Magufuli aufufua mradi utakaoweza kusambaza umeme Afrika Mashariki nzima!

Cicero

JF-Expert Member
Jan 20, 2016
2,924
3,072
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia wananchi wa mkoa wa pwani kwamba serikali ya awamu ya tano imejipanga kuhakikisha kwamba miradi mikubwa ya maendeleo yenye manufaa kwa mkoa huo na taifa kwa ujumla inatekelezwa kama alivyoahidi.

Mhe. Rais ameitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa reli ya kati, ujenzi wa barabara njia sita Dar-Chalinze na ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge) ambao mipango ya ushirikiano katika utekelezaji na Ethiopia imeshaanza.

NOTE: Kwa msiofahamu mradi wa Stiegler's Gorge ni moja ya key priority projects zilizotajwa kwenye East African Power Master Plan. Huu mradi, pamoja na mingine ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia, utaiwezesha Tanzania kuwa power house ya Afrika Mashariki, ukizingatia kwamba grid za umeme za mataifa ya Afrika Mashariki sasa zimeunganishwa tayari.
Mradi utazalisha hadi MW 2100 za umeme, ambazo ni zaidi ya umeme wote unaozalishwa hapa Tanzania kwa sasa.

Viva JPM Viva Tanzania na Viva EAC!
 
HUU MRADI UMEKUWA UNAPIGWA VITA SANA MDA MREFFU SIJUI JPM KAMA ATAWEZA KUKAMLISHA HII NDOTO. WAZUNGU HAWAUPENDI NA WATAKUJA NA HADITH ZA MAZINGIRA NA BLABLA NYINGI.ILA KIUKWELI WAKIUWEKEA MPANGO MZURI LILE IKIWA NA MIUNDO MBINU YA UMWAGILIAJI LILE BODE LINATOSHA KUONDOA NJAA TANZANANI


Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia wananchi wa mkoa wa pwani kwamba serikali ya awamu ya tano imejipanga kuhakikisha kwamba miradi mikubwa ya maendeleo yenye manufaa kwa mkoa huo na taifa kwa ujumla inatekelezwa kama alivyoahidi.

Mhe. Rais ameitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa reli ya kati, ujenzi wa barabara njia sita Dar-Chalinze na ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge) ambao mipango ya ushirikiano katika utekelezaji na Ethiopia imeshaanza.

NOTE: Kwa msiofahamu mradi wa Stiegler's Gorge ni moja ya key priority projects zilizotajwa kwenye East African Power Master Plan. Huu mradi, pamoja na mingine ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia, utaiwezesha Tanzania kuwa power house ya Afrika Mashariki, ukizingatia kwamba grid za umeme za mataifa ya Afrika Mashariki sasa zimeunganishwa tayari.
Mradi utazalisha hadi MW 2100 za umeme, ambazo ni zaidi ya umeme wote unaozalishwa hapa Tanzania kwa sasa.

Viva JPM Viva Tanzania na Viva EAC!
 
Akamate magaidi wanaouwa ndugu zetu katika wilaya za Mkuranga, kibiti na rufuji kwanza.
 
Tuliambiwa mradi Wa Kinyerezi ungeondoa tatizo LA umeme. Mbona sioni matunda na mmeanza na kiki Nyingine ?
 
Tuliambiwa mradi Wa Kinyerezi ungeondoa tatizo LA umeme. Mbona sioni matunda na mmeanza na kiki Nyingine ?
Mkuu unamaanisha tatizo lipi labda?
Maana tatizo kubwa zaidi lilikuwa ni Mgao wa Umeme ambao kwa Sasa umepunguzwa sana kama sio kuondolewa kabisa.
 
Huo umeme mtautumia wenyewe? AU haujui Tanzania peak demand ya umeme bado ni ndogo mno kwa sasa?
Kama sera ya viwanda itatekelezwa ipasavyo, bado umeme wa Stiegler hauwezi kutosheleza mahitaji miaka 10 baada ya kukamilika. Mfano, vikijengwa viwanda vipya vya saruji hata 5, huo umeme unaweza usitoshe. South Africa ina idadi sawa ya watu na sisi, lakini wao wanazalisha umeme ambao ni mara 25 ya ule tunaozalisha na bado wanakuwa na mgao wa umeme.

Kwahiyo programu za REA na Viwanda, zitaumeza huo umeme hata kabla haujakamilishwa.
 
Fikiria kinachowezekana kwa sasa...
Ndio mambo ya kufanya vitu nusunusu badala ya kufanya kwa maramoja kiishe, tunadonoa kidogo mahitaji yakiongezeka tunadonoa tena kidogo, mwisho wa siku tunatumia gharama kubwa kuliko tungekifanya kwa ukamilifu tangia mwanzo
 
Back
Top Bottom