'Mafisadi hawapaswi kukaa meza moja na Kawawa, Mwinyi'

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Posted Date::6/2/2008
'Mafisadi hawapaswi kukaa meza moja na Kawawa, Mwinyi'

Na Salma Said, Zanzibar
Mwananchi

MFANYABIASHARA maarufu mjini hapa, Mohammed Raza amedai kushangazwa na Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kushindwa kuwachukulia hatua wajumbe wake wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kusisitiza hawapaswi kukaa meza moja na wazee wanaoheshimika, Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Rashid Mfaume Kawawa.

Kauli hiyo aliitoa jana nyumbani kwake Kibweni mjini hapa, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tuhuma hizo ambazo zinawakabili baadhi ya wanachama wa chama hicho.

Raza, alisisitiza kuwa, CC ya CCM ni chombo nyeti na chenye dhamana kubwa kwa Taifa kwa vile kinawajumuisha viongozi wakuu wa kitaifa na marais wastaafu, hivyo haitakuwa busara kwa mafisadi kushiriki katika vikao hivyo.

Ingawa hakutaja jina wala cheo, Raza, alidai katika vikao hivyo vya kamati hiyo, wamo wajumbe wanaotuhumiwa kwa ufisadi, hivyo katika hali ya kawaida wanawasononesha wazee kama waziri mkuu mstaafu, Rashid Kawawa, Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi na wengine ambao wanaheshimika sana nchini.

Raza ambaye alikuwa mshauri wa michezo wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), alikishauri CCM kuhakikisha kila mwanachama wake aliyetuhumiwa kwa ufisadi, anahojiwa na kufikishwa katika vyombo vya kisheria.

" CCM kingewahoji hawa wanaotuhumiwa kwa ufisadi ambao wengine ni wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu, tukisema tunamficha maiti chumbani kwa kuogopa kilio, siku moja tutakimbia sisi wenye nyumba kwa harufu, alisema.

Alisema ni vyema urafiki ukawekwa kando na kutangulizwa maslahi ya umma mbele kwa kuwa nchi hii ni ya Watanzania wote na akasisitiza kuwa kamwe kundi haliwezi kuongoza nchi.

Inanipa mashaka Kamati Kuu inakutana katika vikao vyake wakiwa na wajumbe ambao ni mafisadi, chama chetu hakina bwana na wala kundi haliwezi kuongoza nchi, kwa hivyo ni muhimu kushughulikiwa suala la mafisadi ili chama chetu kiendelee kushinda, alisema.

Mfanyabiashara huyo alimuomba Rais Jakaya Kikwete kushughulikia ufisadi nchini kwa kuwa Watanzania wengi wako nyuma yake wakimuunga mkono.

Raza, alisema mabilioni ya fedha yaliyochotwa na mafisadi katika akaunti ya nje ya ulipaji madeni EPA ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zingetosha kuhudumia jamii kama sekta za afya, elimu na muhimu kwa wananchi, lakini zimeishia kuwanufaisha wachache.

Alidai umefika wakati wananchi wakaguna kwa kususia kununua bidhaa zinazozalishwa na kampuni ambazo wamiliki wake wanahusishwa na ufisadi nchini kwani biashara zao, utajiri wao unatokana na wao kuzinunua.

Katika mkutano huo, alizungumzia tatizo la umeme visiwani Zanzibar, akijigamba kuwa yuko tayari kushirikiana na serikali kulipatia ufumbuzi mbadala kwa sababu yeye ana marafiki wengi katika nchi za Arabuni ameshafanya nao mazungumzo ya awali na kuonyesha dhamira ya kusaidia kulitatua.

Alisema kwamba ingawa jambo lenyewe linahitaji ufuatiliaji, lakini yeye kwa uzalendo wake atalifanya hila pasipo ujira wowote, kwani anaogopa yaliyotokea katika sakata la umeme wa dharura kwa Tanzania Bara maarufu kama Richmond.

Raza, alisema katika kutatua tatizo la umeme Zanzibar, Serikali ya Jamhuri ya Muungano inawajibika kusaidia kwa hali na mali kwa kuwa Zanzibar ni sehemu yake na hivyo isisubiri mpaka kuombwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

Ndugu zangu waandishi suala la kununua jenereta kwa ajili ya Zanzibar lenye uwezo wa kuzalisha umeme megawati 40 kwa serikali ya Muungano ni sawa na vijisenti tu, hivyo tunaomba watusaidie wenzetu kwani hata wao walipokuwa wana matatizo tuliwasaidia, " alisema.
 
Raza anaogopa kuwa Rostam! Stori inafurahisha sana, hususan discussion ya Umeme Zanzibar.

Well, kama Marekani walivyosema kuhusu kutusaidia kumpata Ballali, kama Serikali ya Mapinduzi haijatuomba, hatuwezi kujiingiza kuwasaidia! LOL!

But then again, sisi wenyewe Umeme unatushinda! LOL!
 
The kissing up by Raza is characteristic of CCM party cadres jockeying for position, this fella is particularly reminiscent of a pre presidential Salmin Amour.

My fear is that facts are distorted to the effect of painting Mwinyi and Kawawa as "ufisadi free".

The Mwinyi Administration, although not as "white collar crime" skillful as Mkapa's, was nonetheless mauled by corruption.This is a matter of record and anybody not seeing this should have their mental eye examined.That is if they are not flattering the old man in the usual CCM "kulindana" "kissing up" and "false heroes" tradition.

Kawawa himself is not above reproach.Way before freedom of press in the days of "Chama kushika hatamu" Kawawa was pressuring bank executives to write off as bad debts money lent to influential party cadres and parastatal bigwigs close to the party.

So are these really our standards in dealing with corruption?
 
Raza aionya CCM

na Waandishi Wetu, Zanzibar
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye ni mmoja wa makada maarufu wa chama hicho visiwani hapa, Mohamed Raza, amekionya chama chake dhidi ya kuwakumbatia mafisadi, akisema kuwa hatua hiyo inaweza kukiletea maafa chama hicho.

Akizungumza na waandishi jana nyumbani kwake Kibweni, Raza alifananisha kitendo cha CCM kuwakumbatia viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi kuwa ni sawa na mtu aliyeficha maiti ndani ya nyumba yake.

Alisema itafika wakati, hali ya mambo itakuwa mbaya zaidi na watu kuanza kuikimbia nyumba hiyo.

Alisema kuwa miongoni mwa viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi ni wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya chama hicho, na kuwaacha waendelee na nyadhifa zao ni kukichafua chama bila sababu ya msingi.

Alisema ingawa inaweza kuonekana kuwa kuwakingia kifua watuhumiwa hao ni muafaka sasa, lakini chama hicho kinapaswa kukumbuka kuwa hivi sasa kipo kwenye mteremko kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Alisema Kamati Kuu ya CCM inapaswa kuchukua hatua kwa vitendo na si kuwakumbatia watuhumiwa hao, huku akitoa wito kwa wananchi kutumia njia mbadala ya kususia biashara za watu ambazo zimechangia katika kufanya ufisadi nchini.

"CCM ingewahoji hawa wanaotuhumiwa kwa ufisadi, ambao wengine ni wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu. Tukisema tunamficha maiti chumbani kwa kuogopa kilio, siku moja tutakimbia sisi wenye nyumba kwa harufu mbaya, maiti haifichwi bwana.

"Mimi nashangaa mtu kama mzee Kawawa au mzee Ali Hassan Mwinyi wanajisikiaje kukaa meza moja wakati wa mikutano ya chama na hawa wanaotuhumiwa kwa ufisadi," alisema.

Aliitaka serikali na CCM kulifanyia kazi suala hilo kwa kuhakikisha kuwa kila aliyetuhumiwa kwa ufisadi anachukuliwa hatua kali bila ya kuogopwa, kwa kuwa viongozi waliopo madarakani wamewekwa kwa ridhaa ya wananchi ili wawatumikie.

Raza alisema katika suala la nchi hakuna urafiki, hivyo ni vyema suala hilo la urafiki likawekwa kando na kutangulizwa masilahi ya umma.

Raza, ambaye ni mfanyabiashara maarufu Visiwani hapa, alisema amesikitishwa sana na mabilioni ya fedha yaliyochotwa na mafisadi ya EPA na Richmond, fedha ambazo zimewanufaisha watu wachache, wakati zingeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika huduma za kijamii, ikiwemo elimu na afya.

Alisema fedha zinazodaiwa kufujwa kwenye kashfa za ununuzi wa rada, ndege ya rais na BoT, zingeweza kutumika kujenga zahanati zenye dawa katika mikoa yote na kusomesha vijana wengi nje ya nchi.
 
The kissing up by Raza is characteristic of CCM party cadres jockeying for position, this fella is particularly reminiscent of a pre presidential Salmin Amour.

My fear is that facts are distorted to the effect of painting Mwinyi and Kawawa as "ufisadi free".

The Mwinyi Administration, although not as "white collar crime" skillful as Mkapa's, was nonetheless mauled by corruption.This is a matter of record and anybody not seeing this should have their mental eye examined.That is if they are not flattering the old man in the usual CCM "kulindana" "kissing up" and "false heroes" tradition.

Kawawa himself is not above reproach.Way before freedom of press in the days of "Chama kushika hatamu" Kawawa was pressuring bank executives to write off as bad debts money lent to influential party cadres and parastatal bigwigs close to the party.

So are these really our standards in dealing with corruption?

Kama hivyo ni kweli, kwa nini Raza ajiharibie mbele ya Powers That Be kwa kujikomba kwa Powers That Have Been?

Si unajua opportunistst huwa wakisha maliza wanatupa? Sasa ata jockey vipi kwa kujiharibia?
 
Kama hivyo ni kweli, kwa nini Raza ajiharibie mbele ya Powers That Be kwa kujikomba kwa Powers That Have Been?

Si unajua opportunistst huwa wakisha maliza wanatupa? Sasa ata jockey vipi kwa kujiharibia?

1.Networks.The so called "Powers that have been" are not really the powers that have been.These powers are still very influential because they dished out many influential appointments and watered many a successful career.The president himself is kissing up to the powers that have been in his "mwacheni mzee apumzike". Mkapa ni "Mzee" kwake kampita miaka mingapi? kama siyo ku kiss up? Raza sees Karume as a lightweight and probably thinks using his name will be more like endorsing him than using him as a power base.Karume is such a joke to the extent mpaka mawaziri wake walimpiga vijembe according to some reports.

2.Tradition. Kuheshimu wazee na wastaafu regardless.Ndiyo maana Lowassa na Chenge bado wabunge despite of all the mess they are in.And this is not only a problem amongst the top echelon of CCM, I have not heard any backlash from Monduli or Bariadi to ask Lowassa or Chenge to resign parliamentary responsibilities based on corruption charges. I don't care much about the rest of the country because they did not elect them.
 
Well, kama Marekani walivyosema kuhusu kutusaidia kumpata Ballali, kama Serikali ya Mapinduzi haijatuomba, hatuwezi kujiingiza kuwasaidia! LOL!

Nyinyi watu mnashangaza sana. Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano, sasa inasubiri iombwe na nani kutoa huduma katika eneo lake. Mbona wakati Zanzibar ilipotaka kujiunga na OIC, haikukaa tu ikasubiri iombwe ruhusa, bali ilikurupuka na kutoa shindikizo na masababu makubwa makubwa ya kuwa eti inatetea "jurisdiction" yake.
 
Mweshimiwa Mbunge..... sasa na yeye anakaa nao Hao Mafisadi Bungeni
 
Back
Top Bottom