zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 18,913
- 28,522
Hii ni timu iliyobeba ubingwa wa La Liga 2013/14. Mchezaji pekee aliyesalia mpaka sasa ni Kiungo Koke Resurrecion ambaye ndio atakuwa nahodha rasmi kuanzia July 1.
Kufuatia kuondoka kwa wachezaji kadhaa muhimu wa Atletico Madrid msimu huu sasa ni rasmi wanaingia kwenye kizazi kipya ukizingatia wachezaji wao wakongwe kama nahodha Diego Godin,Felipe Luis na Juanfran ambao mikataba yao imeisha na umri kuwatupa mkono hivyo kuondoka mwezi huu.
Pia staa wao mkuu Griezmann ametangaza kuhama mwezi ujao na kuelekea Barca,PSG au Man utd. Huku Kiungo kisiki Rodrigo Hernandez akitarajiwa kujiunga na Man city kwa dau la €70 Million.
waliosajiliwa msimu huu lakini hawakufua dafu akiwemo Gelson martins na Nikola kalinic wataondoka pia dirisha hili.
Mchezaji mtukutu Diego costa pia anatarajiwa kuondoka kuelekea China baada ya kutofautiana na uongozi wa klabu akiwalaumu kutomtetea alipofungiwa mechi 8 kwa kumtukana refa.
Kwa mabadiliko haya ina maana Atletico madrid italazimika kusajili wachezaji zaidi ya 7 ili kuziba mapengo ya wanaoondoka dirisha hili.
Beki Lucas hernandez alishatimkia Fc bayern toka mwezi march kwa dau la €80 Million hivyo Atletico imebaki na mabeki 3 pekee katika list ya mabeki 8 ilionao!! Yaani Savic,Arias na Gimenez.
Mabadiliko (Beki)
Atletico tayari imemsajili beki wa kati kutoka FC porto kuziba pengo la Godin yaani Felipe Kwa €20 Million. Pia inatarajiwa kumsajili Mario Hermoso kutoka Espanyol kuziba pengo la lucas. Huku Alex Telles (Fc porto) na Ben Chilwell (Leicester) ama Alonso wa (chelsea) wakitazamiwa kuziba pengo la beki za kushoto. Pia kati ya Trippier(Spurs),Samedo(Barca) ama Aiden Hysaj( Napoli) anatarajiwa kuziba pengo la Juanfran na Santiago Arias.
Viungo
Kuziba pengo klabu inakaribia kumsajili Hector herrera (Fc porto) anayekuja bure. Pia Kama Rodri ataondoka Marcos Llorente (Real Madrid) ataziba pengo.
Washambuliaji
Dybala ama kinda machachari wa Benfica Joao felix ndio wanatazamiwa kurithi nafasi hiyo ya Griezmann. Pia kama Costa akiondoka pengo linatarajiwa kuzibwa na Edinson Cavani wa PSG.
PS: Atletico itakuwa na uwezo wa kufanya sajili zote hizi maana kabla hata ya kupewa fungu na utawala tayari Simeone atakuwa na takribani €250+ Million kwa mauzo ya wachezaji 3 tu yaani Rodri,Griezmann na Lucas. Na kama Oblak ataelekea PSG basi fungu litafika €370+ Million.
#Aupa Atleti #Los Colchoneros
UPDATE
Atletico yamsajili kiungo mkabaji Marcos Llorente kutoka Real Madrid kwa thamani ya €40 Million kwa mkataba wa miaka 5. Na amewasili ili kuziba pengo la Rodri Hernandez anayetimkia Man city
UPDATE 2
Atletico Madrid tayari imewasilisha Dau la €126 Million kwa klabu ya Benfica kwa ajili ya kinda mwenye kipaji Joao Felix hivyo inasubiriwa mpaka wiki ijayo atangazwe rasmi katika viunga vya Wanda Metropolitano.