Mag3 nasubiri kuona nchi inayumba kama itayumbishwa !!

Mkuu,

"Tumelilia Demokrasia tukapewa....." Hivi Demokrasia ni nini katika kufahamu kwako? Au kukubaliwa kwa mfumo wa vyama vingi kwa mbinu za kuuridhisha ulimwengu kwa kiini macho, kwako wewe ndio Demokrasia?

Hatamu za nchi, kwa maneno ya Mzee Julius Nyerere na kwa vitendo zilishikwa na bado zinaendelea kushikwa na CCM. Rais ndio Mwenyekiti wa CCM. Kukaa kwake kitini ni kwa ridhaa ya CCM. Naye ataendelea kwa hali na mali kuipendele
a CCM kwa kuwa ndio nguzo yake.

Unavyofikiri wewe huyo akiwa ndiye mwenye kuichagua tume ya uchaguzi, tunaweza kweli kuwa na tume huru? Uchaguzi ulio huru unajikita katika tume huru. Kimsingi Demokrasia ya kweli inategemea sana kiwanja sawa cha ushindani wa vyama vya kisiasa, ambao kwa hivi sasa hatuna.

Katika nchi yoyote iliyohuru, hatamu za nchi hushikwa na wananchi wenyewe na sio kushikiwa na chama chochote cha siasa. Na hatamu hizo zimo katika kuwawezesha wananchi kuwaweka viongozi madarakani na kuwaondoa hali kadhalika. Mtindo tulionao hauwawezeshi wananchi kuwaweka wala kuwaondoa. Uwezo huo ni wa CCM peke yake.

Je, hiyo ndio Demokrasi tuliyolilia na tuliyopewa?

Kama tuna Demokrasi kweli iweje leo hii tuna Katiba ile ile ya Chama kimoja iliyojaa viraka? Iweje mwananchi asiyekuwa mwanachama wa chama chochote
anyimwe haki yake ya msingi ya kugombea uongozi katika nchi yake mwenyewe? Iweje wakati wa kampeni na uchaguzi washindani watembezewe mkong'oto wao peke yao?

Che Nkapa akiwa Rais na Mwenyekiti wa CCM aisema hadharani kuwa atahakikisha ushindi wa CCM katika uchaguzi mkuu hata kwa kutumia vyombo vya dola. Naam, sote tuliushuhudia "ushindi wa tsunami na ushindi wa kishindo."

Je, hiyo ndio Demokrasi tuliyolilia na tuliyopewa?

Unalalamika kutembezewa chuki, nasi tunadai tutandaziwe haki na ukweli. Mizengwe ikizidi, wenyewe mnaita "wembe ule ule" na chuki haitakosekana.
Huwezi kucheza mpira na wakati huo huo kuwa mwamuzi ukategemea timu unayocheza nayo kushinda. Halafu unatuhimiza tujiunge na vyama vingine. Tukafanye nini kama si kuwa wasindikizaji tu? Au unatusanifu?

Ukumbuke tu kuwa hata Himaya ya Roma ilitoweka.

- Kwanza punguza jazba kwa sababu mimi sio rais wa jamhuri wala kiongozi wa jamhuri licha ya chama chochote cha siasa, ila ninasaidia kuongoza NGO ya kuwasaidia watoto wasiojiweza kwenda kupata elimu, that is all.

- Kwamba ninalilia anything hapana, ila ninatoa mawazo yangu, ambayo ni clear kuwa yako tofauti na yako, naona una vitisho vingi sana lakini mimi I have nothing to with anything, kwa hiyo jaribu kuheshimu haki yangu ya kuchangia mada hapa JF na sio lazima niwe na mawazo kama yako.

- Simjui mwananchi yoyote wa Tanzania aliyelazimishwa kwa bunduki kukubali demokraisa uchwara tuliyonayo sasa, kulifanyika makubaliano kati ya the then watawala na wawakilishi wetu wananchi kutoka upinzani, makubaliano yalifanyika yakatiwa saini na wahusika wote pale Ikulu na picha ninazo, mmoja wa waliosaini ni baba mkwe wangu kwa hiyo ninaelewa vizuri sana what happened na what did not, hakuwahi kuniambia kwamba waliwekewa bunduki kukubali, ila alikubali makosa katika haraka zao za kukubali yale makubaliano, ambayo sasa hivi wengi hapa JF hatuyapendi, lakini sio taifa zima la Tanzania.

- Unaonekana una some complex maana unajaribu kunitisha na maneno mengi hewa why? Kwa sababu mawazo yangu yako kushoto na yako au una mengine mkuu? I mean umesema maneno mengi sana ambayo mimi nikiwa mwananchi kama wewe hayanihusu kabisa, vipi mkuu are you okay maana ya Roma yanatoka wapi? Samahani mimi sio mkazi wa huko Roma ila ninatoka Dodoma?

Ahsante

william.
 
- Kwanza punguza jazba kwa sababu mimi sio rais wa jamhuri wala kiongozi wa jamhuri licha ya chama chochote cha siasa, ila ninasaidia kuongoza NGO ya kuwasaidia watoto wasiojiweza kwenda kupata elimu, that is all.

- Kwamba ninalilia anything hapana, ila ninatoa mawazo yangu, ambayo ni clear kuwa yako tofauti na yako, naona una vitisho vingi sana lakini mimi I have nothing to with anything, kwa hiyo jaribu kuheshimu haki yangu ya kuchangia mada hapa JF na sio lazima niwe na mawazo kama yako.

- Simjui mwananchi yoyote wa Tanzania aliyelazimishwa kwa bunduki kukubali demokraisa uchwara tuliyonayo sasa, kulifanyika makubaliano kati ya the then watawala na wawakilishi wetu wananchi kutoka upinzani, makubaliano yalifanyika yakatiwa saini na wahusika wote pale Ikulu na picha ninazo, mmoja wa waliosaini ni baba mkwe wangu kwa hiyo ninaelewa vizuri sana what happened na what did not, hakuwahi kuniambia kwamba waliwekewa bunduki kukubali, ila alikubali makosa katika haraka zao za kukubali yale makubaliano, ambayo sasa hivi wengi hapa JF hatuyapendi, lakini sio taifa zima la Tanzania.

- Unaonekana una some complex maana unajaribu kunitisha na maneno mengi hewa why? Kwa sababu mawazo yangu yako kushoto na yako au una mengine mkuu? I mean umesema maneno mengi sana ambayo mimi nikiwa mwananchi kama wewe hayanihusu kabisa, vipi mkuu are you okay maana ya Roma yanatoka wapi? Samahani mimi sio mkazi wa huko Roma ila ninatoka Dodoma?

Ahsante

william.

...wow......good initiative!......welcome back "william"
 
- Wanasonga mbele kwa kulipia kodi mfukoni mwa Kagame, kwa kulipia hata hata kuku wa kufuga nyumbani, are you ready for that?

William.

Hivi uko Tanzania kweli? mbona tunalipa kodi nyingi afadhali hata hiyo ya kufuga bata
Ukweli hawa jamaa hawana rasilimali kuliko sisi,hawana wasomi kuliko sisi,hawana amani kuliko sisi lakini kasi yao ya maendeleo ni kubwa kuliko yetu
 
1.

CCM kama chama haijawahi kupora mali za wananchi, lakini inao viongozi wachache waliofanya hivyo, na hata sisi wananchi wa kawaida pia tumehirikia sana kwenye kulipora taifa letu wenyewe, Mama Mary Kejo sio mwenyekiti wa CCM wa tawi lolote nchini.

William.

Kwa taarifa yako CCM wamepora viwanja vya michezo karibia mikoa yote ya Tanzania
Kirumba,Sokoine,Amri Abeid na vingine vingi
Kama ni viongozi wachache kwa nini msiwaondoe hamuoni kama wanachafua jina la chama
 
-
- Simjui mwananchi yoyote wa Tanzania aliyelazimishwa kwa bunduki kukubali demokraisa uchwara tuliyonayo sasa, kulifanyika makubaliano kati ya the then watawala na wawakilishi wetu wananchi kutoka upinzani, makubaliano yalifanyika yakatiwa saini na wahusika wote pale Ikulu na picha ninazo, mmoja wa waliosaini ni baba mkwe wangu kwa hiyo ninaelewa vizuri sana what happened na what did not, hakuwahi kuniambia kwamba waliwekewa bunduki kukubali, ila alikubali makosa katika haraka zao za kukubali yale makubaliano, ambayo sasa hivi wengi hapa JF hatuyapendi, lakini sio taifa zima la Tanzania.
Ahsante

william.

William, naomba usijaribu kurahisisha mambo kama unavyojaribu kufanya - je unajua kuwa kuna waliopata vilema vya maisha katika harakati za kudai demokrasia ya vyama vingi ? Je unajua njaa na kiu yetu kutaka utawala wa haki na sheria vyote vilitusukuma kukubali japo kwa shingo upande hako kadirisha kadogo ambako kangeingiza angalau kahewa kasafi ka utawala bora? Unajua kuwa tulichohitaji kwa wakati huo ni uzima (kwa kuwa tulikuwa na njaa kali) ili tuweze kuendeleza mapambano siku nyingine ? William, kukubali was only one step but a giant one for a country like Tanzania which had been under a one party dictatorship for over 30 years !

Kilichofuatia baada ya hapo ni hadaa, ulaghai na usaliti uliofanywa na chama tawala kwa lengo la kubakia madarakani. Wakati wapinzani wakiwa na imani kuwa tumeingia kwenye mfumo mpya, CCM ikajikita katika kufunga milango ya haki na usawa. Kumbe walikubali tu ili waweze kuendelea kufaidika na kutafuna misaada ya wahisani - misaada ambayo hadi leo matunda yake hayaonekani. Wakakataa katiba mpya, wakakataa kufuta sheria gandamizi, wakakataa kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi, wakakataa wagombea huru na wakakataa nguzo zote muhimu ambazo zingewezesha demokrasia ya kweli kushamiri.

Matokeo ya usaliti huu tunayashuhudia hadi leo kwa vyama pinzani kunyanyaswa na hivyo kudumaa ( wao hili hawalioni?), rushwa kushamiri kwenye chaguzi (si wana pesa?), unyanyasaji wa vyombo vya habari, uporaji wa miradi ya wananchi (kama majumba na viwanja vya mishezo na maegesho ya magari), bunge kuendeshwa kama kamati ya CCM na mahakama kutokuwa huru na hivyo haki kutolewa kwa upendeleo. Namkumbuka Wakili wa kujitegemea Marehemu Balonzi aliyejaribu kuishitaki CCM kwa kupora mali zilizochumwa na watanzania wote kwa ujumla wao na kuzimiliki - kesi ambayo ilishindwa kabla ya hata kuanza kusikilizwa !!

William, adui mkubwa wa taifa kwa hivi sasa ni CCM, period.​
 
- Punguzeni majungu na uzushi, toeni solutions sio kutuchonganisha wananchi na serikali yetu, kuna wananchi mnaonekana mngependa kuwona taifa letu linakuwa kama Rwanda, kila kukicha ni ku-preach chuki tu hapa solutions hakuna, hili ni taifa la ki-demokrasia sasa, jiungeni na vyama vya siasa mtusaidie taifa uchaguzi umekaribia, hizi tabiri kama za Sheikh Yahya hazina nafais tena kwenye demokrasia kama tuliyonayo.

- Tulilia demokrasia tukapewa sasa tuitumie kushiriki siasa ya taifa letu, sio ku-preach chuki kila kukicha wengine mnaonekana mnatoka Rwanda sijui, I mean hamuwezi mkaongea conctructive ila kupandikiza chuki tu katika jamii.

- Rais amewateuwa watendaji wa sheria, sheria tunazo sasa kama huridhiki na mamuzi ya serikali on sheria basi nenda ufungue kesi against serikali, mbona kina familia za kina Kombe waliishitaki serikali na kuishinda? Mara ngapi Mtikila ameishinda serikali mahakamani? Wakuu punguzeni kuhubiri chuki katika jamii tumieni demokrasia tuliyonayo kwa sababu mifano ipo kwamba it works!


William.

Mkulu Yaani hata kumaliza kusoma siwezi unatutisha kama kawaida yenu CCM kwa mifano ya Rwanda na Burundi, sisi hatutafika huko bali mkingangani madara hakuna njia nyingine.

Nakuomba hukiwa hapa kuwa na heshima na Nidhamu kwa wananchi badala ya kuwatisha, wewe unaona ndugu zako walivtoiba pesa za serikali wakati wananchi wanakufa na njaa halafu unasema tunataka tuwe kama Rwanda na Burundi.

Wakuu naomba kutoa Hoja

Huyu mtu aombe msamaha kwa kuwatisha wananchi kwa kuwa waendelee kuumia kwani vinginevyo wakatukwa kama Rwanda na Burundi

Mambo ya kutishana hakuna tutadai haki zetu kwa njia zote
 
- Kwanza punguza jazba kwa sababu mimi sio rais wa jamhuri wala kiongozi wa jamhuri licha ya chama chochote cha siasa, ila ninasaidia kuongoza NGO ya kuwasaidia watoto wasiojiweza kwenda kupata elimu, that is all.

- Kwamba ninalilia anything hapana, ila ninatoa mawazo yangu, ambayo ni clear kuwa yako tofauti na yako, naona una vitisho vingi sana lakini mimi I have nothing to with anything, kwa hiyo jaribu kuheshimu haki yangu ya kuchangia mada hapa JF na sio lazima niwe na mawazo kama yako.

- Simjui mwananchi yoyote wa Tanzania aliyelazimishwa kwa bunduki kukubali demokraisa uchwara tuliyonayo sasa, kulifanyika makubaliano kati ya the then watawala na wawakilishi wetu wananchi kutoka upinzani, makubaliano yalifanyika yakatiwa saini na wahusika wote pale Ikulu na picha ninazo, mmoja wa waliosaini ni baba mkwe wangu kwa hiyo ninaelewa vizuri sana what happened na what did not, hakuwahi kuniambia kwamba waliwekewa bunduki kukubali, ila alikubali makosa katika haraka zao za kukubali yale makubaliano, ambayo sasa hivi wengi hapa JF hatuyapendi, lakini sio taifa zima la Tanzania.

- Unaonekana una some complex maana unajaribu kunitisha na maneno mengi hewa why? Kwa sababu mawazo yangu yako kushoto na yako au una mengine mkuu? I mean umesema maneno mengi sana ambayo mimi nikiwa mwananchi kama wewe hayanihusu kabisa, vipi mkuu are you okay maana ya Roma yanatoka wapi? Samahani mimi sio mkazi wa huko Roma ila ninatoka Dodoma?

Ahsante

william.

Wewe ndio unatumia vitisho kwa kuwatisha wananchi wewe kaa chini ule pesa ya EPA lakini kumbuka kuwa hipo siku historia itawalipa.

Rudisheni pesa mlizoiba kwa KAGODA halafu huje tuongee hapa, ndio maana unakuja na vitisho unafikiri watu wataogopa? no one day mtalipa hata kama kwa mate.
 
Hivi uko Tanzania kweli? mbona tunalipa kodi nyingi afadhali hata hiyo ya kufuga bata
Ukweli hawa jamaa hawana rasilimali kuliko sisi,hawana wasomi kuliko sisi,hawana amani kuliko sisi lakini kasi yao ya maendeleo ni kubwa kuliko yetu

- Kama kweli wanayo maendeleo basi wame-sacrifice maisha na wananchi wao karibu Millioni moja, je are you ready for that?

William.
 
Kwa taarifa yako CCM wamepora viwanja vya michezo karibia mikoa yote ya Tanzania
Kirumba,Sokoine,Amri Abeid na vingine vingi
Kama ni viongozi wachache kwa nini msiwaondoe hamuoni kama wanachafua jina la chama


- Mkuu ni wapi nimewahi kusema kwamba mimi ni mwanachama wa CCM?

- By the way wewe ni mwanachama wa chama gani hicho Tanzania ambacho ni kisafi?

William.
 
If you are among great thinkers then I dont deserve to be in JF and call myself great thinker

- Sina mpango wowote wa kuwekeza kwenye ile kampuni, kwa hiyo usiwe na wasi wasi na mimi na usiogope kivuli chako mwenyewe cha ufisadi.

William.
 
1.
Jamco_Za;413470]Mkulu Yaani hata kumaliza kusoma siwezi unatutisha kama kawaida yenu CCM kwa mifano ya Rwanda na Burundi, sisi hatutafika huko bali mkingangani madara hakuna njia nyingine.

- Again, mimi sio mwanchama wa CCM, au chama chochote kile bado nina-shop arround kuona chama gani kina-fit mawazo niliyonayo juu ya taifa letu, kwa hiyo rekebisha hilo mkuu, na by the way wewe ni mwanachama wa chama gani cha siasa Tanzania?

2.
Nakuomba hukiwa hapa kuwa na heshima na Nidhamu kwa wananchi badala ya kuwatisha, wewe unaona ndugu zako walivtoiba pesa za serikali wakati wananchi wanakufa na njaa halafu unasema tunataka tuwe kama Rwanda na Burundi.

- Shujaa kama unavyojaribu ku-sound, kwanza ungeingia kwa jina lako la kweli, halafu ukawataja ndugu zangu kwa majina walioiba hela za serikali, wameiba ngapi? Lini na wapi?

- Nilipoamua kuingia kama nilivyo nilijua sana kuwa kutakuwepo wananchi kama wewe, watakaojaribu kutafuta ushujaa bila facts ili tu waoneakane na jamii hii kwamba ni mashujaa, mkuu jiunge na chama cha siasa Tanzania halafu kusaidie kuwashawishi wananchi kukichagua ili kurekebisha matatizo yaliyopo, badala ya kutishia nyau huku kwenye internent!

3.
Wakuu naomba kutoa Hoja

Huyu mtu aombe msamaha kwa kuwatisha wananchi kwa kuwa waendelee kuumia kwani vinginevyo wakatukwa kama Rwanda na BurundiMambo ya kutishana hakuna tutadai haki zetu kwa njia zote

- Cheap shots za kujaribu kukimbia kivuli chako, Tanzania tuna demokrasia mkuu sasa chagua utashiriki vipi katika hii demokrasia kulisaidia taifa letu, hakuna msaada kutoka hewani utashuka kukusaidia, ni mimi na wewe kuingia ndani ya demokrasia yetu na kuchacharika, acha kutafuta short cuts za kukimbia kivuli chako!

Ahsante Mkuu, so far so good tuendelee kuelimishana na kuelimisha taifa letu..



William.
 
- Kama kweli wanayo maendeleo basi wame-sacrifice maisha na wananchi wao karibu Millioni moja, je are you ready for that?

William.

Hivi nyie wakina malecela mkoje nyie? Mmelogwa? kaka yako juzi anachuchengua tu maneno kama mtoto wa std 7 wewe nawe unakuja na mifananisho isiyo na kichwa wala miguu. Kuwa great thinker ni kuwa na ng'ombe mia tatu halafu ijumaa unakwenda kuomba kwa wahindi? ukitizama sana utaona hiyo ndiyo mind yako sawa na ya asili yako!
 
Back
Top Bottom