Elections 2010 Mafisadi kumng'oa mbunge Mahiri 2010....

Jamani tusije tukanogewa kuongea lugha moja wooote humu ndani! nadhani mtoa hoja kasema pia bwana Mpendazoe anachafuliwa kuambiwa 'eti' anatengeneza makundi. Gazeti kama mtanzania ambalo mara nyingi limetumiwa na mmliki wake kuendeleza uma-kundi leo hii limekuwa linapinga tabia hii kirahisirahisi tu? Isije tukaingizwa kwenye mkumbo wa kuunga mkono mambo ambayo wengi wetu tumekuwa tukiyapinga kwa nguvuzetu zote! Hebu fikiri, kwa mfano ikawa ni kweli kuna njama hizo,..... sisi tutakuwa tumecheza mechi upande gani?

vyovyote vile....tusiwadharau wananchi.....tuwaache ndio wawe waamuzi wa mwisho....ideally wananchi watamu-evaluate Mbunge wao kutokana na aliyo ahidi na anayotakiwa kutekeleza akiwa kama mwakilishi wao bungeni + jimboni.....kama wanajimbo ni Kabuntas na wakamchagua tena kabuntas......still the ball uko uwanjani kwao kuamua.......
 
Jamani tusije tukanogewa kuongea lugha moja wooote humu ndani! nadhani mtoa hoja kasema pia bwana Mpendazoe anachafuliwa kuambiwa 'eti' anatengeneza makundi. Gazeti kama mtanzania ambalo mara nyingi limetumiwa na mmliki wake kuendeleza uma-kundi leo hii limekuwa linapinga tabia hii kirahisirahisi tu? Isije tukaingizwa kwenye mkumbo wa kuunga mkono mambo ambayo wengi wetu tumekuwa tukiyapinga kwa nguvuzetu zote! Hebu fikiri, kwa mfano ikawa ni kweli kuna njama hizo,..... sisi tutakuwa tumecheza mechi upande gani?

Naam usemacho ni kweli kabisa tusije tukajikuta tunacheza mdundiko unaopigwa na fisadi Rostam na kundi lake bila kujijua na yeye huko aliko kukenua gego mpaka gego na kutamba kwamba Watanzania hawana msimamo. Lazima tuwe makini mno katika uchambuzi wetu dhidi ya vita vinavyoendelezwa na kundi la mafisadi, vinginevyo tunaweza kabisa tukajikuta tuko nao upande mmoja.
 
vyovyote vile....tusiwadharau wananchi.....tuwaache ndio wawe waamuzi wa mwisho....ideally wananchi watamu-evaluate Mbunge wao kutokana na aliyo ahidi na anayotakiwa kutekeleza akiwa kama mwakilishi wao bungeni + jimboni.....kama wanajimbo ni Kabuntas na wakamchagua tena kabuntas......still the ball uko uwanjani kwao kuamua.......

Wananchi hakuna anae wadharau, ila uzoefu unaonyesha wakati mwingine wanalazimishwa kupiga kura kwa mbinu za "kisanii". Rejea kishindo cha asilimia 80 mwaka 2005 na kilio chetu sasa hivi kuwa tulichagua udhaifu. Yaani wananchi asilimia 80 walichagua kiongozi dhaifu kwa makusudi ya potelea mbali? au sanaa.... tusichoke kufikiri jamani, fikra ni uwanja mpana.
 
Ogah, Mkuu wangu humu JF ama kweli watu wanakurupuka sana bila hata kupima...
Kinachoendelea ndani ya CCM ni siasa za majungu wala sii swala la Taifa....Huyo mbunge wa Mshapu Nd. Mpendazoe anacholia ni kilio cha ndani mwake, he has all the rights, kufanya hivyo kwa sababu ni mgombea, hajakataza mtu..na Mafisadi wapo na wapo ndani CCM! hili halina ubishi, na wao wanajua zaidi kuliko sisi nani ni nani! na huyu bwana hana haja ya kuwaridhisha wananchi isipokuwa wanachama wa CCM kwani uchaguzi anaozungumzia ni wa ndani ya chama.

Majungu yapo, mbona Chacha Wangwe alipiga kelele na majungu ndani ya Chadema tukamwelewa na kuomba majibu na tukaweza kutenganisha na utawala wa nchi nzima..
Kwa nini wananchi bado mna fikra kwamba ukiwa mbunge wa CCM au ukiwa mgombea kiti chochote ndani ya CCM basi bila shaka wewe ni mwakilishi wa Taifa zima... kama vile tunaunga mkono system mbovu inayobomoa badala ya kujenga..
It's about time wananchi mnatakiwa kufikiria nje ya kabati la CCM..lakini kama watu bado akili zetu ni CCM tuuu na uchaguzi mzima ni ndani ya CCM, basi tumekwisha na hakika CCM itatawala milele..
 
Jamani mbona mnamshambulia Mhe. Mpendazoe wakati si yeye alielalamika?

Mada hii imeanza kwa Bill kutoa maoni yake kutokana na mtiririko wa nakala za magazeti kuhusiana na mkakati alioona yeye wa kumng'oa Mbunge huyo. Siasa inahitaji subira. Mpeni nafasi na Mpendazoe kutetea kiti chake. Hajalalamika wakuu.
 
Jamani mbona mnamshambulia Mhe. Mpendazoe wakati si yeye alielalamika? Mada hii imeanza kwa Bill kutoa maoni yake kutokana na mtiririko wa nakala za magazeti kuhusiana na mkakati alioona yeye wa kumng'oa Mbunge huyo. Siasa inahitaji subira. Mpeni nafasi na Mpendazoe kutetea kiti chake. Hajalalamika wakuu.

Inaonekana kama ameweka ubia na lile jimbo, mteule ama sijui wa milele hadi kifo chake....take home meseji ....kama hakuna alichokifanyia wananchi wake basi apishe wengine...!
 
Mzee wa sauti ZA umeme heshima mkuu.
Mimi nadhani kuna haja ya kubehua mfumo mbovu uliopo na kuleta mfumo workable.
Kwanza mawaziri wasiwe wabunge, pili katiba itamke majina ya wizara ili kuondoa kadhia ya uundwaji holela wa wizara. tatu waziri mkuu awe mtendaji na nafasi ya raisi iwe ni mpepeaji i mean ceremonial, nne posho za wabunge zipunguzwe kulinganisha mfumo wa mishahara ya serikali na walipe kodi kwa kila senti ya posho inayowadondokea. tano ukabila na udini viwekewe penal code zake. sita sheria ya usajili wa vyama iweke ukomo wa wagombea uraisi walioshindwa kupata popular vote ili kutoa nafasi kwa wengine kuingia ktk soko la kura. saba gavana wa benki kuu na wakurugenzi wa idara nyeti za serikali wapitishwe kwa kura bungeni ktk kuunga au kukataliwa uteuzi wao. nane Mahakama isiwe idara ktk wizara ya sheria na katiba, ipewe nafasi yake sawa ya mhimili wa dola pia utafutwe utaratibu muafaka wa kumpata na kumwapisha jaji mkuu. tisa sheria ya maadili ya viongozi wa umma irekebishwe ili kuchechemiza uwajibikaji zaidi. kumi kiongozi yeyote wa serikali ajivue au avuliwe madaraka yake YOTE ktk chama alichotoka ili awajibike na kutoa nguvu ya accountability....
Nina mengi kichwani ila nimeyawekea hakimiliki ili wasije wakaiga na kudandia hoja kwa nchani.

Mkuu Msanii heshima kwako.

Nakubaliana sana na mapendekezo yako karibu yote. Kama hayo uliyoyapendekeza hapo yakifanyika hivyo, nadhani tutaweza kuwa na uongozi bora zaidi nchini.

Tatizo ninaloliona katika moja ya mapendekezo yako ni la Gavana wa BoT na wakurugenzi wa idara zake (nyeti) kupitishwa na Bunge. Mkuu, labda unieleweshe zaidi. Ila naona Gavana wa BoT na Mkurugenzi wa idara za BoT ni wataalam wa fedha na masuala mengine ya kitaaluma na Bunge ni la wanasiasa. Sina uhakika kuwa Bunge lina uwezo wa kutusaidia katika hilo kwa ufanisi mkubwa. Kwa maoni yangu, Bunge linaweza kupata shida kusaidia kutokana na ufahamu wa Bunge zima kuhusiana na taaluma za viongozi hao ambao si wa kisiasa.
 
Nahamasa kweli na uchaguzi wa mwakani - maana swali langu kubwa litakuwa - hivi kuanzia uchaguliwe ubunge, na kuwa mbunge, umekaa muda gani jimboni hapa! Ama ukichakuguliwa kuwa mbunge tutahakikishaje unaishi katika jimbo hili uone hali halisi ya maisha yetu, uwe na ofisi ambayo tutagonga na kukuta! Tulete maswali yetu uyapeleke huko bungeni!
 
Ninafahamu kwa hakika kwamba Shigela alikuwa anahusika na hii kesi hapa chini akiwa mtuhumiwa muhimu. Siku ambayo alikuwa aitwe kuandika maelezo ya ziada polisi, akatangazwa kuwa Mkuu wa Wilaya. Ninachoweza kusema ni kwamba, tuna tatizo kubwa katika mfumo wetu wa sasa wa uteuzi ambapo watu wetu wa UWT hawana muda wa kufanyia upekuzi wateule, ama wanakuwa wako pamoja na wanaotakiwa kuteuliwa kwa hiyo kuwafichia mambo yao. Hii kesi hadi sasa imekufa.


IGP takes over police probe over State House 'forgery'

Thisday, Friday, August 11 2006


THE Inspector General of Police, Mr Saidi Mwema, is now personally supervising investigations into a scam involving forgery of State House documents, police sources said yesterday.

''In July, following complaints from a number of parties, the investigation has been reassigned to officers who are now reporting directly to the Inspector General of Police,'' a police source said.

The forgery of State House documents was first published by THISDAY and its sister KULIKONI newspaper in April, this year, but there has been concerns on progress in the investigation of the case.

The conmen had forged official Ikulu documents and Coat of Arms purportedly from the President's Office in an attempt to prevent a British business investor, Mr Mark Foley, from entering Tanzania. The case was originally being investigated by the office of the Director of Criminal Investigation (DCI).

However, sources say the investigations are now being led by a police inspector who is acting on instructions received directly from the IGP with the State House closely monitoring the probe.

''The detective handling the case now is a qualified accountant and has been assigned to this case in order to investigate allegations of serious fraud,'' the source said.

Allegations of fraud were linked to changes in management and ownership of a local company known as Construction Equipment Africa Limited in September 2004.

Mr Foley was the original investor of Construction Equipment Africa Limited, which he claims was later taken away from him through fraudulent means.

The company provides generators and support services to cellphone service providers in Tanzania, including Vodacom, Celtel and Mobitel. It was originally incorporated in Tanzania in April 2001.

Police have since called Mr. Raymond Orr, the firm's Finance Director, for questioning in connection with the issuance of a share certificate that was signed by Mr. Orr and granted the Company's Managing Director, Robert Thomson, 50 per cent ownership of Construction Equipment Africa.

Mr. Orr is also being questioned on the opening of a bank account at Standard Chartered Bank in June 2004.

Police have also questioned officials from State House and journalists familiar with the matter.

Investigators are questioning witnesses about representations made by various parties to Immigration authorities in April 2005 that led to Mr Foley being apprehended by immigration officers and wrongfully accused of being an illegal immigrant.

http://www.thisday.co.tz/News/547.html
 
Last edited:
Uongo mtupu, kwa lipi hasa alilolifanya katika mapambano dhidi ya mafisadi mpaka wamfuate. Ni akili finyu sana kufikiri mtu kama Rostam atumie pesa zake kwa mtu dhaifu kama huyu. Mlovezoe.............. huna kitu kaka, kila mtu ana haki ya kugombea. Kama hukutimiza ahadi zako jiandae kukaa pembeni.
Onyo msiwape nafasi waongo kuleta dhread za kujaza kurasa
 
Uongo mtupu, kwa lipi hasa alilolifanya katika mapambano dhidi ya mafisadi mpaka wamfuate. Ni akili finyu sana kufikiri mtu kama Rostam atumie pesa zake kwa mtu dhaifu kama huyu. Mlovezoe.............. huna kitu kaka, kila mtu ana haki ya kugombea. Kama hukutimiza ahadi zako jiandae kukaa pembeni.
Onyo msiwape nafasi waongo kuleta dhread za kujaza kurasa
 
Mishahara na posho yao vipunguzwe tu na kuwekwa kima cha chini kabisa tuone kama watakimbilia ,maana kila mtu itambidi athamini kile alichokisomea ,utamkuta mtu serikali imetoa gharama za kumfundisha uinjinia na udakitari na elimu zingine za ufundi akirudi anaenda kutafuta mambo ya siasa na kujiunga huko na ile hela yote aliyofundishiwa inakuwa imepotea bila kuonekana matunda yake ,ni wizi tu.

hapo ndio bunge litakuwa la mafisadi tu kwa ajili wao ndio watakuwa wana hela za kugombea....
lazima uwelewe kuna wabunge wengi kuwa bungeni si kufata kipato bali kinga kutokana na mambo yao waliyoyafanya na wanaweza kuzamini wabunge wengine
hii sera ya mishahara ya wabunge lazima muifikirie vizuri, embu fikiria mmbunge baada ya miaka mitano hana hela ya kugombea si itabidi aende kwa RA, alafu unazani ataweza kumuhukumu kweli
 
- Wakipata ubunge tu wanayakimbia majimbo yao, halafu wanataka kusingizia mafisadi wanatayarisha mtu, nonesense!

- Ni majimbo mawili tu ambayo ninajua for a fact kwamba mafisadi wanayawinda nayo ni ya Sitta na Mama Makinda, kwa sababu hawa ndio kikwazo chao bungeni, kama unaelewa vizuri siasa za bongo then uanjau wkamba tatizo la mafisadi sio media wala wananchi, ila wanaumizwa bungeni na hawa viongozi wawili tu, na ndio wamewakamia sana, lakini wengine waache magirini hawana record tu sasa wasidanganye umma!


FMES
hamna kuwindwaa yeyote atakayedondoka ni uwezo mdogo tuuu wa kuwahudumia watu wakeee...na wabunge wengi ccm waliingia kifisadi (wizai wa kura na rushwaaa kubwaaa)..

mafisadi ni akina nani na kwa nn??? (naomba kufahamu)

hatuwezi kuendelea hivi jamani kwani nchi ni zaidi ya majunguuu na wivu wa kijingaaaaa...

hatujaibiwa chochote mpaka sasa kwani rasilimali baki ni mara 100,000,000,000,0000 ya zilizotumikaaa...
 
Na mimi najiandaa kumng'oa Yono Kevela kuleeeeeee Njombe sijui mtasema ufisadi....na kuna jamaa angu nae anamdondosha mtu mzima Jackson Makwete hawa wabunge wamekuwa mzigo kwa sisi wananchi hawana chao 2010...
Msije mkasema nimetumwa na mafisadi kama hawa mmewahi waskia wanapigana vita ya ufisadi basi nitakuwa nimetumwa lakini kama hamjawahi sikia basi ndo hivyo hawa bungeni hawarudi 2010.
Sawa mkuu, ni busara zaidi ugombee kupitia upinzani.Kung'ang'ania kugombea kupitia CCM hilo bundi la ufisadi litakuandama.Nasema hivyo kwa sababu CCM tayari wana makundi matatu,yaani CCM Asili(Nyerereists),Mtandao Masilahi(Mafisadi) na Mtandao Matumaini(Anti-mafisadi).Yapimeni makundi hayo ili ujitambulishe uko kundi gani.
Huu ni ushauri wa bure kwa wote mnaotaka kugombea!
 
Kwani nani alimuambia huyo Mpendazoe kuwa hilo jimbo ni mali yake? Yaani yeye akwia Mbunge watu wengine hawaruhusiwi kuja kugombea unapofika wakati wa uchaguzi!

Tena huyu Mpendazoe ameripotiwa kuwa ni mjumbe wa bodi ya William Diamonds (samahani kama nimekosea kuliandika jina vizuri) na huwa haendi kwenye vikao kutoa maoni ya serikali hivyo tunaendela kuibiwa tu madini yetu.
 
Jamani wana JF.Watu wakiona maji ni mazito jimboni kwao, then wanakimbilia kusema kuwa fulani ni fisadi ili kuomba huruma ya magazeti.Magazeti ya kimwandika mara moja basi huyo tayari ni maarufu na wana JF kuanza kum support

Wana JF tusiwe wajinga.Hao wanao wataja mafisadi waulizeni kwanza kuwa kule kwenye majimbo yao wamewafanyia nini wananchi?

Sasa nimegundua kuwa,kinachotuangusha sana katika nchi hii ni haya magazeti.

Jamaa akienda bungeni na kusema Rostam fisadi basi huyo ni mzalendo na anafaa kuchaguliwa.Je huko anako toka ahadi zake amezitekeleza.

IPPMEDIA.Angalieni sana huyo Mwakyembe wetu. Usanii mtupu.Tsh 76m zetu tulizomchangia pale ubungo TBS amejengea ghorofa yake kule kunduchi.Sasa huo ni uzalendo?
 
IPPMEDIA.Angalieni sana huyo Mwakyembe wetu. Usanii mtupu.Tsh 76m zetu tulizomchangia pale ubungo TBS amejengea ghorofa yake kule kunduchi.Sasa huo ni uzalendo? Reply With Quote

76m hazijengi ghorofa wewe ni nyumba ya kawaida kabisa....ebooo....ubungo TBS ndo nini bureau of standards?
 
Hapa ndipo usanii wa wabunge wetu unapokuwa wazi na napata ugumu kuuelewa msimamo wa umma wa watanzania na wenzetu wengi humu JF. Giza na mwanga haviishi pamoja - ama kuna mwanga na giza halipo au giza limetanda na mwanga hauonekani, full stop.

Hii habari kuwa kuna wabunge mahiri ndani ya CCM wanaotetea maslahi ya taifa na hapo hapo kuna wabunge mafisadi ndani ya CCM hiyo hiyo inanipa shida. Either you are with them or you are against them, period - CCM haiwezi kukamata huku na huko, moja lazima iwaponyoke.

Kila kukicha tunashuhudia mwisho wa siku wakikumbatiana na kupongezana kwa kumwadhibu Zitto au kwa kukataa mabadiliko ya katiba au kwa kukebehi hoja ya Dr. Slaa au kwa kuunga mkono bajeti hewa ya fedha au kwa kupinga hoja ya kuiwajibisha serikali - ndio, wako pamoja !!
CCM na ufisadi ni kama konokono na gamba lake.​
 
76m hazijengi ghorofa wewe ni nyumba ya kawaida kabisa....ebooo....ubungo TBS ndo nini bureau of standards?

S
Code:
Mkuu,
Upeo wako mdogo kuelewa.
Hapo unataka maana ya neno TBS au kujua ufisadi wa huyo kaka yako msema ovyo?.
76M alitumbukiza kwenye ujenzi wa Nyumba yake ambayo ni Ghorofa.
 
Upeo wako mdogo kuelewa
.

Haya bwana nakubali


Hapo unataka maana ya neno TBS

TBS can mean anything ie Taking Back Sunday, Towcester Building Supplies, Trinitarian Bible Society, ndo sababu ya kukuuliza....naona umefanya dili...
kujua ufisadi wa huyo kaka yako msema ovyo?
.

Mtazamo wako wa kijinga huo, can substantiate that?

76M alitumbukiza kwenye ujenzi wa Nyumba yake ambayo ni Ghorofa.

Shida yako iko wapi hapo?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom