The Tomorrow People
JF-Expert Member
- Jul 11, 2013
- 2,662
- 2,744
Katika kile ambacho wachunguzi wa mambo ya kisiasa wamekiita tukio la kimapinduzi na mwanzo wa mabadiliko mapya ndani ya CCM, Mgombea wa Urais kwa ticket ya CCM Dr. John Magufuli amefanya kile ambacho Rais Jakaya Kikwete na Edward Lowassa wameshindwa, kumtosa Andrew Chenge hadharani.
Mwanasheria huyo mkuu wa zamani ambaye anahusika kwenye kashfa mbalimbali zilizozikumba taifa hili, ambaye ndio alikuwa mratibu wa kampeni za Urais za Edward Lowassa alipokuwa CCM alijikuta kwenye wakati mgumu leo pale ambapo Dr. Magufuli alipogoma kumpandisha jukwaani na kumkabidhi ilani ya CCM kama anavyofanya kwenye majimbo mengine. Magufuli ambaye mpaka sasa ameweka wazi adhma yake ya kuanzisha Mahakama ya Mafisadi, inasemekana aliweka msimamo wake wazi mbele ya Mwenyekiti wa kampeni za CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwamba hana mpango wa kuwanadi wana CCM wowote ambao wana kashfa za ufisadi, na amepewa baraka zote za kukisafisha Chama cha Mapinduzi ili kuonyesha tofauti na mgombea wa UKAWA ambaye ana kashfa lukuki za ufisadi.
Tukio hili la leo linaelezewa na wachambuzi wa Siasa kama mwanzo mzuri wa Magufuli kujitofautisha na makada wa CCM wasio wasafi na kurejesha imani ya Watanzania kwamba yeye ndio atakayeleta mabadiliko bora zaidi kwa Wananchi.
Itambuliwe pia, Dr. Magufuli amefanya kazi katika awamu zote mbili za Rais Mkapa na Kikwete na hajapata kashfa yoyote, tofauti na mgombea wa UKAWA ambaye kwa kipindi cha miaka 40 aliyokuwa ndani ya CCM amepata kashfa lukuki ikiwemo ya Richmond, Ranchi za serikali, na kwa sasa kuna sintofahamu kubwa kuhusu kauli zake za kuomba kura- kanisani na hali yake ya kiafya.
Kwa sasa Dr. Magufuli amefaulu kizingiti hiki kikubwa cha Mheshimiwa Chenge, na kugoma kwake kumnadi kunatuma ujumbe kwa wale mafisadi wote wa ndani na nje ya chama kujipanga kwani anaonekana ana nia ya dhati kusafisha Chama na Serikali ili kuwapa Watanzania mabadiliko chanya wanayoyahitaji.
HAPA NI KAZI TU.
Mwanasheria huyo mkuu wa zamani ambaye anahusika kwenye kashfa mbalimbali zilizozikumba taifa hili, ambaye ndio alikuwa mratibu wa kampeni za Urais za Edward Lowassa alipokuwa CCM alijikuta kwenye wakati mgumu leo pale ambapo Dr. Magufuli alipogoma kumpandisha jukwaani na kumkabidhi ilani ya CCM kama anavyofanya kwenye majimbo mengine. Magufuli ambaye mpaka sasa ameweka wazi adhma yake ya kuanzisha Mahakama ya Mafisadi, inasemekana aliweka msimamo wake wazi mbele ya Mwenyekiti wa kampeni za CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwamba hana mpango wa kuwanadi wana CCM wowote ambao wana kashfa za ufisadi, na amepewa baraka zote za kukisafisha Chama cha Mapinduzi ili kuonyesha tofauti na mgombea wa UKAWA ambaye ana kashfa lukuki za ufisadi.
Tukio hili la leo linaelezewa na wachambuzi wa Siasa kama mwanzo mzuri wa Magufuli kujitofautisha na makada wa CCM wasio wasafi na kurejesha imani ya Watanzania kwamba yeye ndio atakayeleta mabadiliko bora zaidi kwa Wananchi.
Itambuliwe pia, Dr. Magufuli amefanya kazi katika awamu zote mbili za Rais Mkapa na Kikwete na hajapata kashfa yoyote, tofauti na mgombea wa UKAWA ambaye kwa kipindi cha miaka 40 aliyokuwa ndani ya CCM amepata kashfa lukuki ikiwemo ya Richmond, Ranchi za serikali, na kwa sasa kuna sintofahamu kubwa kuhusu kauli zake za kuomba kura- kanisani na hali yake ya kiafya.
Kwa sasa Dr. Magufuli amefaulu kizingiti hiki kikubwa cha Mheshimiwa Chenge, na kugoma kwake kumnadi kunatuma ujumbe kwa wale mafisadi wote wa ndani na nje ya chama kujipanga kwani anaonekana ana nia ya dhati kusafisha Chama na Serikali ili kuwapa Watanzania mabadiliko chanya wanayoyahitaji.
HAPA NI KAZI TU.