Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Kiukweli na pasina shaka Rais Magufuli amefanya mambo mengi sana katika taifa hili la Tanzania hasa Ujenzi wa barabara, Kuzirejesha meli zilizokuwa hazifanyi kazi kwa muda mrefu, Kukarabati shule kongwe zilizokuwa zimechakaa mfano Pamba Secondary ya Mwanza ilikuwa imejaa popo ukiiangalia sasa hivi imekuwa kama mpya na nyingine nyingi, Kuanzisha ujenzi wa treni ya mwendo kasi SGR, Kuboresha jiji la Dar es Salaam, Kuhamishia makao makuu Dodoma. Kuanza safari za treni kutoka Dar mpaka Arusha , Kuboresha huduma za Afya, Usambazaji wa umeme vijijini mfano siku nilipotembelea kijiji cha wazazi wangu na kukuta umeme unawaka sikuamini kabisa lakini ndivyo hivyo. Nawaasa vijana tusipendelee sana ushabiki wa kisiasa katika mitandao tuwe wazalendo wakufanya mambo yanayohihusu jamii kubwa na sio kujiangalia wewe kama wewe hujafanyiwa nini Rais unayemtuhumu kila siku ni kutoa matusi yasiyoleta tija kwa jamii.

Ndiyo amefanya hayo lakini kwanini asiwaongeze mishahara watumishi kama pesa ya kufanya hayo anayo hivi hayo aliyofanya yatamsaidia nini mtanzania kama mwalimu na daktari hawaongezewi mshahara ili waweze kufanya kazi yao kwa weledi hivyo ni vitu kwanini hajali watu, wastaafu wanahangaika hawalipwi pension yao kwanini.

Pesa za mifuko ya hifadhi ya jamii zimechukuliwa zote kwanini. Kutowaongeza mishahara wafanyakazi kumrfanya maisha yamekuwa magumu sana kwa watanzania walio wengi ambao sasa hawaoni faida yoyote kama maisha yao hayana nafuu. Chuki inatokana na maisha ya wananchi walio wengi kuzidi kuwa magumu kila siku huku wakihubiriwa kuwa wamefika uchumi wa kati.

Wananchi wanaona maisha yao yamezidi kuwa duni kinyume na matarajio yao halafu mtu anasema unataka Rais akupe pesa, hivi kutomuongeza mfanyakazi mshahara wake kwa miaka mitano huku hali ya maisha inazidi kupanda si ni kumfanya awe fukara zaidi nini kisichojulikana.

Hata biashara zinategemea wafanyakazi wanunue hata wakulima wanategemea wafanyakazi wanunue hata viwanda vinategemea wafanyakazi wanunue sasa usipomuongezea mshahara mfanyakazi unamnyima mkulima kupata soko la mazao yake sababu mfanyakazi hana uwezo wa kununua, unamnyima mwenye kiwanda uwezo wa kuuza bidhaa zake sababu mfanyakazi hana uwezo wa kununua unamnyima mfanya biashra kupata mauzo sababu mfanyakazi hana uwezo wa kununu ndiyo tumefikishana hapa tulipo kila mtu analalamika maisha magumu. Chanzo ni serikali kushindwa kupandisha mishahara ya wafanyakazi ili iendane na gharama ya maisha.
 
Binafsi nimefurahishwa na kasi ya Rais Dkt. Magufuli. Naamini wapo pia wengi wanaoungana nami katika furaha hii. Rais Magufuli ameanza kwa kasi ambayo kama ataimaintain, Tanzania haimalizi miaka mitano itakuwa tayari ni nchi yenye kipato cha kati.

Hata hivyo wapo baadhi yetu ambao wanakejeli kasi hiyo. Hao kwangu ni watu waliozoea ubwete na bora liende!. Wanamwona Magufuli kuwa ni mtu atakayekuwa kauzibe kwao!...
Ninaumia sana ninapoona uzi niliouanzisha mimi mwenyewe Mjenga, Nov 9, 2015 leo hii umebadilishwa na kumilikishwa mtu mwingine. Mods hii inakera sana!. Nitalalamika hadi mtakaporudisha uzi huu mikononi mwangu ama mnifungie tu ijulikane moja!. Kwa watu wote mnaochangia uzi huu, hebu fuatilieni kama kipindi hicho uzi huu haukuwa unasomeka kwa authority yangu mimi Mjenga!?
 
Anachukiwa na watoa rushwa, mafisadi na madubwasha yasiyosingatia sheria na taratibu za nchi.

Wengi tunampenda Magu
Labda mnaompenda ni Mafisadi Papa mliopo serikalini kwa sababu hadi sasa Magufuli ame-prove beyond reasonable doubt kwamba anawaogopa mafisadi wa kweli waliofisidi hii nchi!!

Kundi la kwanza ambalo limeiba sana kwenye hii nchi ni High Profile CCM Politicians! Nitajie MMOJA TU ambae amechukuliwa hatua na Magufuli!!!

Top Government Executives, kama vile Makatibu Wakuu ni kundi lingine ambalo limefanya ufisadi mkubwa sana nchi hii: Again nitajie ONLY ONE Top Government Official at ministerial level aliyewahi kuchukuliwa hatua na Magu!!!

Hao akina Rugemalila na wenyewe bado wapo Segerea kwa sababu WAMEGOMA kukamiliwa pesa na Mlinzi wa Mafisadi Papa Nchini!!!
 
Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imeongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma za afya 1,769, zikiwemo zahanati 1,198, vituo vya afya 487, hospitali za wilaya 71, hospitali za mikoa 10, ikiwemo Hospitali ya Mkoa wa Mara, (Mwalimu Nyerere Memorial Hospital) ambayo ujenzi wake ulikwama tangu miaka ya 1970.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imejenga hospitali za rufaa za kanda 3. Hii imefanya vituo vya kutolea huduma za afya kuongezeka kutoka 7,014 mwaka 2015 hadi kufikia 8,783 hivi sasa.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imeajiri watumishi wapya wa afya wapatao 14,479, wakiwemo madaktari wapya 1,000 walioajiriwa hivi karibuni. Hii imeongeza idadi ya watumishi wa afya nchini kutoka 86,152 mwaka 2015 hadi 100,631 mwaka 2020.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imeimarisha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba, ambapo iliongeza bajeti yake kutoka shilingi bilioni 31 mwaka 2015 hadi shilingi bilioni 270 hivi sasa na pia imenunua na kusambaza magari ya kubeba wagonjwa (Ambulances) 117.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imefanikiwa kusomesha madaktari bingwa 301 ambao wamewezesha kuimarisha matibabu ya kibingwa nchini, hususan kwa magonjwa ya moyo, masikio, figo, mifupa, ubongo, kansa, na kadhalika.

Kutokana na hatua hizo, Miaka mitano ya Magufuli, Tanzania imeongeza idadi ya akina mama wanaojifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kutoka asilimia 64 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 83 hivi sasa.

Miaka mitano ya Magufuli, vifo vya watoto wachanga (wenye chini ya siku 28) vimepungua kutoka wastani wa vifo 25 hadi vifo 7 kwa kila vizazi hai 1,000; na idadi ya rufaa za kwenda nje ya nchi zimepungua kwa asilimia 95.

Kutokana na kuimarishwa kwa matibabu ya kibingwa, Miaka mitano ya Magufuli, Tanzania imeweza kupokea baadhi ya wagonjwa kutoka mataifa jirani ambao wameanza kuja kutibiwa nchini, hususan magonjwa ya moyo.

#UshindikwaCCM
#Magufulimitanotena
 
Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imeongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma za afya 1,769, zikiwemo zahanati 1,198, vituo vya afya 487, hospitali za wilaya 71, hospitali za mikoa 10, ikiwemo Hospitali ya Mkoa wa Mara, (Mwalimu Nyerere Memorial Hospital) ambayo ujenzi wake ulikwama tangu miaka ya 1970.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imejenga hospitali za rufaa za kanda 3. Hii imefanya vituo vya kutolea huduma za afya kuongezeka kutoka 7,014 mwaka 2015 hadi kufikia 8,783 hivi sasa.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imeajiri watumishi wapya wa afya wapatao 14,479, wakiwemo madaktari wapya 1,000 walioajiriwa hivi karibuni. Hii imeongeza idadi ya watumishi wa afya nchini kutoka 86,152 mwaka 2015 hadi 100,631 mwaka 2020.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imeimarisha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba, ambapo iliongeza bajeti yake kutoka shilingi bilioni 31 mwaka 2015 hadi shilingi bilioni 270 hivi sasa na pia imenunua na kusambaza magari ya kubeba wagonjwa (Ambulances) 117.

Miaka mitano ya Magufuli, Serikali imefanikiwa kusomesha madaktari bingwa 301 ambao wamewezesha kuimarisha matibabu ya kibingwa nchini, hususan kwa magonjwa ya moyo, masikio, figo, mifupa, ubongo, kansa, na kadhalika.

Kutokana na hatua hizo, Miaka mitano ya Magufuli, Tanzania imeongeza idadi ya akina mama wanaojifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kutoka asilimia 64 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 83 hivi sasa.

Miaka mitano ya Magufuli, vifo vya watoto wachanga (wenye chini ya siku 28) vimepungua kutoka wastani wa vifo 25 hadi vifo 7 kwa kila vizazi hai 1,000; na idadi ya rufaa za kwenda nje ya nchi zimepungua kwa asilimia 95.

Kutokana na kuimarishwa kwa matibabu ya kibingwa, Miaka mitano ya Magufuli, Tanzania imeweza kupokea baadhi ya wagonjwa kutoka mataifa jirani ambao wameanza kuja kutibiwa nchini, hususan magonjwa ya moyo.

#UshindikwaCCM
#Magufulimitanotena
 
Mkuu, bila hata ya kujali usahihi na uhalisia wa takwimu ulizoziweka. Ebu tuambie sasa ubora wa huduma za afya ktk maeneo tajwa. Nia aibu kujificha ktk wingi wa vitu huku ubora wake ukiwa hafifu sana.
 
Nimefuatilia kampeni za dk Magufuli na kufanya mahojiano na watu mbalimbali wasio na mlengo wowote Arusha,Dar na Mwanza kwa sampling ndogo sana. Inaonekana iwapo uchaguzi ungefanyanyika leo angeshinda kwa asilimia 60,asilimia 10 wangepigia upinzani na asilimia 30 hawajaamua(undecided).

Hivyo hawa 30% wanahitaji ushawishi ili kuwabadilisha kupigia CCM angalau kufikia 85% kura za urais. Changamoto kubwa ni kupata ushindi kwenye Ubunge na udiwani kutokana na sababu mbalimbali ambapo ni asilimia 52 wangepigiwa kura ya ushindi upande wa CCM. Haya ni maoteo ya uchambuzi wangu binafsi wa maoni yaliyotokana na mahojiano ya wazi.wapiga kura wengi wakisema Rais Dk Magufuli wanampigia kura kutokana na :

1.Uchapakazi wake na ufuatiliaji uliotukuka

2.Ubunifu wa mifumo mbalimbali i.e malipo serikalini

3. Ujasiri wa utekelezaji wa maamuzi i.e miradi mikubwa kufufua shirika la ndege etc

4.maono yake wakirejea suala la korona

5.uwezo mkubwa wa kushughulikia masuala ya kimaadili serikalini

6. Miradi ya kitaifa aliyoianzisha akamilishe yeye

7.msimamo wake usioyumba kwenye masuala mazito ya kitaifa

8. Maamuzi ya papo kwa papo kwenye field i.e ziara za kutatua kero

9.Muwazi na Mkweli

10. Amejenga ushawishi wa kimataifa kama Rais mwenye kujiamini na wa kipekee mzalendo wa nchi yake na Afrika. Hivi ni baadhi ya vigezo wanavyotumia baadhi ya wananchi kumpigia kura Dk.Magufuli. LaKini wanakiri pia kuwepo na changamoto kadhaa za uongozi, kiuchumi na kijamii wanazoamini kipindi kijacho ataweza kuzikabili kutokana na uzoefu alioupata kwenye awamu ya hii ya kwanza.

Wananchi wengi waliohojiwa kuhusu upinzani walikuwa na hofu na vyama vya upinzani kuhusu uwezo wao wa kioganaizeni kuongoza nchi na exposure kuhusu mambo ya kiserkali na utayari wa kushika madaraka makubwa ya nchi. Haya ni maoni ya wananchi siyo conclusive. tuyajadili kwa hoja
 
Wapiga kura tumeanza kumuelewa,hakika JPM mitano tena ni lazima ili kulifikisha taifa letu kwenye neema zajuu zaidi ya zilizopo sasa.
 
Nilidhania ni katika nyanja ya kuifungua nchi kwa mtandao wa barabara tu...kumbe anaweza na amefanikiwa kufikisha huduma za afya kote nchini.
Hii ni icon ya mabadiliko
 
Nilidhania ni katika nyanja ya kuifungua nchi kwa mtandao wa barabara tu...kumbe anaweza na amefanikiwa kufikisha huduma za afya kote nchini.
Hii ni icon ya mabadiliko
Si hivyo tu pote ukitaka akuonyeshe nyaya za umeme anakuonyesha zile pale

Ukimuuliza shule za Bure anakuonyesha zile pale nk
 
Halafu hospital ya rufaa ya mkoa wa Dodoma haina gloves? Hivyo vituo vya afya vitaziokota wapi?

Achilia mbali medical facilities zingine tuanze na gloves tu
 
Nilidhania ni katika nyanja ya kuifungua nchi kwa mtandao wa barabara tu...kumbe anaweza na amefanikiwa kufikisha huduma za afya kote nchini.
Hii ni icon ya mabadiliko
Kabla ya hapo hakukuwa na zahati na vituo vya afya nchi hii? Mbona kama vile nchi imeanza miaka 5 iliyopita? Hivi mnadhani nani atadanganyika kwa mambo haya ya kizushi?
 
Halafu hospital ya rufaa ya mkoa wa Dodoma haina gloves? Hivyo vituo vya afya vitaziokota wapi?

Achilia mbali medical facilities zingine tuanze na gloves tu
Uhitaji na matumizi ya gloves lazima uongezeke kwa kuwa facilities zimeongezeka ndani ya muda mfupi...in two years kutakuwa na forecasting nzuri ya bidhaa tiba
 
Nilidhania ni katika nyanja ya kuifungua nchi kwa mtandao wa barabara tu...kumbe anaweza na amefanikiwa kufikisha huduma za afya kote nchini.
Hii ni icon ya mabadiliko
huko mahospitalini hakuna hata dawa,hebu imagine MUHIMBILI hakuna paracetamol kweli???? Yaani hakuna panadol hospitali ya taifa!
 
Uhitaji na matumizi ya gloves lazima uongezeke kwa kuwa facilities zimeongezeka ndani ya muda mfupi...in two years kutakuwa na forecasting nzuri ya bidhaa tiba
Acha ujinga wewe huo uhitaji umeongezeka kwa minajiri ipi wagonjwa wameongezeka ama?

Wodi namba 11 hospital ya mkoa wa Dodoma kwa siku za hivi karibuni ikizidi sana idadi ya wagonjwa ni watano (5) tu!

Leba hakuna gloves wanaojifungua wanaambiwa waende nazo!
ICU hakuna gloves, all over the hospital hakuna gloves wala sterilise.
Wanafunzi wakienda field wanaambiwa waje na gloves.

Hivyo vituo vya afya vitakuwa na nini kama hospital kubwa kama ya Dodoma haina gloves tu?
Magufuli to HELL
 
Acha ujinga wewe huo uhitaji umeongezeka kwa minajiri ipi wagonjwa wameongezeka ama?

Wodi namba 11 hospital ya mkoa wa Dodoma kwa siku za hivi karibuni ikizidi sana idadi ya wagonjwa ni watano (5) tu!..
Wagonjwa wanaofika hosoitali wameongezeka mfano wajawazito waliokuwa wanajifungulia majumbani mwaka 2015 walikuwa around 45% sasa ni 80 %. vituo vinavyofanya upasuaji vimeonhezeka.
 
115 Reactions
Reply
Back
Top Bottom