabunge wa CCM DSM ndani ya 20yrs wamefanya nini ku-address hayo uliyoyaweka hapo?
Kuwa fair kidogo.

Uamuzi haukua sahihi kivipi? ..... mambo ya kubemelezana ni siasa za kipuuzi. weka X kwenye nyumba, halafu pitisha greda! .... Nairobi wamefyeka maghorofa sita ya nguvu ili flyovers zipite .... sembuse mabanda. Acheni kupigia debe mambo holela ili mpate umaarufu.
Mkuu, unataka kusema Mnyika ndio kakataza walio mabondeni wasiondolewe, au waliojenga barabarani wasivunjiwe? What a CRAP.
Wakati Maghufuli alipopigwa stop na Pinda, kwa nini hukumuwakia Pinda? Kama hufuatilii anayoyafanya Mnyika ni afadhali ukanyamaza kuliko kutoa maneno ya jumla jumla kwenye issue specific na inayojieleza kama hii.
 
Hivi wewe kama Pombe yuko right kwanini asibomoe anamuogopa pinda,ina maana haboi kisheria maana kama anasimamia sheria kwa nini asibomoe?je sheria gani wabunge wa Dar hawazitii?na je unaunga mkono kiongozi wa juu kama Pombe kuwaambia watu wapige Mbizi?je ina maana hata wakijenga daraja ambalo litagharamiwa pesa nyingi watu watakuwa wanatozwa hela japo watavuka kwa miguu,kama sio je hiyo huduma imekaaje kama inazidi kupandishiwa nauli wakati ilitakiwa hata kuwa bure?zaidi fafanua ni wakati gani wabunge wa DAR hawatii sheria na kwanini wanaangaliwa tu?
 
Mnyika nawe kubali sheria zinakupiga chenga,
EWURA,SUMATRA na TICRA ukisoma sheria zao ndo wana mamlaka ya kuitisha mikutano ili kupata maoni ya wadau wote, na wanazunguka nchi nzima kutafuta maoni hayo. Kabla ya hapo TANESCO na TTCL majukumu ya kupandisha bei yalikuwa ni ya waziri husika na hakukuwa na haikuwahi kutoke wananchi wakausishwa ili kutoa maoni. So unaweza kupinga sheria ''mbovu'' ya vivuko lakini ukweli ni kwamba Magufuli anayo mamlaka ya kile amefanya. Halazimishwi kuwauliza wananchi, kwani hiyo nauli ya zamani wananchi waliusishwa?

Na hebu tuwe wakweli, kwani michakato kama ya EWURA na TICRA ya kuwahusisha wananchi unadhani ingefanya nauli isipande? Kwa taarifa yako EWURA wanataka kuhakikisha hizi huduma zinatolewa kwa kiwango cha kujiendesha, so hata kama ingeapply kwa TEMESA nauli ya 200 isingetosha.

Lazima tukubali kama tunataka huduma nzuri tuwe tayari kulipia. Leo hii tuna huduma mbovu za daladala sababu ya nauli kuwa ndogo na hakuna investor anaweza wekeza kwenye hii sekta sababu nyie wanasiasa mnawashawishi watu wasilipie ghalama ili wapate huduma nzuri wakati nyie mnajiongezea posho bila kujali.
Acheni porojo kuweni wakweli.
 
Siasa za bongo zimekuwa Taarab, hata vijana pia wanafata yale yale, we mnyika, achana na mipasho na fanya kazi yako bana. CDM umebaki wewe na Zitto ndio mnaheshimika.
 
DSN rudia kusoma mkuu,hakuna mahali aliposema mh Mnyika na conflict of interest,labda kama unataka kuipandikiza au ni mtizamo wako usio sahihi,kwani Mnyika akikomaa sheria,kanuni na mfumo ukabadilishwa kwa maslahi ya watanzania wote wapi unaona kuna conflict of interest?au wewe nae ni mmoja wa sehemu ya matatizo ya watanzania?kwani alikuambia yeye anataka tenda au anataka kivuko kiendeshwe kwa tenda ili aje ampiganie ndugu yake?ina maana sheria hizo anaona kuna haja ya kuziboresha na sehemu pekee kwake yeye ni bungeni ulitaka amwambie jukwaani kisha sheria au kanuni zingerekebishwa,ku-promise kuwa watakutana bungeni ni sawa kabisa wala hakuna kilichoharibika maana huko ndiko anaweza kushikiza badiliko.ulitaka ahinikize badiliko kwetu wananchi?hapo ina maana tuandamane ambako nako mnatutafasiri vibaya,alichokiahidi Mh Mnyika cha kukutana bungeni ni kauli ya kawaida kabisa ambako mbunge anaweza akapaza sauti ikasikika,hakuna conflict of interest hapo.
Long live mh Mnyika!
 
big up mnyika...your the best...everybody knows that....am proud to have you as our MP.
 
Pamoja na kutoa majibu kwa Mhe.Magufuli, kama haya yote hasa la barabara yangekuwa yameripotiwa kwa wapiga kura wako, leo usingekuwa na haja ya kujieleza hivyo. Tatizo wabunge wa DSM mmeanza kuwa wabunge wa matukio, au wa kujibu mapigo.Sisi wananchi wako tunateseka sana barabara mbovu zisizo na madaraja, hatukupi credit kwa kuandika lengthy explainations, jinamizi la Keenja linaweza likakumeza. For once, tembelea maeneo ya matosa, goba (I"m not sure when was your last visit) kuna kero nyingi that need your attention.
 
Hizo ndo changamoto kiongozi, ndo kwanza mchana kweupeeeee.........:poapamoja sana
 
Utapanuaje hii barabara?
3260462255_5cc8982219.jpg

Kwa kumtumia mkandarasi wa ujenzi wa barabara na kwa kuzingatia tafsiri sahihi ya sheria ya barabara.
 
Utapanuaje hii barabara?
3260462255_5cc8982219.jpg

Ni vyema ukasoma post kabla ya kukurupuka na kujibu. Nimeonyesha kwa kutumia vielelezo vya kisheria kuwa katika barabara ya Morogoro Mhe John Magufuli anazo Mita 30 kila upande toka katikati ya barabara zenye uwezo wa kuzalisha njia mpya (lanes) 9.2 kila upande na kufanya njiia mpya za barabara 18; ni kwanini kila siku anawasumbua wtu waliojenga nyumbza zao nje ya hizo Mita 30 hadi Mita 120? Huo ndio uzushi na upotoshaji anazungumzia Mnyika
 
Pamoja na kutoa majibu kwa Mhe.Magufuli, kama haya yote hasa la barabara yangekuwa yameripotiwa kwa wapiga kura wako, leo usingekuwa na haja ya kujieleza hivyo. Tatizo wabunge wa DSM mmeanza kuwa wabunge wa matukio, au wa kujibu mapigo.Sisi wananchi wako tunateseka sana barabara mbovu zisizo na madaraja, hatukupi credit kwa kuandika lengthy explainations, jinamizi la Keenja linaweza likakumeza. For once, tembelea maeneo ya matosa, goba (I"m not sure when was your last visit) kuna kero nyingi that need your attention.

Wewe hujui majukumu ya mbunge kasome Katiba jukumu la mbunge nikusimamia na kuishauri Serikali. Ni kutokana na wapiga kura kama ninyi mnaotaka wabunge waje kuwatengenezea barabara zenu ndio maana madini na raslimali za Tanzania hazina msimamizi. Wabunge wanatakiwa kutumia muda wao waote wakilinda raslimali kwa maana ya kuisimamia Serikali ili nchi iweze kupata mapato yatakayotumika kutengeneza hizo barabara. Hali hii ya Serikali kukosa usimamizi wa kutosha toka kwa wabunge kwa kuwa wanajitahidi kuwaridhisha wapiga kura wao ikiendelea ufisadi hauwezi kukoma kamwe. Na Mnyika ni mmoja wa wabunge wachache sana wanaotimiza jukumu la kuisimamia Serikali.
 
Sasa tunahitaji vichwa kama hivi kwa taarifa makini na yenye data za kufa mtu acha data za magufuli za kuclaim kichwani amabazo ameandaliwa na katibu tena mbon siku hizi atoi toi zile namba za mabarabara magapi yemetengenezwa au katibu wake wa sasa ni kimeo?Viva Mnyika viva CDM
 
Baraza la Maadili la Kiislamu Tanzania, limelaani kitendo cha kuzomewa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kilichofanywa na baadhi ya wakazi wa Kigamboni, huku likiwaonya pia wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kumshambulia waziri huyo, kutokana na uamuzi wake wa kuongeza nauli ya huduma ya kivuko cha Magogoni-Kigamboni.

Hivi huo uamuzi ni wa Waziri au serikali???

Anyway, ni aibu kwa serikali kudeal na shughuli ndogondogo kama za vivuko na vituo vya mabasi. Ndiyo sababu wanakumbana na vikwazo kama hivi. Kwa mtazamo wango kazi hizo zilitakiwa zifanye na zisimamiwe na local authorities. Ofcourse kutokana na uwezo mdogo wa local authorities nyingi, serikali ilitakiwa tu kuwasaidia kuwawezesha. Kwa jinsi ilivyo sasa serikali imekuwa inatumia too much resources kukusanya kitu kidogo. Hii inamewafanya washindwe kumanage na ndiyo maana watu wa TRA wanakula kilaini.
 
acheni ushabiki wa kisiasa nyie ,comment zenu zote zimeegemea kichadema zaid.magufuli yupo sawa lakini mnyika alijichanganya asitake kulialia hapa ili aonewe huruma na wananchi...mnyika anatakiwa kuomba radhi wananchi tunaomkubali na si kuanza kujitetea kukuda kma anavyofanya,,,,,acheni unazi wa ki CDM vs CCM toeni hoja za msingi....VIVA DR MAGUFULI...ALUTA CONTINUA
 
Mkuu, naomba usisahau kuwapelekea copy wale wazee wa baraza la maadili la kiislam, ili wajaribu kulinganisha taarifa yako kwa umma na tamko lao.
 
Mnyika upo smart sana, lakini tatizo lako mnyika ni mwoga na mwongeaje tuu. Maneno matamu kama asali lakini hatuhitaji wandishi wa habari kwenye mambo yanayo hitaji tough decisions. Ndio maana slaa kakupa kitengo cha kuongea. Nimekua nikikufatilia kwenye mitandao yote ya jamii, mambo mengi ni mipasho.

Mambo mengine yaache kama yalivyo, nenda kashughlikie yale yanayo taka kufa. Ubungo ni jimbo linalo kua kwa kasi, kama tutakwenda kwa mwendo wenu wa wabunge wa DSM hatuta fika mkuu. Kama ungejua watu makini wameuchukulia uamuzi wa Magufuli kuwa makini hata usingetumia muda wako kutueleza umahili wako wa lugha.

Magufuli anacho fanya kipo sahihi kabisa na hajakurupuka. Maneno yako mengi hayata rudisha nauli iwe 200 na wala kushinda kwako hapa jf hakuta saidia chochote. Cha msingi onyesha uongozi kwa vitendo na sio longolongo. Nnchi hii kwa sasa tunahitaji kina Magufuli hata 200, ili tuweze kutoka ktk umaskini tulio nao.
 
Back
Top Bottom