Mafanikio ya Royal Tour yaanza kuonekana kwa kasi ya kutisha, Hongera Rais Samia

Leo gazeti za Citizen limeripoti mawakala wa Utalii kutoka Nchini Marekani wameingia Tanzania kujionea vivutio vya Utalii vilivyopo hapa nchini Kwa ajiri ya kuwaleta Wamarekani. Hii ni wiki chache tu tangu Rais Samia Suluhu Hassan afanye kipindi maarufu duniani kinachohusiana na utalii na fursa za uwekezaji cha The Royal Tour.

Ikumbukwe kuwa pamoja na kuwa na vivutio vingi vya utalii na fursa nyingi za uwekezaji, Tanzania imekuwa nyuma sana katika kupokea watalii wengi hapa Africa Kwa kupokea watalii chini ya Milioni 2 kwa mwaka. Hili limekuwa linatokea huku sekta ya utalii ikiwa ndo sekta inayochangia kwa Kiwango kikubwa zaidi pato la Taifa kabla ya kutokea Kwa janga la corona!

Kwa mafanikio haya makubwa yanayoanza kuonekana katika sekta ya utalii Tanzania inaweza kufikisha watalii Mil 5 ifikapo mwaka 2025 na pato la Taifa kukua kwa kiwango cha kutisha.

Hongera sana Rais Samia kwa Ubunifu wa kufanya program ya Royal Tour na hakika The future is now promising for Tanzania.

Go Samia! Go Tanzania

Shida yako ni moja tu! Hujui ulichokiandika! Zezetaa za magogoni
 
YAni ukiona BAk kaandika kitu au erythrocyte lazuma kiwe Cha kuiponda serikali yaani mtakuja kuaibika wakati tukihesabu mafaniki nyie mmekalia majungu
 
Mdogo wake Shaka kaandika uzi...😁😁😁

Hao huwa wanakuja tu kila mara wewe
 
Kwa akili yako unadhani ni Tanzania tu inayotegemea utalii?

Fuatilia nchi kama Uswisi, France na Brazil zinaingiza mapato makubwa kutokana na nini Kama sio utalii!

Alafu huo ndo ushamba wenu ambao kila siku umekuwa unaturudisha nyuma? Kwani kukuza uchumi kwa kutumia utalii ni mbaya? Sio kufanya kazi?
tuache kutegemea Wazungu na hela zao ndio tujenge uchumi wetu, hebu tujaribu kufikiria namna nyingine kukuza uchumi wetu baadala ya hii ya miaka mingi ya kutemea utalii na watalii...

Linchi likubwa sana, lina mapoli kibao, mito inayotiririka usiku na mchana, bahari iliyojaa samaki, ardhi yenye rutuba na madini lukuki..lakini lingine la muhimu ni idadi kubwa ya watu zaidi ya 50mill..

Nini kifanyike?,, hakuna namna zaidi ya kizazi hiki kujitolea na kufanya kazi kwa bidid usiku na mchana kuijenga nchi kwa jasho na damu ili vitukuu vyetu vije kuishi kwa heshima...
 
Endeleeni kukariri! Ndo mjivunze wazungu wanavyojua kutengeneza fursa!

Hawa na agent wamekuja kuweka mikataba na ma hoteli ya kitanzania pamoja na kampuni za bongo ili booking zitakapoanza wawe kwenye biashara tayari kuingiza pesa
Wewe ndiye umekaririshwa Kuja kutulisha propaganda hapa. Hao viewers wa kuangalia hiyo tour itategemea na Channel itakayorusha. Kama hizo tour zingekuwa popular basi wote tungeshaiona tour ya Kagame.
 
Mbona tourist agents wamekuwa wakija nchini toka kitambo!

Achana na hao mapimbi wanajaribu kutuaminisha Mambo ambayo hawajui.

Kabla ya ujio wa corona watalii waliokuwa wakitumia KIA pekee yake kwa miaka 3 mfululuzo walifikia 600,000 mpaka 700,000 kwa mwaka.

Mashirika ya ndege yafukia 13 sasa hiyo Royal tour sijui mdudu gani ni mbwe mbwe tu haina lolote.

Kuhusu uwekezaji labda watu hamjui Grumeti Reserves au Four Seasons Safari Lodges inamilikiwa na wawekezaji wa kiwango gani.

Ebu tuondoleeni ushamba na ushambenga.
 
Kwa akili yako unadhani ni Tanzania tu inayotegemea utalii?

Fuatilia nchi kama Uswisi, France na Brazil zinaingiza mapato makubwa kutokana na nini Kama sio utalii!

Alafu huo ndo ushamba wenu ambao kila siku umekuwa unaturudisha nyuma? Kwani kukuza uchumi kwa kutumia utalii ni mbaya? Sio kufanya kazi?

ni njia ambayo tunaitumia miaka yote na hatufanikiwi, hao waliowataja wanaitumia na inaleta manufaa kwao....Ni vyema nguvu tukaiweka kwenye vitu vingine na issue ya utalii tukaiacha kwanza tudeal na mengineyo siku huko mbele tukipata akili nyingine tutaendelea nayo..
 
Kwani pingapinga fc mnakosaga maneno? Nyie si ndo mnadai Hamza aliporwa madini na polisi mkiombwa ushahidi mnapotea
Wewe ndiye umekaririshwa Kuja kutulisha propaganda hapa. Hao viewers wa kuangalia hiyo tour itategemea na Channel itakayorusha. Kama hizo tour zingekuwa popular basi wote tungeshaiona tour ya Kagame.
 
Kwani pingapinga fc mnakosaga maneno? Nyie si ndo mnadai Hamza aliporwa madini na polisi mkiombwa ushahidi mnapotea
Mkuu Angalia lini nilijiunga JF. Sisi ndiyo waanzilishi wa jukwaa hili. Nyinyi ndiyo mlioingia na siasa zenu mkatuharibia jukwaa.
 
Kwa iyo wewe watalii laki 6 Au 7 ndo unaona mafanikio? Misri, Algeria, South Africa na Morocco wanaoingiza watalii milioni si chini ya 5 na hadi kufikia Mil 10 kwa mwaka wao wasemeje?

Kama sekta ya utalii ndo inayoongoza kwa kuchangia pato la Taifa pamoja na kuingiza hao watalii laki 6 au 7 huoni Kuna haja kuweka nguvu kubwa zaidi ili tufanye vizuri zaidi na tupate hela nyingi zaidi kwa maendeleo yetu?
Achana na hao mapimbi wanajaribu kutuaminisha Mambo ambayo hawajui.

Kabla ya ujio wa corona watalii waliokuwa wakitumia KIA pekee yake kwa miaka 3 mfululuzo walifikia 600,000 mpaka 700,000 kwa mwaka.

Mashirika ya ndege yafukia 13 sasa hiyo Royal tour sijui mdudu gani ni mbwe mbwe tu haina lolote.

Kuhusu uwekezaji labda watu hamjui Grumeti Reserves au Four Seasons Safari Lodges inamilikiwa na wawekezaji wa kiwango gani.

Ebu tuondoleeni ushamba na ushambenga.
 
Nani kasema hatufanikiwa wakati ndo sekta inayoongoza kwa kuchangia pato la Taifa nchini? Tena kipindi cha covid tu ndo imeshuka?

Huoni kuwa kuna hata ya kuongeza jitihada zaidi? Huoni jitihada zinazofanyika ndo jambo sahihi zaidi?
ni njia ambayo tunaitumia miaka yote na hatufanikiwi, hao waliowataja wanaitumia na inaleta manufaa kwao....Ni vyema nguvu tukaiweka kwenye vitu vingine na issue ya utalii tukaiacha kwanza tudeal na mengineyo siku huko mbele tukipata akili nyingine tutaendelea nayo..
 
Leo gazeti za Citizen limeripoti mawakala wa Utalii kutoka Nchini Marekani wameingia Tanzania kujionea vivutio vya Utalii vilivyopo hapa nchini Kwa ajiri ya kuwaleta Wamarekani. Hii ni wiki chache tu tangu Rais Samia Suluhu Hassan afanye kipindi maarufu duniani kinachohusiana na utalii na fursa za uwekezaji cha The Royal Tour.

Ikumbukwe kuwa pamoja na kuwa na vivutio vingi vya utalii na fursa nyingi za uwekezaji, Tanzania imekuwa nyuma sana katika kupokea watalii wengi hapa Africa Kwa kupokea watalii chini ya Milioni 2 kwa mwaka. Hili limekuwa linatokea huku sekta ya utalii ikiwa ndo sekta inayochangia kwa Kiwango kikubwa zaidi pato la Taifa kabla ya kutokea Kwa janga la corona!

Kwa mafanikio haya makubwa yanayoanza kuonekana katika sekta ya utalii Tanzania inaweza kufikisha watalii Mil 5 ifikapo mwaka 2025 na pato la Taifa kukua kwa kiwango cha kutisha.

Hongera sana Rais Samia kwa Ubunifu wa kufanya program ya Royal Tour na hakika The future is now promising for Tanzania.

Go Samia! Go Tanzania


Naona unapulizia kinyesi perfume.
 
Kwa iyo wewe watalii laki 6 Au 7 ndo unaona mafanikio? Misri, Algeria, South Africa na Morocco wanaoingiza watalii milioni si chini ya 5 na hadi kufikia Mil 10 kwa mwaka wao wasemeje?

Kama sekta ya utalii ndo inayoongoza kwa kuchangia pato la Taifa pamoja na kuingiza hao watalii laki 6 au 7 huoni Kuna haja kuweka nguvu kubwa zaidi ili tufanye vizuri zaidi na tupate hela nyingi zaidi kwa maendeleo yetu?

70% walikuwa wakishuka Nairobi.
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom