Magenge ya utapeli Tanzania: Tupe stori kama umekumbana na kadhia zao

1. Papa Msofi
2. Ndama mtoto ya Ng'ombe
3. Mzamiri Katunzi
4. Jack Pemba!

Hawa watu kaa nao mbali sana,unapigwa pesa huku unajiona!
Papa Msofe walikua na ofisi ya Madini Mtaa wa Allykhan Upanga,wako vizuri mno ukiingia kwenye anga huchomoki
 
Kwa wanaosaka ajira sina cha kuwalaumu,maisha magumu sana wako njia panda ni rahisi sana kuwapiga maskini ya Mungu.

Ila hawa wa kwenye maisha ya kawaida,hapana kwakweli.tulizeni akili jamani.

Alikuja jamaa kijiweni kwetu akasema anaunga vifurushu vya internet bila kikomo kwa elfu 15,mimi kupewa taarifa nikabisha maana huwa mjuaji sana kwa kawaida.jamaa yangu akanitoa hofu na kunionyesha applications mbili ambazo jamaa huziweka kwenye simu yako,kisha kuingiza code ambazo yeye huziita pin kutoka kwa sever za boss wake,nikalainika.kumbuka kwamba taarifa hapa napewa na jamaa yangu ambaye kwa wakati huo anaperuzi kwa kasi ya 4g,mhusika keshaondoka.

Nikamkubalia jamaa kwamba ampigie jamaa huyo na kumweleza nia yangu,tunamcheki jamaa anauliza nyie akina nani,sisi-tunataka huduma yako ya vifurushi.akakataa hafanyi hiyo kazinikamtizama jamaa kwa ishara kwamba baba umepigwa.
Lisaa mojabele na intenet ikakata.
Ukiwa mtu wa kupenda kubishana Kwa hoja kutapeliwa ni vingum Sana maana matapel hawa pend watu wanao jifanya wajuaji
 
Back
Top Bottom