Nimefutilia kwa ukaribu sana matatizo mbali mbali yanayoikumba nchi yetu,na kutadhmini kwa kina utayari wa serikali yetu kuyatatua.Katika mambo yote ninayo 'conclusion' moja tu,nayo ni kwamba,serikali ama haina watendaji wenye uwezo wa kutekeleza wajibu wao,ama 'it's controlled by outside forces' au watendaji wana uwezo, lakini wanafanya wafanyayo kwa ajili ya maslahi binafsi.Nashawishika kusema kwamba, yote hayo matatu yamo katika uongozi wa nchi yetu and 'hence the magnitude of the problem.'Juzi tu tumeshuhudia mambo ambayo yanachefua.Jamani watu ambao wamechangia katika umaskini wa wananchi wetu wanawekwa 'VIP rooms' Keko?Kama sio matusi kwa wanachi maskini wa Tanzania ni nini.La kujiuliza hapa ni kwamba hawa wafanyakazi wa magereza wanaowaweka watu hawa katika vyumba vya VIP, wanafanya hivyo kwa amri ya nani.Kwanza hili wazo la 'VIP rooms' magereza, linatoka wapi.Kwangu mimi mhalifu ni mhalifu tu,swala la uVIP linatoka wapi.Watanzania maskini wenzangu, tuangalie matukio haya kwa umakini mkubwa sana.Hili na utendaji wa serikali yetu wenye kutiliwa mashaka kwa muda mrefu sasa, unanipa picha moja tu' kwamba serikali haiko 'serious' katika kuwashughulikia mafisadi inavyopaswa na hatimaye kuwaletea wananchi maendeleo yao.Nimesema mara nyingi kwamba serikali imewakosea wanachi wa Tanzania kwa kiwango cha kutisha sana.Ingekuwa vema kama serikali ingewaomba radhi wanachi na ikaadhimia kuanza upya kusaidia wananchi wa Tanzania.Mimi sioni hilo badala yake ninaona kichwa ngumu na 'business as usual.'Hakika hatufiki!