Magufuli alijitofautisha, Kikwete anajaribu kusawazisha kumwokoa, Tundu Lissu anamtetea!

Tila-lila2

JF-Expert Member
Oct 20, 2019
653
1,058
Inawezekana nawe umegundua trend hii. Kila JPM akiongea kuelezea yaliyofanyika anaelezea kana kwamba yamefanyika kwake. Amekuwa hata akidiriki kutumia maneno mabaya kwa waliomtangulia mfano "uchumi ulikuwa mikononi wa majizi", "Waliishi kama malaika sasa wataishi kama mashetani", "mimi huwa sipangiwi (kama waliopita - may be!)" , "mimi ni Rais kwelikweli" (sio kama wengine may be!) n.k. Mfano mwingine ni kuonesha kuwa zoezi la kuhamia Dodoma lilikuwa limesimama tangu Mwalimu Nyerere aondoke mdarakani.

Kwa kuona hali hiyo JK kila akipata nafasi kwenye kadamnasi anaonesha kuwa hii mipango yote ilikuwepo na imekuwa ikitekelezwa karibu katika kila awamu ya uongozi. Wengi mtakumbuka kwa mfano, siku ya uzinduzi wa Ikulu ya Chamwino, alivyoelezea zoezi la kuhamia Dodoma lilivyotekelezwa katika awamu karibia zote. Alielezea yaliyofanywa kipindi cha Mkapa., aliyoyafanya yeye ikiwa ni pamoja na kuamua mahali pa kujengwa Ikulu. Hivi karibuni JK alielezea vizuri sana namna Hayati Bw Mkapa alivyoasisi mpango wa uchumi ambao unatarajiwa kufikia Mwaka 2025 pato la kila MTZ liwe dola elfu tatu.

Ukifuatilia kwa makini JK amekuwa akijaribu kumkumbusha JPM kuwa anayoyafanya leo ni vizuri kuelezea yalianzia wapi ili hata kama yamekosewa asionekane yeye JPM kakosea peke yake. Pamoja na ufafanuzi wa JK bado watendaji wa JPM hawafurahii ufafanuzi huo kw sababu wanataka tu kumpamba JPM aonekana e amekwa akitekeleza yote yeye tu - kama utakumbuka yule Msemaji wa Serikali alitaka kuanza kukanusha kuhusu pato la dola elfu tatu kufikia 2025 - akapingwa vikali sana. Yote aliyokusudia kuyafanya ilikuwa ni kujipendekeza tu.

Sasa hivi ametokwa mtetezi wa JPM - yaani Tundu Lissu. Huyu amekuwa akielezea kwa ufasaha yale yaliyofanywa na JPM na kuonesha yale ambayo yamekuwa yakifanyika awamu zote. Tundu Lissu ameonesha kwa ufasaha sana sana. Mf. ameonesha kuwa JPM amejenga kiwanja cha ndege Chato wakati waliomtangulia hawakujenga viwanja vya ndege vijijini kwao. Ameonesha jinsi JPM ambavyo mara zote anatumia lugha ambazo kwa kiasi fulani hazina staha na zinazalilisha utu na hasa jinsia wakati watangulizi wake hawakuwa wakifanya hayo mambo.

Ninachojiuliza - maneno ya Tundu Lissu ya ukweli yamekuwa yakiwaumiza wanaCCM hata humu JF - sasa wanataka waelezwe nini? Je Tundu Lissu anaongea uwongo kwani? Mbona anafafanua tu ukweli? Kwani ni kweli kuwa ndege zimeanza kununuliwa kipindi chake tu? Kwani ni kweli madaraja yameanza kujengwa kipindi chake tu? Kwani ni kweli kuwa bwawa la umeme tunalitegemea ni hili tu analojenga yeye? Ninakumbuka sisi Shinyanga miaka ya nyuma tulikuwa tunatumia umeme wa jenereta - lakini baadaye nafikiri miaka ya themanini na usheee kuelekea miaka ya 90 ndiyo tukapata umeme - nafikiri wa Kidatu au Mtera (sikna kumbukumbu nzuri).

Angalia pia suala la elimu ya msingi na sekondari bure - hili suala halikuanza kwa JPM - elimu ya msingi bure imeanza siku nyingi. Tena kuna wakati hata chakula cha bure wanafunzi walipewa. Rungwe mwenyewe ninavyofikiri anakumbuka enzi hizo ndiyo maana kaja na sera hiyo ya lishe ya ubwabwa!

Nina mengi ya kuandika - lakini ngoja niache kwanza nitafute wateja asubuhi hii ili leo niiongize hata elfu ishirini tu!

Karibuni Idukilo - Kishapu - Shinyanga ndiyo kwetu, tulewe Tila Lila!
 
Kisera, kimpango, kimkakati na kiushawishi timu kijani imeshafeli kinachofanyika sasa ni hadaa na kutumia ubabe kwa msaada wa dola taasisi tanzu zake.

Itosehe sasa kusema TBC sio shirika la utangazaji la Taifa bali shirika la utangazaji la chama cha mapinduzi hivyo ni haki kabisa likabadili jina kuwa CBC1
 
Jambo kubwa alilolifanya JPM (linalomtofautisha na wengine) ni msisitizo kwamba kila senti yetu inayokusanywa ijenge mambo yakitaifa yatakayonufaisha watanzania wote. Inaweza akawa hajafanikiwa kwa asilimia 100 katika hilo maana bado kuna watu wajanja wajanja wanaotafuta fursa ya kupiga wapige kila inapopatikana.

Ila sisi tunaangalia moyo wa dhati, nia ya dhati na matendo yanayoashiria kuwa mzee anamaanisha nchi hii iende mbele. Na viongozi watarajiwa 2025 watake note, hatutaki tena viongozi wasio na maono wala moyo wa kizalendo kwa nchi yetu.
 
Jambo kubwa alilolifanya JPM (linalomtofautisha na wengine) ni msisitizo kwamba kila senti yetu inayokusanywa ijenge mambo yakitaifa yatakayonufaisha watanzania wote. Inaweza akawa hajafanikiwa kwa asilimia 100 katika hilo maana bado kuna watu wajanja wajanja wanaotafuta fursa ya kupiga wapige kila inapopatikana.

Ila sisi tunaangalia moyo wa dhati, nia ya dhati na matendo yanayoashiria kuwa mzee anamaanisha nchi hii iende mbele. Na viongozi watarajiwa 2025 watake note, hatutaki tena viongozi wasio na maono wala moyo wa kizalendo kwa nchi yetu.
Zile za kununua wapinzani ili waunge mkono juhudi umezijumuisha?
 
Jambo kubwa alilolifanya JPM (linalomtofautisha na wengine) ni msisitizo kwamba kila senti yetu inayokusanywa ijenge mambo yakitaifa yatakayonufaisha watanzania wote. Inaweza akawa hajafanikiwa kwa asilimia 100 katika hilo maana bado kuna watu wajanja wajanja wanaotafuta fursa ya kupiga wapige kila inapopatikana.

Ila sisi tunaangalia moyo wa dhati, nia ya dhati na matendo yanayoashiria kuwa mzee anamaanisha nchi hii iende mbele. Na viongozi watarajiwa 2025 watake note, hatutaki tena viongozi wasio na maono wala moyo wa kizalendo kwa nchi yetu.
Kweli kabisa - lakini sasa kwa nini huwa hataki kuonesha hata appreciation kwa yaliyofanywa na wenzake? Na inakuwaje maneno yake ya kudhalilisha? Huoni kuwa huo ni utopolo?
 
Tila-lila2,

Mbona husemi kila wakati amesema anaendeleza kazi za watangulizi wake na kuwasifu. Mbona husemi kila wakati anawaalika na kuwashukuru kwa kazi zao. Usifiki urais ni sawa na ukarani. Hata yeye akitoka atabakiza madudu mengi tu. Ufisadi unadhibiwa tu haumaliziki ndio maana zipo dola na tawala.
 
Gazeti lote hili! Magu hahitaji kupambwa! Tayari matendo yake yameshampamba! JK na kundi lake akae tu pembeni maana hawakuwa na dhamira thabiti ya kuikwamua Tz! Wao, hasa JK aliliacha liende lenyewe mpaka litakapogota! Magu kaingia na kubadili upepo!

Kwa trend aliyokuwa akienda nayo JK hata Kama tungekaa miaka 100 bado hata robo ya yaliyofanyika ndani ya miaka 4 ya Magu yasingewezekana kufanyika! Kuhamia dom, Nyerere dam, kujikomboa kutoka simbian na Richmond, SGR, Fly over zingebaki Kuwa ndoto za mchana! Maana priority ulikuwa kusafiri kutoka nchi moja kwenda nyingine hata kwenda kusaini autograph za Akina PDD wakati wananchi wanahanjahanja! Hiyo fedha ya kufanya miradi ya kimkakati isingepatikana maana Kila mtu alikuwa amejibinafisishia kipande Cha mapato ya serikali!

Huyo mzee JK nafikiri anyamaze kimya maana watz tuna kumbukumbu ambazo bado mbichi kabisa!
JK aliwaachia Akina Mende na kundi lake kutuingiza ktk mikataba ya wiziwizi...asitake kutukumbusha machungu unajua ohooool!
 
Mbona husemi kila wakati amesema anaendeleza kazi za watangulizi wake na kuwasifu. Mbona husemi kila wakati anawaalika na kuwashukuru kwa kazi zao. Usifiki urais ni sawa na ukarani. Hata yeye akitoka atabakiza madudu mengi tu. Ufisadi unadhibiwa tu haumaliziki ndio maana zipo dola na tawala.
Ameanza kugeuka juzi hapa baada ya msiba wa Mkapa. Kwanza alikuwa hapangiwi! Au hukuona hapo kuwa alitufokea?
 
Gazeti lote hili! Magu hahitaji kupambwa! Tayari matendo yake ysmeshampamba! JJ na kundi lake akae tu pembeni maana hawakuwa na dhamira thabiti ya kujikwamua Tz! Wao, hasa JK aliliacha license lenyewe mpaka litakapogota! Magu kaingia na kubashiri upepo! Kwa trend aliyokuwa akienda mayo JK hata Kama tungekaa miaka 100 bado hata robo ya yaliyofanyika ndani ya miaka 4 ya Magu yasingewezekana kufanyika! Kuhamia dom, Nyerere dam, kujikomboa kutoka simbian na Richmond, SGR, Fly over zingebaki Kuwa ndoto za mchana! Maana priority ulikuwa kusafiri kutoka nchi moja kwenda nyingine hata kwenda kusaini autograph za Akina PDD wakati wananchi wanahanjahanja! Hiyo fedha ya kufanya miradi ya kimkakati isingepatikana maana Kila mtu alikuwa amejibinafisishia kipande Cha mapato ya serikali!
Huyo mzee JK nafikiri anyamaze kimya maana watz tuna kumbukumbu ambazo bado mbichi kabisa!
JK aliwaachia Akina Mende na kundi lake kutuingiza ktk mikataba ya wiziwizi...asitake kutukumbusha machungu unajua ohooool!
Na kwenye kampeni mseme hivi hivi mtashinda dadangu!
 
Mbali na kwamba tunataka Tundu Lissu aongoze nchi na pia akabidhiwe kwa amani lakini pia tunaomba mungu amtume malaika wa kifo kwa JPM ili tuishi kwa amani.
 
Dada mwenyewe! Hatuhitaji kusema chochote! Utekelezaji wa ilani unatosha! Mwenye macho na masikio na utimamu wa akili ameshajiandaa kumrudisha Magu kwa mafuriko!
Unanifokea! Mmerithi kwa JPM nini?
 
Mi nimesoma Forodhani sec. Miaka ya 80 tulikuwa tunakula shuleni,chai ya maziwa mayai, juice, matunda, na tunafatwa na magari ya mashirika,

alafu mpuuzi mmoja anadai eti yeye ndo kaanzisha elimu bure
Eti bhana! Mie mwenyewe nilikuwa ninatoka Idukilo Kishapu (enzi hizo Shinyanga Vijijini) ninasafiri hadi Dodoma - Mazengo Sekondari halafu ninatunza tiketi nainaenda kurudishiwa nauli yangu. Yaani JPM bhana, haya yote ameyasahau wakati nina uhakika hata yeye atakuwa aliwahi kulipwa. Isitoshe nina uhakika hata Chuo Kikuu atakuwa alisoma bure bila hata kukopeshwa! Leo sijui tunaelezwa takataka gani hizi!
 
Inawezekana nawe umegundua trend hii. Kila JPM akiongea kuelezea yaliyofanyika anaelezea kana kwamba yamefanyika kwake. Amekuwa hata akidiriki kutumia maneno mabaya kwa waliomtangulia mfano "uchumi ulikuwa mikononi wa majizi", "Waliishi kama malaika sasa wataishi kama mashetani", "mimi huwa sipangiwi (kama waliopita - may be!)" , "mimi ni Rais kwelikweli" (sio kama wengine may be!) n.k. Mfano mwingine ni kuonesha kuwa zoezi la kuhamia Dodoma lilikuwa limesimama tangu Mwalimu Nyerere aondoke mdarakani.

Kwa kuona hali hiyo JK kila akipata nafasi kwenye kadamnasi anaonesha kuwa hii mipango yote ilikuwepo na imekuwa ikitekelezwa karibu katika kila awamu ya uongozi. Wengi mtakumbuka kwa mfano, siku ya uzinduzi wa Ikulu ya Chamwino, alivyoelezea zoezi la kuhamia Dodoma lilivyotekelezwa katika awamu karibia zote. Alielezea yaliyofanywa kipindi cha Mkapa., aliyoyafanya yeye ikiwa ni pamoja na kuamua mahali pa kujengwa Ikulu. Hivi karibuni JK alielezea vizuri sana namna Hayati Bw Mkapa alivyoasisi mpango wa uchumi ambao unatarajiwa kufikia Mwaka 2025 pato la kila MTZ liwe dola elfu tatu.

Ukifuatilia kwa makini JK amekuwa akijaribu kumkumbusha JPM kuwa anayoyafanya leo ni vizuri kuelezea yalianzia wapi ili hata kama yamekosewa asionekane yeye JPM kakosea peke yake. Pamoja na ufafanuzi wa JK bado watendaji wa JPM hawafurahii ufafanuzi huo kw sababu wanataka tu kumpamba JPM aonekana e amekwa akitekeleza yote yeye tu - kama utakumbuka yule Msemaji wa Serikali alitaka kuanza kukanusha kuhusu pato la dola elfu tatu kufikia 2025 - akapingwa vikali sana. Yote aliyokusudia kuyafanya ilikuwa ni kujipendekeza tu.

Sasa hivi ametokwa mtetezi wa JPM - yaani Tundu Lissu. Huyu amekuwa akielezea kwa ufasaha yale yaliyofanywa na JPM na kuonesha yale ambayo yamekuwa yakifanyika awamu zote. Tundu Lissu ameonesha kwa ufasaha sana sana. Mf. ameonesha kuwa JPM amejenga kiwanja cha ndege Chato wakati waliomtangulia hawakujenga viwanja vya ndege vijijini kwao. Ameonesha jinsi JPM ambavyo mara zote anatumia lugha ambazo kwa kiasi fulani hazina staha na zinazalilisha utu na hasa jinsia wakati watangulizi wake hawakuwa wakifanya hayo mambo.

Ninachojiuliza - maneno ya Tundu Lissu ya ukweli yamekuwa yakiwaumiza wanaCCM hata humu JF - sasa wanataka waelezwe nini? Je Tundu Lissu anaongea uwongo kwani? Mbona anafafanua tu ukweli? Kwani ni kweli kuwa ndege zimeanza kununuliwa kipindi chake tu? Kwani ni kweli madaraja yameanza kujengwa kipindi chake tu? Kwani ni kweli kuwa bwawa la umeme tunalitegemea ni hili tu analojenga yeye? Ninakumbuka sisi Shinyanga miaka ya nyuma tulikuwa tunatumia umeme wa jenereta - lakini baadaye nafikiri miaka ya themanini na usheee kuelekea miaka ya 90 ndiyo tukapata umeme - nafikiri wa Kidatu au Mtera (sikna kumbukumbu nzuri).

Angalia pia suala la elimu ya msingi na sekondari bure - hili suala halikuanza kwa JPM - elimu ya msingi bure imeanza siku nyingi. Tena kuna wakati hata chakula cha bure wanafunzi walipewa. Rungwe mwenyewe ninavyofikiri anakumbuka enzi hizo ndiyo maana kaja na sera hiyo ya lishe ya ubwabwa!

Nina mengi ya kuandika - lakini ngoja niache kwanza nitafute wateja asubuhi hii ili leo niiongize hata elfu ishirini tu!

Karibuni Idukilo - Kishapu - Shinyanga ndiyo kwetu, tulewe Tila Lila!
JK? Holes Filler
Ni kweli Magufuli kafanya kazi na kuna tofauti kati ya wakati wa JK na JPM. Tunasahau tu. Magufuli ni Mchapa Kazi.
Human rights - zero, na ni katili

Lisu - Inteligent, bombastic, flamboyant, honest, inspirer, agile - a Leader
 
Back
Top Bottom