Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Taarifa ya habari ya saa moja jioni ya leo ya TBC1, Waziri wa Miundo mbinu Dr. Magufuli amesambaza Ilani ya uchaguzi za CCM kwa watendaji Wizarani kwake katika hali inayoonyesha anachapa siasa zaidi na kuwataka watendaji wote kwenye Wizara yake kuisoma, kuielewa na kuifuata..................au vinginevyo waache kazi au wataondolewa.....................
Vile vile amesimamisha zoezi la ajira mpya TANROADS katika hali inayoonyesha mwingiliano kati ya Bodi ya Wakurugenzi na Wizara Mama.............Kiutaratibu Wizara Mama haipaswi kujiingiza katika shughuli za kiutendaji za TANROADS..........Hayo ni majukumu ya Bodi na Menejimenti.......
La kusikitisha zaidi ni sababu alizozitumia katika kuhalalisha Uongozi wa Wizara kuingilia zoezi la ajira mpya za Wahandisi wa Mikoa wa TANROADS............alidai wao wanataka barabara zijengwe tu..........kama vile waliopo kazi hiyo huifanya kwa ufanisi wakati sivyo hata kidogo..................
Magufuli anashindwa kuelewa ya kuwa ni sera ya TANROADS ili kuimarisha ufanisi ajira ni za mikataba na kama watendaji wataelewa ajira ni za kudumu hawatakuwa na motisha wa kuongeza ufanisi...............................Pia TANROADS ina kashfa nyingi za matengenezo bomu ya barabara ikilinganishwa na fedha ambazo serikali hutumiwa kwenye shughuli hizo zikiongeza kasi ya umuhimu wa kuubadilisha uongozi mzima wa TANROADS....................
Mbaya zaidi, zoezi la mabadiliko ya uongozi ndani ya TANROADS yamekuwa yakipingwa na wabunge hususani Bunge la 9 kwa sababu hizohizo za kujenga barabara wakati barabara nyingi ni bomu................hii yaashiria Regional Engineers na watendaji ndani ya TANROADS wana sauti kubwa kuliko hata Bodi yao ya wakurugenzi katika kuchelewesha mabadiliko ya uongozi ndani ya TANROADS kwa masilahi yao binafsi tu......Kwa mwelekeo huu usitegemee jipya kutoka kwa Magufuli........aonekana ni mchovu sana kifikra na sasa ategemea jina kuisukuma Wizara hii atakako..........
Magufuli alishakaa kwenye wizara hiyo na of course ndiyo iliyompatia umaarufu mkubwa. Miye na-assume kwamba anaujua udhaifu wa TANROAD vizuri sana. Sina hakika kama utakumbuka, lakini kuna wakati Magufuli alimkoromea sana Chief wa TANESCO wakati akiwa jamaa mmoja kama sikosei alikuwa ni Mghana. Alichomkoromea Magufuli ilikuwa ni matumizi makubwa ya fedha za walipa kodi kwa mambo yasiyo na tija. Kwenye tukio hilo, alisitisha ununuzi wa jengo moja Jijini Mwanza ambalo TANROAD walikuwa mbioni kununua. Baada ya mkwala huo, TANROAD walifanya kazi na walibanwa mbavu kila kona na matokeo yake ndiyo hayo tunayoyaona hata leo. Barabara nyingi na bora zilijengwa.
Kwa hiyo, ninachoweza kusema hapa ni kwamba ebu tumwache Magufuli aiongoze wizara ambayo amepewa dhamana na rais na tumpe muda tuone mambo atakayofanya. Uzalendo wa Mhe. Magufuli kwa taifa lake siutilii shaka hata chembe.