MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 20,897
- 63,408
Siku hizi sichangii kabisa siasa, lakini naomba nikuulize: Hivi umekutwa na nini ???Kosa moja kubwa alilofanya ni kuminya demokrasia na kukataza watu kumpa challenge kwa muda wote wa uongozi. Angekuwa ameruhusu watu kuampa changamoto ya kukosoa na kukoselewa angekuwa amejifunza mengi na kupata uzoefu. Unajua kwenye mijadala siku zote bila kushiriki inakuwa ngumu kujifunza hasa ikizingatiwa yeye hana kipaji cha kutoa hoja.
Mtu kama Membe na Lissu wanaweza kumshinda vibaya sana kwenye hoja na ndiyo maana Membe anajiamini sana. Na kingine ni kuwa ndani ya CCM amejeruhi wengi kutokana na tabia yake ya ubabe na kutotaka ushauri na challenge. Hayo mahojiano aliyofanya Membe na Mwanahalisi ndiyo yamenifungua akili kwani kama mpaka Dr Bashiru alikuwa anataka kujiuzulu basi inaonyesha Magufuli anawapelekesha sana.
Japo najua mategemeo yake yote ameyaweka kwenye dola kumbeba lakini hata hivyo ana wasiwasi sana kwani anajua wengi ndani ya CCM wanaona hafai.
Kile kiburi, kashfa na kejeli ulizokuwa unawatolea watu hapa kisa mahaba na Raisi viko wapi ?