Kaji Bagome
Member
- Nov 5, 2019
- 15
- 21
JMT; Kazi iendelee.
Nilishaandika mara kadhaa kuhusu udhaifu wa uongozi wa Shule ya Msingi Magu; nikiomba uongozi wa Elimu Msingi (W) urekebishe hali hiyo, lakini kila uchao inakuwa kama heri ya jana.
Sasa hivi baadhi ya waalimu wanafanya biashara shuleni hapo (wao wenyewe), tena wakati wa kazi; wakirusha biashara zao kwenye mitandao ya kijamii.
Ujasiriamali sawa Ni kuongeza kipato; lakini kuufanyia eneo la kazi wakati wa kazi siyo sawa. Hayo yanafanyika Mwl. Mkuu akiwepo ofisini kwake bila kukemea mwenendo huo ili ukomeshwe.
Shule imechakaa kimazingira, kitaaluma, kiuongozi, kimahusiano, uchafu umekithiri vyooni, maji hakuna wakati bomba lipo n.k.
Yote hayo yanaendelea, licha ya kuyaweka bayana kwa Afisa Elimu Msingi (W) Magu kwenye jukwaa hilihili mnamo tarehe 17/11/2022 na hata kabla ya hapo.
Huenda Afisa Elimu Msingi (W) anakwamishwa na baadhi ya maofisa wake hapo ofisini kumchukulia hatua Mwl. Mkuu Njalla, maana ofisi yake ina maofisa wakongwe kuliko yeye na ni wala rushwa wakubwa; ambao huwa wanachukua pesa kwa waalimu na kuwapigania ili wapate ualimu mkuu.
Afisa wa aina hiyo ofisini hapo ni Bw. Nyagabona; ambaye ni Afisa Taaluma asiye hata na barua ya uteuzi kutoka TAMISEMI, lakini anayumbisha sana ofisi hiyo.
Huenda Mwl. Mkuu Ezekiel Njalla, alitoa chochote kwa Bwn. Nyagabona; hivyo DEO Msingi Magu kila anapotaka kuchukua hatua anakwamishwa.
Najua DED Magu mambo ni mengi, Idara zote yeye ndiye overseer, mambo mengine haelewi hata yanakwendaje kwenye vituo.
I wish Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI (Elimu) Mr. Msonde angepita ghafla hapo shuleni Magu akajionea hali halisi, yeye angesema na mambo yangerekebishwa.
Wahusika tafadhalini chukueni hatua kurekebisha kasoro nyingi zilizoko kituoni hapo kama hizi:
Nilishaandika mara kadhaa kuhusu udhaifu wa uongozi wa Shule ya Msingi Magu; nikiomba uongozi wa Elimu Msingi (W) urekebishe hali hiyo, lakini kila uchao inakuwa kama heri ya jana.
Sasa hivi baadhi ya waalimu wanafanya biashara shuleni hapo (wao wenyewe), tena wakati wa kazi; wakirusha biashara zao kwenye mitandao ya kijamii.
Ujasiriamali sawa Ni kuongeza kipato; lakini kuufanyia eneo la kazi wakati wa kazi siyo sawa. Hayo yanafanyika Mwl. Mkuu akiwepo ofisini kwake bila kukemea mwenendo huo ili ukomeshwe.
Shule imechakaa kimazingira, kitaaluma, kiuongozi, kimahusiano, uchafu umekithiri vyooni, maji hakuna wakati bomba lipo n.k.
Yote hayo yanaendelea, licha ya kuyaweka bayana kwa Afisa Elimu Msingi (W) Magu kwenye jukwaa hilihili mnamo tarehe 17/11/2022 na hata kabla ya hapo.
Huenda Afisa Elimu Msingi (W) anakwamishwa na baadhi ya maofisa wake hapo ofisini kumchukulia hatua Mwl. Mkuu Njalla, maana ofisi yake ina maofisa wakongwe kuliko yeye na ni wala rushwa wakubwa; ambao huwa wanachukua pesa kwa waalimu na kuwapigania ili wapate ualimu mkuu.
Afisa wa aina hiyo ofisini hapo ni Bw. Nyagabona; ambaye ni Afisa Taaluma asiye hata na barua ya uteuzi kutoka TAMISEMI, lakini anayumbisha sana ofisi hiyo.
Huenda Mwl. Mkuu Ezekiel Njalla, alitoa chochote kwa Bwn. Nyagabona; hivyo DEO Msingi Magu kila anapotaka kuchukua hatua anakwamishwa.
Najua DED Magu mambo ni mengi, Idara zote yeye ndiye overseer, mambo mengine haelewi hata yanakwendaje kwenye vituo.
I wish Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI (Elimu) Mr. Msonde angepita ghafla hapo shuleni Magu akajionea hali halisi, yeye angesema na mambo yangerekebishwa.
Wahusika tafadhalini chukueni hatua kurekebisha kasoro nyingi zilizoko kituoni hapo kama hizi: