Magufuli ana nia ya kulisogeza mbele Taifa lakini anapaswa kuwa makini kwenye Mambo 5 yafuatayo!!

jepro

Member
Oct 28, 2011
90
6
1. Kwanza awezeshe kuwa na uhuru wa Vyombo vya Habari.

2. Demokrasia ni jambo muhimu awape wapinzani uhuru wa kuikosoa serikali kwa kuwa hakuna aliyekamilika duniani kila mtu hutenda makosa na kukosolewa ndo njia pekee ya kujifunza ulipokosea na ukajirekebisha na mambo yakaendelea kama ilivyo ada.

3. Afanye uchunguzi yakinifu kwa habari anazoletewa na watendaji wake kabla ya kuziwasilisha kwa wananchi.

4. Aweze kusikiliza malalamiko ya wananchi kwa kuwa hawa ndio waliomchagua na akumbuke sauti ya wengi ni sauti ya Mungu asitie pamba masikioni kwa malalamiko ya wengi pindi jambo Fulani linapozungumziwa au kuhitaji ufafanuzi wa kina kutoka kwake au Mamlaka husika.

5. Azingatie sheria, kanuni na taratibu zinazotumika kuliongoza hili Taifa namaanisha aongoze Taifa kwa kufuata nini Katiba inavoelekeza

Nadhani kwa kuyafuata hayo mambo matano pamoja na uchapakazi wake mahiri hili Taifa naliona lina bright future katika ukuaji kiuchumi vinginevyo tutajikuta tunarudi nyuma miaka Zaidi ya 50

Ni hayo Tuu
 
Hiyo inaitwa ngumu kumeza, umenikumbusha moja ya kauli ya Mahatma Gandhi kwamba hakuna haja ya kuwa kama hakuna uhuru wa watu kufanya makosa na kukosoana kwa uhuru pasipo kubughudhiwa
 
Ukiruhusu uhuru wa nyombo vya habari africa utaleta vita kutokana na waandishi wengi wa habari kuto kua na elimi tosha

Ukiruhusu demokrasia africa kwa maana ya kuruhusu kila mtu kusema na kutenda anavyo taka basi ujiandae kushuhudia vita au machafuko kutokana na siasa sa africa kujawa na chuki na ufinyu wa elimu ya kutosha kwa wananchi, akitokea zuzu mmoja anasema wananchi wachome nyumba za wapinzani watafanya hivyo, hivyo hana budi kudhibiti vyama vyote hasa ccm wenye maneno mengi.
 
Huu uzi anaovuta aendelee kuukaza. Ukiona watu mapovu yanawatoka basi wameshikwa pabaya
 
Aendelee kujipoteza mana watu wamemchoka haswaaaaaaaa
Mana chai na uji vimemshinda
 
Huu uzi anaovuta aendelee kuukaza. Ukiona watu mapovu yanawatoka basi wameshikwa pabaya
Kashikwa pabaya yy
Vitu vya uji na chai vimemshinda
Amebaki ki shari shari hasira kibaoooo
Vp boom la wadogo zetu mnapeleka lin mana s mlisema mapato ni trillion 1.3 au sio nyie
Hahahaaa mmepoteana ila basi tuu kujikaza
 
Magu uongozi wake ni wa kuji defend sana ka timu inayolinda goal. Hana mipango endelevu sasa anaona upinzani ndo kikwazo. Kumbe hana vision ata deal na upinzani badala ya kujienga uchumi huku mda ukienda
 
Demokrasia ni muhimu lakini isipite kiasi. Kwa nchi zetu hizi za kiafrika ukiruhusu sana demokrasia watu watakupanda hadi kichwani kwa kisingizio cha demokrasia. Kwa maoni yangu ili tuweze kupiga hatua za maendeleo ni muhimu kuchanganya demokrasia na udikteta kidogo yaani DEMOKRASIA 75% na UDIKTETA 25%.
 
Hoja zikiwashinda
Ooh mtaleta vita sasa kazeni ivo ivo tuone kama waasi hawatapatikana
Ukiruhusu uhuru wa nyombo vya habari africa utaleta vita kutokana na waandishi wengi wa habari kuto kua na elimi tosha

Ukiruhusu demokrasia africa kwa maana ya kuruhusu kila mtu kusema na kutenda anavyo taka basi ujiandae kushuhudia vita au machafuko kutokana na siasa sa africa kujawa na chuki na ufinyu wa elimu ya kutosha kwa wananchi, akitokea zuzu mmoja anasema wananchi wachome nyumba za wapinzani watafanya hivyo, hivyo hana budi kudhibiti vyama vyote hasa ccm wenye maneno mengi.[/QUOTEm
Tatizo hapo ni mental emotional disorder pole sana
 
Leo nimekutana na Dada mmoja alikuwa mpenzi sana wa Rais Magufuli, lakini ananiambia hamu imemwisha kabisa, haamini kinachotokea
 
Back
Top Bottom