Magari aina ya BMW na Mercedez Benz huwa na matatizo gani?

Wakuu Ni kwa nini watu wengi hawapendelei gari hizi? Tatizo ni bei na gharama za maintainance ama ni nini shida kubwa ya haya magari..?)

Kwanza hazitaki mafuta yenu haya mnachanganya na mafuta ya vitumbua pili pesa waswahili mnazo za kununulia michemsho madem kwahyo mstick na passo zenu lakin watu kama wakongo Zambia na kusini mwa africa hzo ndio gari zao toyota unatafuta kwa tochi hzo nchi...!af pia waswahil mshazoea kuigana kununua vitu bila kujua ubora niaje.
 
Nyingi naona kwa upande wangu hua pump zinasumbua kutokana na mafuta toka kwenye sheli tofauti mi nnanayo c class ila ni gari ambayo hutajuta kuitumia kama tu utaipenda kwenye services
 
Kwanza hazitaki mafuta yenu haya mnachanganya na mafuta ya vitumbua pili pesa waswahili mnazo za kununulia michemsho madem kwahyo mstick na passo zenu lakin watu kama wakongo Zambia na kusini mwa africa hzo ndio gari zao toyota unatafuta kwa tochi hzo nchi...!af pia waswahil mshazoea kuigana kununua vitu bila kujua ubora niaje.
 
Bmw na Merc sio gari za kawaida. Ni gari luxury kwahio hata maintanance yake ipo juu, sio sawa na carina,corolla etc. Ila ukiangalia bei ya used from Japan haina tofauti sana na toyota kwasababu ya demand. Ila gharama ya maintanance iko juu vile vile kwahio ukiwa nalo jipange usije kuambiwa shock absorber moja tzs 350,000 ukapata ugonjwa wa moyo.

Ila ni gari za starehe kweli na mbio mbio kweli.
Unaongea lak350 mi nina Nissan hardbody double cab shock ya monoroe mkuu juzi nimeweka 4set 2.2m moja laki5 nusu
 
Unaongea lak350 mi nina Nissan hardbody double cab shock ya monoroe mkuu juzi nimeweka 4set 2.2m moja laki5 nusu
Ila Nissan hard body ni gari ngumu sana....nafikiri ni Moja ya gari ambayo mjapani hakukosea...
 
Wakuu Ni kwa nini watu wengi hawapendelei gari hizi? Tatizo ni bei na gharama za maintainance ama ni nini shida kubwa ya haya magari..?)
Hakuna ubaya kwenye gari hizo ulizotaja lakini tatizo kubwa ni kasumba tuliyojijengea sisi waswahili kuwa hizo ni gari za gharama.....mie niliwahi kuwa na C-Class kompressor toka 2007-2012 sikuwahi hata kubadili fan belt wala plague. Na kuihudumia hiyo chuma ni cheap kuliko hata mark x.
 
Hakuna ubaya kwenye gari hizo ulizotaja lakini tatizo kubwa ni kasumba tuliyojijengea sisi waswahili kuwa hizo ni gari za gharama.....mie niliwahi kuwa na C-Class kompressor toka 2007-2012 sikuwahi hata kubadili fan belt wala plague. Na kuihudumia hiyo chuma ni cheap kuliko hata mark x.
Kweli mkuu...gari cheap sana Ku run....
 
View attachment 443027
Benz ya 2015 model zipo vizuri hizo mashine ni vile kodi yake ipo sawa na bei yake ndio maana tunakimbilia kwenye toyota hiyo gari ugusi kitu zaidi ya kumwaga oil kwa kipindi kirefu sana..
Mkuu hv German vrsn na intl vrsn km zle made in USA, znafanana ubora.....?? nackia mnyama ana mifupa migumu balaa sasa kwa za USA nazo zkakuwa hvyhvy........??
 
German Engineering = lets make simple things complicated so we can earn more from the pockets of our customers! Gari zao nzuri zikiwa mpya, warantee ikiisha, bora uiuze kabla haijageuka na kuwa jini kisirani. Hizi gari zao jamaa katika maintainance ndo utajua kwanini hata ukikaa katika AC unatokwa na jasho. Bei mkuu, na hasa 7 series au S class, uwe na pesa za kuchezea. Bakhressa Zanzibar anayo BMW 7 series i think imekaa pale katika nyumba yake, tangu nianze kuiona saivi yafika miaka + lakini gari haijawahi kusogea hata centimetre moja, sijui inatatizo gani. Lakini kwa nlivozisoma reviews za gari hizi inaonekana failure kubwa ni kutokana na system yake ya iDrive na mambo ya gearbox, ngoma inaweza kukugomea njiani tu bila sababu ya msingi, ikaganda gia ikawa haipandi wala haishuki
 
Natamani siku 1 nimiliki bmw 7 series Ile 545Li v8 kwa ajili ya matumizi ya weekend tu. Najua ni ugonjwa wa moyo lakini nta vumilia manake kwa gari ya 2002 inafika bongo na kukaa barabarani kwa m15 lakini ukipita nayo sehem hata ukutane na mtu ana land cruiser v8 ya 2017 hakugusi kwa attention na respect.
 
Natamani siku 1 nimiliki bmw 7 series Ile 545Li v8 kwa ajili ya matumizi ya weekend tu. Najua ni ugonjwa wa moyo lakini nta vumilia manake kwa gari ya 2002 inafika bongo na kukaa barabarani kwa m15 lakini ukipita nayo sehem hata ukutane na mtu ana land cruiser v8 ya 2017 hakugusi kwa attention na respect.
Mkuu hio unayosema wewe sio 7 series, io ni 5 series, 7 series ni kama 745i 745li 750, yaani ianze 7 ndio 7 series, i think umekusudia 745i, mkuu hizi gari zitakupa attention kutoka kwa watu sana tu, hata mwenye mark x new model ni cha mtoto kwako atakuwa, mana hii gari ni kama upo ndani ya ndege. ila wenyewe wanasema ni vyema ukatafuta za mwakaa 2004 kupanda juu, 2002 zimekuwa na matatizo mengi hasa kwenye idrive yake ambayo sana ndio inatumika kucontrols vitu vya ndani. Ukiwa nayo ujitaarishe kuishughulikia, ni zaid ya mke hio. Oil yake tu ya afadhali si chini ya 200,000, ukiweka izi za kila sik za buku 50 gari unaielekeza kwenye kaburi. Uzur wa toyota ni very easy kurepair, yani vitu vingi unaweza repair juu juu bila kufungua engine, ila hio 7 series ndugu, na hasa za 2002 zina ishu ya kuvuja maji, kuifix mpaka ufungue header i think, na hio repair kit yake, juzi niliona moja ambayo sio official recommended na BMW wenyewe ina cost kama $1500, hio ni ki pipe tu cha kupitisha maji. Wakati toyota pengine water pump laki 1 tu!

Ingekuwa BMW reliability yake ni kama toyota na parts zake ni cheap, amini mungu haikusimamii 15m, labda 25 au 30m mana kitu kiachwe tu tena. mimi BMW zinanimaliza luxury features zake tu
 
Mkuu hio unayosema wewe sio 7 series, io ni 5 series, 7 series ni kama 745i 745li 750, yaani ianze 7 ndio 7 series, i think umekusudia 745i, mkuu hizi gari zitakupa attention kutoka kwa watu sana tu, hata mwenye mark x new model ni cha mtoto kwako atakuwa, mana hii gari ni kama upo ndani ya ndege. ila wenyewe wanasema ni vyema ukatafuta za mwakaa 2004 kupanda juu, 2002 zimekuwa na matatizo mengi hasa kwenye idrive yake ambayo sana ndio inatumika kucontrols vitu vya ndani. Ukiwa nayo ujitaarishe kuishughulikia, ni zaid ya mke hio. Oil yake tu ya afadhali si chini ya 200,000, ukiweka izi za kila sik za buku 50 gari unaielekeza kwenye kaburi. Uzur wa toyota ni very easy kurepair, yani vitu vingi unaweza repair juu juu bila kufungua engine, ila hio 7 series ndugu, na hasa za 2002 zina ishu ya kuvuja maji, kuifix mpaka ufungue header i think, na hio repair kit yake, juzi niliona moja ambayo sio official recommended na BMW wenyewe ina cost kama $1500, hio ni ki pipe tu cha kupitisha maji. Wakati toyota pengine water pump laki 1 tu!

Ingekuwa BMW reliability yake ni kama toyota na parts zake ni cheap, amini mungu haikusimamii 15m, labda 25 au 30m mana kitu kiachwe tu tena. mimi BMW zinanimaliza luxury features zake tu
Kuna jirani yangu ana 745li kila nikimuona anapita nywele zina nisimama japo mara zote nanyoa kipara.
 
German Engineering = lets make simple things complicated so we can earn more from the pockets of our customers! Gari zao nzuri zikiwa mpya, warantee ikiisha, bora uiuze kabla haijageuka na kuwa jini kisirani. Hizi gari zao jamaa katika maintainance ndo utajua kwanini hata ukikaa katika AC unatokwa na jasho. Bei mkuu, na hasa 7 series au S class, uwe na pesa za kuchezea. Bakhressa Zanzibar anayo BMW 7 series i think imekaa pale katika nyumba yake, tangu nianze kuiona saivi yafika miaka + lakini gari haijawahi kusogea hata centimetre moja, sijui inatatizo gani. Lakini kwa nlivozisoma reviews za gari hizi inaonekana failure kubwa ni kutokana na system yake ya iDrive na mambo ya gearbox, ngoma inaweza kukugomea njiani tu bila sababu ya msingi, ikaganda gia ikawa haipandi wala haishuki

Hata Benz C class Zipo na Tabia Kama hizi???
 
Back
Top Bottom