Niccolo Machiavelli
JF-Expert Member
- Feb 7, 2017
- 1,881
- 3,636
Nianze kwa kusema mimi sio muumin wa chama chochote cha siasa Tanzania, lakini naipenda sana nchi yangu Tanzania.
Nimekua nikimfuatilia kwa ukaribu Rais Magufuli toka ameingia madarakani mwaka 2015. Huyu mzee ni mtu ambaye nimegundua ana nia nzuri na hii nchi, ila tatizo ana maadui wengi.
Kipindi hiki cha corona ndo nimeona kwamba huyu mzee ana mapenzi na wanachi wake na pia ni mzalendo. Nakumbuka mwaka 2016, Magufuli alimfuta kazi Mkurugenzi wa NIMR kwa kutangaza kua ZIKA virus imeingia Tanzania.
Cha kushangaza, baada ya kutangaza kuwepo kwa ZIKA Tanzania na kufukuzwa kazi kuyu DG, hatukuweza kuona kisa chochote cha ZIKA Tanzania. Huenda huu ulikua mpango wa kuanza kusambaza huu ugonjwa Afrika Mashariki lakini huyu mzee alitupigania. Cha ajabu waliombeza huyu Mzee, hakuna aliejitokeza kusema kwamba Rais alikua sahihi alivosema hakuna ZIKA.
Limekuja janga la corona, huyu Mzee nina imani anajua mipango ya hawa “mabeberu” ya kusababisha taharuki. Wengi wamembeza huyu Mzee lakini mimi nina imani anachofanya ni sahihi. Kuna video clip nimeona Mbunge wa Italia akiwatuhumu Marekani kupika data za vifo vya corona Italia ili waweze kuweka kiongozi wanaemtaka.( nimeambatanisha video mwishoni)
Nina amini hizi nchi zinazofunga mipaka na nchi yetu zinatumika kumuumiza huyu Mzee ili wananchi tumchukie. Ni ombi langu kwa WaTanzania tushikamane tumpe support Rais wetu.
NB: Ninafahamu kwamba Magufuli ana mapungufu mengi tu, ila kwa leo naomba tumuunge mkono kwenye vita dhidi ya corona.
Nimekua nikimfuatilia kwa ukaribu Rais Magufuli toka ameingia madarakani mwaka 2015. Huyu mzee ni mtu ambaye nimegundua ana nia nzuri na hii nchi, ila tatizo ana maadui wengi.
Kipindi hiki cha corona ndo nimeona kwamba huyu mzee ana mapenzi na wanachi wake na pia ni mzalendo. Nakumbuka mwaka 2016, Magufuli alimfuta kazi Mkurugenzi wa NIMR kwa kutangaza kua ZIKA virus imeingia Tanzania.
Cha kushangaza, baada ya kutangaza kuwepo kwa ZIKA Tanzania na kufukuzwa kazi kuyu DG, hatukuweza kuona kisa chochote cha ZIKA Tanzania. Huenda huu ulikua mpango wa kuanza kusambaza huu ugonjwa Afrika Mashariki lakini huyu mzee alitupigania. Cha ajabu waliombeza huyu Mzee, hakuna aliejitokeza kusema kwamba Rais alikua sahihi alivosema hakuna ZIKA.
Limekuja janga la corona, huyu Mzee nina imani anajua mipango ya hawa “mabeberu” ya kusababisha taharuki. Wengi wamembeza huyu Mzee lakini mimi nina imani anachofanya ni sahihi. Kuna video clip nimeona Mbunge wa Italia akiwatuhumu Marekani kupika data za vifo vya corona Italia ili waweze kuweka kiongozi wanaemtaka.( nimeambatanisha video mwishoni)
Nina amini hizi nchi zinazofunga mipaka na nchi yetu zinatumika kumuumiza huyu Mzee ili wananchi tumchukie. Ni ombi langu kwa WaTanzania tushikamane tumpe support Rais wetu.
NB: Ninafahamu kwamba Magufuli ana mapungufu mengi tu, ila kwa leo naomba tumuunge mkono kwenye vita dhidi ya corona.