Mafisadi wakuu Tanzania

Kokolo

JF-Expert Member
Mar 20, 2008
1,768
2,766
Orodha ya MAFISADI WALIOKUBUHU

1. Zakhia Meghji:-
(A) aligawa holela vitalu vya uwindaji akaipotezea Tanzania Tsh 3,304, 903,050/- akiwa waziri wa Mali Asili na Utalii.Ovyo zaidi hata wanafamilia wake walijiingiza katika ufisadi huo kwa kumiliki baadhi ya vitalu kibadhilifu
(B) Alipotosha ripoti ya mkaguzi wa BOT mwaka 2005/2006
(C) Kuchonga bajeti angamizi ya mwaka 2007/2008
(D) Kuidhinisha matumizi mabovu zaidi ya millioni 143 kwa mawaziri mafisadi kwenda kuifagilia bajeti ya kihuni ya 2007/2008 mikoani. Mafisadi hao hawakusita kukomba millioni 143 Tsh kwenda kuzomewa mikoani.
(E) Kufumbia macho shughuli fisadi na za kitaprli za BOT ambayo iliipatia Tangold ltd Kampuni feki kiasi zaidi ya Sh 37.7 billioni ambayo haikuwa na usajiri wowote, akidanganya kuwa ni matumizi nyeti ya serikali kumbe ni ulaji wake na vigogo wenzake
(F) Kubarikli uporaji wa fedha BOT tsh 18,465,755,495.39/- zilizopelekwa kwenye makampuni mbalimbali feki kuanzia decemba 2005 hadi 2007.

2. Benjamini Mkapa:
(A) Kufanya biashara akiwa ikulu ambacho ni kinyume kabisa na katiba ya nchi yetu
(B) Kuanzisha makampuni mufilisi akiwa ikulu ambayo yamelipora taifa zaidi ya Tsh 908,798,045,050/- akiwa ikulu hadi leo kwa makampuni ya kihuni kama ANBEN ltd, Fosnik ltd na Tanpower
(C) Wizi wa zaidi ya Tsh Trillioni 8,86 BOT kwenye kampeini za uraisi na ubunge zilizotuwekea rais mufilisi. Mkapa anatakiwa asimame kuelekea kizimbani na kujibu wizi huo ulioifilisi nchi ikawa kama dampo la umasikini
(D) Uporaji fedha za taia hili kupitia ununuzi wa rada feki Tsh 50 billioni ambayo aliishupalia kama ruba
(E) Uuzwaji angamizi wa mashirika ya umma na viwanda kwa hila zote, kwani hata yale yaliyokuwa yakijiendesha kwa faida kubwa yaliuzwa kwa bei ya tupatupa (throw away prices)
(F) Kushiriki mikataba mibovu ya madini alilipotezea taifa zaidi ya Tsh 959,588,789,005/- kwa kipindi chote Hivyo huyu ni fisadi lililokubuhu.

3. Edward Lowassa
(A) Anahusika moja kwa moja na ufisadi kupitia kampuni haramu ya RICHMOND na shoga wake DOWANS ambao wamelipora taifa zaidi y ash billioni 273/- kwa umeme hewa
(B) Upotevu wa sh millioni 12.5 /- kupitia kampuni feki ya Water City ambayo aliibariki licha ya kuambiwa kuwa ilikuwa haifai, lakini E.L. aliingilia kama alimasi
(C) Kuliingiza taifa kwenye mkataba mufilisi ,fisadi na angamizi wa Buzwagi . E.L. alikuwa pamoja na fisadi kuu Karamagi kusaini mkataba angamizi na filisi hotelini uingereza. Hivyo analipotezea taifa zaidi ya billioni 3,895/- kila mwaka kwa muda wa miaka 25 kama ulivyo mkataba
(D) Kujiingiza kwenye uporaji kwa kutumia ujenzi wa mahekalu ya hoteli ambayo hayalingani na kipato chake, akibisha data hallisi tutazianika hadharani.

4. David Ballali
(A) Amelipotezea taifa kifisadi zaidi ya sh 693,795,398,805.39/- kupitia BOT kwa malipo hewa kwa makampuni hewa ya kitapeli ya EPA, Jeetu P.ltd, Alex Stewart, Tangold ltd, Mwananchi gold co.ltd, Green F. Co.ltd na mengine mengi,
(B)Kulipotezea taifa matrillioni ya fedha kwa kukwamisha ukaguzi halisi wa BOT
(C) Trillioni 5.3 alizochota kwa ajiri ya kampeini haramu za urais za mwaka 2005 zilizozaa rais mlea mafisadi. The breeder of corrupt leaders at all level

5. Basil Pesambili Mramba

(A)Alibarikina kuhusika na uporaji wa sh 17,697,556,594.85/- kutoka BOT akiwa waziri wa fedha kwenda kwa makampuni mbalimbali feki na watu binafsi hasa magabacholi wa kihindi na kiarabu
(B) ununuzi wa ndegefeki ya rais, rada feki ya rais. Alitangaza Watanzania hata wakila majani ndege feki ya rais lazima ingenunuliwa. Je, mr.. Mrmba, uliona Watanzania ni mbuzi hata wale majani?
(C) Uuzaji feki wa Air Tanzania kwa makaburu. Asingeiingilia kikwete Hapa Mrambaji angetajirika ukomo. (D) Ubinafisaji holela na kwa kiburi na uhujumu wa rasilimali za tiafa kwa masilahi yake akiwa waziri wa fedha , walishirikiana na fisadi ambaye ni rafiki wake wa damu -Abdallah Kigoda

6. Andrew Chenge
(A) Kalipotezea taifa zaidi ya sh 17,857,616,400/- zilizoporwa na Tangold ltd kutoka BOT . Chenge hili hawezi kukwepa kwani alikuwa mkurugenzi wa Tangold ltd at the same time akiwa mkurugenzi wa BOT
(B) Kulipotezea taifa mabillioni ya fedha kwa kuridhia mikataba mibovu/feki/angamizi ya madini akiwa mwanasheria mkuu wa serikali. Takribani zilipotea zaidi y ash 2,890,687,084,573/- kwa kipindi chake chote. Kama anabisha tutazitoa kwa unyambulisho wake.
(C) Zaidi ya billioni 800 zianpotea kwa mwaka kwa mikataba mibovu ya ujenzi wa barabara ama kwa kuweka makampuni feki ambayo huishia kuchota fedha na kutoroaka nchini na vitita vya fedha. Ana kurugenzi wezi wizarani kwake lakini amefumbia macho kwa manufaa yake binafisi. Chenge unasubiri nini kungCcā,?ā"catuka?

7. Gray Mgonja

(A) Alibariki na kuhisika na uporaji wa sh 17,857,616,400/- BOT kwenda kampuni yao ya tangold ltd akiwa mkurugenzi wa BOT pia hapo hapo akiwa mkurugenzi wa Tangold ltd kampuni ambyo hikuwa na usajili.
(B) Kunyamazia ufisadi wa uporaji wa trillioni za fedha BOT kenda kwenye makampuni hewa akiwa mkurugenzi BOT

8. Peter Msolla
(A) Uporaji wa sh billioni 5 zilizokuwa zimetolewa na EUROPEAN OVERSEAS AGENTS miaka ya 90 akiwa makamu mkuu wa SUA. Fedha hiyo ilikuwa imetolewa kukiendeleza chuo(SUA) kitaaluma, miundo mbinu kama barabara za ndani , tafiti mbalimbali na kuwa dila ya maendeleo ya kanda ya mashariki mwa Tanzania (Morogoro, Pwani, Tanga, Dar-es salaam). Cha ajabu fedha hiyo iliishia kwenye midomo ya mamba mafisadi (Prof Msolla, Prof Ishengoma, Mr A.. Magoma (Mhasibu wa kufoji ), keshia Prof Mgongo na maswahiba wao.. Planner mkuu wa wizi huo alikuwa Magoma wakisaidiana na Msolla. Wakaamua kununua magari ya kifahali na kujenga majumba ya kifahari yakiwapo magesti house kwa siri.
(B) Uporaji wa fedha za DANIDA millioni 490 zilizokuwa zimetolewa kwa ajili ya mradi wa OTAITISI (OTITIS) .Fedha hiyo iligawanywa hapo vet SUA na kunguru mafisadi wachache. Msola akachukua 80% ya fedha hiyo na kujenga majumba makubwa ya kifahali . Ngombe wa Mradi huo wakaishia kulala kwenye matope yafikayo kwenye kimo cha tumbo lao wakiwa wamesimama.. Wafadhili walikasirika kupita upeo, wakajitoa. Ukweli huu hauhitaji hata kupeleleza pale VET-SUA.
(C) Hujuma ya fedha ya punguzo la wafanyakazi SUA Tsh 2,245,045,000/- ilyotolewa na benki ya dunia 30/6/1996. Ilipangwa kwamba mtu mwenye mshahara mdogo kabisa apewe Tsh millioni 8. Jambo la kushangaza ni kwamba kila mtu aliyepunguzwa kazi alipewa asilimia kumi tu (10%) ya malipo yake. Hivyo mwenye mshahara mdogo alipewa sh 300,000/- tu. Aliyekuwa anatakiwa kulipwa millioni 20/- alipewa millioni tatu tu. Yeye Msolla na mafisadi wenzie (A.Magoma, Prof Luoga akiwa VC-SUA, Prof Mgongo, keshia na maswahiba wao waligawana 90% ya fedha yote iliyotolewa na benki ya dunia... Mafisadi hawa wakawa wanaishi kama wapo peponi. Wakanunua magari ya kifahali na kujenga majumba ya KUFURU yakiwamo magesti house bubu (kwa siri) na kununua mashamba kila kona Mkoani Morogoro.
(D) Wizi wa millioni 442 SUA kuamkia tarehe 22/4/2006.Yaani, Kati ya shs 442, shs millioni 400/- zilikuwa peti keshi zilizokusanywa kwa miaka miwili . Hivyo Msolla, Keshia, Prof Luoga na Magoma waliziiba zile millioni 400/- mchana kweupe tarehe 21/4/2006 kutoka kwenye sefu, baadaye wakaingiza sh millioni 42/- za malipo ya wafanya kazi SUA, ndipo kesho yake tarehe 22/4/2006 wakatangaza kuwa sh millioni 42/- za malipo ya wafanyakazi SUA ziliibiwa. Kwa uhakika zilizohamishwa kiporaji zilikuwa sh millioni 442(millioni 42 zikiwa malipo ya wafanyakazi SUA na millioni 400 zikiwa peti keshi ) . Sababu ya uporaji huo wa kifisadi ni:
(i) kujiandaa kwa kustaafu kwa prof. Luoga, Mr Magoma na Msolla
(ii) Kutokuwa na imani na Kikwete kwani SUA walitegemea Sumaye ndiye angekuwa rais ambaye ni fisadi mwenzao. Hata hivyo hawakujua kuwa hata Kikwete ni mama na mlezi wa mafisadi
(iii) Kupata fedha lukuki za kufanyia kampeni za ubunge kwa Msolla na hatimaye uwaziri. Hivyo kesi hiyo aliisimamia Prof Monera kwa ahadi kwamba kama angefanikiwa kuivunja kesi hiyo angekuwa VC. Monera alifanikiwa kuizima kesi hiyo, Prof Luoga na Msolla wakampendekeza kwa rais awe VC ili siri hii isifichuke. Kikwete akaingia kwa jeuri yake kichwakichwa akaweka fisadi pandikizi kuwa VC- la SUA ambalo linakomba fedha ya SUA na ya wafadhili likishirikiana na Mufilisi mwenzie Prof Msolla kiasi kwamba, fedha ya wafadhili inayopitia Wizarani (Sayansi na Elimu ya juu) kwenda SUA igawanwe na kukombwa vizuri.

9. Joseph Mungai

(A) Aliingiza silabasi feki kuanzia chekechea hadi elimu ya sekondari kwa Watanzania wa kawaida huku watoto wao wanasoma nje ya nchi.Watoto hapa nchini hawakujua walichokuwa wanasoma, si jogg ama mchemsho. Akaua elimu kupindukia. Alifanya hivyo ili fedha nyingi zibaki wizarani ili azitumie na mafisadi wenzie kwa masilahi binafsi. Zaidi ya billioni 300 zilikuwa zinaliwa wizarani kwa ufisadi huu.
(B) Alikula takribani sh millioni 8/- za bima na likizo za waalimu na mapunjo mbalimbali ya waalimu yakiwamo ya mishahara ya walimu wa shule za msingi na sekondari.Waalimu wakapiga kelele kudai haki zao wakaonekana kutimiza usemi kwamba KELELE ZA MLANGO HAZIMKOSESHI USINGIZI MWENYE NYUMBA.
(C) Kupora fedha inayobaki wizarani mwisho mwa mwaka. Kapuya alichagua baadhi ya maofisa wa elimu wa mikoa/wilaya na mahedimasta wa shule za sekondari ambako alikuwa akituma fedha mwishoni mwa mwaka (mwezi wa 5) na baadaye kutuma wahasibu mafisadi kuifuata fedha hiyo. Alikuwa akipora kati ya sh billioni 3-4 kwa mtindo huo kila mwaka alitafuna na maswahiba wake

10. Juma Ngasongwa
(A) Kalipotezea taifa zaidi ya sh Billioni 9,845/- kwa kipindi akiwa waziri wa Mali Asili na Utalii kwa kupewa pipi kidogo na kuachia uwindaji haramu na angamizi kwa rasilimali na uchumi wa nchi. Ufisadi huu ulimfanya afukuzwe uwaziri wakati wa MZEE RUKSA kwani mzee ruksa alikuwa makini. Hakuwa kama Kikwete ambaye amefunga ndoa na mafisadi kama Kapuya, Ngasongwa, Meghji, Ballali, Msolla, Diallo, Benno Ndullu nk.
(B) Kuchochea vurugu SUA... Yeye alipoona kuwa wanafunzi wa SUA wamemkataa kwa kuwa alikuwa haeleweki anachofundisha , si DS ama DESKI CHAFU, alianza vurugu zilizomfanya afukuzwe kazi SUA katika miaka ya 90. akakimbilia siasa. Vilevile mzee ruksa akamfukuza kazi Mali asili na utalii katika miaka ya 90. Bwege Mkapa akamrudisha kuhujumu, pia Kikwete akameza matapishi hayo hayo.

11. Stephan Wasira

Mamillioni ya fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya kupunguza makali ya mbolea ameyakomba.. Yaani, fedha ya sabsidi ya mbolea zaidi ya sh billioni 12,5 ameifagia na kufanya bei ya mbolea kuanza kupaa juu kama kunguru kila kukicha katika mikoa ya nyanda za juu kusini The big four (Mbeya, Iringa, Ruvuma na Rukwa). Kilimo katika mikoa hiyo hutegemea mbolea asilimia mia moja(100%). Sasa mbolea haishikiki kwa wakulima wengi (90%) kwani ni kati ya sh 40,000/-sh 55,000/- kwenye mfuko wa kilo 50. Kwa ekari moja inahitajika mifuko 4-5 kutegemea na hali ya udongo husika. Mbaya zaidi , si Kikwete wala Wasira anayetembelea mikoa ya Mbeya, Iringa ama Rukwa tangu wawahadae wananchi kuwaletea maisha mazuri. Huu ni utapeli wa unaotakiwa ulaaniwe na kila mpenda haki. Kila leo utamwona Kikwete akitembelea KWA WASUKUMA (MWANZA NA SHINYANGA), BUKOBA NA MUSOMA, PWANI NA MOROGORO MAANA AMEYAONA MAJITU HAYO ZUMBUKUKU.

11. Nazir Karamagi
(A) Kufanya ufisadi wa kusaini mikataba angamizi ya madini kama ya Buzwagi nje ya nchi hotelini!!!!!!!!!!!! Uliolikosesha taifa sh 9,239,389,394.25/- kwa kipindi chote
(B) Kuligharimu taifa zaidi ya billioni 173 kutokana na uroho wa kujitumbukiza kwenye sakata la kampuni tapeli ya RICHMOND na binti yake DOWANS
(C) Kunyamazia kupanda kwa umeme kwa walipa kodi maskini ili kufidia gharama angamizi za TANESCO zinazotokana na mafisadi vigogo kutolipa gharama za umeme.

12. Ibrahim Msabaha
(A) Kulipotezea taifa zaidi ya sh billioni 174 kutokana na kufunga ndoa na kampuni mufilisi , feki na tapeli ya RICHMOND . Anatakiwa akamatwe atiwe ndani na alipe deni hilo .

13. Benno Ndullu
(A) Kabariki ufisadi na uharamia wa sh 693,795,398,800/- zilizohamishwa kijambazi na kaka zake (Ballali, Mramba, Zakhia M) akiwa naibu gavana wa BOT. Hili halikwepi. Tunajua amewekwa pale na Kikwete ili kuficha ushahidi wa mafisadi wenzie wakiwemo watoto wa vigogo. Hapa tayari anaingia kwenye kundi la mafisadi.
(B) Kutomshauri Kikwete avunje bodi inayoshughulikia kutafuta kiini cha ufisadi BOT, kwani bodi hiyo imejaa mafisadi kama G. Mgonja, Zakhia Meghji nk Hivyo hakuna chochote kitakachofanyika zaidi ya kwenda kuficha ushahidi.

14. Edward Hosea

(A) Amekomba zaidi ya billioni 65 kwa kupokea rushwa nene na kutoa taarifa feki kwenye uchunguzi wa RICHMOND , sakata la Buzwagi, mikataba mibovu ya madini, sakata na hujuma za wahindi kupanga kwenye nyumba nzuri za National Housing kuliko wazawa, Sakata la DOWANS na hujuma nyingine nyingi... Ni fisadi anayetakiwa ajiuzuru mara moja.

USHAURI KWA WAPINZANI
(1) Shinikizeni kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi itakayochaguliwa na wabunge mseto. Yaani wabunge 2 CCM, 2 CHADEMA, 2 CUF, I TLP, I UDP na isiwajibike kwa kingunge yoyote bali kwa maslahi ya kitaifa. Msipofanya hivyo, mtakuwa wasindikizaji watindikiwa katika uchaguzi wa mwaka 2010. Hata taahira huwa hashiki moto.
(2) Tembeleeni vijijini mkawaelimishe watu wanaodanganywa na CCM kila kukicha, kwani huko ndiko kuna zaidi ya 85% ya wapiga kura nchini..Wanaishi maisha magumu kama wako mahabusu ya uhaini ndani ya nchi yao lakini hakuna wa kuwaelimisha Kikwete ndio amewasusa watu wa Mbeya, Iringa, Rukwa na Ruvuma huku akiita mikoa hiyo THE BIG FOUR na kunadi kuwa kilimo ni uti wa mgongo na kuwasuta akisema kuwa mbolea ya ruzuku haipo , wasibweteke, watainunua tu hata kama bei yake inapaa kama tai kila kukicha.. Kwa akili finyu ya watanzania, mwaka 2010 atajipitisha kwao na kuwafanya wasahau kuwa aliwahi kudondoka chini akiwahadaa maisha bora katika kura za mwaka 2005. Hivyo wapinzani tembeleeni vijijini maana mjini watu wanawaelewa.
(3) Piteni mkiwaambia watanzania kuwa MAFIGA MATATU YA KIKWETE ni kurudisha utawala wa chama kimoja wenye kubariki kila ufisadi na mafisadi wa uchumi wetu na rasilimali za taifa. Utawala wa kidikiteta na mufilisi bila kuhojiwa na mtu yeyote kwani bunge linakuwa na mafisadi wanaotetea mafisadi , ufisadi na hujuma ya kila aina kwa Watanzania ili mradi tu yapore utajiri wa taifa hili.

USHAURI KWA JK

(1) Wale wote wanaohusika na ufisadi usiwarudishe madarakani (uwaziri ama ukatibu mkuu ama ukurugenzi, kwa mfano:

(A)WIZARA YA MIFUGO IMEOZA TANGU WAZIRI WAKE,MAKATIBU WAKUU NA KURUGENZI ZAKE NDIYO MAANA HAIPAFOMU CHOCHOTE. FEDHA ZAIDI YA MILLIONI 600 ZIMEKUWA ZIKITUMWA KWENYE RANCHI ZA KUZALISHA MITAMBA NA KWENDA KUCHUKULIWA BILA KUFANYA KAZI ILIYOKUSUDIWA

(B) WIZARA YA KILIMO OVYO M KWANI MBOLEA ZIMEPANDA NA ZINAPANDA KILA KUKICHA, WASIRA AMEKOMBA FUNGU LA MBOLEA ZA RUZUKU TAKRIBANI BILLIONI 12.5... DATA TUNAZO.

(2) ACHANA NA KUCHAGUA WATU KWA KUFUATA URAFIKI, UKOO, NAFIKIRI UMEYAONA MWENYEWE
 
Good to have this...

Kuna watu walikuwa bado wanataka kupata list hii natumaini ikiwa na maelezo haya.
 
1. Zakhia Meghji:-
(A) aligawa holela vitalu vya uwindaji akaipotezea Tanzania Tsh 3,304, 903,050/- akiwa waziri wa Mali Asili na Utalii.Ovyo zaidi hata wanafamilia wake walijiingiza katika ufisadi huo kwa kumiliki baadhi ya vitalu kibadhilifu
(B) Alipotosha ripoti ya mkaguzi wa BOT mwaka 2005/2006
(C) Kuchonga bajeti angamizi ya mwaka 2007/2008
(D) Kuidhinisha matumizi mabovu zaidi ya millioni 143 kwa mawaziri mafisadi kwenda kuifagilia bajeti ya kihuni ya 2007/2008 mikoani. Mafisadi hao hawakusita kukomba millioni 143 Tsh kwenda kuzomewa mikoani.
(E) Kufumbia macho shughuli fisadi na za kitaprli za BOT ambayo iliipatia Tangold ltd Kampuni feki kiasi zaidi ya Sh 37.7 billioni ambayo haikuwa na usajiri wowote, akidanganya kuwa ni matumizi nyeti ya serikali kumbe ni ulaji wake na vigogo wenzake
(F) Kubarikli uporaji wa fedha BOT tsh 18,465,755,495.39/- zilizopelekwa kwenye makampuni mbalimbali feki kuanzia decemba 2005 hadi 2007.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, huyu mama naona wanamtandao wamemtengeneza kweli kweli...sasa hivi nasikia yuko bench. Nimefatilia habari za huyu mama, toka akiwa afya, mali asili etc. Mengi si kubaliani nayo, je ni kweli hii bajeti ni angamizi?je ni kweli ni yeye peke yake amepitisha hii bajeti? Waliofanya naye kazi utalii, afya tuambieni. Huyu mama mpaka leo pale utalii ufanisi wake unaongelewa, huyu mama kaingizwa mjini mambo ya EPA, tuangalie kipindi (time frame) na mambo yaliyofanyika. Mengi sijui nawaachia JF, lakini binafsi, huyu mama nillishakutana naye miaka michache iliyopita, sipendi kuwapigia debe viongozi wetu wabovyu period, lakini kwa kweli in my opinion ni mmoja wa viongozi wachache wa CCM wa kuigwa mfano..
 
Orodha ya MAFISADI WALIOKUBUHU

1. Zakhia Meghji:-
(A) aligawa holela vitalu vya uwindaji akaipotezea Tanzania Tsh 3,304, 903,050/- akiwa waziri wa Mali Asili na Utalii.Ovyo zaidi hata wanafamilia wake walijiingiza katika ufisadi huo kwa kumiliki baadhi ya vitalu kibadhilifu
(B) Alipotosha ripoti ya mkaguzi wa BOT mwaka 2005/2006
(C) Kuchonga bajeti angamizi ya mwaka 2007/2008
(D) Kuidhinisha matumizi mabovu zaidi ya millioni 143 kwa mawaziri mafisadi kwenda kuifagilia bajeti ya kihuni ya 2007/2008 mikoani. Mafisadi hao hawakusita kukomba millioni 143 Tsh kwenda kuzomewa mikoani.
(E) Kufumbia macho shughuli fisadi na za kitaprli za BOT ambayo iliipatia Tangold ltd Kampuni feki kiasi zaidi ya Sh 37.7 billioni ambayo haikuwa na usajiri wowote, akidanganya kuwa ni matumizi nyeti ya serikali kumbe ni ulaji wake na vigogo wenzake
(F) Kubarikli uporaji wa fedha BOT tsh 18,465,755,495.39/- zilizopelekwa kwenye makampuni mbalimbali feki kuanzia decemba 2005 hadi 2007.

2. Benjamini Mkapa:
(A) Kufanya biashara akiwa ikulu ambacho ni kinyume kabisa na katiba ya nchi yetu
(B) Kuanzisha makampuni mufilisi akiwa ikulu ambayo yamelipora taifa zaidi ya Tsh 908,798,045,050/- akiwa ikulu hadi leo kwa makampuni ya kihuni kama ANBEN ltd, Fosnik ltd na Tanpower
(C) Wizi wa zaidi ya Tsh Trillioni 8,86 BOT kwenye kampeini za uraisi na ubunge zilizotuwekea rais mufilisi. Mkapa anatakiwa asimame kuelekea kizimbani na kujibu wizi huo ulioifilisi nchi ikawa kama dampo la umasikini
(D) Uporaji fedha za taia hili kupitia ununuzi wa rada feki Tsh 50 billioni ambayo aliishupalia kama ruba
(E) Uuzwaji angamizi wa mashirika ya umma na viwanda kwa hila zote, kwani hata yale yaliyokuwa yakijiendesha kwa faida kubwa yaliuzwa kwa bei ya tupatupa (throw away prices)
(F) Kushiriki mikataba mibovu ya madini alilipotezea taifa zaidi ya Tsh 959,588,789,005/- kwa kipindi chote Hivyo huyu ni fisadi lililokubuhu.

3. Edward Lowassa
(A) Anahusika moja kwa moja na ufisadi kupitia kampuni haramu ya RICHMOND na shoga wake DOWANS ambao wamelipora taifa zaidi y ash billioni 273/- kwa umeme hewa
(B) Upotevu wa sh millioni 12.5 /- kupitia kampuni feki ya Water City ambayo aliibariki licha ya kuambiwa kuwa ilikuwa haifai, lakini E.L. aliingilia kama alimasi
(C) Kuliingiza taifa kwenye mkataba mufilisi ,fisadi na angamizi wa Buzwagi . E.L. alikuwa pamoja na fisadi kuu Karamagi kusaini mkataba angamizi na filisi hotelini uingereza. Hivyo analipotezea taifa zaidi ya billioni 3,895/- kila mwaka kwa muda wa miaka 25 kama ulivyo mkataba
(D) Kujiingiza kwenye uporaji kwa kutumia ujenzi wa mahekalu ya hoteli ambayo hayalingani na kipato chake, akibisha data hallisi tutazianika hadharani.

4. David Ballali
(A) Amelipotezea taifa kifisadi zaidi ya sh 693,795,398,805.39/- kupitia BOT kwa malipo hewa kwa makampuni hewa ya kitapeli ya EPA, Jeetu P.ltd, Alex Stewart, Tangold ltd, Mwananchi gold co.ltd, Green F. Co.ltd na mengine mengi,
(B)Kulipotezea taifa matrillioni ya fedha kwa kukwamisha ukaguzi halisi wa BOT
(C) Trillioni 5.3 alizochota kwa ajiri ya kampeini haramu za urais za mwaka 2005 zilizozaa rais mlea mafisadi. The breeder of corrupt leaders at all level

5. Basil Pesambili Mramba

(A)Alibarikina kuhusika na uporaji wa sh 17,697,556,594.85/- kutoka BOT akiwa waziri wa fedha kwenda kwa makampuni mbalimbali feki na watu binafsi hasa magabacholi wa kihindi na kiarabu
(B) ununuzi wa ndegefeki ya rais, rada feki ya rais. Alitangaza Watanzania hata wakila majani ndege feki ya rais lazima ingenunuliwa. Je, mr.. Mrmba, uliona Watanzania ni mbuzi hata wale majani?
(C) Uuzaji feki wa Air Tanzania kwa makaburu. Asingeiingilia kikwete Hapa Mrambaji angetajirika ukomo. (D) Ubinafisaji holela na kwa kiburi na uhujumu wa rasilimali za tiafa kwa masilahi yake akiwa waziri wa fedha , walishirikiana na fisadi ambaye ni rafiki wake wa damu -Abdallah Kigoda

6. Andrew Chenge
(A) Kalipotezea taifa zaidi ya sh 17,857,616,400/- zilizoporwa na Tangold ltd kutoka BOT . Chenge hili hawezi kukwepa kwani alikuwa mkurugenzi wa Tangold ltd at the same time akiwa mkurugenzi wa BOT
(B) Kulipotezea taifa mabillioni ya fedha kwa kuridhia mikataba mibovu/feki/angamizi ya madini akiwa mwanasheria mkuu wa serikali. Takribani zilipotea zaidi y ash 2,890,687,084,573/- kwa kipindi chake chote. Kama anabisha tutazitoa kwa unyambulisho wake.
(C) Zaidi ya billioni 800 zianpotea kwa mwaka kwa mikataba mibovu ya ujenzi wa barabara ama kwa kuweka makampuni feki ambayo huishia kuchota fedha na kutoroaka nchini na vitita vya fedha. Ana kurugenzi wezi wizarani kwake lakini amefumbia macho kwa manufaa yake binafisi. Chenge unasubiri nini kungCcā,?ā"catuka?

7. Gray Mgonja

(A) Alibariki na kuhisika na uporaji wa sh 17,857,616,400/- BOT kwenda kampuni yao ya tangold ltd akiwa mkurugenzi wa BOT pia hapo hapo akiwa mkurugenzi wa Tangold ltd kampuni ambyo hikuwa na usajili.
(B) Kunyamazia ufisadi wa uporaji wa trillioni za fedha BOT kenda kwenye makampuni hewa akiwa mkurugenzi BOT

8. Peter Msolla
(A) Uporaji wa sh billioni 5 zilizokuwa zimetolewa na EUROPEAN OVERSEAS AGENTS miaka ya 90 akiwa makamu mkuu wa SUA. Fedha hiyo ilikuwa imetolewa kukiendeleza chuo(SUA) kitaaluma, miundo mbinu kama barabara za ndani , tafiti mbalimbali na kuwa dila ya maendeleo ya kanda ya mashariki mwa Tanzania (Morogoro, Pwani, Tanga, Dar-es salaam). Cha ajabu fedha hiyo iliishia kwenye midomo ya mamba mafisadi (Prof Msolla, Prof Ishengoma, Mr A.. Magoma (Mhasibu wa kufoji ), keshia Prof Mgongo na maswahiba wao.. Planner mkuu wa wizi huo alikuwa Magoma wakisaidiana na Msolla. Wakaamua kununua magari ya kifahali na kujenga majumba ya kifahari yakiwapo magesti house kwa siri.
(B) Uporaji wa fedha za DANIDA millioni 490 zilizokuwa zimetolewa kwa ajili ya mradi wa OTAITISI (OTITIS) .Fedha hiyo iligawanywa hapo vet SUA na kunguru mafisadi wachache. Msola akachukua 80% ya fedha hiyo na kujenga majumba makubwa ya kifahali . Ngombe wa Mradi huo wakaishia kulala kwenye matope yafikayo kwenye kimo cha tumbo lao wakiwa wamesimama.. Wafadhili walikasirika kupita upeo, wakajitoa. Ukweli huu hauhitaji hata kupeleleza pale VET-SUA.
(C) Hujuma ya fedha ya punguzo la wafanyakazi SUA Tsh 2,245,045,000/- ilyotolewa na benki ya dunia 30/6/1996. Ilipangwa kwamba mtu mwenye mshahara mdogo kabisa apewe Tsh millioni 8. Jambo la kushangaza ni kwamba kila mtu aliyepunguzwa kazi alipewa asilimia kumi tu (10%) ya malipo yake. Hivyo mwenye mshahara mdogo alipewa sh 300,000/- tu. Aliyekuwa anatakiwa kulipwa millioni 20/- alipewa millioni tatu tu. Yeye Msolla na mafisadi wenzie (A.Magoma, Prof Luoga akiwa VC-SUA, Prof Mgongo, keshia na maswahiba wao waligawana 90% ya fedha yote iliyotolewa na benki ya dunia... Mafisadi hawa wakawa wanaishi kama wapo peponi. Wakanunua magari ya kifahali na kujenga majumba ya KUFURU yakiwamo magesti house bubu (kwa siri) na kununua mashamba kila kona Mkoani Morogoro.
(D) Wizi wa millioni 442 SUA kuamkia tarehe 22/4/2006.Yaani, Kati ya shs 442, shs millioni 400/- zilikuwa peti keshi zilizokusanywa kwa miaka miwili . Hivyo Msolla, Keshia, Prof Luoga na Magoma waliziiba zile millioni 400/- mchana kweupe tarehe 21/4/2006 kutoka kwenye sefu, baadaye wakaingiza sh millioni 42/- za malipo ya wafanya kazi SUA, ndipo kesho yake tarehe 22/4/2006 wakatangaza kuwa sh millioni 42/- za malipo ya wafanyakazi SUA ziliibiwa. Kwa uhakika zilizohamishwa kiporaji zilikuwa sh millioni 442(millioni 42 zikiwa malipo ya wafanyakazi SUA na millioni 400 zikiwa peti keshi ) . Sababu ya uporaji huo wa kifisadi ni:
(i) kujiandaa kwa kustaafu kwa prof. Luoga, Mr Magoma na Msolla
(ii) Kutokuwa na imani na Kikwete kwani SUA walitegemea Sumaye ndiye angekuwa rais ambaye ni fisadi mwenzao. Hata hivyo hawakujua kuwa hata Kikwete ni mama na mlezi wa mafisadi
(iii) Kupata fedha lukuki za kufanyia kampeni za ubunge kwa Msolla na hatimaye uwaziri. Hivyo kesi hiyo aliisimamia Prof Monera kwa ahadi kwamba kama angefanikiwa kuivunja kesi hiyo angekuwa VC. Monera alifanikiwa kuizima kesi hiyo, Prof Luoga na Msolla wakampendekeza kwa rais awe VC ili siri hii isifichuke. Kikwete akaingia kwa jeuri yake kichwakichwa akaweka fisadi pandikizi kuwa VC- la SUA ambalo linakomba fedha ya SUA na ya wafadhili likishirikiana na Mufilisi mwenzie Prof Msolla kiasi kwamba, fedha ya wafadhili inayopitia Wizarani (Sayansi na Elimu ya juu) kwenda SUA igawanwe na kukombwa vizuri.

9. Joseph Mungai

(A) Aliingiza silabasi feki kuanzia chekechea hadi elimu ya sekondari kwa Watanzania wa kawaida huku watoto wao wanasoma nje ya nchi.Watoto hapa nchini hawakujua walichokuwa wanasoma, si jogg ama mchemsho. Akaua elimu kupindukia. Alifanya hivyo ili fedha nyingi zibaki wizarani ili azitumie na mafisadi wenzie kwa masilahi binafsi. Zaidi ya billioni 300 zilikuwa zinaliwa wizarani kwa ufisadi huu.
(B) Alikula takribani sh millioni 8/- za bima na likizo za waalimu na mapunjo mbalimbali ya waalimu yakiwamo ya mishahara ya walimu wa shule za msingi na sekondari.Waalimu wakapiga kelele kudai haki zao wakaonekana kutimiza usemi kwamba KELELE ZA MLANGO HAZIMKOSESHI USINGIZI MWENYE NYUMBA.
(C) Kupora fedha inayobaki wizarani mwisho mwa mwaka. Kapuya alichagua baadhi ya maofisa wa elimu wa mikoa/wilaya na mahedimasta wa shule za sekondari ambako alikuwa akituma fedha mwishoni mwa mwaka (mwezi wa 5) na baadaye kutuma wahasibu mafisadi kuifuata fedha hiyo. Alikuwa akipora kati ya sh billioni 3-4 kwa mtindo huo kila mwaka alitafuna na maswahiba wake

10. Juma Ngasongwa
(A) Kalipotezea taifa zaidi ya sh Billioni 9,845/- kwa kipindi akiwa waziri wa Mali Asili na Utalii kwa kupewa pipi kidogo na kuachia uwindaji haramu na angamizi kwa rasilimali na uchumi wa nchi. Ufisadi huu ulimfanya afukuzwe uwaziri wakati wa MZEE RUKSA kwani mzee ruksa alikuwa makini. Hakuwa kama Kikwete ambaye amefunga ndoa na mafisadi kama Kapuya, Ngasongwa, Meghji, Ballali, Msolla, Diallo, Benno Ndullu nk.
(B) Kuchochea vurugu SUA... Yeye alipoona kuwa wanafunzi wa SUA wamemkataa kwa kuwa alikuwa haeleweki anachofundisha , si DS ama DESKI CHAFU, alianza vurugu zilizomfanya afukuzwe kazi SUA katika miaka ya 90. akakimbilia siasa. Vilevile mzee ruksa akamfukuza kazi Mali asili na utalii katika miaka ya 90. Bwege Mkapa akamrudisha kuhujumu, pia Kikwete akameza matapishi hayo hayo.

11. Stephan Wasira

Mamillioni ya fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya kupunguza makali ya mbolea ameyakomba.. Yaani, fedha ya sabsidi ya mbolea zaidi ya sh billioni 12,5 ameifagia na kufanya bei ya mbolea kuanza kupaa juu kama kunguru kila kukicha katika mikoa ya nyanda za juu kusini The big four (Mbeya, Iringa, Ruvuma na Rukwa). Kilimo katika mikoa hiyo hutegemea mbolea asilimia mia moja(100%). Sasa mbolea haishikiki kwa wakulima wengi (90%) kwani ni kati ya sh 40,000/-sh 55,000/- kwenye mfuko wa kilo 50. Kwa ekari moja inahitajika mifuko 4-5 kutegemea na hali ya udongo husika. Mbaya zaidi , si Kikwete wala Wasira anayetembelea mikoa ya Mbeya, Iringa ama Rukwa tangu wawahadae wananchi kuwaletea maisha mazuri. Huu ni utapeli wa unaotakiwa ulaaniwe na kila mpenda haki. Kila leo utamwona Kikwete akitembelea KWA WASUKUMA (MWANZA NA SHINYANGA), BUKOBA NA MUSOMA, PWANI NA MOROGORO MAANA AMEYAONA MAJITU HAYO ZUMBUKUKU.

11. Nazir Karamagi
(A) Kufanya ufisadi wa kusaini mikataba angamizi ya madini kama ya Buzwagi nje ya nchi hotelini!!!!!!!!!!!! Uliolikosesha taifa sh 9,239,389,394.25/- kwa kipindi chote
(B) Kuligharimu taifa zaidi ya billioni 173 kutokana na uroho wa kujitumbukiza kwenye sakata la kampuni tapeli ya RICHMOND na binti yake DOWANS
(C) Kunyamazia kupanda kwa umeme kwa walipa kodi maskini ili kufidia gharama angamizi za TANESCO zinazotokana na mafisadi vigogo kutolipa gharama za umeme.

12. Ibrahim Msabaha
(A) Kulipotezea taifa zaidi ya sh billioni 174 kutokana na kufunga ndoa na kampuni mufilisi , feki na tapeli ya RICHMOND . Anatakiwa akamatwe atiwe ndani na alipe deni hilo .

13. Benno Ndullu
(A) Kabariki ufisadi na uharamia wa sh 693,795,398,800/- zilizohamishwa kijambazi na kaka zake (Ballali, Mramba, Zakhia M) akiwa naibu gavana wa BOT. Hili halikwepi. Tunajua amewekwa pale na Kikwete ili kuficha ushahidi wa mafisadi wenzie wakiwemo watoto wa vigogo. Hapa tayari anaingia kwenye kundi la mafisadi.
(B) Kutomshauri Kikwete avunje bodi inayoshughulikia kutafuta kiini cha ufisadi BOT, kwani bodi hiyo imejaa mafisadi kama G. Mgonja, Zakhia Meghji nk Hivyo hakuna chochote kitakachofanyika zaidi ya kwenda kuficha ushahidi.

14. Edward Hosea

(A) Amekomba zaidi ya billioni 65 kwa kupokea rushwa nene na kutoa taarifa feki kwenye uchunguzi wa RICHMOND , sakata la Buzwagi, mikataba mibovu ya madini, sakata na hujuma za wahindi kupanga kwenye nyumba nzuri za National Housing kuliko wazawa, Sakata la DOWANS na hujuma nyingine nyingi... Ni fisadi anayetakiwa ajiuzuru mara moja.

USHAURI KWA WAPINZANI
(1) Shinikizeni kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi itakayochaguliwa na wabunge mseto. Yaani wabunge 2 CCM, 2 CHADEMA, 2 CUF, I TLP, I UDP na isiwajibike kwa kingunge yoyote bali kwa maslahi ya kitaifa. Msipofanya hivyo, mtakuwa wasindikizaji watindikiwa katika uchaguzi wa mwaka 2010. Hata taahira huwa hashiki moto.
(2) Tembeleeni vijijini mkawaelimishe watu wanaodanganywa na CCM kila kukicha, kwani huko ndiko kuna zaidi ya 85% ya wapiga kura nchini..Wanaishi maisha magumu kama wako mahabusu ya uhaini ndani ya nchi yao lakini hakuna wa kuwaelimisha Kikwete ndio amewasusa watu wa Mbeya, Iringa, Rukwa na Ruvuma huku akiita mikoa hiyo THE BIG FOUR na kunadi kuwa kilimo ni uti wa mgongo na kuwasuta akisema kuwa mbolea ya ruzuku haipo , wasibweteke, watainunua tu hata kama bei yake inapaa kama tai kila kukicha.. Kwa akili finyu ya watanzania, mwaka 2010 atajipitisha kwao na kuwafanya wasahau kuwa aliwahi kudondoka chini akiwahadaa maisha bora katika kura za mwaka 2005. Hivyo wapinzani tembeleeni vijijini maana mjini watu wanawaelewa.
(3) Piteni mkiwaambia watanzania kuwa MAFIGA MATATU YA KIKWETE ni kurudisha utawala wa chama kimoja wenye kubariki kila ufisadi na mafisadi wa uchumi wetu na rasilimali za taifa. Utawala wa kidikiteta na mufilisi bila kuhojiwa na mtu yeyote kwani bunge linakuwa na mafisadi wanaotetea mafisadi , ufisadi na hujuma ya kila aina kwa Watanzania ili mradi tu yapore utajiri wa taifa hili.

USHAURI KWA JK

(1) Wale wote wanaohusika na ufisadi usiwarudishe madarakani (uwaziri ama ukatibu mkuu ama ukurugenzi, kwa mfano:

(A)WIZARA YA MIFUGO IMEOZA TANGU WAZIRI WAKE,MAKATIBU WAKUU NA KURUGENZI ZAKE NDIYO MAANA HAIPAFOMU CHOCHOTE. FEDHA ZAIDI YA MILLIONI 600 ZIMEKUWA ZIKITUMWA KWENYE RANCHI ZA KUZALISHA MITAMBA NA KWENDA KUCHUKULIWA BILA KUFANYA KAZI ILIYOKUSUDIWA

(B) WIZARA YA KILIMO OVYO M KWANI MBOLEA ZIMEPANDA NA ZINAPANDA KILA KUKICHA, WASIRA AMEKOMBA FUNGU LA MBOLEA ZA RUZUKU TAKRIBANI BILLIONI 12.5... DATA TUNAZO.

(2) ACHANA NA KUCHAGUA WATU KWA KUFUATA URAFIKI, UKOO, NAFIKIRI UMEYAONA MWENYEWE

Brilliant job Kokolo! Mayn, we truly must be f#cked! Bila mtutu, Watanzania will continue taking it up their arses for real. And thats no lie.
 
Baada kuisoma ninaona kuna upotoshaji uliojaa siasa zaidi kuliko ukweli na zaidi hujatushawishi ktk taarifa ulizobandika hapa huenda una kusudio lako binafsi na unataka JF waingie kazini kwa hao uliowataja au umefuata mkumbo na kukurupuka ama pengine utafiti na kujiridhisha ktk yale uliyoyatafiti si sehemu ya maisha yako,si vema kuitendea JF mambo kama haya ila ni vema ukarudi ktk taarifa yako jina kwa jina na urekebishe kwa umakini kisha utuombe radhi kuwa umekosea ktk uwasilishaji na taarifa na takwimu zilizotolewa hazi tally.

Nway,naheshimu jitihada zako.
 
8. RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE


Rais Jakaya Kikwete amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Desemba 2005. Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994. Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo , SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.

Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada . Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto , Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.
 
Ooo wakuu sijafikia haki ya kuwa msemaji wenu JF bali munkari baada ya kusoma bandiko la mtoa hoja. Nakiri kuwa binafsi sijaridhishwa na bandiko lake hata kama lina chembechembe za fact lakini amezi copy humuhumu na zingine nyingi sana ni uongo,JF si mahala pa Uongo tena wa makusudi.Natoa hoja.
 
Baada kuisoma ninaona kuna upotoshaji uliojaa siasa zaidi kuliko ukweli na zaidi hujatushawishi ktk taarifa ulizobandika hapa huenda una kusudio lako binafsi na unataka JF waingie kazini kwa hao uliowataja au umefuata mkumbo na kukurupuka ama pengine utafiti na kujiridhisha ktk yale uliyoyatafiti si sehemu ya maisha yako,si vema kuitendea JF mambo kama haya ila ni vema ukarudi ktk taarifa yako jina kwa jina na urekebishe kwa umakini kisha utuombe radhi kuwa umekosea ktk uwasilishaji na taarifa na takwimu zilizotolewa hazi tally.

Nway,naheshimu jitihada zako.

Apparently, na wewe vilevile una-suffer from same "intellectual laziness" ambayo unamlaumu KOKOLO who in my view has done nothing but a superb effort in providing us with this summary of Big Fisadis. Sasa ni nini kinachokuzuia kuonyesha wapi, nani, nini na vipi KOKOLO amekosea au kupotosha?
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, huyu mama naona wanamtandao wamemtengeneza kweli kweli...sasa hivi nasikia yuko bench. Nimefatilia habari za huyu mama, toka akiwa afya, mali asili etc. Mengi si kubaliani nayo, je ni kweli hii bajeti ni angamizi?je ni kweli ni yeye peke yake amepitisha hii bajeti? Waliofanya naye kazi utalii, afya tuambieni. Huyu mama mpaka leo pale utalii ufanisi wake unaongelewa, huyu mama kaingizwa mjini mambo ya EPA, tuangalie kipindi (time frame) na mambo yaliyofanyika. Mengi sijui nawaachia JF, lakini binafsi, huyu mama nillishakutana naye miaka michache iliyopita, sipendi kuwapigia debe viongozi wetu wabovyu period, lakini kwa kweli in my opinion ni mmoja wa viongozi wachache wa CCM wa kuigwa mfano..

Mkulu maliasili paliaribika wakati wa huyu mama, ugawaji holela wa vitalu vya uwindaji, Utengenezaji wa jangwa Tanzania kwa kufyeka misitu ya asili bila magogo kulipiwa ushuru na wachina, akina severe waliota pembe wakati wa huyu mama kiasi kwamba hata alipoamishwa alikataa kwenda kwenye kituo chake kipya cha kazi and the like, check tena data zake mkulu.
 
Huyu mama sasa anakula mafao tuu..kuna vijana wake wa kazi wapo kkoo aliwakopesha bil 6 kujengea maghorofa ya biashara na mtoto wake amepmatia same lamp sum ajili ya hotel....mitaa ya magomeni....ana shida gani???anakula 10% zakee tu sasa....maana tz siku hizi ukibainika unaambiwa jiuzulu fasta ili ule kimya kimya..........2010..tufanye kitu tofauti
 
Hoja hupingwa kwa Hoja, mtu anapotuarifu habari kisha mtu kama FDR Jr anapinga utadhani kama yeye ni mtoto wa miongoni wa waliotajwa hii ni hatari sana
 
Mkulu maliasili paliaribika wakati wa huyu mama, ugawaji holela wa vitalu vya uwindaji, Utengenezaji wa jangwa Tanzania kwa kufyeka misitu ya asili bila magogo kulipiwa ushuru na wachina, akina severe waliota pembe wakati wa huyu mama kiasi kwamba hata alipoamishwa alikataa kwenda kwenye kituo chake kipya cha kazi and the like, check tena data zake mkulu.

Asante mkulu, huyu mama ameshika ile wizara kwa muda mrefu, lazima kuna kasoro. Lakini mimi ninavyokumbuka huyu mama alisimamisha usafirishaji wa magogo ata kule bungeni kuna wabunge walikuja juu kwa sababu wanazozijua
Unakumbuka hizi habari?


Posted Date:10/9/2007
Magogo ya mamilioni yakamatwa Dar yakienda nje

Tausi Mbowe na Jackson Odoyo

MAKONTENA12 yakiwa yamesheni magogo yamekamatwa jijini Dar es Salam yakiwa njiani kupelekwa bandarini kwa ajili ya kusafirishwa kwenda nchini China.

Magogo hayoya miti aina ya mkuruti, yalikamatwa jana na maafisa misitu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, yakiwa yamepakiwa katika malori sita ya mizigo.

Magari hayo yenye tela mbili kila moja yalikamatwa kwa nyakati tofauti kuanzia saa 8.00 usiku juzi.

Akizungumza katika eneo la tukio, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mali Asili na Utalii, Blandina Nyoni, alisema magogo hayo mali ya Kampuni ya Micco Import and Export yana thamani ya zaidi ya Sh51milioni.

Kwa mujibu wa Nyoni, magogo hayo aina ya 'Sleeper' yalikamatwa baada ya kuweka mtego katika eneo la Chang'ombe, jijini Dar es Salaam baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema.

"Maafisa wa maliasili waliweka mtego katika eneo hili baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema, na kufanikiwa kuyakamata makontena hayo kwa nyakati tofauti," alisema Nyoni na kuongeza kuwa katika kufanikisha zoezi hilo maafisa hao waliwanyang'anya simu madereva wa magari hayo ili kuwanyima nafasi ya kuwasiliana na wenzao waliokuwa nyuma.

Nyoni alisema kampuni hiyo ilifanya udanganyifu kwa kusafirisha magogo hayo badala ya mbao kama kibali walichopewa kinavyoonyesha..

"Wataalamu wetu wa maliasili walienda kukagua mbao zinazotakiwa kusafirishwa na kampuni hiyo iliyopo Mbagala, siku chache zilizopita, ambapo waliridhika na kutoa kibali cha kusafirisha mbao hizo, lakini wenyewe wamefanya udanganyifu na kubadili mbao hizo kwa kuweka magogo," alisema.

Alisema imegundulika kuwa kumekuwa na udanganyifu katika usafirishaji huo ambapo sehemu ya mbele zimewekwa mbao chache zinazoonekana na nyuma wanaweka magogo.

Nyoni alisema kampuni hiyo imewahi kufungiwa kwa kujishughulisha na biashara ya magogo baada ya kuonekana kuwa inatumia leseni ya kusafirisha mbao, badala yake inasafirisha magogo.

Alisema kwa mujibu wa sheria ni kosa kusafirisha magogo nje ya nchi na kwamba sheria hiyo inaainisha kuwa usafirishaji wa mbao unatakiwa kusafirishwa nyakati za mchana mpaka saaa 12 jioni na si usiku kama kampuni hiyo ilivyofanya.

Nyoni alisema kwa mujibu wa sheria ya misitu magari yanayokamatwa yakisafirisha magogo hayo hutaifishwa pamoja na magari yaliyobeba bidhaa hizo.

Kufuatia hali hiyo, Nyoni aliamrisha magogo hayo kushushwa katika magari hayo na kukaguliwa na maafisa wa wizara yake.

Akizungumza na waandishi wa habari mmiliki wa magogo hayo, Merck Mzirai alisema kuwa madai hayo ni ya uongo na kwamba kampuni yake ilifuata taratibu zote za kisheria za usafirishaji wa bidhaa hiyo.

"Huku ni kupakana matope, kampuni yangu inafuata taratibu zote zilizowekwa kwa mujibu wa sheria, tuna nyaraka zote zinazoturuhusu kusafirisha mzigo huu," alisisitiza.

Alipoulizwa kwanini kampuni yake inasafirisha usiku badala ya mchana kama sheria inavyotaka, alisema kampuni yake hulazimika kusafirisha usiku kutokana na bandari kutokuwa na nafasi ya kutosha

Serikali ilikataza biashara ya usafirishaji wa magogo nje ya nchi na huko nyuma
aliyekuwa W
aziri wa Maliasili na Utalii, Zakhia Meghji aliwahi kufanya msako wa kushitukiza na kukamata makontena ya bidhaa hiyo yakiwa bandarini tayari kusafirishwa.

Magogo yanayovunwa hapa nchini yamekuwa yakisafirishwa kwa njia ya kinyemela kupelekwa katika nchi za China, Thailand, Malaysia, India na Taiwan ambako yanauzwa kwa bei kubwa.
 
Ooo wakuu sijafikia haki ya kuwa msemaji wenu JF bali munkari baada ya kusoma bandiko la mtoa hoja. Nakiri kuwa binafsi sijaridhishwa na bandiko lake hata kama lina chembechembe za fact lakini amezi copy humuhumu na zingine nyingi sana ni uongo,JF si mahala pa Uongo tena wa makusudi.Natoa hoja.


Kwa hakika utakuwa si mzalendo halisi. Au utakuwa upo upande wao!
 
Orodha ya MAFISADI WALIOKUBUHU



8. Peter Msolla

(ii) Kutokuwa na imani na Kikwete kwani SUA walitegemea Sumaye ndiye angekuwa rais ambaye ni fisadi mwenzao. Hata hivyo hawakujua kuwa hata Kikwete ni mama na mlezi wa mafisadi



USHAURI KWA WAPINZANI

(3) Piteni mkiwaambia watanzania kuwa MAFIGA MATATU YA KIKWETE ni kurudisha utawala wa chama kimoja wenye kubariki kila ufisadi na mafisadi wa uchumi wetu na rasilimali za taifa. Utawala wa kidikiteta na mufilisi bila kuhojiwa na mtu yeyote kwani bunge linakuwa na mafisadi wanaotetea mafisadi , ufisadi na hujuma ya kila aina kwa Watanzania ili mradi tu yapore utajiri wa taifa hili.


USHAURI KWA JK
(1) Wale wote wanaohusika na ufisadi usiwarudishe madarakani (uwaziri ama ukatibu mkuu ama ukurugenzi, kwa mfano:

(A)WIZARA YA MIFUGO IMEOZA TANGU WAZIRI WAKE,MAKATIBU WAKUU NA KURUGENZI ZAKE NDIYO MAANA HAIPAFOMU CHOCHOTE. FEDHA ZAIDI YA MILLIONI 600 ZIMEKUWA ZIKITUMWA KWENYE RANCHI ZA KUZALISHA MITAMBA NA KWENDA KUCHUKULIWA BILA KUFANYA KAZI ILIYOKUSUDIWA

(B) WIZARA YA KILIMO OVYO M KWANI MBOLEA ZIMEPANDA NA ZINAPANDA KILA KUKICHA, WASIRA AMEKOMBA FUNGU LA MBOLEA ZA RUZUKU TAKRIBANI BILLIONI 12.5... DATA TUNAZO.

(2) ACHANA NA KUCHAGUA WATU KWA KUFUATA URAFIKI, UKOO, NAFIKIRI UMEYAONA MWENYEWE


Mkuu pole sanakwa kazi nzito ya kupigana na mafisadi aidha katika post yako nimeona yafuatayo.

1. Kumtaja JK bila kuogopa kuwa ni fisadi, siku za karibuni kumekuwa na tuhuma hapa jamvini na baadhi ya waandishi nguli kuogopa kumtaja JK moja kwa moja kuwa ni mmoja wa mafisadi waliokubuhu! huwezi kumtfauitsh JK na BMW! no way under CCM. Nimewachallenge wengi akiweo mwandishi nguli wa mwanahalisi, nikamuulza HIVI KATIKA HABARI ZAKO ZA KIFISADI KIKWETE HAYUMO HATA KATIK TOLEO MOJA? JK na rungu ana kila kitu cha kutokomeza ufisadi hata kama ni kwa asilimia 98%! lakini wapi, anawaza kuoa mke wa tatu. Watanzania tunfurahia sana habari hizi lakini hatuendi kuona chanzo na kukiharibu, rais wa nchi aweza kuwa chanzo, mlezi na mtokomezaji, JK na sifa ya chanzo na mlezi

2. Nimeona ukitoa vithibitisho vya uwizi na tarehe , hii pia ni nzuri na ni heshima katika forum hii


3. Stop by any means, kumpa ushauri JK wa kupambana na ufisadi ili hali ukijua yeye ni fisadi number moja! huna haja ya kumpoza, kujikomba, au kuwa na woga wowote ule, kama standar yako ya kuita mafisadi wakuu is valid basi JK is above all

4. Katika vita ya ufisadi tujifunze kuwa inaanzia katika gazi ya kaya, kata, wilaya..... mtu yeyote anayeiba senti yeyote hata kama ni senti moja, ni fisadi mkuu, tumekuwa tukijificha nyuma ya hizi public figures na kufanya ufisadi unaotisha, nimefanya kazi vodacom for two yrs, hutaamini kuwa just normal workers wanafanya ufisadi wa mpaka milioni 100! and is common, wakati naacha kazi mentality ya kila mtu ilkuwa 'ameshachuma za kutosha' ! this is proof kuwa vita hii ya ufisadi ni kubwa mno, kuna watu tunaishi nao mitaani wanakula rushwa kama vile ni maji ya kunywa. Kwa sababu tunaona VITA RUSHWA NI KWA VIONGOZI TU, tunasahau kuwa viongozi wanatoka huku tuliko!

5.Naona umewapa changamoto vyama vya siasa! sio CHADEMA nao kuna wakati wanafanya kosa kama wewe,kusifia individual ndani ya CCM, kuna mmoja nilimtania CHADEMA mtasimamisha mgombea jimbo la Mwakyembe?
strategy should be however how much good somebody does, so long he is in 'monster party' like CCM there is no way to complement him/her or even come closeness to them by any means. VYAMA Vytu vya siasa kama ni kama vile vya kirafiki, haviko serious,undugu, kujikombakomba serikalini, kucheckacheka na hawa mafisadi n.k Ushauri ulioutoa wamekuwa wakipewa lakini wapi!!!!!!!!

Haikuniingia akilini kusikia Chenge ana bilioni moja nje, still JK nalazimishwa huyu mtu ajiuzulu!
 
8. RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE


Rais Jakaya Kikwete amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Desemba 2005. Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994. Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo , SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.

Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada . Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto , Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.

Mapambano asante sana kwa hii summary nzuri sana ya huyu kiongozi wa nchi hii! I will be quoting this, My sunday is good!

Natamani kama ni research au thesis titles basi ningezitoa hapa.

Hatuna usalama wa taifa? wa kuangalia usafi wa viongnozi wanaotegemewa kuwa marais? maana umbumbumbu wa wana CCM katika uchaguzi hauleti tija na faida Tz, matokeao yake ni kumweka rais

1. Hana rekodi yeyote ya kazi nzuri
2. Ana rekodi za ufisadi
3. Hana professional experience
4. Si msafi wa tabia zake za kimwili

Ndiyo maana nasema hivi tunaipenda nchi yetu au tumotumo tu!

kuna tatizo somewhere!!

JAZENI POST, TOENI VITHIBITISHO, WASEMENI MAFISADI WOTE, KAMA KIONGOZI WA NCHI NAYE NI FISADI HAKUNA KINACHOFANYIKA! TUTARUKARUKA HAPAHAPA, kama JK nagekuwa msafi basi JF na pos zote hizo zlifaa kabisa kumsaidia na kuiweka nchi katika mstari sahihi

I sometime think and I belive IQ ya MKJJ na many JF members katika uongozi iko juu sana zaidi ya JK! I also think JK ni kama ile sanamu ya askari aliyeshika bunduki.

CCM to hell!
 
Baada kuisoma ninaona kuna upotoshaji uliojaa siasa zaidi kuliko ukweli na zaidi hujatushawishi ktk taarifa ulizobandika hapa huenda una kusudio lako binafsi na unataka JF waingie kazini kwa hao uliowataja au umefuata mkumbo na kukurupuka ama pengine utafiti na kujiridhisha ktk yale uliyoyatafiti si sehemu ya maisha yako,si vema kuitendea JF mambo kama haya ila ni vema ukarudi ktk taarifa yako jina kwa jina na urekebishe kwa umakini kisha utuombe radhi kuwa umekosea ktk uwasilishaji na taarifa na takwimu zilizotolewa hazi tally.

Nway,naheshimu jitihada zako.


FDR Jr, heshima kwako mkuu. Kama unaona kuwa taarifa ina makosa na inahitaji marekebisho basi ni dhahiri wewe unazo hizo taaifa zisizopotosha na ingekuwa vyema ukatumwagia hapa badala ya kutaka uombwe radhi!
 
Mafundisho juu ya maadili ndio dawa ya kudumu ya kuondoa ufisadi. Kazi hii si ndogo ni kubwa sana na inahitaji uvumilivu wa muda. Kwa sababu itawalenga zaidi wanafunzi toika shule za msingi mpaka vyuo vikuu.

Kama tutakuwa tunanyosheana vidole kweli ni vigumu kumpata msafi, na nchi haiwezi kukaa bila kiongozi. Kwani hata tukiwapa nafasi wapinzani basi nao ndio hao hao. Si jana tu tulikuwa na akina Taambwe na Makongoro kama wapinzani wetu.

Hivyo hizo list kwangu hazisemi kitu sana zaidi ya propaganda ya kukipalilia chaama fulani njia ya kwenda ikulu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom