Mageuzi.....tumaini lililopotea Tanzania

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,055
22,754
Kama kuna wakati mageuzi ya kweli yangeweza kutokea chini Tanzania ni katika ile miaka ya mwanzoni 1990 (early nineties). Nakumbuka 'wind of change' ilipoanza kuvuma na kuzikumba nchi za dunia ya tatu na hasa nchi za Afrika. Kwa masikitiko makubwa Tanzania pamoja na kuongoza kwenye hatua za mwanzo, ilipoteza nafasi yake katika kushika hatamu kwenye harakati za mabadiliko. Nani alisababisha kupotea kwa matumaini ya wanamageuzi Tanzania.

Kwa mara ya kwanza kijana wa Kitanzania aliweza kumwita Baba wa Taifa mufilisi kisiasa kama ilivyoripotiwa kwenye gazati la kwanza la binafsi kwa lugha ya Kiingereza "Family Mirror". Huyu Kijana, Mabere Marando, baada ya tamko hilo aliogopwa kama ukoma na alitengwa hata na baadhi ya ndugu zake. Hata hivyo yeye pamoja wanamageuzi wenzake waliweza kuteka mioyo ya wananchi kadhaa na wakisaidiwa na pressure kutoka nje, waliweza kuupiga vita ukiritimba wa CCM na kuushinda.

CCM ilipinga mageuzi kwa kutumia kila mbinu kama hofu, vitisho, ubabe, laghai na rushwa, lakini haikuweza kuzuia mabadiliko. Hata Baba wa Taifa baadaye alikiri kuwa hiyo tsunami ya mabadiliko ilikuwa haizuiliki. Tulishuhudia tena Mabere Marando akikataa uteuzi wa Rais Mwinyi kumwingiza kwenye tume ati ya kutafuna pesa nchi nzima kuwauliza wananchi kama wanaafiki vyama vingi. NCCR-Mageuzi ilizaliwa na chati yake ilianza kupanda kwa kasi iliyokuwa tishio kwa chama tawala, CCM.

CCM, kwa kutambua hatari iliyokuwa inawanyemelea, ilikuja na wazo la kupandikiza watu wake ndani ya NCCR-Mageuzi na wengine kuanzisha vyama lukuki , lengo likiwa kukisambaratisha. Mtu mmoja aliyetumiwa bila kujua anatumiwa alikuwa Augustino Mrema, mpinzani wa Mageuzi aliyekuwa msitari wa mbele kupinga mageuzi hata ikilazimu kutumia dola (FFU). Kashfa ya dhahabu uwanja wa ndege ilikuwa chachu tosha kumdhibiti Mrema na kuhakikisha anaondoka CCM na kundi la wafuasi.

Kitendo cha Mrema kuamua kuingia NCCR-mageuzi badala ya kuanzisha chama chake, kilifurahiwa na CCM kwa kuwa kiliwapunguzia kazi ya kukisambaratisha. Mapungufu ya Mrema yalijulikana hata kwa kipofu na haikuchkua muda mrefu mitafaruku ilianza kuiandama NCCR. Kitendo cha NCCR kumpokea Mrema na kumpa uongozi ndiko kuliua mageuzi ya kweli ya awali Tanzania.

Hivi sasa tuko kwenye mazingira yanayofanana na ya wakati huo. Nchi imedidimia kwenye tope la UFISADI. Kiongozi wetu ameonyesha udhaifu kama ule wa awamu ya pili na mabadilko hayazuiliki tena na ni muda tu. Tunaye kiongozi kiongozi ambaye ameonyesha kutokuogopa kusema bila woga na kuamsha hisia za wananchi wengi.

Je, safari hii tutasubiri tena pandikizi la CCM lije lituongoze katika hizi harakati. Naingiwa woga na watu wanaosubiri CCM ipasuke ndio apatikane Mrema mwingine. Hakuna mwalimu kama historia lakini tusipokuwa makini katika maamuzi HISTORIA INAWEZA IKAJIRUDIA - tusiipe nafasi.
 
maneno machache lakini ndani yake kuna busara... sasa ni jinsi gani wapinzani wa leo wanaweza kujifunza kutoka katika sataka la NCCR?
 
maneno machache lakini ndani yake kuna busara... sasa ni jinsi gani wapinzani wa leo wanaweza kujifunza kutoka katika sataka la NCCR?
Mkulu MMJJ, mimi kuhusu siasa kidogo pananichanganya. Ati mara waseme Mrema ni ccm mara walishasema Mabere Marando alikuwa ccm, mara waseme hata Mbowe naye ni ccm, sasa pananichanganya sana hapa. Sasa kama yote ni hivi, ni ngumu sana kwa wananchi wa kawaida kuchambua maana uwezo wa kuelewa ni mdogo sana kwa wengi. Naomba kufahamishwa kuhusu hili maana hapa akili yangu imeganda wakulu.
 
Mkulu MMJJ, mimi kuhusu siasa kidogo pananichanganya. Ati mara waseme Mrema ni ccm mara walishasema Mabere Marando alikuwa ccm, mara waseme hata Mbowe naye ni ccm, sasa pananichanganya sana hapa. Sasa kama yote ni hivi, ni ngumu sana kwa wananchi wa kawaida kuchambua maana uwezo wa kuelewa ni mdogo sana kwa wengi. Naomba kufahamishwa kuhusu hili maana hapa akili yangu imeganda wakulu.

Hii habari imekuwa twisted!
Si kweli...Hiyo ni version yake tu ya tofauti.
Ukweli unajulina.
Si unajuwa mambo kama ya Afro and Euro Centric point of views?
 
Hii habari imekuwa twisted!
Si kweli...Hiyo ni version yake tu ya tofauti.
Ukweli unajulina.
Si unajuwa mambo kama ya Afro and Euro Centric point of views?
Sasa nieleweje hapo Mkulu wangu, nani ni nani maana mimi siku nyingi nashindwa kuhusu hili, wakati mwingine unachanganyikiwa maana kama Mrema ana fujo kweli na unajiuliza mbona kila anapokaa panakuwa ni shida mkulu?
 
Sasa nieleweje hapo Mkulu wangu, nani ni nani maana mimi siku nyingi nashindwa kuhusu hili, wakati mwingine unachanganyikiwa maana kama Mrema ana fujo kweli na unajiuliza mbona kila anapokaa panakuwa ni shida mkulu?

Mwalimu keshakufa...Na kwahiyo huna wa kumuuliza kuwa ni kwanini alimpa nchi Mkapa zaidi ya kushangazwa na siri za usalama wa taifa wa meremeta na ufisadi mwingine ambao bado tunautafutia jina jipya kwenye kamusi yetu wazalendo.
 
Mwalimu keshakufa...Na kwahiyo huna wa kumuuliza kuwa ni kwanini alimpa nchi Mkapa zaidi ya kushangazwa na siri za usalama wa taifa wa meremeta na ufisadi mwingine ambao bado tunautafutia jina jipya kwenye kamusi yetu wazalendo.
Nakumbuka na hata wananchi wote walijua Mwalimu alimkataa Lowassa, Malecela na wengine akisema wazi ni watu wenye tamaa na ni wezi wakubwa hawafai kupewa madaraka. Nakubali pia kwamba hawa ndio waliomsaidia Kikwete kushika madaraka, Je, hatuwezi kumwuliza huyu huyu JK kuhusu haya maana anayajua?
 
Mkulu MMJJ, mimi kuhusu siasa kidogo pananichanganya. Ati mara waseme Mrema ni ccm mara walishasema Mabere Marando alikuwa ccm, mara waseme hata Mbowe naye ni ccm, sasa pananichanganya sana hapa. Sasa kama yote ni hivi, ni ngumu sana kwa wananchi wa kawaida kuchambua maana uwezo wa kuelewa ni mdogo sana kwa wengi. Naomba kufahamishwa kuhusu hili maana hapa akili yangu imeganda wakulu.

Akilimtindi,

Mrema kama Makamu wa Waziri Mkuu na Waziri wa mambo ya ndani katika serikali ya CCM aliyapinga mageuzi kwa nguvu zake zote na alikuwa kipenzi cha wakereketwa kwa staili yake ya siku saba na operesheni za zimamoto. Alianza kuwa na ndoto za kusonga mbele zaidi mpaka alipovuka mipaka yake ya kazi kwa kuwakera vigogo wenzake ndani ya CCM - kwa mfano alipovamia mali za wakubwa zikitoroshwa uwanja wa ndege.

Wakati anarukia gari la wanamageuzi alishaonja joto la jiwe na hiyo ikawa ni katika jitihada za kuipa uhai ndoto yake ya kufika ikulu. NCCR wakati huo ilikuwa imeshajipanga vilivyo kwa vijana wasomi na wasiokuwa na papara.
Watetezi wa Mrema wako wengi lakini ukweli ni kuwa alikuwa akitaka kula kivulini baada ya wahanga kuhangaika juani.
 
Wahanga gani?
Baada ya chama kupata umaarufu na wananchama wengi wakajidai kugeuka makubaliano yao ya awali kwani matumbo tu!
Wakatumia usomi wao kujenga hoja kwa kula na ccm!
Si unajuwa ni nani anakula kuku na ni nani anasota hadi sasa?
Si unajuwa ni nani bado ananyanyaswa na serikali?
Hapa jf utapata shida kama ukileta propaganda.
 
Wahanga gani?
Baada ya chama kupata umaarufu na wananchama wengi wakajidai kugeuka makubaliano yao ya awali kwani matumbo tu!
Wakatumia usomi wao kujenga hoja kwa kula na ccm!
Si unajuwa ni nani anakula kuku na ni nani anasota hadi sasa?
Si unajuwa ni nani bado ananyanyaswa na serikali?
Hapa jf utapata shida kama ukileta propaganda.

Kweli ukipenda chongo utaita kengeza.
 
wewe endelea kupenda kengeza na mimi nitabaki kupenda chongo...Shida ikwapi.
 
Akilimtindi,

Mrema .

Wakati anarukia gari la wanamageuzi alishaonja joto la jiwe na hiyo ikawa ni katika jitihada za kuipa uhai ndoto yake ya kufika ikulu. NCCR wakati huo ilikuwa imeshajipanga vilivyo kwa vijana wasomi na wasiokuwa na papara.
Watetezi wa Mrema wako wengi lakini ukweli ni kuwa alikuwa akitaka kula kivulini baada ya wahanga kuhangaika juani.

...acha fix zako wewe,bila Mrema NCCR was just a bunch of waganga njaa tuu na hakuna yeyote alikuwa anawajua zaidi ya pale Dar,haya kiko wapi baada ya Mrema kuwaachia chama chao? wameishia wote kurudi CCM kwa njaa zao.
 
maneno machache lakini ndani yake kuna busara... sasa ni jinsi gani wapinzani wa leo wanaweza kujifunza kutoka katika sataka la NCCR?

Mzee Mwanakijiji,

Hilo hasa ndilo lengo langu kubwa katika kutoa mada hiyo. Naamini mpaka sasa tunao watu kama Dr. Slaa ambao wameonyesha uwezo, ushupavu na ari kubwa ya kuongoza mabadiliko. Tunavyo vyama lukuki vimeshiriki katika chaguzi mbalimbali (na tunao watu wengi tu wamejitokeza kugombea uongozi) na mara zote tumeshuhudia vikisambaratishwa na CCM.

Kwa wenye nia njema na nchi yetu muda mwafaka wa kumtafuta kamanda ni sasa. Impact ya JF katika wazo kama hili ni kubwa. Tuunge mkono jitihada hizi na kuwaweka kwenye mizani wale wote wanaoonekana wana sifa sahihi na tuwapime kwa michango yao katika kupiga vita uovu unaoliandama taifa kwa wakati huu. Tusitake tena kubahatisha kama ambavyo imekuwa desturi yetu kila mara.

Tuwa"discourage" wasindikizaji wa kila msimu na tuwe tayari kuwanyoshea kidole na kuwaambia mapema kwamba "this time hapana" usituharibie. Kuongoza chama kusiwe tena kigezo cha kugombea Urais.
 
mageuzi ya kweli tanzania yanachelewa kuja kwa sababu watu takriban wote walioko madarakani wanaamini kufanya ufisadi ni haki yao.

hadi pale jamii itakapoamka na kujua kuwa mtu kutajirika akipewa tu wadhifa sio lengo la kupewa cheo kile ndio mageuzi yatakapopatikana.

hivi sasa japo kuwa watu wanajiita wanaunga mkono upinzani, lakini haki zao na haki za viongozi zao hawazijui. mtu anashangaa mkuu wa wilaya hana nyumba ya kifahari na kumuona fala badala ya kumtizama kwa kazi anazofanya.

mentality yetu ibadilike kwanza..
 
Kama kuna wakati mageuzi ya kweli yangeweza kutokea chini Tanzania ni katika ile miaka ya mwanzoni 1990 (early nineties). Nakumbuka 'wind of change' ilipoanza kuvuma na kuzikumba nchi za dunia ya tatu na hasa nchi za Afrika. Kwa masikitiko makubwa Tanzania pamoja na kuongoza kwenye hatua za mwanzo, ilipoteza nafasi yake katika kushika hatamu kwenye harakati za mabadiliko. Nani alisababisha kupotea kwa matumaini ya wanamageuzi Tanzania.

Kwa mara ya kwanza kijana wa Kitanzania aliweza kumwita Baba wa Taifa mufilisi kisiasa kama ilivyoripotiwa kwenye gazati la kwanza la binafsi kwa lugha ya Kiingereza "Family Mirror". Huyu Kijana, Mabere Marando, baada ya tamko hilo aliogopwa kama ukoma na alitengwa hata na baadhi ya ndugu zake. Hata hivyo yeye pamoja wanamageuzi wenzake waliweza kuteka mioyo ya wananchi kadhaa na wakisaidiwa na pressure kutoka nje, waliweza kuupiga vita ukiritimba wa CCM na kuushinda.

CCM ilipinga mageuzi kwa kutumia kila mbinu kama hofu, vitisho, ubabe, laghai na rushwa, lakini haikuweza kuzuia mabadiliko. Hata Baba wa Taifa baadaye alikiri kuwa hiyo tsunami ya mabadiliko ilikuwa haizuiliki. Tulishuhudia tena Mabere Marando akikataa uteuzi wa Rais Mwinyi kumwingiza kwenye tume ati ya kutafuna pesa nchi nzima kuwauliza wananchi kama wanaafiki vyama vingi. NCCR-Mageuzi ilizaliwa na chati yake ilianza kupanda kwa kasi iliyokuwa tishio kwa chama tawala, CCM.

CCM, kwa kutambua hatari iliyokuwa inawanyemelea, ilikuja na wazo la kupandikiza watu wake ndani ya NCCR-Mageuzi na wengine kuanzisha vyama lukuki , lengo likiwa kukisambaratisha. Mtu mmoja aliyetumiwa bila kujua anatumiwa alikuwa Augustino Mrema, mpinzani wa Mageuzi aliyekuwa msitari wa mbele kupinga mageuzi hata ikilazimu kutumia dola (FFU). Kashfa ya dhahabu uwanja wa ndege ilikuwa chachu tosha kumdhibiti Mrema na kuhakikisha anaondoka CCM na kundi la wafuasi.

Kitendo cha Mrema kuamua kuingia NCCR-mageuzi badala ya kuanzisha chama chake, kilifurahiwa na CCM kwa kuwa kiliwapunguzia kazi ya kukisambaratisha. Mapungufu ya Mrema yalijulikana hata kwa kipofu na haikuchkua muda mrefu mitafaruku ilianza kuiandama NCCR. Kitendo cha NCCR kumpokea Mrema na kumpa uongozi ndiko kuliua mageuzi ya kweli ya awali Tanzania.

Hivi sasa tuko kwenye mazingira yanayofanana na ya wakati huo. Nchi imedidimia kwenye tope la UFISADI. Kiongozi wetu ameonyesha udhaifu kama ule wa awamu ya pili na mabadilko hayazuiliki tena na ni muda tu. Tunaye kiongozi kiongozi ambaye ameonyesha kutokuogopa kusema bila woga na kuamsha hisia za wananchi wengi.

Je, safari hii tutasubiri tena pandikizi la CCM lije lituongoze katika hizi harakati. Naingiwa woga na watu wanaosubiri CCM ipasuke ndio apatikane Mrema mwingine. Hakuna mwalimu kama historia lakini tusipokuwa makini katika maamuzi HISTORIA INAWEZA IKAJIRUDIA - tusiipe nafasi.

Ndugu yangu una maoni mazuri sana. Lakini ni lazima ukumbuke kuwa NCCR lilikuwa ni pandikizi. Kilikuwa ni kikundi kilichoanzishwa na serikali kwa lengo la kuwa weaken wote walikuwa threat wakati ule kwa chama na serikali. NCCR was never meant to be opposition it was rather "opposition" kuwalaghai watu wa nje na kuifanya Tanzania ionekane kama kweli ni nchi yenye siasa za ushindani, ili wafadhili waendelee kutoa mapesa.
Lakini ukiangalia wengi wa waliokuwa NCCR walikuwa ni maofisa wa usalama wa taifa wenye lengo la kuwashughulikia watu kama kina Mrema, Kolimba etc hata Marando amewahi kukiri hilo. Kina Fundikira, Mapalala, Marando etc etc hao wote walikuwa maofisa usalama wasiokuwa na mema kwa nchi. Ndio maana Mrema alishindwa NCCR na wengine wote walioko NCCR watashindwa vilevile kile ni chama kinachotumika kuweaken opposition.
 
Back
Top Bottom