Elections 2010 Magazeti yalivyouripoti uchaguzi leo................

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
Majira..................Chadema na CCM ni balaa hapatoshi.......utabiri wa Sheikh Yahya wakwama.............

Habari Leo.........CCM, Chadema waumana Bara..................................

Mwananchi...............Masha, Batilda na Mramba maji shingoni..........................

Nipashe..........................JK, Dr. Slaa mchuano mkali..................................
 
Majira..................Chadema na CCM ni balaa hapatoshi.......utabiri wa Sheikh Yahya wakwama.............

Habari Leo.........CCM, Chadema waumana Bara..................................

Mwananchi...............Masha, Batilda na Mramba maji shingoni..........................

Nipashe..........................JK, Dr. Slaa mchuano mkali..................................

Haaa haaaa

Mtanzania na Uhuru je?
 
Jamani na huko Igunga na Monduli bado wanaopiga kura hawajamaliza?
 
Hii kali kwa michuzi mpaka sasa hivi kimyaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!
 
Mtu mpole, JK awezi kuitwa Dr huo ni kubaka taaluma tu, kinachotakiwa ni kuitwa jakara risho kikwekte tu.
 
jamani jamani nimecheka huku nasikitika, nimeona heading kwenye habari leo bibi ataka kumchagua nyerere
yaani watu wanafikiri nyerere yu hai!!!???? kweli elimu bado
 
UCHAGUZI uliofanyika jana nchini uligubikwa na vituko mbalimbali, kikiwamo cha bibi kizee kugoma kupiga kura mpaka aoneshwe picha ya Mwalimu Nyerere kwa wagombea urais.

Pia yaliyojitokeza ni pamoja na kutaka kuhujumu uchaguzi wenyewe, kwa baadhi ya watu kukutwa na vifaa vya kura saa chache kabla ya upigaji kuanza.

Jasmin Shamwepu anaripoti kutoka Dodoma kwamba kabla ya kupiga kura, kulibainika njama za wizi wa kura baada ya mmoja wa wasimamizi kubambwa akiwa na masanduku ya kura yenye karatasi za kura za ubunge na urais.

Hali hiyo ilijitokeza juzi saa mbili usiku, nyumbani kwa Msimamizi wa Kituo cha Makole, Mwalimu Wabuga Tarimo, ambaye alidai ilikuwa ni kwa usalama wa masanduku hayo kwani anaishi mbali na kituo

Nako Sumbawanga, Peti Siyame, anaripoti kwamba Polisi Mpanda mkoani Katavi imekamata wafuasi wanane wa CCM, akiwamo mgombea udiwani wa Kashaulili kwa tuhuma za kutembea usiku na silaha wakidai kusaka wafuasi wa Chadema.

Wafuasi hao wa Chadema wanadaiwa kuandika katika barabara za mji huo maneno ya kuhimiza wananchi wachague mgombea ubunge wa Mpanda Kati kwa tiketi ya chama hicho, Said Arfi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Isuto Mantage, alimtaja mgombea huyo wa udiwani kuwa ni Yasin Mlewa ‘Kantampa (52)' na kwamba tukio hilo lilitokea juzi saa moja usiku mjini humo.

Wengine waliokamatwa ni Deogratias Libe (22), Said Bernado (32), Stella Thomas (34), Naktu Abel (26), Anthony Abel (21), Boniphace Stephen (23) na Joachim Kwela (46).

Wakati huo huo, bibi kizee mwenye umri wa miaka 80 alikataa kupiga kura baada ya kutoiona picha ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwenye karatasi ya kura za urais, hata hivyo alipiga baada ya kushawishiwa na kueleweshwa.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Mji wa Mpanda, Hery Haule, alisema baadhi ya vituo wananchi waligoma kupiga kura baada ya kutangaziwa kuwa majimbo ya Mpanda Mjini na Mpanda Vijijini, hawatapiga kura za wabunge.

John Mhala, anaripoti kutoka Arusha, kwamba Polisi inamshikilia Mussa Abdallah Mussa (32), kwa kumpiga jiwe mgombea ubunge wa Arusha kupitia Chadema, Godbless Lema, wakati akikagua vituo vya kura.

Kamanda Basilio Matei alisema Mussa alimpiga jiwe mgombea huyo jana katika kituo cha shule ya msingi ya Uhuru kata ya Mjini Kati saa 4.30 asubuhi.

Mbali na Musa, Polisi pia inamshikilia Msimamizi wa Uchaguzi wa kituo cha Sombechini E, Charles Munisi akidaiwa kuzembea na kuporwa Daftari la Wapiga kura lenye majina ya watu 170.

Kwa mujibu wa Matei, Daftari hilo liliporwa mikononi mwa Munisi na waporaji kutoroka nalo.

Kuhusu Lema, Matei alisema mgombea huyo alikwenda katika kituo hicho kuangalia shughuli za upigaji kura kama zinakwenda sawa, lakini ghafla alijitokeza Musa na kumshambulia kwa maneno makali na kisha kumpiga jiwe mguuni.

Nakajumo James anaripoti kutoka Moshi kwamba Polisi Kilimanjaro, inamshikilia askari wake wa upelelezi, Sajini Marystella Soko, kwa tuhuma za kukutwa na kadi sita za wapiga kura kinyume cha sheria.

Kamanda Lucas Ng'hoboko alisema jana kuwa askari huyo alikamatwa Oktoba 30 saa 11 jioni akiwa na kadi hizo akidhaniwa kuzinunua kwa wahusika.

"Huyu ni askari wa upelelezi, hatujajua ni kwa nini alikutwa na kadi hizo … tunaendelea kumhoji kwa muda na upelelezi utakapokamilika tutajua hatua za kuchukua," alisema Kamanda.
 
TO BE CALLED Dr......There is technical certified requirements which jk DOES NOT AFFORD N;B this is why you see he was silence to claim!!
BESIDES ARE YOU ALSO THE SAME CHAIN TO THE MAN,WHY DON'T YOU KNOW IT EARLIER....

Ebu weka sawa kwenye gazeti la NIPASHE. Mbona Dr. kwa JK haipo?
 
Leo shehe Yahaya aongee na waandishi wa habari labda ataeleza namna ambavyo nguvu za Mungu zimemvurugia dili.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom