Kwa ile nyomi ya Uwanja wa Tanganyika jana, wapinzani wajipange sana. Kigoma ni moja ya mikoa ya kwanza kupokea upinzani. Sijui wataenda nao mbele kwa umbali gani, maana siasa za sasa ni za kuwashika mkono walio wengi na wakiamua watakusambaratisha...wapiga kura halali
Aisee, sijui alijisikiaje jamaa. Na Mkulu anapenda wapinzani wa dizaini hii, wanaohujumu vyama vyao kwa maslahi mapana ya CCM. Ndiyo maana Zitto aliitwa mpinzani mzalendo na yule wa Kakonko "kambunge ka CHADEMA"
Kwa maelezo aliyoyatoa Jana Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi JPM kwa mbunge wa kaliua -CUF Magdalena Sakaya, Je ni Sahihi Chama cha wananchi CUF kuendelea na mbunge huyo? Je sakaya ni mpinzani wa kweli? Kubaki na mwanachama wa aina hiyo ni athari gani chama kinaweza kupata?
Tukumbuke sakaya ktk bunge lililopita amepigia kura ya ndio bajeti ya serikali kinyume na msimamo wa Vyama vya upinzani.
Sakaya katika jimbo lake hakuna diwani wa CUF hata mmoja.
Hivi nyie upinzani mnauelewaje? Mbona ni mazuzu kiasi hicho? Sasa mlitaka jpm awaambie ccm wasishirikiane na sakaya na hapo hapo aseme analeta maendeleo kweli! Aise upinzani hapa bongo ni uadui kila kitu wao ni kupiga na kuponda tu. Kwa misingi hii bora vyama vya upinzani vifutwe mana havina nia nzuri bali kukwamisha lolote lisifanikiwe
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.