Duh, naona mpaka umepata aibu. Hizi mbinu za zama za mawe zimepitwa na wakati. #HapaKaziTuHao ni wananchi ambao hawaitaki CCM na wala siyo wafusi wa Lowassa. muwe mnaripoti vizuri.
Na pia hiyo picha ya hao waangalizi wa EU haikupigwa TZ. Uongo mwingine ni wa kitoto sana.Halafu hii video ni ya Mbeya wakati ambapo European Union observers walikuwa hawajaanza kuangalia uchaguzi. hii ni sawa na yule aliyeweka picha za guinea akidai ni za arusha.
Na pia hiyo picha ya hao waangalizi wa EU haikupigwa TZ. Uongo mwingine ni wa kitoto sana.
Huyu Magufuli anajifanya kama ana uwezo wa kuibadilisha CCM. Hataweza kubadilisha kitu. Ifike wakati tupate akili japo kidogo. Eti umati wa watu wote hao wamenunuliwa kumzomea. Kweli? Ni watanzania wangapi wanafia hapo Mhimbili bila hata panadol! Kwa nini? Inakuwaje wanapokufa kina Kombani hufia India? Ni watoto wangapi wanasoma shule hawana kitabu, dawati, mwalimu, chaki, library, penseli, nk. Hivi mnafikiri ni kwa nini? Tembo walikuwepo Tanzania tangu kuumbwa kwa dunia. Wamevunwa chapuchapu. Miaka mitano asilimia karibia 70 imeshayeyuka. Ni nani amechukuliwa hatua hata kuulizwa swali hata kama dunia yote inapiga kelele? Mnafikiri ni kwa nini? Viongozi wa CCM wameongozana juzi juzi kugawana kodi ya watanzania kwa marambo. Kelele zikapigwa weee! Leo tunaambiwa tusahau tu eti CCM inabadilishwa na Magufuli! Watanzania wakizomea mnakuja na story. Kweli? Wamama wanakufa wakijifungua na kupoteza watoto kwa mamia. Bado hadith hizi haziishi. Viongozi wanakimbizana kuzunguka dunia nzima eti wanaaga. Kweli? Unaweza kutumia kodi ya watu ambao hawana hata panadol ya kutuliza maumivu ya kansa kujitembeza kila upande kuaga. Unamwaga nani? Wao wanapomaliza madaraka yao wanakuja kwako kuaga? Inafika mahali hawa wadanganyifu wazomewe. Tena wazomewe sana kwani wameiachia nchi kuwa shamba la bibi huku wakisahau hata kuwapatia wananchi angalao panadol kwenye hospitali za umma.Sikatai upinzani wana mapungufu yao. Acha tuangalie upande mwingine. Labda tutaweza kusimamisha biashara haramu kwenye mbuga zetu na kuserve hao wanyama wachache waliobaki. Labda watahakikisha angalao wazee, wamama, na watoto wana hata kidonge cha kutuliza maumivu. Lada elimu yetu itarudi mahali pake. Ladba kilimo ambacho ni uti wa mgongo kitapatiwa kipaumbele. Labda heshima ya Tanzania ambayo imepotea kabisa itarudi. Labda tutachagua viongozi na sio kuridhishana toka kwa wazazi kwendaa kwa watoto hata kama ni wauza madawa ya kulevya. Ladba gasi na mafuta yetu yatafanyiwa mikataba ya maana na sio deals za wachina na marafiki wa viongozi. Tumechoka sana na CCM na kilichobaki ni kuzomea maana ahadi ni zilezile na hakutakuwa na mabadiliko yeyoye yale. Mzee ana miaka 54 eti unatoka bila haya mimi mwanangu nitambadili kabisa atakuwa sijui mwema na mtakuwa na viwanda na sijui nini. Kweli? Viwanda? Makampuni feck yanawaibia watanzania, elimu, barabara hakuna, kina kitu chini ya viwango. Tuseme hapana tena hapana kwa nguvu zote.
Hakuna kazi yeyote itakayofanywa na CCM. Propanda hizi zimedumu miaka zaidi ya 50 na watanzania bado sana tu wanalia. Kama unategemea mabadiliko yaletwe na CCM utangoja sana. Eti hapa kazi tu ni barabara ipi ya maana aliyojenga Magufuli? Tuache ushabiki wa kijinga. Tunalia huku tukishabikia vitu ambavyo viko wazi kabisa kwamba havitakaa vifanyike. CCM ni ile ile. Endeleeni kushabia, ila haitachukua muda kabla hamjaleta kilio chenu hapa. Ona Kombani amekufa. Wanamweka nani badala yake? Msigwa alipokufa ni nani aliwekwa badala yake? Ni nani mbunge wa Chalinze? Escrow na mambo yake mmeshasahau kisha tu fulana na kanga za njano. Hakuna kazi hapa. CCM itaendelea kuwahadaa watanzania hadi tupate akili na tuache kushabikia ujinga.
Weka nyama kidogo, wengine hatuwezi kudownload video humu JF.