Magharibi ya Kenya Wanaongoza kwa Kunywa Chai ya Moto Duniani. Chai ya Moto Inaweza Kusababisha Kansa ya Koo

Kinyungu

JF-Expert Member
Apr 6, 2008
17,230
32,630
Watafiti Wanasema Upo Uwezekano wa Chai ya Moto Kusababisha Kansa ya Koo.

Katika utafiti uliochapishwa katika jarida la Cancer Epidemiology watafiti wamegundua kuwa wenyeji huko Magharibi ya Kenya wanaongoza kwa kunywa chai ya moto zaidi Duniani. Kwa wastani wenyeji hao hunywa chai yenye nyuzi joto 72.1. Upande huo wa Magharibi ya Kenya wenyeji pia wanaongoza kwa kupata kansa ya koo (oesophagus) nchini Kenya.

Tanzania inafuatia kwa kuwa ya pili kwa unywaji wa chai ya moto duniani. Japo kuwa utafiti huu haujahitimisha bado kwa ukamilifu juu ya suala hili lakini watafiti hao wanaoanisha juu ya unywaji wa chai ya moto na kupata kansa ya koo.

60bf8b40-7c1a-4956-8393-62ba8c31c0ce.jpg

=================================
Western Kenyans 'drink hottest tea'
Scientists research possible cancer link

Scientists investigating a possible connection between the average temperature that people have tea and cancer of the oesophagus have suggested that people in Kenya, particularly in the west, drink the hottest tea in the world.

The study, published in the journal Cancer Epidemiology, looks into trying to explain why there are many cases of the cancer in western Kenya. "Thermal injury from hot food and beverages" has been mooted as a possible cause, it says.

According to a summary, the researchers have not drawn any definitive conclusions but suggest that the evidence should be evaluated further.

But Cancer Epidemiology has published a tea temperature chart indicating that, among the countries surveyed, Kenyans like it the hottest - at 72.1C.

 
Hizi tafiti nyingine zina taarifa za kutengeneza? Ina maana wanywa chai ni wengi kuliko wanywa pombe? nimesikitika sana kuwemo kwenye hili taifa la watu wanaopoteza muda wao na kunywa vinywaji visivyo na stimu
 
Lakini mkuu si inasemekana haijulikani hasa chanzo cha cancer ni nini au ni porojo tu
Huu utafiti bado sio conclusive. Lakini kama walivyosema walichogundua maeneo wanakokunywa chai ya moto sana pia wanaongoza kwa kupata kansa ya koo.

Pia upo utafiti unaosema kula vyakula vya moto sana kwenye vyombo vya plastic kunaweza sababisa kansa. Cha muhimu we jiongeze tu na kuchukua tahadhari.
 
This implies that western Kenyans wanaongoza kwa kuwa na kansa ya koo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom