Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 220,745
- 728,548
Taarifa ya habari ya saa moja jioni ya leo ya TBC1, Waziri wa Miundo mbinu Dr. Magufuli amesambaza Ilani ya uchaguzi za CCM kwa watendaji Wizarani kwake katika hali inayoonyesha anachapa siasa zaidi na kuwataka watendaji wote kwenye Wizara yake kuisoma, kuielewa na kuifuata..................au vinginevyo waache kazi au wataondolewa.....................
Vile vile amesimamisha zoezi la ajira mpya TANROADS katika hali inayoonyesha mwingiliano kati ya Bodi ya Wakurugenzi na Wizara Mama.............Kiutaratibu Wizara Mama haipaswi kujiingiza katika shughuli za kiutendaji za TANROADS..........Hayo ni majukumu ya Bodi na Menejimenti.......
La kusikitisha zaidi ni sababu alizozitumia katika kuhalalisha Uongozi wa Wizara kuingilia zoezi la ajira mpya za Wahandisi wa Mikoa wa TANROADS............alidai wao wanataka barabara zijengwe tu..........kama vile waliopo kazi hiyo huifanya kwa ufanisi wakati sivyo hata kidogo..................
Magufuli anashindwa kuelewa ya kuwa ni sera ya TANROADS ili kuimarisha ufanisi ajira ni za mikataba na kama watendaji wataelewa ajira ni za kudumu hawatakuwa na motisha wa kuongeza ufanisi...............................Pia TANROADS ina kashfa nyingi za matengenezo bomu ya barabara ikilinganishwa na fedha ambazo serikali hutumiwa kwenye shughuli hizo zikiongeza kasi ya umuhimu wa kuubadilisha uongozi mzima wa TANROADS....................
Mbaya zaidi, zoezi la mabadiliko ya uongozi ndani ya TANROADS yamekuwa yakipingwa na wabunge hususani Bunge la 9 kwa sababu hizohizo za kujenga barabara wakati barabara nyingi ni bomu................hii yaashiria Regional Engineers na watendaji ndani ya TANROADS wana sauti kubwa kuliko hata Bodi yao ya wakurugenzi katika kuchelewesha mabadiliko ya uongozi ndani ya TANROADS kwa masilahi yao binafsi tu......Kwa mwelekeo huu usitegemee jipya kutoka kwa Magufuli........aonekana ni mchovu sana kifikra na sasa ategemea jina kuisukuma Wizara hii atakako..........
Vile vile amesimamisha zoezi la ajira mpya TANROADS katika hali inayoonyesha mwingiliano kati ya Bodi ya Wakurugenzi na Wizara Mama.............Kiutaratibu Wizara Mama haipaswi kujiingiza katika shughuli za kiutendaji za TANROADS..........Hayo ni majukumu ya Bodi na Menejimenti.......
La kusikitisha zaidi ni sababu alizozitumia katika kuhalalisha Uongozi wa Wizara kuingilia zoezi la ajira mpya za Wahandisi wa Mikoa wa TANROADS............alidai wao wanataka barabara zijengwe tu..........kama vile waliopo kazi hiyo huifanya kwa ufanisi wakati sivyo hata kidogo..................
Magufuli anashindwa kuelewa ya kuwa ni sera ya TANROADS ili kuimarisha ufanisi ajira ni za mikataba na kama watendaji wataelewa ajira ni za kudumu hawatakuwa na motisha wa kuongeza ufanisi...............................Pia TANROADS ina kashfa nyingi za matengenezo bomu ya barabara ikilinganishwa na fedha ambazo serikali hutumiwa kwenye shughuli hizo zikiongeza kasi ya umuhimu wa kuubadilisha uongozi mzima wa TANROADS....................
Mbaya zaidi, zoezi la mabadiliko ya uongozi ndani ya TANROADS yamekuwa yakipingwa na wabunge hususani Bunge la 9 kwa sababu hizohizo za kujenga barabara wakati barabara nyingi ni bomu................hii yaashiria Regional Engineers na watendaji ndani ya TANROADS wana sauti kubwa kuliko hata Bodi yao ya wakurugenzi katika kuchelewesha mabadiliko ya uongozi ndani ya TANROADS kwa masilahi yao binafsi tu......Kwa mwelekeo huu usitegemee jipya kutoka kwa Magufuli........aonekana ni mchovu sana kifikra na sasa ategemea jina kuisukuma Wizara hii atakako..........