Mafuriko Dar, mvua kali ikiambatana na radi yanyesha, umeme wakatwa

Nadhani hamkuelewa kwa nini niliandika Dar hakuna mvua. Mleta thread (Gaza) amesema "anasikia Dar kuna mvua, mwenye taarifa atoe". Ukiangalia muda aliobandika, ni saa kumi kasoro dakika kumi na sita jioni (15.44 pm). Mvua ya Dar imeanza saa kumi na moja alfajiri (5.00 am hivi). Angalieni interval ya time kutoka mvua ilipoanza hadi jamaa anapokuja kuulizia mafuriko (saa kumi na moja asubuhi hadi saa tisa jioni). Kwa mwana JF aliyejiunga Novemba 2010 ana uzoefu wa mwaka mmoja humu. Alichotakiwa kukifanya kabla ya kuanzisha thread ni kupitia title za walau page mbili hivi za 'New Posts' ambazo kila page ina post 50, so page mbili ni post 100. Ninasema apitie titles, si lazima azifungue. Kwa kupitia title za page mbili, utapata overview ya kinachoendelea nchini na duniani, so kama utataka kuuliza kitu ambacho ni breaking news, huenda ukakuta tayari watu walishabandika na hivyo hauna haja ya kuanzisha thread just kwa ajili ya kuuliza, kwa kuwa utapata majibu.

Tukirudi kwenye topic, mkuu Gaza wakati anauliza kwenye thread yake mpya hiyo saa tisa jioni, tayari kulikuwa kuna zaidi ya thread tatu zinazozungumzia mafuriko ya Dar. Kama angepitia titles kwanza, angekuwa na haja gani ya kuuliza kama ni kweli Dar kuna mafuriko? Nilitaka nitoe fundisho kwa wanaokimbilia kuanzisha threads bila kwanza kupitia zinazoendelea; hiyo ndo nia yangu.

Najua kuna watu wameudhika kwa maandishi yangu, nawaombeni msamaha. Lakini nami niliudhika kwa kuona mathread yenye maudhui yanayofanana yakiwa yanaanzishwa tu bila watu kuchungulia waliotangulia wameweka nini. Nina akili timamu, aliyeelewa atagundua hilo akisoma vizuri haya, na atakayeendelea kuunga mkono tabia ya uanzishwaji hovyo wa mathread, aendelee tu.
 
By DAILY NEWS Reporters, 20th December 2011 @ 18:00

Four
people have drowned and 8 others were seriously injured following three hours of heavy downpours that pounded Dar es Salaam on Tuesday morning.

The Dar es Salaam Regional Commissioner (RC), Mr Saidi Meck Sadiki, told the 'Daily News' in a telephone interview that four bodies were recovered from different areas of the city that were submerged in flood waters.

"So far, we can confirm that 4 people have lost their lives, and 8 others suffered serious injuries," said the RC who is also the chairman of the region's disaster committee.

He named areas that were severely hit by flashfloods as Tabata Valley, Kigogo, Mburahati (Ilala municipality), Tandale, Kwa Mtogole and Magomeni (Kinondoni municipality), a junction of Temeke and Kilwa road (Temeke municipality).

Mr Sadiki mentioned the names of the deceased as Ibrahim Tulihama,65, Maganga Saidi aged between 10 and 15, a woman, Gathi Mseti,39, and a baby whose identity was not known. He said the woman died after an electric post fell on her.

The RC added that Maganga Saidi was struck by lightning at his Mbagala home in Temeke.
"The remains of the victims have been preserved at Amana Hospital in Ilala pending burial arrangements," he said.

He said the injured were taken to Amana Hospital for medical treatment.

Mr Sadiki also said that the Msewe Bridge at Ubungo area in Kinondoni municipality was washed away by the floods and so were several city roads.

He quoted the Tanzania Meteorological Agency (TMA), as saying that the rains would continue to fall for some days.

In a random
survey, the 'Daily News' established that a number of Jangwani Valley residents along Morogoro Road had evacuated to the roadside, waiting for the floods to subside.

"We have been waiting since morning; I have a granddaughter trapped inside the house," said an old lady, who preferred anonymity. She was in the company of two granddaughters and two sons.

Reports from Morogoro say that flash floods have destroyed the railway at Gulwe Station in Kilosa District. The Tanzania Railways Limited thus suspended the passenger train on the central line on Tuesday.

In Dodoma rains accompanied by strong winds have destroyed 74 houses, leaving 269 residents of Ntyuka and Iyumbu homeless, according to Acting Dodoma Municipal Council Director, Nicolaus Buretta.

Meanwhile, a pedestrian died after being hit by a car near Mwananyamala Hospital along Mwinjuma Road in Kinondoni municipality on Monday.

According to the Kinondoni Regional Police Commander (RPC), Mr Charles Kenyela, the accident occurred at around 2:15 pm. He said the body was taken to Mwananyamala Hospital pending collection by his relatives.
 
Mvua kubwa ya aina yake inaendelea kunyesha usiku huu jijini Dar, ni mvua kubwa inayoambatana na radi kali, pengine leo kutakuwa na madhara makubwa kuliko yale ya jana iwapo kama watu waliojenga maboneni walirudi tena katika makazi yao. Hizi ni mvua za aina gani! Au ndio Mungu anafanya majaribio ya gharika!
 
...Nakumbuka kuna mvua moja iliwahi kunyesha Dar (sikumbuki mwaka gani) ilikuwa mvua kubwa sana ambayo hadi hii leo sijawahi kushuhudia mvua kubwa kama ile ambayo iliambatana na radi za kutisha sana. Tulijikusanya na kuanza kusali kwa woga uliosababishwa na mvua ile.
 
...Nakumbuka kuna mvua moja iliwahi kunyesha Dar (sikumbuki mwaka gani) ilikuwa mvua kubwa sana ambayo hadi hii leo sijawahi kushuhudia mvua kubwa kama ile ambayo iliambatana na radi za kutisha sana. Tulijikusanya na kuanza kusali kwa woga uliosababishwa na mvua ile.
el nino?
 
Jamani poleni sana. sasa naona serikali itabidi ichukulie hatua drainage za mji...
 
Dah!jamni kimara baruti wapeleke pantoni kwasababu kushageuka kigamboni
 
Mvua kubwa ya aina yake inaendelea kunyesha usiku huu jijini Dar, ni mvua kubwa inayoambatana na radi kali, pengine leo kutakuwa na madhara makubwa kuliko yale ya jana iwapo kama watu waliojenga maboneni walirudi tena katika makazi yao. Hizi ni mvua za aina gani! Au ndio Mungu anafanya majaribio ya gharika!

Vipi wandugu Ngeleja hajaambiawa kuhusu hiyo mvua manake tumechoka na mgao wa umeme na kawimbo kake ka MeGaTi. Eeh mungu wetu leta mvua ijaze mabwawa yetu ya umeme.!!
 
Jamani poleni sana. sasa naona serikali itabidi ichukulie hatua drainage za mji...

Aisee kwa mvua kama hii, serikali tutaionea. Manake hapa hata uwe na mifereji ya aina gani. Lazima ikubali sheria. Manake nimeona wingu linapita chini chini si kawaida hii.
 
Vipi wandugu Ngeleja hajaambiawa kuhusu hiyo mvua manake tumechoka na mgao wa umeme na kawimbo kake ka MeGaTi. Eeh mungu wetu leta mvua ijaze mabwawa yetu ya umeme.!!


Mkuu Chetmo, hayo mambo yanaenda mtera au kidatu au hare? Hayo maji yanapotelea baharini. Labda kama maeneo hayo nako kuna mvua za kutosha.
 
...Nakumbuka kuna mvua moja iliwahi kunyesha Dar (sikumbuki mwaka gani) ilikuwa mvua kubwa sana ambayo hadi hii leo sijawahi kushuhudia mvua kubwa kama ile ambayo iliambatana na radi za kutisha sana. Tulijikusanya na kuanza kusali kwa woga uliosababishwa na mvua ile.

Ilikuwa tarehe 13-01-2002 ilikuwa birthday ya mwanangu shughuli ilishia hapo kwa sababu radi ilipasua nguzo za umeme na kuunguza transfoma 3 pale Kijichi
 
Sababu nyingine nzuri ya kuendeleza mgao!!Ndugu waTZ shirika linapenda kuwaomba radhi kutokana tatizo la umeme lililotokana na ku haribika kwa nguzo moja hivi hukooo maeneo ya mabondeni maeneo yatakayo athirika ni. Nchi nzima kwa ujumla mtatusamehe please. Nyie wenyewe si mliona mvua?
 
Back
Top Bottom