G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Mgombea urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ndugu John Pombe Magufuli leo ameshusha lundo la tuhuma kwa naibu spika wa bunge na mgombea ubunge wa jimbo la Kongwa kwa tiketi ya CCM ndugu Job Ndugai, imethibitishwa.
Magufuli amemtuhumu Job Ndugai kwa kitendo chake cha kueleza hadharani kuwa anaiunga mkono kauli ya Edward Lowassa ya kuunda tume maalum kushughulikia migogoro ya wakulima na wafugaji jimboni humo.
Magufuli amesema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi ambavyo Job Ndugai asivyo na imani naye kama mgombea wa urais kupitia chama chake na wala asisingizie migogoro.
Aidha habari za ndani zilizopatikana jimboni humo ni kuwa Job Ndugai alikuwa miongoni mwa wana CCM walio na imani kubwa na Edward Lowassa ingawa kwa sasa hajaeleza msimamo wake baada ya Lowassa kuitosa CCM.
..................
Mimi nipo na timu ya watu wa ndani kabisa wa John Magufuli mikoani.
Magufuli amemtuhumu Job Ndugai kwa kitendo chake cha kueleza hadharani kuwa anaiunga mkono kauli ya Edward Lowassa ya kuunda tume maalum kushughulikia migogoro ya wakulima na wafugaji jimboni humo.
Magufuli amesema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi ambavyo Job Ndugai asivyo na imani naye kama mgombea wa urais kupitia chama chake na wala asisingizie migogoro.
Aidha habari za ndani zilizopatikana jimboni humo ni kuwa Job Ndugai alikuwa miongoni mwa wana CCM walio na imani kubwa na Edward Lowassa ingawa kwa sasa hajaeleza msimamo wake baada ya Lowassa kuitosa CCM.
..................
Mimi nipo na timu ya watu wa ndani kabisa wa John Magufuli mikoani.