macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 21,771
- 39,555
Ndugu zanguni,
Leo tumepatwa na msiba mkubwa baada ya ghorofa refu kuanguka na kufunika watu.
Ni dhahir kuwa kuanguka kwa jengo hili kunatokana na makosa ya kiufundi kwani hakuna ripoti inayosema jengo limepigwa bomu.
Hii inatisha sana, nimekaa nimejiuliza swali moja
Ikiwa leo hii jengo linaanguka lenyewe , jee kesho likitokea tetemeko la ardhi ni majengo mangapi yatabaki
Ndugu zangu tusije kuwa tunaishi kwenye time bomb.
Naiomba serikali ifanyie ukaguzi majengo yote nchini yenye urefu wa zaidi ya ghorofa mbili na jengo lolote litakaloonekana kuwa liko kwenye hatari ya kuporomoka libomolewe kabla halijaua watu
Mie sijasomea uhandisi lakini najua tuna civil engineers, architectures na quantity surveyors wa kutosha kufanya operesheni hii ili kuepusha majanga mengine kutokea.
Kila mtu anajua uchakachuaji wa sementi na zana nyingine kwenye uienzi na tabia ya wamiliki wengi wenye majengo marefu kuajiri wajenzi wasio na ujuzi wala uzoefu ili kupunguza gharama za ujenzi wanasahau kuwa wakati wa kuporomoka hata wao wanaweza kuwa ndani ya hayo majengo.
BORA LAWAMA KULIKO FEDHEHA, MAJENGO HATARI YABOMOLEWE!
Angalia haya mazuzu yalivyooza vichwani. Wewe ndio unafikiria kitu kilichokwisha fanyika miaka kadhaa iliyopita