Maghorofa yote marefu yakaguliwe, yatakayoonekana ni hatari yavunjwe kuepusha maafa zaidi

Ndugu zanguni,

Leo tumepatwa na msiba mkubwa baada ya ghorofa refu kuanguka na kufunika watu.
Ni dhahir kuwa kuanguka kwa jengo hili kunatokana na makosa ya kiufundi kwani hakuna ripoti inayosema jengo limepigwa bomu.

Hii inatisha sana, nimekaa nimejiuliza swali moja
Ikiwa leo hii jengo linaanguka lenyewe , jee kesho likitokea tetemeko la ardhi ni majengo mangapi yatabaki

Ndugu zangu tusije kuwa tunaishi kwenye time bomb.
Naiomba serikali ifanyie ukaguzi majengo yote nchini yenye urefu wa zaidi ya ghorofa mbili na jengo lolote litakaloonekana kuwa liko kwenye hatari ya kuporomoka libomolewe kabla halijaua watu

Mie sijasomea uhandisi lakini najua tuna civil engineers, architectures na quantity surveyors wa kutosha kufanya operesheni hii ili kuepusha majanga mengine kutokea.

Kila mtu anajua uchakachuaji wa sementi na zana nyingine kwenye uienzi na tabia ya wamiliki wengi wenye majengo marefu kuajiri wajenzi wasio na ujuzi wala uzoefu ili kupunguza gharama za ujenzi wanasahau kuwa wakati wa kuporomoka hata wao wanaweza kuwa ndani ya hayo majengo.

BORA LAWAMA KULIKO FEDHEHA, MAJENGO HATARI YABOMOLEWE!

Angalia haya mazuzu yalivyooza vichwani. Wewe ndio unafikiria kitu kilichokwisha fanyika miaka kadhaa iliyopita
 
Ablessed, kama Baba mwenye nyumba anakula rushwa, mama anatoa rushwa ya......, hapo familia imekufa. Ndio ya TZ!!!! Rushwa kila kipande ya nchi na njia zingine. Angalia wakuu wa wilaya, walio wengi hawastahili kuwa na nafasi hizo lakini kwa rushwa ya kujuana, wamo manesi ni wakuu wa wilaya, waandishi wa habari school failures, wapo etc, etc, etc, etc,,,,,,,,huu ni mfano mmoja tu! Chenge na vijisenti vyake bado anapewa kuwa mwenyekiti sijui wa kamati ya fedha/bajeti ya bunge ???????
That is too bad. Kusonga mbele itakua miujiza anyway sijui
 
Aaah, kumbe siyo kosa lako. Kuna mwaka pale Chang'ombe kuna gorofa lilishuka, likaua watu wawili kama sikosei. Kutoka hapo rais wako akatoa tamko kali la kutaka mtu asiruhusiwe kujenga ghorofa hadi apate kibali cha nani na nani sijui. Ikaundwa na tume ya kukagua ubora wa majengo nchi nzima. Na ikapendekeza majengo kadhaa pale Dar yavunjwe. Na kutoka hapo ikawa ni marufuku kwa mtu yeyote au shirika lolote kujenga ghorofa bila idhini ya hiyo tume. To my surprise, leo tena jengo limeanguka, tena karibu na Ikulu, na si ajabu ni karibu na makao makuu ya hiyo tume ambayo sijui ofisi yake ilipo. Seriousness ya viongozi wetu ni ndogo sana, ni lazima tuwe wakweli.

Na kinachosababisha yote haya ni uwezo mdogo wa Kikwete kumuwajibisha mtu anayeshindwa kutimiza wajibu wake katika sehemu yake ya kazi. Mabomu yanalipuka yanaua watu, rais anamtetea waziri eti halikuwa kosa lake, kwani Mwinyi alipojiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani siku zile ni yeye aliyewaua wafungwa? Kama mawaziri wangejua kwamba likitokea kosa chini ya uongozi wao wanapaswa kuwajibika, katu wasingemchekea yeyote aliye chini yao. Lakini hivi sasa CCM wanatengeneza majanga ili wajionyeshe kwa wananchi kwamba wanawajali. Kama ambavyo leo Kikwete amefanya. Jengo limevunjika kizembe eti anajifanya kwenda kuungana na wananchi katika kulishangaa jengo. Kumbe nilidhani anakwenda kutangaza kumfukuza kazi mkandarasi wa mkoa pamoja na waziri anayehusika na masuala ya makazi. Kwa nchi maskini inayotafuta kujikwamua kiuchumi na kijamii kama Tanzania, kuongozwa na kiongozi kama Kikwete ni hasara kubwa sana kwa watu binafsi na kwa taifa kwa ujumla wake.

Lukosi najua sana kwamba wewe ni shabiki mkubwa wa CCM, lakini una bahati mbaya, CCM imepoteza dira, ni chama cha maulaji na si chama cha kulinda na kutetea maslahi, ustawi na usalama wa watanzania. Nakushauri wewe ndugu yangu mwanaIringa mwenzangu uungane na sisi wenzako, kuwahurumia watanzania maskini ambao CCM inaendelea kuwatia umaskini na kuwaua kizembe kila kuchapo.

Mkuu huyu jamaa ni wala asikusumbue. Kwanza kuishi nje sio sababu ya kutofahamu kwani wapo wengi wanaoishi nje na wanajua. Pili sio kwamba hajui bali ni mtu wa kutaka sifa za kujionyesha na ni mchumia tumbo. Hizi sarakasi zooote unazoziona za kuanzisha thread ni kuwa anawania kupewa tenda ya kukagua magari kwa hiyo ni katika kujipendekeza pendekeza kwenye huu mfumo uliooza wa Kikwete ili wamfikirie. Wamjua jamaa anayejiita Le Mutus aka William? Basi yeye ni huyu ni kama pacha kitabia
 
Katika wapumbavu bila shaka unashika namba moja. Hoja aliyokuja nayo Lukosi hapa inaeleweka vyema kabisa. Ni nini usichoelewa katika hoja hiyo ya Lukosi?. Nina mashaka sana na elimu yako pamoja na uelewa wako, unaweza kujua ku -type na kutumia computer lakini unaonesha bado unaishi enzi za Ujima.

Hakuna msomi anayekurupuka!!!... Hakuna mwenye akili timamu anayefanya mambo yenye ishara ya kupungukiwa na akili bado akaendelea kuutetea upumbavu!!!!!...

LUKOSI ni mtu anayeelewa!!! Alipokuwa hajaelewa nizungumziacho alikuja juu kistaarabu!!!... Mwanzo tulitofautiana alipozidi kusoma kile nikisemacho tukafika mahali tukawa kitu kimoja!!!!!....

HUWEZI KUKURUPUKA NAMNA HIII na kujiiita mtu wa kizazi kipya!!!... SOMA POST ZILIZOFUATA ktk thread hii ILI UPATE AKILI badala ya kumwaga matusi kama mtu aliyekosa malezi!!!!!!!!... Hata mwanzilishi wa hii thread ametambua posti yake inaheshima zoote zinazostahili!!!!... Hata ingekuwa bungeni kila mmoja angeunga mkono hoja kwa 100%!!!!
 
Mkuu huyu jamaa ni wala asikusumbue. Kwanza kuishi nje sio sababu ya kutofahamu kwani wapo wengi wanaoishi nje na wanajua.
Pili sio kwamba hajui bali ni mtu wa kutaka sifa za kujionyesha na ni mchumia tumbo. Hizi sarakasi zooote unazoziona za kuanzisha thread ni kuwa anawania kupewa tenda ya kukagua magari kwa hiyo ni katika kujipendekeza pendekeza kwenye huu mfumo uliooza wa Kikwete ili wamfikirie. Wamjua jamaa anayejiita Le Mutus aka William? Basi yeye ni huyu ni kama pacha kitabia

Kwenye red Mkuu
Hao Serikali ndio wameruhusu hayo majengo yote kujengwa, Ukiyapitia yote yana vibali halali toka ofisi halali na yamethibitishwa na wataalam hao hao kuwa yanafaa kwa matumiz ya binadamu!
Ndugu yangu Lukosi siku moja niliwahi kukwambia kuwa kuishi kwako ughaibuni huenda kumekufanya kutokujua kwa uhakika nchi yetu ina serikali mbovu kwa kiasi gani.
Katikati ya miaka ya tisini kuna kampuni ya ujenzi ilikuwa inaitwa zakem hii ilijenga sehemu ya barabara ya Mwanza Shinyanga, barabara ile ilianza kubomoka ndani ya mwaka mmoja chini ya serikali hii hii!
Hili si Jengo la kwanza kuanguka mkuu na yataendelea kuanguka na hiyo serikali itaendelea kuwapa pole wananchi waliofikwa na maafa. If you think our government is serious and values people's life ur are making a bid mistake.

Chris Lukosi,Siku mojamoja huwa unaamka vizuri au leo ulisahau kuwa umefunga ndoa na serikali/ccm?(sijui nani amemuoa mwenzake).
Anyway,naunga mkono hoja.
Naskia kuna tume ya majengo,hivi kazi yake ni nini?


Kidatu, ..kumkosoa mtu si kosa!!!.. Kumtukana mtu ndiko kubaya, ...Soma maneno yaliyo kwenye bold nyeusi, Kila mmoja anafurahia kuona Post ya Lukosi inamuonesha karudi kwenye HOJA!!! ..matusi hayakujengi!!!!... Tafuta posti ambazo zilimfanya bro hata wengine (NIKIWEMO MIMI) tumwone ni mtu asiyejali matatizo ya watanzania!!!!
 
Kidatu, ..kumkosoa mtu si kosa!!!.. Kumtukana mtu ndiko kubaya, ...Soma maneno yaliyo kwenye bold nyeusi, Kila mmoja anafurahia kuona Post ya Lukosi inamuonesha karudi kwenye HOJA!!! ..matusi hayakujengi!!!!... Tafuta posti ambazo zilimfanya bro hata wengine (NIKIWEMO MIMI) tumwone ni mtu asiyejali matatizo ya watanzania!!!!
Kuna mtu mwenye matusi mabaya hapa JF kama wewe ukitumia zile ID zako nyingine?
 
Mkuu huyu jamaa ni wala asikusumbue. Kwanza kuishi nje sio sababu ya kutofahamu kwani wapo wengi wanaoishi nje na wanajua. Pili sio kwamba hajui bali ni mtu wa kutaka sifa za kujionyesha na ni mchumia tumbo. Hizi sarakasi zooote unazoziona za kuanzisha thread ni kuwa anawania kupewa tenda ya kukagua magari kwa hiyo ni katika kujipendekeza pendekeza kwenye huu mfumo uliooza wa Kikwete ili wamfikirie. Wamjua jamaa anayejiita Le Mutus aka William? Basi yeye ni huyu ni kama pacha kitabia

Hivi hapa JF kuna nini kinaendelea?. Hivi mtu kuja na mada ya kuisifia serikali kwa mazuri inayoyafanya imekuwa nongwa?. Mada aliyokuja nayo Lukosi ni nzuri na inaeleweka kabisa. Haiko Ki-CCM wala Ki-CDM bali iko Kitaifa, lakini kwa sababu Lukosi ni mwanachama wa CCM basi imekuwa nongwa. Watu wanaanza kumtupia maneno machafu Lukosi na Serikali. Jamani tafadhali tubadilike na kuwa wakweli ama la hatuendi popote. Tuipe serikali pongezi kwa yale mazuri inayoyafanya na tuikosoe kwa mabaya inayoyafanya huo ndiyo ukomavu wa kisiasa.

Mijitu hapa JF imekuwa inapinga kila kitu ama kila jambo linalofanywa na serikali iliyopo madarakani hata kama ni jambo zuri. Kibaya zaidi wanachama wengi wa JF wanafurahia mambo mengi ya CDM hata kama hayana faida kwa Taifa. Huo ni uzandiki na kukosa uzalendo. Tuwe wakweli na tuache fitina kwani ni hatari. "Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko"
 
Hivi hapa JF kuna nini kinaendelea?. Hivi mtu kuja na mada ya kuisifia serikali kwa mazuri inayoyafanya imekuwa nongwa?. Mada aliyokuja nayo Lukosi ni nzuri na inaeleweka kabisa. Haiko Ki-CCM wala Ki-CDM bali iko Kitaifa, lakini kwa sababu Lukosi ni mwanachama wa CCM basi imekuwa nongwa. Watu wanaanza kumtupia maneno machafu Lukosi na Serikali. Jamani tafadhali tubadilike na kuwa wakweli ama la hatuendi popote. Tuipe serikali pongezi kwa yale mazuri inayoyafanya na tuikosoe kwa mabaya inayoyafanya huo ndiyo ukomavu wa kisiasa.

Mijitu hapa JF imekuwa inapinga kila kitu ama kila jambo linalofanywa na serikali iliyopo madarakani hata kama ni jambo zuri. Kibaya zaidi wanachama wengi wa JF wanafurahia mambo mengi ya CDM hata kama hayana faida kwa Taifa. Huo ni uzandiki na kukosa uzalendo. Tuwe wakweli na tuache fitina kwani ni hatari. "Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko"
Haa haa.... Eti Kidatu! Waujua uzalendo wewe? Kanywe dawa ya tegu kwanza ujiponye kwani naona wamekuathiri ubongo wako
 
Hiyo Technologia unayo? Hapo lilipo anguka mkandarasi huyohuyo anajenga jingine na mpaka sasa lina zaidi ya gorofa kumi, na kwa vyovyote itabidi livunjwe, Je tunaweza?
 
Kuna jirani zangu hapa wanajenga magorofa wakapigwa stop order maana nyumba hizo ziko bondeni kabisaa,na nondo na ratio ya cement ni mbaya yaweza bomoka,chakushangaza wamehonga wanaendelea kujenga wakuu wamekula chao wamesepa.rushwa ndio inayotumaliza.
 
Duh,
mkuu Kumbe siku Hizi tuna kwenda kiitikadi?
Sijui ni nini lakini siku zote napenda kuweka itikadi nyuma,lakini tatizo mambo ya Chama dume/Dola nikiyaona nywele zinanisimuka tena kwa nature ya watu wanaohama vyama vya upinzani kwenda chama tawala(si tawala tu ccm),natambua pia Uhuru huo wa kikatiba lakini watu hao huwa nakua na mgogoro nao mara nyingi,hata hivyo unisamehe nakiri na kuamini kuwa huo ni
udhaifu....
 
Hivi ni lini watanzania tutafanya kazi bila rushwa jamani. Kama kuna harufu ya rushwa hatua zichukuliwe , tunaangamia jamani. Rushwa imekua ibada sasa, yaani kuna maeneo ukiwa unaona mbali hautahitaji rushwa.
Sekta a ujenzi ijitathimini na ije na msmamo kulinda hadhi yao. iweje majengo yaliyojengwa enzi ya Mjerumani bado yapo lakini haya ya kwetu mhhh! makandarasi wasikubali au wanataka tutafute wachina na waisraeli? Aibu! Kwa nini ukubali rushwa uharibu taaluma yako? angalia haya mashule yanajengwa leo kesho nyufa na mashimo ya kufa mtu JE HUU NI UUNGWANA???
 
Lukosi UMEKURUPUKA tena bila kufanya upembuzi angalau kidogo tu!

Baada ya kuanguka na kuua ghorofa la Chang'ombe iliundwa tume maarufu kama "TUME YA LOWASSA"kuleta serikalini nini kifanyike kunusuru maafa ya kuanguka kwa maghorofa yasitokee tena Dar!

"TUME YA LOWASSA"ilifanya kazi nzuri tu na ikakagua maghorofa mengi Dar na ikaleta majibu kuwa majengo mengi makubwa Dar sio salama maana wamiliki wake hawakufuata mikataba ya vibali walivyoomba kukamilisha ujenzi wa majengo yao;walitoa hadi majina ya maghorofa 122 ambayo kwa kuanzia waliyaona ni hatari!

"TUME YA LOWASSA"iligundua kuwa mmiliki wa jengo anaomba kibali cha kujenga ghorofa labda 3 lkn yy baadae anaziendeleza ghorofa hadi 14 akitumia msingi wa kuhimili ghorofa 3 tu!Serikali ya CCM HAIKUFANYIA KAZI ripoti ya"TUME YA LOWASSA"lkn yakijirudia maafa yaleyale tena viongozi wanakuwa wa kwanza kufika kwenye maafa eti kutoa pole na rambirambi!

Ushauri wako Lukosi ulitolewa tayari na TUME YA LOWASSA miaka karibia 6 iliyopita;serikali ikapuuza ushauri wa "TUME YA LOWASSA"!Ukiendelea kutuletea kama ushauri habari ambayo serikali ilishauriwa miaka mingi iliyopita bila utekelezaji sio tu unaonekana kituko mbele za watu bali watu wanaweza wakadharau ushauri wako hapo baadae kwa kuonekana ni wa hovyohovyo hata kama ungeisaidia jamii!
 
Sekta a ujenzi ijitathimini na ije na msmamo kulinda hadhi yao. iweje majengo yaliyojengwa enzi ya Mjerumani bado yapo lakini haya ya kwetu mhhh! makandarasi wasikubali au wanataka tutafute wachina na waisraeli? Aibu! Kwa nini ukubali rushwa uharibu taaluma yako? angalia haya mashule yanajengwa leo kesho nyufa na mashimo ya kufa mtu JE HUU NI UUNGWANA???

Yaani we acha tu hadi inatia hasira. Hivi umeona baadhi ya majengo yalivyoinama. Mimi nashangaa sana ninapoona haya. Tunapotembea nchi za wenzetu unakuta jengo refu lkn liko wima halijabend hata kidogo. Ina maana hatuna civil engineers wazuri au nini hasa tatizo. Je budget yetu ni ndogo sana kiasi kwamba hatuwezi kuwa na wataalam waliobobea .Na mwisho tujiulize je vyuo vyetu havitoi tena wataalam wazuri au nini hasa tatizo. Mimi nadhani uadilifu ni mali adimu sana siku hizi kila kukicha kuna hili au lile. Uadilifu tutakupata wapi wewe mbona unakimbia mbali kila kukicha??????
 
Lukosi UMEKURUPUKA tena bila kufanya upembuzi angalau kidogo tu!

Baada ya kuanguka na kuua ghorofa la Chang'ombe iliundwa tume maarufu kama "TUME YA LOWASSA"kuleta serikalini nini kifanyike kunusuru maafa ya kuanguka kwa maghorofa yasitokee tena Dar!

"TUME YA LOWASSA"ilifanya kazi nzuri tu na ikakagua maghorofa mengi Dar na ikaleta majibu kuwa majengo mengi makubwa Dar sio salama maana wamiliki wake hawakufuata mikataba ya vibali walivyoomba kukamilisha ujenzi wa majengo yao;walitoa hadi majina ya maghorofa 122 ambayo kwa kuanzia waliyaona ni hatari!

"TUME YA LOWASSA"iligundua kuwa mmiliki wa jengo anaomba kibali cha kujenga ghorofa labda 3 lkn yy baadae anaziendeleza ghorofa hadi 14 akitumia msingi wa kuhimili ghorofa 3 tu!Serikali ya CCM HAIKUFANYIA KAZI ripoti ya"TUME YA LOWASSA"lkn yakijirudia maafa yaleyale tena viongozi wanakuwa wa kwanza kufika kwenye maafa eti kutoa pole na rambirambi!

Ushauri wako Lukosi ulitolewa tayari na TUME YA LOWASSA miaka karibia 6 iliyopita;serikali ikapuuza ushauri wa "TUME YA LOWASSA"!Ukiendelea kutuletea kama ushauri habari ambayo serikali ilishauriwa miaka mingi iliyopita bila utekelezaji sio tu unaonekana kituko mbele za watu bali watu wanaweza wakadharau ushauri wako hapo baadae kwa kuonekana ni wa hovyohovyo hata kama ungeisaidia jamii!
Mkuu hata kama nimekurupuka ni kwa faida ya taifa letu.
Kwa hiyo unataka kuniambia kwa sababu tayari ushauri huo ulitolewa na haukufanyiwa kazi basi tukae kimya.?
Au ulitaka tufanye maandamano nchi nzima?
 
Hivi hapa JF kuna nini kinaendelea?. Hivi mtu kuja na mada ya kuisifia serikali kwa mazuri inayoyafanya imekuwa nongwa?. Mada aliyokuja nayo Lukosi ni nzuri na inaeleweka kabisa. Haiko Ki-CCM wala Ki-CDM bali iko Kitaifa, lakini kwa sababu Lukosi ni mwanachama wa CCM basi imekuwa nongwa. Watu wanaanza kumtupia maneno machafu Lukosi na Serikali. Jamani tafadhali tubadilike na kuwa wakweli ama la hatuendi popote. Tuipe serikali pongezi kwa yale mazuri inayoyafanya na tuikosoe kwa mabaya inayoyafanya huo ndiyo ukomavu wa kisiasa.

Mijitu hapa JF imekuwa inapinga kila kitu ama kila jambo linalofanywa na serikali iliyopo madarakani hata kama ni jambo zuri. Kibaya zaidi wanachama wengi wa JF wanafurahia mambo mengi ya CDM hata kama hayana faida kwa Taifa. Huo ni uzandiki na kukosa uzalendo. Tuwe wakweli na tuache fitina kwani ni hatari. "Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko"
Kwa issue kama ya kuanguka jengo na kuua watu, serikali inahitaji pongezi? Hata kama ni unafiki basi jitahidi kuwa na kiasi pia.
 
kuna ghorofa jingine linajengwa hapa sinza kwa remi nyuma ya shell ya big bon. likaguliwe
 
Mkuu hata kama nimekurupuka ni kwa faida ya taifa letu.
Kwa hiyo unataka kuniambia kwa sababu tayari ushauri huo ulitolewa na haukufanyiwa kazi basi tukae kimya.?
Au ulitaka tufanye maandamano nchi nzima?
Nawasikitikia waalimu waliokufundisha. Walitwanga maji.
 
isipokuwa kama wewe ni mgeni tz, kuna ukaguzi ulifanyika baada ya ghorofa kuporomoka chang'ombe village...badae jingine likaporomoka kariakoo......kisha jingine maeneo ya kisutu. Kumbukumbu ya haraka hili ghorofa la nne kurudi mavumbini.

Haya yametokea kati ya 2006 - 2013.

Sasa ndugu sijui unaiomba serikali ipi kukagua majengo haya

hata ukifanya utafiti kesho utaona kwamba katika maghorofa matano moja tu ndio lililo fuata taratibu. Je tupoteza hela za walipa kodi kuunda kamati ambayo ripoti yake itakuwa imechakachuliwa au haitaonekana kabisa .menye maghorofa hapo watalindwa tu. Ngoja yatokee mabadiliko serikalini kama kutakuwa na kuoneana aibu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom