Magendo ya sukari in 2011?

Nyambala

JF-Expert Member
Oct 10, 2007
4,465
1,170
1. Wakuu hii habari ya sukari kuvushwa kwenda Kenya inasababishwa na nini?

2. Upungufu au ukosefu wa sukari nchini Kenya ni temporary?

3. Kwa nini serikali yetu isihamasishe sekta binafsi kuongeza uzalishaji sukari kwa kupanua mashamba, viwanda na miundo mbinu? Hizi si ndiyo zingekuwa ajira tunazoonyeshwa takwimu tu wkt hali halisi sivyo?

4. Ni kwa nini mpaka leo 2011 bado Tanzania haikitoshelezi kwa bidhaa hii ambayo ni very basic?

5. How come kanchi kadogo kama Malawi kanaweza kuzalisha sukari sustainably kwa watu wake na for exports kwa miaka yote hii?

My Take:
1. Inasikitisha kuona hii hali wakati Mtibwa ndiyo inajifia hivyo.

2. Mikoa kama Mbeya, Rukwa na Kagera walishaisahau sukari ya Tanzania kuanzia miaka ya 80, sasa na wao wakiwa included kwenye hii demand hali itakuwaje?

3. Kwa nini mpaka leo serikali yetu haioni kwamba hi demand ya bidhaa zetu za kilimo is a blessing, na hivyo kuweka mipango madhubuti kukuza sekta hii?

4. Hiii biashara ya sukari ya magendo hasa kutoka Zambia na Malawi ilikuwa popular sana miaka ya 80 na 90. How come mpaka leo 2011 kuna kitu kinaitwa magendo kwenye sukari?

5. Nini kinazuia sekta binafsi kujitanua katika uzalishaji wa sukari???????/
 
Nyambala:

Ubabaishaji na Ulegevu ndani ya SERIKALI unatupeleka pabaya ... Ipo siku hata chumvi itakuwa adimu ...

Well: Upungufu wa SUKARI (na any other basic commodity) unatengenezwa na kikundi fulani kwa manufaa yao ndani ya watawala ... Na ndiyo maana kila panapotokea "upungufu" hatua za haraka kuchukuliwa huwa ni "kuondoa KODI" kwenye bidhaa husika!
 
Jibwa lenyewe koko, wenye viwanda malawi na zambia ndio wenye kilombero sasa lazima watengeneze soko la viwanda vyao kwa kuweka shortage nyanda za juu kusini.
Wafanya biashara ya sukari hawafiki 6 na hakuna mmatumbi hata mmoja, zakaria ananunua zaidi ya nusu ya sukari yote na wanacheza na soko kupiga supernormal profit. Nyie mnapiga politike na kuuza magazeti na kudhani mungu atasaidia mambo yanyoke, katika value chain ya sukari mbongo yuko wasita na mlaji hana influence yeyote katika bei yeye ni price taker
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom