Elections 2015 Magufuli asema Mafisadi wanamwogopa ndio maana hawataki aingie Ikulu

Asahau kuingia ikulu hatuwezi kumpeleka ikulu mtu mropokaji na mwenye kujaa mihemko

kiongozi lazima awe na hekima

Mbona ukawa mna mihemko ila hatusemi? Tena mihemko haswaaaaa yenye mahaba na yule mlikuwa mnaambiwa ni fisadi mpaka gia ilipobadilika angani?
 
Eti mafisadi wananiogopa!!!Kwani nchi ina mafisadi wangapi??Nani mwl wa hao anaowaita mafisadi km sio chama chake??
LENGO LETU SIO KUCHAGUA FISADI BALI NI KUIONDOA CCM MADARAKAN NA HILI LIKISHINDIKANA BASI NITAAMINI KABISA MANENO YA MH BEN MKAPA KUWA SISI NI MALOFA,wapumbavu na MAMBUMBUMBU!

Jiongelee mwenyewe ndugu, usiseme sisi, dunia hii kila mtu anaingia kivyake na anatoka kivyake hata pacha wako hamjaingia pamoja hata kama mmezaliwa siku moja. We subiri kupiga kura mwenye kushinda akabidhiwe kiti maisha yaendelee nini kulumbana bila hoja za msingi?
 
Katika orodha ya wenye hekima Lowasa do ndiyo wa mwisho? Kung'ang'ania kuwa rais ni kukosa hekima tena ni dharau na chuki kwa viongozi waliomlea Lowasa na asivyo na hekima akishindwa kwenye kura atakataa na wafuasi wake watasababisha damu imwagike kwani hata sasa wana mihemko na wamekosa busara na ni waropokaji.

tulia wewe gamba hekima unaijua wewe? LOWASSA NDIO RAIS WAKO
VIVA UKAWA!!!
 
Alivyokua anaongea hayo alijijumuisha na yeye mwenyewe? RAIS NI LOWASSA
VIVA UKAWA!!!
 
Magufuli kitu ambacho inatakiwa akitamke ni Kurudisha katiba ya wananchi hapo inamuongezea credit sasa hivi hata kweye mikutano anasema Magufuli Oye anataka kuwa sahaulisha habari ya CCM.
 
Wanamuogopa sana humuoni Lowasa anavyohangaika anajua kiboko wa mafisadi anakuja.
Akisimama na kutamka wazi kwamba ata mshughulikia kikamilifu Rais kikwete na genge lake kwa kulifikisha taifa hapa lilipo fikia leo hii nitampigia kura yangu ya " NDIO"
 
Wasalaam, kumekua na tetesi huku kwetu shinyanga kwamba rais wetu na serikali ya wanyonge ya awamu ya tano wanaogopa kuwachukulia hatua mafisadi papa ili hali mahakama ya mafisadi imejengwa nakukamilika ikigharimu mabilioni ya wavuja jasho wa Tanzania.

Inasemekana mafisadi wote waliolitia hasara taifa hili wapo ccm na kitendo cha kuwagusa itakisambaratisha chama cha mapinduzi. Watu wanahoji wakinukuu kauli ya mh rais magufuli alioitoa ktk kampeni 2015 na katika hotuba zake baada ya kuapishwa kwamba, nanukuu" MAFISADI WAMEKIMBILIA CHADEMA/UPINZANI" mwisho wa nukuu.

Sasa swali linabaki je kama kweli mafidi wapo upinzani kwanini wasikamatwe na kupelekwa mahakama ya mafisàdi na hatimae wafungwe segerea? Je hizi tetesi kwamba mafisadi wote wapo ccm tena ni vigogo wakubwa na hawagusiki zina ukweli wowote?

Naomba kuwasilisha.
 
Mbona kama vile una delayed milestones...yaani huu mjadala tulishaujadili humu ...hebu chukua muda wa kupitia threads za JF kabla ya kupost
 
Mafisadi lazima washughulikiwe kwanza kwa ufisadi wao na pili kwa kutomchagua jembe...ha ha ha
 
Mafisadi lazima washughulikiwe kwanza kwa ufisadi wao na pili kwa kutomchagua jembe...ha ha ha
Nani kakwambia mafisadi wanapendana, wezi hawateteani. Mwizi akikamatwa ni wezi wenzake ndio huwa mstari wa mbele kumpa kisago. Mafisadi nao humuogopa fisadi mwenzao anaposukumiziwa uongozi, hamna la kushangaza hapo
 
Nani kakwambia mafisadi wanapendana, wezi hawateteani. Mwizi akikamatwa ni wezi wenzake ndio huwa mstari wa mbele kumpa kisago. Mafisadi nao humuogopa fisadi mwenzao anaposukumiziwa uongozi, hamna la kushangaza hapo
Vyovyote unavyotafsiri lakini Magufuli anawanyoosha mafisadi vilivyo
 
Vyovyote unavyotafsiri lakini Magufuli anawanyoosha mafisadi vilivyo
Ni kweli anawanyosha, ndio maana kwa mara ya kwanza trilioni imeyeyuka hivi hivi under his watch...ni kutesa kwa zamu!
 
Back
Top Bottom