Mjadala: Je, ni kweli Magari aina ya Nissan Xtrail ni mabovu?

Wacheni kuwadanganya na kuwatisha watu, Nissan xtrail ni gari nzuri sana kama zilivyogari nyingine ikiwa utaitunza vizuri, kila kitu kinataka matunzo, hata mke au mume usipojitunza au kutunzwa utachakaa tu. Mimi ninayo Xtrail na sijawahi kusumbuka kwa chochote, na kwa safari za mikoani ndio utaifurahia inavyotulia barabarani.
 
Asante High Vampire kwa uzi mzuri.
Naomba nijue ubovu wa hz nissan x-trial.

Binafsi nazipenda coz naona ni gari yenye nafasi sana na je kwa ushauri wako kama nataka kuagiza nikiagiza Voxy au Noah ntakuwa nimecheza vema na opportunity cost (kwa ku forgone xtrial)

Asante.
Voxy na Noah model inayofanana na Voxy sio gari zile. Chukua Exurb Noah, hujajutia pesa yako.
 
Spea original zipo mkuu, labda huku pats fundi mzuri. Na ni gari ambazo ukifunga spea original unafuta namba ya simu ya fundi, sababu hautamuhitaji tena kwa siku za karibuni
Uko sahihi kabisa, gari za Nissan haziharibiki hovyo na hiyo inaweza kuwa moja ya sababu kwanini spea zake original kupatikana ni ngumu kwa sababu ya wauzaji kuona zinakaa muda mrefu madukani mwao.
 
Kuna jirani hapa limelala chini tumelitafutia mafundi hadi . kila Fundi anakuja na majibu yake kifupi limeatamia. sijui tatizo ninini

Kama alikosea kuanzia service ya kwanza hasa ktk kubadili ATF basi imekula kwake. Wengi hawaangalii ATF inayopendekezwa na nissan mwisho wa siku gear box inazingua sanaa. Lkn kama umeweka oil zake za kiwango huwez kupata ttizo lolote zaid utabadili sensor kama imechoka au plug. Nina uzoefu na hayo nissan xtrail. Tatizo la mafundi hawayajui haya magari na ukizingatia uwezo wao wa kufikiri wengi wao ni wa chini sanaaa.
 
Mkuu, naona nimekuja late.

Nissan X-trail zipo za aina mbili, zile zilizoundwa kati ya mwaka 2001-2007 na zile za tokea 2007 hadi sasa.

Hizi za 2001-2007 zinaweza kupata tatizo la engine kuunguruma kwa muda mrefu na kulifanya gari kama liwe linajivuta. Hii husababishwa na sensors kuanza kulegea hivyo kukosekana mawasiliano kati ya engine, sendors na engine management system.


Mara nyingi utaona taa ya njano kuashiria tatizo hili.

Tatizo lingine ni la camshaft ambapo timing belt inakuwa imechoka hivyo kuanza kuwa loose na kusababisha ku-jam na kupelekea pia brakes kushindwa kufanya kazi.

s-l1600.jpg

Nissan X trail lililoundwa kati ya mwaka 2000 na 2007

Pia kuna tatizo la mafuta kuvuja kwa X-trail za kati ya mwezi june mwaka 2000 - na November mwaka 2007 ambapo ule mpira wa kuingizia mafuta kwenda kwenye tank ya mafuta unakubali kutu kutambaa kwa kasi ya ajabu na kuleta uwezekano wa mafuta kuwa yanaishia hewani.

Hivyo kama unanunua gari hili la 2001- 2007, basi inakupasa uwe na fundi wako ambae ataangalia masuala haya mawili.

Kuhusu Nissan X-trail za mwaka 2007 hadi sasa nazo zina tatizo la steering control ambapo steering shaft inaanza kulegea na kusikika ikipiga kelele wakati wa kukata kona hivyo kupelekea siku moja dereva kushindwa kulidhibiti gari na kusababisha ajali mbaya sana.

Matatizo mengine ni kama yafutayo:

Turbo chargers kuanza kupiga kelele na moshi kuanza kuonekana kwenye engine na hii ni kwa yale magari ya Diesel.

Diesel filter kwa X-trail za diesel huwa zinajaza uchafu mapema Zaidi kuliko kawaida na hii hutokana na uharaka wa kuipiga moto engine na kutaka kuanza kuendesha wakati huohuo na kushindwa kuliacha gari lipige moto na engine ipate joto linalotakiwa.

Baadhi ya X-trail za kuanzia 2007 na kuendelea zina tatizo la umeme ambapo vifaa muhimu kama muziki , madirisha na dashboard kwa ujumla zinakuwa hazipati umeme wa moja kwa moja kutokana na hitilafu na wiring.

Hivyo basi , wakuu unapotaka Nissan Xtrail ya nguvu basi uzingatie matatizo hayo na uhakikishe anekununulia amefanya ukaguzi wa kueleweka kabla hajakabidhi mpunga uliouhangaikia.
Napenda x-trail ya 2007na kuendelea .spea zake zinapatikana dar.tatizo LA steering na umeme linauvumbuzi hapa bongo
 
Kwa hiyo ukishindwa kununua Xtrail bora ununue Subaru Forester ya 2008 tu. Manake ndo gari za kiumeni zilizobaki
 
Katika magari ninayotamani kuendesha ni hii Nissan, lakini maelezo ya wakuu hapo juu yamenikatisha tamaa kabisa. Bora niangalie uwezekano wa Brevis.
 
Hii gari iko stable barabarani. Kama ni suala la spare kuwa taabu ni tatizo la magari ya Nussan yote. Ila tatizo board yake plastic na ulaji wa mafuta uko juu.
 
Back
Top Bottom