Magufuli anawa-prove wrong waliodai tatizo ni mfumo na sio mtu

Muwindaji

JF-Expert Member
Feb 28, 2015
245
206
Mfumo ni muunganiko wa muundo, njia zilizowekwa na watu(au sheria) katika kutatua shughuli flani, kufanya kazi fulani na kuhakikisha jambo fulani linafanyika kama linavyotakiwa lifanyike.

Mfumo unabeba watendaji, wasimamizi na viongozi ambao kazi yao inakua ni kuhakikisha mambo yanakwenda sawa kama yalivyowekwa.

Mfumo unaweza ukawa halali au sio halali.

Kitendo cha watendaji fulani, kutengeneza mfumo wa kujinufaisha wao kinaweza kuhesabika kwamba watendaji hao wametengeneza mfumo usio wa halali.

Kipindi cha kampeni, kundi fulani la upinzani(UKAWA) walisikika wakisema kua, hata aingie nani hatoweza kuleta mabadiliko kwasababu hatoweza kubadilisha mfumo uliokuwepo(Mfumo usio wa halali).

Inakua ngumu kukataa kwamba kuna udhaifu mwingine wa kimfumo unasababishwa na kuwepo kwa sheria zenye utata, yaani zinazoshindwa kutibu matatizo yaliyopo sasa, na hata Katiba ya sasa ni chanzo cha baadhi ya mfumo mbovu mfano: kama pale waziri anapoteuliwa kutoka kwenye ubunge na hii inaharibu mfumo mzima wa kazi ya bunge kuisimamia serikali ipasavyo, ni mfano.

Wapinzani walijisahau kwamba mfumo ambao wanauona hauwezi kutoa raisi mzuri kwa asilimia kubwa ni mifumo isiyo ya halali, na inaweza kutibika barabara.

Na hivyo wakawaaminisha watanzania kwamba, hata Magufuli akiingia hatofanya lolote kwasababu ya mfumo uliokuwepo umeoza. Na wakasahau kwamba mfumo unajieleza vizuri, isipokua mfumo ulikosa msimamizi mzuri wa kuufanya ulete tija kwa wananchi.

Magufuli endelea kufanya kazi, endelea kutoa tiba kwa mfumo uliokuwepo na kukata mifumo yote haramu iliyotengenezwa ndani ya mifumo halali.

Tatizo lilikua ni mtu, na sio mfumo.
 
Mfumo ni muunganiko wa muundo, njia zilizowekwa na watu(au sheria) katika kutatua shughuli flani, kufanya kazi fulani na kuhakikisha jambo fulani linafanyika kama linavyotakiwa lifanyike.

Mfumo unabeba watendaji, wasimamizi na viongozi ambao kazi yao inakua ni kuhakikisha mambo yanakwenda sawa kama yalivyowekwa.

Mfumo unaweza ukawa halali au sio halali.

Kitendo cha watendaji fulani, kutengeneza mfumo wa kujinufaisha wao kinaweza kuhesabika kwamba watendaji hao wametengeneza mfumo usio wa halali.

Kipindi cha kampeni, kundi fulani la upinzani(UKAWA) walisikika wakisema kua, hata aingie nani hatoweza kuleta mabadiliko kwasababu hatoweza kubadilisha mfumo uliokuwepo(Mfumo usio wa halali).

Inakua ngumu kukataa kwamba kuna udhaifu mwingine wa kimfumo unasababishwa na kuwepo kwa sheria zenye utata, yaani zinazoshindwa kutibu matatizo yaliyopo sasa, na hata Katiba ya sasa ni chanzo cha baadhi ya mfumo mbovu mfano: kama pale waziri anapoteuliwa kutoka kwenye ubunge na hii inaharibu mfumo mzima wa kazi ya bunge kuisimamia serikali ipasavyo, ni mfano.

Wapinzani walijisahau kwamba mfumo ambao wanauona hauwezi kutoa raisi mzuri kwa asilimia kubwa ni mifumo isiyo ya halali, na inaweza kutibika barabara.

Na hivyo wakawaaminisha watanzania kwamba, hata Magufuli akiingia hatofanya lolote kwasababu ya mfumo uliokuwepo umeoza. Na wakasahau kwamba mfumo unajieleza vizuri, isipokua mfumo ulikosa msimamizi mzuri wa kuufanya ulete tija kwa wananchi.

Magufuli endelea kufanya kazi, endelea kutoa tiba kwa mfumo uliokuwepo na kukata
 
Sasa sijui watwambie huu wa leo uliopo ni imported? walikutana na wahuni tu
 
Tatizo ni mfumo mbovu wa ccm, magufuli akitaka mafanikio awaondoe viongoz wote wa ccm madarakani
 
Bado mapema Hii post ungeileta mwaka 2017 ningekuwa na cha kuchangia, sasa Magufuli amemaliza mwezi unasema ameprove wapinzani wrong? Furahia matokeo sio mchakato
 
On the contrary Magufuli anathibitisha tatizo ni mfumo !

Kwa mfumo wa nchi hii na katiba iliyopitwa na wakati, Rais ana mamlaka makubwa na ana uwezo mkubwa (akitaka) kubadilisha mambo......Katika hali hiyo hiyo Rais akiwa mbaya anaweza akayatumia mamlaka hayo hayo (akitaka) kuharibu na kuifanya hii nchi kama mali yake binafsi kwa kiwango kikubwa.....

Tunapoongelea mfumo ni kuweka utaratibu ambao kwa kiwango kikubwa unapunguza utegemezi wa nchi kwa mtu bali kwa vitu vingi iwezekanavyo utegemezi unakuwa kwa taasisi zilizowekwa kikatiba. Hii inasaidia kwamba hata kama atachaguliwa Rais ambaye si mzuri sana bado unaweza kukuta anaweza kuaffect (negatively) lets say kama 30% tu kwani unakuta 70% zinakuwa handled na taratibu zilizowekwa kikatiba....na akipatikana Rais mzuri ataweka mambo vizuri kwa hiyo 30% kwani tayari 70% is guaranteed.....

Sasa hivi tukipata Rais mzuri, then anatu-affect (positively) kwa almost 100% na tukimpata mbaya anatu-affect (negatively) kwa almost 100%......hicho ndio tunachotaka kukiondoa !. Kama unakumbuka Mkapa alijitahidi sana kuimarisha uchumi, kubana matumizi ya serikali, akalipa hata madeni na wakati anaondoka alimwachia Kikwete nchi ikiwa na akiba ya kutosha.....Kikwete pamoja na kufanya mambo mengine, lakini kwa upande huo amerudisha juhudi za Mkapa nyuma ! Je unataka baada ya Magufuli kuondoka (kama tukimpata Rais hovyo) tuanze kurudi nyuma tena ? By the way Magufuli hana mkataba na Mungu wa kuishi mpaka mwisho wa muda wake wa kuwa Rais, anaweza akafa hata kesho !

Elewa tunapozungumzia kubadilisha mfumo, tunataka kuondoa utegemezi wa nchi (kwa kiwango kikubwa) kwa mtu mmoja au watu wachache bali kwa taasisi imara zilizowekwa kikatiba......hivyo ndio nchi zinazojielewa zilivyo !

Mfumo ni muunganiko wa muundo, njia zilizowekwa na watu(au sheria) katika kutatua shughuli flani, kufanya kazi fulani na kuhakikisha jambo fulani linafanyika kama linavyotakiwa lifanyike.

Mfumo unabeba watendaji, wasimamizi na viongozi ambao kazi yao inakua ni kuhakikisha mambo yanakwenda sawa kama yalivyowekwa.

Mfumo unaweza ukawa halali au sio halali.

Kitendo cha watendaji fulani, kutengeneza mfumo wa kujinufaisha wao kinaweza kuhesabika kwamba watendaji hao wametengeneza mfumo usio wa halali.

Kipindi cha kampeni, kundi fulani la upinzani(UKAWA) walisikika wakisema kua, hata aingie nani hatoweza kuleta mabadiliko kwasababu hatoweza kubadilisha mfumo uliokuwepo(Mfumo usio wa halali).

Inakua ngumu kukataa kwamba kuna udhaifu mwingine wa kimfumo unasababishwa na kuwepo kwa sheria zenye utata, yaani zinazoshindwa kutibu matatizo yaliyopo sasa, na hata Katiba ya sasa ni chanzo cha baadhi ya mfumo mbovu mfano: kama pale waziri anapoteuliwa kutoka kwenye ubunge na hii inaharibu mfumo mzima wa kazi ya bunge kuisimamia serikali ipasavyo, ni mfano.

Wapinzani walijisahau kwamba mfumo ambao wanauona hauwezi kutoa raisi mzuri kwa asilimia kubwa ni mifumo isiyo ya halali, na inaweza kutibika barabara.

Na hivyo wakawaaminisha watanzania kwamba, hata Magufuli akiingia hatofanya lolote kwasababu ya mfumo uliokuwepo umeoza. Na wakasahau kwamba mfumo unajieleza vizuri, isipokua mfumo ulikosa msimamizi mzuri wa kuufanya ulete tija kwa wananchi.

Magufuli endelea kufanya kazi, endelea kutoa tiba kwa mfumo uliokuwepo na kukata mifumo yote haramu iliyotengenezwa ndani ya mifumo halali.

Tatizo lilikua ni mtu, na sio mfumo.
 
AJITOKEZE HAPA MWAKA UKAWA WA UKWELI, sio hawa BAVICH-wA maji, mwana ukawa halisi na wa ukweli, atueleze mfumo uliokisudiwa na ukawa endapo wangeokota dodo chini ya mnazi.
 
Huyo magufuli anafanya haya yote akijua kuna upinzani imara utamtetea au utakuwa pamoja nae. Hata kikwete angekuwa kachaguliwa mwaka huu angefanya kama magufuli haya ni matunda ya upinzani imara na usijue kuwa magufuli yuko imara.
 
Bado mapema Hii post ungeileta mwaka 2017 ningekuwa na cha kuchangia, sasa Magufuli amemaliza mwezi unasema ameprove wapinzani wrong? Furahia matokeo sio mchakato

Mbona ni mwezi tu ila bavicha washaamza kuponda bila hoja?
 
Huyo magufuli anafanya haya yote akijua kuna upinzani imara utamtetea au utakuwa pamoja nae. Hata kikwete angekuwa kachaguliwa mwaka huu angefanya kama magufuli haya ni matunda ya upinzani imara na usijue kuwa magufuli yuko imara.
Ukawa wataendelea kuwa 'bunge', dola kuishika wasahau!
 
Bado mapema Hii post ungeileta mwaka 2017 ningekuwa na cha kuchangia, sasa Magufuli amemaliza mwezi unasema ameprove wapinzani wrong? Furahia matokeo sio mchakato

Thanks for this relief mkuu.
Kuna watu wanadhani kazi ndo inaelekea kuisha hivyo ushindi ndo huu ama ule kwa haya machache ambayo ameshafanya hadi sasa. No, Hata bunge hllijakaa kuchambua mambo flani flani kama kawaida yake, tayari mnadhani mmemaliza!!! hasha. Bado ukweli nikwamba JPM akitaka afike salama lazma abadili mfumo huu ulioko ndani ya chama. LAZIMA. Kwanza ona wanvyoanza kumuwaza maana ni kama hayuko nao sambamba vile, you knwo why??? wanatamani aunge mkono mfumo wao ila yeye anaendesha serikali yake kwa mfumo wake ambao taratiiibu haukubaliki ndani ya chama. Asisahau vipengele muhiku vya kubadilisha ndani ya KATIBA. NAAAAAAM!!!!!!!!!!!!! samahani nimeitwa, ntarudi usjali best.
 
Tatizo bado ni mgumo tu wala usibishe ndugu, haya anayoyafanya Magufuli yanatakiwa yawekwe kwenye mfumo/ sheria za uendeshaji nchi. Vinginevyo, muda wake ukipita akaingia Rais mwingine na mfumo huu, anaweza akaamua nae kuendesha anavyotaka si mfumo unamruhusu? Anaweza unda Wizara mia, akawa na mawaziri mia na manaibu mia, akaongeza Mikoa ikafika sabini. Tunaposema mfumo na sio mtu watu wengine hawaelewi. Magufuli, Nyerere, hawa ni utashi wao na uzalendo wao tu lakini sio mfumo ndiyo unawafanya watende hivi. Mfumo unatakiwa umlazimishe Rais kutenda jambo fulani kwa manufaa ya nchi. Kumbuka watu tunatofautiana tabia na mtazamo na ndiyo maana hata hao Marais wetu, wengine waliona ni sawa kwenda nje sana na wengine wanaona si sawa. Lakini ukiwepo mfumo wa kuzuia safari za nje mpaka kwa kibali maalum, hapo hata aingie nani Ikulu atafuata mfumo unavyosema. Mfumo wetu wa sasa ni mbovu kiasi kwamba kama Magufuli hata uweka kwenye sheria/ katiba, 2025 akiingia mwingine anawezafanya atakavyo.
 
Hah Hah! Hii tabiaya waTZ kuendeshwa ni mihemko sijui tutaacha lini! Fanyeni kazi achene majungu.Yaani pamoja na mgombea wa ccm kutangazwa mshindi bado mnawafuatilia watu wa UKAWA? Huyu kwa sasa ni Raisi wa TZ nzima. Kuhusu suala la mfumo ni kweli ni tatizo. Pia katiba ni sehemu ya mfumo, bado ni tatizo. Tunachotakiwa kufanya ni kufanya kazi ili taifa lisonge mbele. Raisi, makamu wake na PM pekeyao hawawezi kuleta maendeleo tunayotaka. Hatuna budi kuwasaidia na sio kuendeleza mijadala a kututenganisha. Bado najivunia na nitaendelea kujivunia kwa kutopigia kura ccm. Ila kwa sasa yote haya sio ya muhimu, ishu ni kutekeleza majukumu yako ktk nafasi uliyonayo
 
Muwindaji acha fikra fupi..je unategemea Magu awepo kila mahali na kusimamia kila jambo?
Safari bado ni ndefu na suluhisho lake sio hili unaloliona..hizi ni hatua tu za kujinusuru lakini suluhisho ni Katiba bora na utawala wa sheria
 
Last edited by a moderator:
Hivi mliwaamini hao?kwanza wao waliprouve wrong baada ya mfumo wao wa kupinga ufisadi kubadilishwa na mtu mmoja tu fisadi baba Lowasa,mtu waliemtukana kwa miaka nane kuwa ni fisadi,ila baada ya kuingia kwenye chama chao kwa siku moja tu wakabadili mfumo wao wa kupinga ufisadi.Mpaka leo wamebaki kupigania maiti tu
 
Back
Top Bottom