Magufuli ang'ara kwenye Sekta ya Kilimo. Hongera sana CCM

Amani Msumari

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
1,830
976
Wanajamvi. Amani kwenu

Leo ni siku nyingine ya kutafakari utendaji mzuri wa Rais Magufuli na serikali yake katika kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 - 2020. Leo tuangalie Sekta ya Kilimo.

Katika jitihada za kuendeleza kilimo, kuliundwa dirisha la kilimo katika Benki ya Uwekezaji (TIB). Akiwa katika miaka yake ya mwisho, mzee Kikwete aliunda benki ya Kilimo. Katika kipindi hiki cha miaka mitano, Rais Magufuli ameendelea kuiimarisha benki ya Kilimo.

Sekta ya Kilimo ni sekta iliyoajiri watanzania wengi zaidi. Ni sekta kubwa. Ninaomba Leo niongelee benki ya Kilimo. Kwa kutambua kuwa wakulima wengi hawakidhi vigezo vya kukopesheka katika mabenki ya biashara, kwa makusudi serikali imeweka utaratibu maalimu wa kuwakopesha wakulima, utaratibu ulio tofauti kabisa na mabenki ya biashara.

Wakulima wadogowadogo wenye mashamba yenye ukubwa wa heka 1 - 50 wanaunda kikundi cha watu 5 - 30. Serikali inawakopesha fedha kw ajili ya kuendeleza kilimo. Fedha inatoka kwa awamu na timu ya Kilimo ya wilaya chini ya afisa kilimo anafanya ufuatiliaji.

Nitatoa mfano wa wakulima wa mihogo wilayani Handeni mkoani Tanga. Hapa vikundi vingi vimepata mikopo na kazi inaendelea. Wakulima wanapata shilingi 1,500,000 kwa heka moja. Fedha hii inatoka kwa awamu kuanzia kuandaa shamba, pembejeo, upandaji, upaliliaji, uvunaji na usafirishaji. Rejesho linafanywa baada ya mavuno kuuzwa. Hii sio hadithi, ni mambo halisi yanayotokea. Mpaka Sasa shilingi bilioni 3.6 zimeshakopeshwa kwa wakulima wilayani Handeni. Hali iko hivi maeneo mengine ya Tanzania.

Nawashauri watanzania wenzangu kufika ofisi za kilimo zilizopo karibu nanyi mpate maelezo ya kina nanyi mfaidike.

Nimelazimika kuandika haya kwasababu mnaulaumu tuu, mnasema hakuna kilichofanyika kwenye kilimo. Tatizo hamfuatilii mambo mnaulaumu tuu huku mkiwa hamna taarifa sahihi.

Mambo yameanza kunoga, mambo yameanza kukaa sawa Ila ni lazima tuwe na subira, Roma haikujengwa ndani ya siku moja. Tinaposema JPM 5 tena, ni mambo kama haya yanayotupa nguvu.

Hongera JPM
Hongera serikali
Hongera CCM

JPM mitano tena #achakaziiendelee
 
Nenda Mtwara na Lindi ukawaambie kuhusu kilimo cha korosho , halafu ukishatoka huko nenda kaangalie kiasi cha pesa kilichotengwa kwa ajili ya wizara ya kilimo tangu awamu ya 5 ilipoingia .

Unajua sehemu kama hii JF si ya kuletea porojo hata kama umelipwa .
Hususani ikiwa ni sehemu pekee iliyojaa wapiga kura wa Lisu!

Lisu akipata walau kura 20% nipigwe ban ya maisha hapa jf
 
Hapo ndipo tatizo lenu lilipo, kupinga kila kitu na kushindwa kuelewa uhalisia wa mambo.
Changamoto zipo, hilo sijakataa. Pili nimeandika kuwa Roma haikujengwa ndani ya siku moja. Hatua zilizofikiwa zinaonesha mafanikio. Nometoa mfano wa sehemu husika, bado mnapinga. Nyie watu vipi? Mnafikiri tunaweka kuwa Kama Ubelgiji ndani ya miaka mitano tuu?
 
Nakushauri uishie humuhumu kwenye ID fake. Ukienda vijijini kuropoka huu uharo wako tutaletewa TANZIA tu humu.
Mkuu washauri wakulima unaowafahamu wapate maelezo juu ya kazi ya benki ya Kilimo na hatua gani wanapaswa kufuata

Infact hata wewe unaweza kuwa mkulima mzuri tuu
 
Una shamba? Umeshawahi kufika benki ya Kilimo?
Bank ya kilimo hii iliyofirisika baada ya magufuli kuiambia itoe hela ipeleke kwenye korosho au ipi???

Mimi ndio ni mkulima wa Mahindi na maguful katusababishia umasikini mkubwa wakulima wa mahindi kutokana na kutupiga marufuku kuuza mahindi nje. Tumepata hasara sana na kukumbwa na umasikini wa kutupwa maana debe moja tuliuza hadi 1000 kwenye local market wakati pembejeo zilitugharimu sana
 
Bank ya kilimo hii iliyofirisika baada ya magufuli kuiambia itoe hela ipeleke kwenye korosho au ipi???

Mimi ndio ni mkulima wa Mahindi na maguful katusababishia umasikini mkubwa wakulima wa mahindi kutokana na kutupiga marufuku kuuza mahindi nje. Tumepata hasara sana na kukumbwa na umasikini wa kutupwa maana debe moja tuliuza hadi 1000 kwenye local market wakati pembejeo zilitugharimu sana
Kilimo hakiendeshwi kisiasa. Pamoja na changamoto hizo lakini tambua kulikiwa na sababu za msingi za kukataza kuuza mahindi nje ya Tanzania. Tangu kipindi hicho, umewahi kusikia Tanzania ina njaa?

Changamoto zipo na zinafahamika na kushughulikiwa
 
Back
Top Bottom