Mafuriko Dar: Ujumbe kwa Nehemia Mchechu na Prof. Tibaijuka

Naweza kukuelewa labda kwa kuwa hawa jamaa wa mabondeni hawana mtetezi. Kama ni suala la utaratibu, vipi wale wa EPA? walichota na wakaambiwa warudishe? je utaratibu ulifatwa? Wabunge wameongezewa posho juzi tu na wote tunajua kuwa utjjaratibu haukufatwa lakini kuna hatua yoyote iliyochukuliwa? Hawa wananchi tokea wanaanza kuenga miaka zaidi ya 20 serikali inawaangalia na naamini hata wakati wa uchaguzi kuna vituo vya kupigia kura huwa vinafunguliwa na tume maeneo hayo. hata chama cha magamba kina watendaji wa kata maeneno hayo. Nadhani bado kuna ,maswali mengi hapo hatuwezi kusema wananchi ndo wana makosa peke yao
Mbunge wa Ilala bwana Zungu alikuwa na makazi yake pale Jangwani sijui kama na yeye ni mhanga ama la! Mwenye taarifa atuhabarishe. Nakumbuk jinsi alivyowatetea hao wa bondeni jangwani wakati mama Tiba aliposema wanatakiwa wahame. Zungu akasema serikali inataka iwahamishe ili wawe wanatoka masaki kwenda kula ice cream pale jangwani. Akasema wananchi wa jangwani waachwe waishi pale na watakuwa wakila ubuyu badala ya kufukuzwa na wa masaki kuja kulia ice cream pale jangwani. Sijui Zungu anasemaje sasa? Pale kuna wapiga kura wengi na Zungu alikuwa anaziwinda lakini madhara yake ndiyo hayo.
 
Kiukweli inaonesha wazi hili shirika la nyumba ni maalum kwa wale wenye uwezo na halilengi kutimiza maslahi ya watanzania ambao wengi wao ni masikini.Mtanzania ambaye baada ya kusota sana akabahatika kupata milioni 68 ni bora ajijengee nyumba yake kubwa!!! kuliko kununua hivyo viapartment,only non residents(foreigners) can afford!!!
 
Wazo lako zuri lakini utekelezaji wake ni mgumu sana kutokana na kwamba waathirika wa mafuriko japo si wote asilimia kubwa uwezo wa kujenga au kulipia nyumba mpya ni mgumu sana,ingawaje uwezekano upo kwa serikali kutumia nafasi hii kuupanga mji wa Dar lakini wasitumie nguvu waendelee kuwashawishi tu hawa waathirika.
 
Back
Top Bottom